Kutoa Ushahidi Biasharani—Mtindo wa Kijapani
AMRI ya Yesu Kristo ya kusukuma kazi ya ushahidi mpaka kwenye “sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” ni lazima ihusishe ndani maeneo ya biashara. (Matendo 1:8, NW) Katika Japani, kuwatolea ushahidi wa Ufalme watu ambao hufanya kazi katika mashirika yenye halaiki ya watu na ofisi za kampuni kubwa-kubwa huwa ni dai lenye kutaka jitihada kweli kweli. Wahubiri wa Ufalme katika kundi moja walipata ruhusa ya kufanya ushahidi wa magazeti katika jengo la ofisi moja ya jijini wakati wa pumziko la chakula cha mchana. Si kwamba wahubiri hao walipelekea Yehova sala tu ili awape moyo mkuu bali waliangalia sana pia mavazi na mwenendo wao na hata wakatayarisha kadi-lapeli (za kuchomekwa kifuani) zikionyesha majina yao na kuwatambulisha kuwa Mashahidi wa Yehova.
Shahidi angefikia mfanya kazi, akisema hivi: “Kunradhi, mimi nimepewa ruhusa ya kuongea na watu hapa. Je! ungeweza kunisikiliza wakati unapokula?” Mashahidi hao walilazimika kuonyesha uamuzi mzuri na kutumia maneno ‘yaliyokolezwa munyu.’ (Wakolosai 4:6) Katika ziara yao ya kwanza, waliangusha magazeti 39, lakini iliwachukua kufikia ziara nne ndipo wakaweza kumaliza jengo zima la ghorofa nane ambapo watu 1,500 hufanya kazi. Waliangusha jumla ya magazeti zaidi ya mia moja na wakaweza kuanza kawaida za kupelekea watu magazeti na kufanya ziara za kurudia.
Mmoja wa wahubiri hao alifanya ziara ya kurudia kwa meneja mmoja. Yeye aliposikia andiko likisomwa katika New World Translation, alisema hivi: “Biblia hii ni rahisi kueleweka. Ile niliyosoma hapo kwanza ilikuwa katika Kijapani cha kale na ilikuwa ngumu sana kusomeka.” Alipelekewa nakala ya New World Translation juma lililofuata.
Je! wewe waweza kufanya mengi zaidi katika eneo la kundi lako ili uhubiri zile habari njema kwa “watu wa namna zote,” kutia na wale walio katika sehemu za biashara?—Linganisha 1 Timotheo 2:4, NW.