Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 12/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kusaidia Wengine Waabudu Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Wahudumu wa Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Wafundishe Watoto Wako Kumsifu Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 12/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ kwa sababu ya zile habari mpya kuhusu kuanza kwa watu wasiobatizwa kwenda nje katika huduma ya peupe, je! mwanafunzi wa Biblia aweza kualikwa aambatane na mtu kwa muda fulani ili aone jinsi kazi ile hufanywa?

Kwa msingi, watu wasiobatizwa ambao huandamana na Mashahidi wa Yehova katika huduma ya shambani ni watu ambao wamestahili kuwa wahubiri wa habari njema.

Watu wengi katika halaiki hustahi Mashahidi wa Yehova kwa ajili ya kazi yao nzuri isiyo na kifani ya ‘kufanya wanafunzi, kuwafundisha’ kutoka mlango kwa mlango na kupitia mafunzo ya nyumbani ya Biblia. (Mathayo 28:19, 20, NW) Basi, halaiki ya watu ingekata shauri gani kuhusu mtu anayeandamana na Shahidi katika huduma hii? Kwa kusababu mambo vizuri wangekata shauri kwamba mwandamani huyo pia ni mhudumu au akaribia sana kuwa hivyo.

Ni kweli kwamba hali fulani zilizo tofauti zaweza kuja akilini.

Katika pindi chache sana wazee wafaao wameruhusu mwandishi wa habari, profesa wa koleji, au watu kama hao waandamane na Shahidi katika huduma ya nyumba kwa nyumba ili aone jinsi hufanywa. Bila shaka, sura na vitendo vya mtu huyo katika pindi hizo havipasi kuhitilafiana na viwango vyetu. Na huenda Shahidi yule akataka kutajia wenye nyumba kwamba mwandamani huyo ni mwandishi wa habari au profesa ambaye anapendezwa na kuona jinsi sisi hufanya kazi yetu ya Biblia iliyo ya umaana.

Pia, wazazi Wakristo huja pamoja na watoto wao katika huduma hata ikiwa ni wachanga mno au kwa njia nyingineyo hawako tayari kuwa wahubiri wasiobatizwa. Hivyo wazazi hawa hawaachi watoto wao bila mtu wa kuwaangalia. Kuwa pamoja nao katika utumishi wa shambani huruhusu wazazi waambie watoto wao kuhusu Neno na njia za Mungu ‘watembeapo njiani.’ (Kumbukumbu 6:4-7) Lakini hii ni sehemu ya maisha ya jamaa ya Kikristo, wala si kama kuleta kwa Shahidi mtu mwingine aandamane naye akiwa mtazamaji tu. Bila shaka, mazoezi hayo ya kimzazi hutayarisha watoto kwa ajili ya wakati ambapo watasifu Yehova wakiwa wahubiri. — Mathayo 21:15, 16; linganisha Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 99, 100.

Ingawa hivyo, namna gani kuhusu mtu ambaye Shahidi anaongoza funzo la Biblia pamoja naye, mtu ambaye yuko njiani kuelekea kuwa mwanafunzi? Yeye ana sababu njema ya kuambia watu wa ukoo, wafanya kazi wenzake, majirani, na wengine kuhusu “matendo makuu ya Mungu” ambayo amejifunza kutokana na Maandiko. (Matendo 2:11) Yatumainiwa kwamba hatua fulani itafika aone uhitaji wa kushiriki pamoja na Mashahidi wa Yehova katika mipango iliyopangwa kitengenezo ya ‘kulihubiri neno la Mungu.’—Matendo 13:5.

Hivi majuzi Mnara wa Mlinzi ulitoa mpangilio wa hatua za kuchukuliwa kabla mwanafunzi huyo hajajiunga na Mashahidi wa kwao katika huduma, akiwa mhubiri asiyebatizwa. Ni jambo la kiakili kabisa kutazamia kwamba apaswa kuwa na maarifa ya msingi juu ya Biblia, apaswa kuelewa viwango vya kiadili vya Mungu na kujipatanisha navyo, na apaswa kutamani kibinafsi ashiriki katika huduma ya peupe pamoja na Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo wazee wawili wa kundi waweza kuwa na zungumzo lenye msaada na la kutia moyo juu ya mambo hayo pamoja naye na Shahidi anayejifunza Biblia pamoja naye.a Jambo hili lapasa kufanywa kabla ya mwanafunzi wa Biblia kualikwa aandamane na mhubiri katika huduma ya shambani ili akapokee mazoezi ya kumsaidia afanye maendeleo.

Ni jambo lenye kueleweka kwamba wakati mwanafunzi astahilipo kwenda nje katika huduma ya shambani halafu afanye hivyo kwa mara ya kwanza, huenda akataka kuambatana na mhubiri yule mara chache ili ajifunze jinsi kazi ya kuhubiri hufanywa hasa. Mhudumu aliye pamoja naye aweza kuandaa mazoezi ya pole kwa pole, kama vile kumwomba asaidie kusoma maandiko kwa muda fulani, halafu baada ya wakati fulani amwache aongoze kutolea mwenye nyumba ushahidi. Hivyo, yeye aweza kutoa ripoti yake ya kwanza ya utumishi wa shambani wakati ashirikipo kikweli katika kutoa ushahidi shambani, Kuendelea kwake kuwa na ushiriki wenye kuongezeka katika kazi ile kwapatana na maneno ya Yesu: “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake.”—Luka 6:40.

[Maelezo ya Chini]

a Ili upate maelezo marefu, ona Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1988, ukurasa 17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki