Kulishinda Pigano Dhidi ya Mshuko wa Moyo
“JAMBO lenye kulemea hisia zaidi ya I yote ambayo nimepata kulazimika kushughulika nayo,” akaungama Lola, “lilikuwa hatia ya kuhisi bila tumaini kwa kuwa nikiwa mmoja wa watumishi wa Yehova, nilifikiri sipaswi kuhisi hivyo.” Mara nyingi welewevu mkosefu huu ulio wa kawaida ndio adui wa kwanza ambaye huwa ni lazima Mkristo aliyeshuka moyo amshinde. Lola aliongeza hivi: “Nilipokwisha kuacha kujipiga mwenyewe kiakilini kwa kuhisi jinsi hiyo na kukaza fikira juu ya kupona, niliweza kukabiliana vizuri zaidi na huo mshuko wa moyo.” Ndiyo, kule tu kuwa na mshuko wa moyo si sababu ya kukufanya ufikiri kwamba umeshindwa kufanyia Mungu yampasayo.
Kama ilivyotajwa katika makala iliyotangulia, kisababishi cha mshuko wa moyo huenda kikawa cha kimwili. Katika 1915, muda mrefu kabla utafiti wa hivi majuzi wenye kuhusianisha magonjwa ya kimwili pamoja na mshuko wa moyo, Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) ulitaarifu hivi: “Uzito huu wa roho, au kuhisi upweke na mshuko wa moyo, nyakati fulani huwa ni jambo la kiasili kwa ainabinadamu yote . . . [Huo] huongezewa kwa kadiri fulani na hali ya afya ya kimwili.” Hivyo, halimoyo ya kushuka hisia ikikaakaa, huenda kuchunguzwa na daktari kukasaidia. Ikiwa hali yenyewe ni ya kupita kiasi, huenda ikafaa mtu atibiwe mchafuko huo na stadi aliyesomea utaalamu wa mshuko wa moyo.a
Lakini hata iwapo kwamba kisababishi si cha kimwili, si jambo la kihalisi kutarajia kwamba mmoja wa watumishi wa Mungu hatahuzunika kamwe au kuvunjika moyo. Ebu fikiria tu jinsi Hana mwenye imani alivyopata kuwa ‘mchungu wa nafsi na kulia sana machozi.’ (1 Samweli 1:7, 10, NW) Nehemia pia ‘alilia machozi na kuomboleza kwa siku nyingi’ na kuwa mwenye “uzito wa moyo.” (Nehemia 1:4; 2:2, NW) Ayubu alidharau uhai wake na kuhisi kwamba Mungu alikuwa amemwacha. (Ayubu 10:1; 29:2, 4, 5) Mfalme Daudi alisema kwamba roho yake ilizimia ndani yake na kwamba moyo wake ulikufa ganzi. (Zaburi 143:4) Na mtume Paulo alinena juu ya kuwa na “hofu za ndani” na ‘kulazwa chini’ au ‘kutupwa chini’ kihisiamoyo.—2 Wakorintho 4:9; 7:5, 6, NW.
Ingawa wote hawa walikuwa watumishi wenye imani wa Mungu, misononeko mbalimbali, wasiwasi, au mitamausho michungu ilikuwa imewasababishia majonzi kwa muda. Hata hivyo, Mungu hakuwa amewaacha wala kuwaondolea roho takatifu yake. Halimoyo yao ya kushuka hisia haikusababishwa na kushindwa kutimiza wajibu wa kiroho. Wakati ambapo Daudi aliteseka, alisihi hivi katika sala: “Fanya nafsi ya mtumishi wako ishangilie.” Mungu alimfariji Daudi wakati wa hii ‘siku ya msononeko’ na katika wakati ufaao akamsaidia kushangilia. (Zaburi 86:1, 4, 7, NW) Vilevile Yehova atasaidia watumishi wake sasa.
Kwa maana kule tu kuwa na mshuko wa moyo si uthibitisho wa kushindwa kutimiza wajibu wa kiroho wala si udhaifu wa kiakili, Mkristo mwenye kukumbwa nao hapaswi kukaa kimya kwa sababu ya kuona haya. Bali, apaswa kuchukua moja ya hatua zilizo za maana zaidi katika kupigana na mchafuko huu. Hatua gani hiyo?
Mimina Hisia Zako
Apaswa kuongea na mtu fulani kuhusu jambo hilo. Mithali 12:25, NW, yataarifu hivi: “Ujalifu wenye wasiwasi katika moyo wa binadamu ndio utausababisha uiname chini, lakini neno lililo jema ndilo huufanya ushangilie.” Hakuna mwanadamu mwingine yeyote awezaye kujua uzito wa ujalifu wenye wasiwasi katika moyo wako usipofungulia hisia zako na kuongea jambo hilo. Kwa kueleza usiri wako kwa mtu mwenye hisiamwenzi ambaye aweza kusaidia, yaelekea utajifunza kwamba wengine wamekuwa na hisia na matatizo kama hayo. Pia, kunena waziwazi kuhusu hisia za ndani ni njia ya maponyo, kwa maana huondolea moyo uzito uliomo ili ueleze umizo lililomo badala ya kulibana humo ndani. Kwa hiyo, nafsi zilizoshuka moyo zapasa kueleza usiri wazo kwa mwenzi wa ndoa, mzazi, au rafiki mwenye hurumio na mwenye kustahili kiroho.—Wagalatia 6:1.
Sehemu ya tatizo la Marie (aliyetajwa katika makala iliyotangulia) ilikuwa kwamba yeye alizibana ndani yake zile hisiamoyo zenye kumsumbua zilizomwongoza kwenye mshuko wa moyo. “Muda wa miaka yote ile, nilikuwa nimekuwa mtu wa kujifanya hivyo tu,” yeye akasema. “Wengine hawangewazia kamwe kwamba nilitatizika sana kushughulika na hisia hizi za utostahiki.” Lakini Marie alifungulia hisia zake za ndani kwa kumweleza mzee mmoja katika kundi. Kupitia maswali ya ufahamu mzee huyo ‘aliteka’ kutoka moyoni mwake wasiwasi ambao Marie alibeba na akamsaidia kujielewa vizuri zaidi. (Mithali 20:5, NW) Maneno yake mema yaliyotoka kwenye Maandiko yalimpa tena uhakikishio. “Kwa mara ya kwanza, nikaanza kupata msaada kushughulika na hisia fulani zilizochangia mshuko wa moyo wangu,” Marie akaeleza.
Kwa hiyo kuongea na mzee mwenye uelewevu huenda kukaandaa “maji” yenye kumburudisha kiroho mtu ambaye “nafsi yake ni kama bara lililoishiwa kabisa.” (Isaya 32:1, 2; Zaburi 143:6, NW) Mshauri wa kiroho mwenye ufahamu huenda hata akakusaidia uone jinsi uwezavyo kuchukua hatua zenye kutumika ili kushughulika na ile ambayo huenda ukawa uliifikiria kuwa hali isiyo na tumaini. (Mithali 24:6) Lakini zaidi ya kueleza mtu mwingine usiri wako kuna mengi zaidi yenye kuhitajiwa.
Tambua Thamani Yako Halisi
Hisia za utostahiki ni kisababishi kikubwa cha mshuko wa moyo. Wakristo fulani wanajishushia staha, labda kwa sababu utoto wao haukuwa wenye furaha. Lakini hata ingawa kutumiwa vibaya kimwili, kihisiamoyo au kingono wakati uliopita kumeacha makovu ya hisiamoyo, hiyo haibadili ustahiki wa mtu. Hivyo, ni lazima ujitahidi kuwa na maoni yenye usawaziko juu ya thamani yako ya kweli ya kiutu. “Mimi ningesema kwa kila mmoja wa nyinyi asijikadiri mwenyewe kuwa juu ya thamani yake halisi, bali afanye ukadirio wa fahamu timamu kuhusu yeye mwenyewe,” mtume Paulo akahimiza. (Warumi 12:3, Charles B. Williams) Japo unalinda dhidi ya kujidai, unapaswa kujaribu kutopita kiasi upande ule mwingine. Wale walio na uhusiano pamoja na Mungu ni wenye thamani sana, wenye kutamanika kwake, kwa maana yeye huchagua wanadamu wawe “mali ya pekee” kwake. Lo, ni pendeleo la kutokeza’ kama nini!—Malaki 3:17; Hagai 2:17, NW.
