Kutangaza Habari Njema-Kwa Kutoa Ushahidi kwa Ujasiri Katika Eneo la Biashara
1 Ujasiri unahitajiwa katika kutoa habari njema. Hiyo ni kweli hasa wakati tunapotoa ushahidi katika eneo la biashara. Baadhi ya wahubiri wanasita kufanya kazi katika eneo la biashara. Lakini huenda hiyo ikawa ni kwa sababu ya kukosa ujuzi. Au huenda ikawa ni eneo linalohitaji ‘kujipatia ujasiri.’—1 The. 2:2, NW.
2 Wahubiri wengi wamepata matokeo mazuri wakitoa ushahidi katika eneo la biashara. Mwangalizi mmoja wa mzunguko aliripoti kwamba katika asubuhi tisa za kufanyia kazi eneo la biashara, jumla ya vitabu 177 viliangushwa. Vingeweza kuangushwa, zaidi lakini ugavi uliwaishia. Wewe pia waweza kuwa na fanikio ukifanya jitihada kushiriki kazi ya eneo la biashara.
ENDELEZA MTAZAMO CHANYA
3 Mara nyingi kuwa mwenye fanikio hutegemea mtazamo wetu. Baadhi ya wahubiri huwa na mbetuko wa kufikiri kwamba kutoa ushahidi kwa waweka duka kungekuwa kugumu sana sana. Mhubiri mmoja aliyechukua oni hili alisema hivi: “Mimi nilitarajia kwamba itikio lingekuwa hasi. Hata hivyo, kwa mshangao wangu, itikio kwa ujumbe wa Ufalme lilikuwa kinyume kabisa. Wao walikuwa wapole kikweli na wenye urafiki kikweli na karibu sikuzote walikubali magazeti.” Ndiyo, wale wanaoshiriki kufanya kazi eneo la biashara huinena kuwa kazi yenye matunda ambayo huleta baraka.
4 Wazee, hasa mwangalizi wa utumishi wapasa kuchukua uongozi. Huenda ikanufaisha kutayarisha ramani za pekee za maeneo ya biashara yenye idadi kubwa sana ya majengo. Katika maeneo mengine, mahali pa biashara paweza kufanyiwa kazi pamoja na eneo la makazi. Hakikisheni kwamba hamsahau maduka, maofisi, viwanda, na kadhalika. Huenda wazee wakaona inafaa kuchagua wahubiri wanaostahili wafanyie kazi maeneo ya biashara yenye idadi kubwa sana ya majengo.
5 Wale wanaoshiriki kazi hii wapaswa kuwa wamevalia kwa nadhifu na wajitahidi kusema kifupi na kutaja mambo wazi wanapowaendea wanabiashara. Utoaji ambao urefu wao si zaidi ya dakika moja hivi ndio wenye kufaa zaidi. Kuchagua siku na nyakati ambazo si zenye shughuli sana ni jambo la umaana katika kupata matokeo bora zaidi wakati wa kufanyia kazi eneo la biashara. Wengine wamepata kwamba saa ya mapema Jumamosi asubuhi inafaa, hali wengine wamelipata kuwa jambo lenye faida kuzuru mapema katika siku za juma wakati wenyeji si wenye shughuli sana na maduka hayasongamani sana watu.
TUNAYOWEZA KUSEMA
6 Tunapofanyia kazi eneo la biashara, tunaweza kuonyesha magazeti, toleo la wakati huo la fasihi, au trakti. Ufikio wetu na toleo waweza kutofautiana kulingana na hali. Tunapotoa magazeti tungeweza kusema: “Kwa kuwa mara nyingi ni vigumu kuwapata wanabiashara nyumbani, tunafanya jitihada hii kuwafikia leo. Katika toleo la karibuni zaidi la Mnara wa Mlinzi, mna makala yenye kichwa [taja kichwa] ambacho kina habari inayokuhusu wewe binafsi. Sisi tunahisi kwamba utashangilia kusoma makala hiyo pamoja na zile nyingine. Tunatoa Mnara wa Mlinzi pamoja na Amkeni! kwa mchango wa ______ tu.”
7 Likiwa toleo badala mwezi huu tunaonyesha kichapo Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Unapotoa kichapo hiki katika eneo la biashara, waweza kusema: “Ukiwa mwanabiashara, wewe unajua kwamba jitihada nyingi yenye kutumia fikira inahitajiwa ili kufanikiwa. Je! nasibu isiyo na akili ingeweza kufanikiwa katika kutokeza uhai na ulimwengu wote mzima? Kitabu hiki kinatoa uthibitisho wa kisayansi kwamba Mungu aliumba uhai. Pia kinaonyesha kusudi la Mungu lenye fikira la kuumba mwanadamu. Wakati wa mwezi huu tunatoa kitabu hiki kiitwacho Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Kina mengi ya kusema kuhusu uhai na mambo ambayo wakati ujao unayo kwa ajili ya aina ya binadamu. Tunakiacha kwa mchango wa ______.”
8 Sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atabariki jitihada zetu za bidii-nyendelevu za kufikia watu tukiwa na hizi habari njema zenye kuokoa uhai. Kuna uhitaji wa kufanya mambo kwa ukamili katika utendaji wetu wa kutoa ushahidi. (Mdo. 20:24) Kwa kuwa mara nyingi ni vigumu kwetu kupata wanabiashara nyumbani, yatupasa tutumie kwa faida fursa tunene nao kwenye mahali pao pa kazi. Ingawa huenda ukawa mwito wenye ushindani kufanyia kazi eneo la biashara, twaweza kufanikio ‘tukijipatia ujasiri wa kunena habari njema za Mungu.’