Pia, ni heshima kama nini kuwa “wafanya kazi wenzi wa Mungu” kwa kujitia katika kazi ya Kikristo ya kufanya wanafunzi. (1 Wakorintho 3:9; Mathayo 28:19, 20) Wakristo wengi wenye mshuko wa moyo wameona kwamba kazi hii hujenga hisia ya ustahiki. “Hata baada ya kuwa Mkristo, mimi nilihisi sana nikiwa bila utoshelevu,” akakiri Marie. Na bado, yeye aliendelea tu katika kazi ya kuhubiri, halafu siku moja akakuta mwanamke kijana mwenye dhara la ubongoni ambaye alitaka kufunzwa Biblia. “Alihitaji mtu ambaye angemsubiri, kwa kuwa alikuwa mjifunzi wa polepole,” akasema Marie. “Kwa sababu yeye alichukua uangalifu wangu mwingi sana, nilijisahau mwenyewe na mambo yangu ya kukosa utoshelevu. Yeye alihitaji msaada wangu, nami nikang’amua kwamba ningeweza kumpa msaada huo kwa imara ya Yehova. Nilitiwa moyo kwa kadiri isiyoelezeka kwa kumwona akibatizwa. Hali yangu ya kujistahi iliongezeka, na ule mshuko mzito wa moyo ukatoweka daima.” Ni kweli kama nini kwamba “mwenye kutilia wengine maji kiuhuru atatiliwa maji yeye mwenyewe kiuhuru”!—Mithali 11:25.
Na bado, watu wengi wenye mshuko wa moyo huitikia kama mwanamke mmoja Mkristo mwenye mshuko mkali wa moyo, aliyekiri hivi: “Ingawa mimi hujibidiisha sana kusafisha na kupika na kuwa mkaribishaji-wageni, mimi hugeuka na kuanza kujichambua-chambua juu ya kila dosari ndogo.” Kujichambua huko kusiko na kiasi hufukua sana hali ya kujistahi. Kumbuka kwamba Mungu wetu ni mwenye uelewevu na ‘hafulizi kutafuta dosari wakati wote.’ (Zaburi 103:8-10, 14, NW) Ikiwa Yehova, aliye na hisi ya juu zaidi ya sisi kuhusu mambo yafaayo, hatuchokori-chokori kuhusu kila dosari ndogo na ana nia ya kuonyesha uhimilivu huo, je! sisi tusijitahidi kumwiga yeye katika mishughuliko yetu pamoja na sisi wenyewe?
Sisi sote tuna walakini na udhaifu mbali-mbali. Hata hivyo, tuna sifa zilizo imara pia. Mtume Paulo hakujitarajia upeo wa jitihada zake zote. “Hata ikiwa mimi si stadi katika uneni, hakika sivyo nilivyo katika maarifa,” yeye akataarifu. Paulo hakuhisi akiwa dhalili kwa sababu tu huenda ikawa hakuwapita wengine akiwa mnenaji wa peupe. (2 Wakorintho 11:6) Vilevile, wenye mshuko wa moyo wapaswa kukaza fikira juu ya vitu wanavyofanya vema.
“Hekima ina wenye kiasi,” au pamoja na wale ambao hutambua na kukubali mipaka yao. (Mithali 11:2, NW) Kila mmoja wetu ni nafsi isiyo na kifani yenye hali, zihi ya kimwili, na uwezo wenye kutofautiana. Utumikiapo Yehova kwa nafsi nzima, huku ukifanya uwezayo wewe, yeye aona raha. (Marko 12:30-33) Mungu si mmoja asiyeridhishwa kamwe na jitihada za waabudu wake waliojitoa. Leora, Mkristo aliyefanikiwa kupigana dhidi ya mshuko wa moyo, alisema hivi: “Mimi sifanyi vema kama kila mtu mwingineye katika mambo fulani, kama vile mahubiri ya huduma ya shambani. Lakini mimi ninajaribu. Kadiri nifanyalo ndilo mimi niwezalo.”
Kushughulika na Makoseo na Hali za Kutoelewa Vema
Ingawa hivyo, namna gani ukifanya koseo zito? Labda wewe wahisi kama Mfalme Daudi, ‘aliyetembea-tembea akiwa amehuzunika mchana kutwa’ kwa sababu ya makosa yake, au dhambi. Lakini hisia hii hii huenda ikawa ni kithibitisho cha kwamba wewe hujapita mipaka na hujatenda dhambi fulani isiyosameheka! (Zaburi 38:3-6, 8, NW) Hisia za hatia huenda zikaonyesha kwamba mtu ambaye ametenda dhambi ana moyo wa kufuata haki na ana dhamiri njema. Kwa hiyo hatia hiyo yaweza kushughulikiwaje? Basi, je! wewe umesali upate msamaha wa Mungu na ukachukua hatua za kurekebisha kosa lile? (2 Wakorintho 7:9-11) Ikiwa ndivyo, uwe na imani katika rehema ya yule Mmoja ambaye husamehe kwa njia pana, huku ukiwa na dhati ya kutorudia dhambi hiyo. (Isaya 55:7) Ikiwa umetiwa nidhamu, ‘usizimie usahihishwapo, kwa maana ambaye Yehova humpenda yeye humtia nidhamu.’ (Waebrania 12:5, 6, NW) Kusudi la sahihisho hilo ni kusaidia kumthibitisha upya kondoo mwenye kuacha njia. Haliondoi thamani ya kuwa yeye ni mtu.
Hata ikiwa moyo wetu wenyewe watulaani vikali, hatuhitaji kukata shauri kwamba Yehova ametulaani vikali. “Sisi tutaipa mioyo yetu uhakikishio mbele zake kwa habari ya lolote lile ambalo huenda mioyo yetu ikatulaani vikali, kwa sababu Mungu ni mkubwa kuliko mioyo yetu na ajua vitu vyote.” (1 Yohana 3:19, 20, NW) Yehova huona mengi zaidi ya dhambi na makoseo yetu tu. Yeye ajua kuhusu hali zenye kupunguza uzito wa dhambi, mwendo mzima wa maisha yetu, matilaba na madhumuni yetu. Ukubwa wa maarifa yake humwezesha kusikia kwa kusikitikia sala zetu zisizo za mchezo za kuomba msamaha, kama vile alivyosikia za Daudi.
Kutoelewana vema na wengine na kuhangaikia mno kupata idhini yao huchangia pia ukosefu wa kujistahi, labda hata hisia ya kuwa tumekataliwa. Kwa sababu ya kutokamilika, huenda Mkristo mwenzi akanena na wewe kwa njia yenye kuonekana ni sugu au hana fadhili. Na bado, kutoelewana vema kwaweza kuondolewa kwa kuambia mtu huyo jinsi wewe ulivyoathiriwa na elezo fulani. (Linganisha Mathayo 5:23, 24.) Pia, Sulemani aliusia hivi: “Usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.” Kwa nini? “Kwa I kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine.” (Mhubiri 7:21, 22) Usitarajie isivyo halisi ukamilifu wako mwenyewe au katika mahusiano yako na wanadamu wengine wasiokamilika. Uwe mwenye haraka ya kusamehe na kuchukuliana na wengine.—Wakolosai 3:13.
Zaidi ya hilo, thamani yako ya kweli haipimwi hasa na kama wewe wapendwa au hupendwi na wengine. Kristo ‘alionwa kuwa asiyefaa kitu,’ na ni thamani kidogo sana ‘aliyokadiriwa kulingana na maoni ya wengine.’ (Isaya 53:3; Zekaria 11:13, NW) Je! hili lilibadili ustahiki wake halisi au thamani ambayo Mungu alimkadiria? Sivyo, kwa maana hata kama sisi tungekuwa wakamilifu, kama Yesu, hatungeweza kufurahisha kila mtu.
Nguvu ya Kuvumilia
Nyakati fulani, huenda mshuko mzito wa moyo ukakaakaa tujapofanya jitihada za kuushinda. Huenda umivu hilo la kihisiamoyo hata likasababisha Wakristo fulani wahisi kama Yona: “Kufa kwangu ni bora kuliko kuwa kwangu hai.” (Yona 4:1-3, NW) Hata hivyo, huzuni kuu yake haikuwa ya kudumu. Aliiweza. Kwa hiyo mshuko wa moyo ukifanya maisha yako yaonekane kama yasiyohimilika, kumbuka kwamba ni kama ile dhiki ambayo Paulo alisema ilikuwa “ya muda.” (2 Wakorintho 4:8, 9, 16-18) Itafikia mwisho! Hakuna hali isiyo na tumaini. Yehova aahidi “kuhuisha moyo wa wale walio katika umivu.”—Isaya 57:15, Lamsa.
Usiache kamwe kusali, hata ikiwa yaonekana kama sala zako ni za bure. Daudi alisihi hivi: “Ee Mungu, ukisikie kilio changu . . I nikizimia moyo, uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.” (Zaburi 61:1, 2) Mungu atuongozaje tuwe na uhakika wa ndani ambao waonekana kuwa usioweza kufikiwa kwa imara yetu wenyewe? Eileen, ambaye ameng’ang’ana na mshuko wa moyo kwa miaka mingi, ajibu hivi: “Yehova hajaacha mimi nikate tamaa. Hiyo hunipa mimi tumaini la kwamba nikiendelea kujaribu, yeye atafuliza kusaidia. Kuujua ukweli wa Biblia kumenitunza hai kihalisi. Kupitia njia nyingi tofauti—sala, huduma, mikutano, vichapo, jamaa, na marafiki—Yehova ameniandalia imara nifulize kujaribu.”
Uone mchafuko kuwa mtihani wa imani yako. “Mwaweza kutegemea Mungu,” mtume Paulo atuhakikishia. “Yeye hataacha mtahiniwe kuliko mwezavyo kusimama. Lakini mtahiniwapo, Yeye atafanyiza pia njia ya kutokea nje ili kwamba nyinyi mweze kuhimili.” (1 Wakorintho 10:13, Beck) Ndiyo, Mungu atakupa wewe “nguvu ipitayo ile ya kawaida” ili ubebe mzigo wowote wa kihisiamoyo.—2 Wakorintho 4:7, NW.
Ulimwengu Mpya Usio na Mshuko wa Moyo
Mungu ameahidi kwamba karibuni, kwa njia ya Ufalme wake wa kimbingu, ataondoa katika dunia yetu hali zote zenye kushusha moyo. Neno lake lajulisha wazi hivi: “Mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya; na vitu vya hapo kwanza havitarudishwa akilini, wala havitainuka kuingia ndani ya moyo. Lakini chachaweni, nyinyi watu, na mjawe na shangwe milele katika kile ambacho mimi ninaumba.” (Isaya 65:17, 18, NW) Kwanza maneno hayo yalitimizwa kule nyuma katika 537 K.W.K., wakati ambapo taifa la kale la Israeli lilirudishwa kwenye bara la nyumbani. Wakati huo watu wake waliimba hivi: “Sisi tukawa kama wale waliokuwa wakiota ndoto. Wakati huo kinywa chetu kilikuja kujawa na kicheko, na ulimi wetu mlio wenye kujaa shangwe.” (Zaburi 126:1, 2, NW) Utimizo wa mwisho ambao karibuni utatukia katika ulimwengu mpya kuhusu unabii huu wenye kuchangamsha moyo utauzidi huo mwingine kwa utukufu ulioje!—2 Petro 3:13; Ufunuo 21:1-4.
Chini ya Ufalme wa Mungu (ambao ndizo “mbingu mpya”), jamii adilifu ya watu duniani (ambayo ndiyo “dunia mpya”) itarudishwa kwenye afya kamilifu ya kihisiamoyo, kimwili, na kiroho. Si kwamba hawa hawatakumbuka jambo lolote la wakati uliopita, lakini kwa sababu ya vitu vya kufurahisha watakavyokuwa navyo kuvifikiria na kuvishangilia wakati huo, hawatakuwa na sababu ya kuvirudisha akilini au kukaza fikira juu ya mambo yote ya kuhuzunisha yaliyowapata wakati uliopita. Weee, wazia ukiamka kila asubuhi ukiwa na akili safi kifuwele, ukiwa na hamu ya kuanza utendaji wa siku hiyo—bila kuzuiliwa tena na hali ya kushuka moyo!
Akiwa na usadikisho kamili kuhusu uhalisi wa tumaini hili, Lola (aliyetajwa pale mwanzoni), alisema hivi: “Msaada wangu mkubwa zaidi ulikuwa kukumbuka kwamba Ufalme wa Yehova utanyoosha tatizo hili. Mimi nilijua kwamba huo mshuko wa moyo haungedumu milele.” Ndiyo, wewe waweza kuwa na uhakika kwamba karibuni Mungu atafanya iwezekane kupata ushindi kamili juu ya mshuko wa moyo!
[Maelezo ya Chini]
a Ona “Kupambana na Mshuko Mkubwa wa Moyo—Matibabu ya Kitaalamu” katika toleo la Oktoba 22, 1981 la Amkeni! (Kiingereza).