Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/1 kur. 3-4
  • Waweza kupata Shangwe Katika Ulimwengu Wenye Kushusha Moyo!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waweza kupata Shangwe Katika Ulimwengu Wenye Kushusha Moyo!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mizizi ya Mshuko Mkali wa Moyo
  • Kulishinda Pigano Dhidi ya Mshuko wa Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kutambua Vyanzo
    Amkeni!—2001
  • Mtu Anahisije Anaposhuka Moyo?
    Amkeni!—2009
  • Ni Nini Kinachoweza Kuwasaidia Vijana Walioshuka Moyo?
    Amkeni!—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/1 kur. 3-4

Waweza kupata Shangwe Katika Ulimwengu Wenye Kushusha Moyo!

MARIE ana welekeo mwangavu, mchangamfu. Ni vigumu kuamini kwamba miaka michache tu iliyopita, mwanamke huyu wa miaka 32 alijieleza kuwa mfu ndani. Marie alikuwa amepatwa na moyo mzito. Yeye afafanua kwamba, “ilikuwa ni kama wingu kubwa lenye giza lililokuwa likiondoka kidato kidato.” Ndiyo, kwa furaha alipona akapata tena shangwe yake.

Kila mwaka mshuko mkali wa moyo hulemaza watu milioni mia moja! Mchafuko huu si hali ya muda tu ya kukosa furaha ambayo huwapata walio wengi kati yetu mara kwa mara. Mshuko mkali wa moyo wahusisha uzito wa moyo usioisha. Mtu mwenye mshuko wa moyo hupoteza upendezi katika maisha, hapati raha katika chochote, na huwa na hisia za utovu wa tumaini na utostahiki wa ujumla. Katika 1983 Tengenezo la Afya Ulimwenguni lilitaarifu hivi: “Kwa sasa hakuna shaka sana kwamba michafuko yenye kushusha moyo hutukia katika sehemu zote za ulimwengu.”

Wanafunzi wa Biblia walio waangalifu hawashangazwi na ripoti hii. Biblia yatambulisha wakati wetu kuwa “siku za mwisho,” zenye kudhihirishwa na “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1-5, NW) Miundo ya kijamii ambayo wakati uliopita ilitegemeza watu nyakati za tatizo kubwa la hisiamoyo imezorota. Katika makala “Enzi ya Majonzi?”, Dakt. Gerald Klerman asema kwamba badiliko hili limesababisha ongezeko la sasa la mshuko wa moyo. Afafanua hivi: “Mifumo tegemezi mitatu ya kijamii iliyo ya kawaida kabisa imekuwa ni jamaa, kanisa, na ujirani wa karibu. . . . Ni tabia ya wakati wa sasa kwamba yote mitatu ya mifumo tegemezi hiyo ya kijamii imo katika viwango mbalimbali vya mpanguko.”

Mvurugiko wa jamaa ya Marie ndio uliomwongoza kukata tamaa. “Mama yangu wa kambo alipoenda zake bila kusema neno, nilihisi kuwa nimesalitiwa na kuwa mpweke. Nilikuwa mwenye miaka 12, na kwa ghafula ulimwengu wangu ulionekana kuwa juuchini,” akumbuka Marie. Muda mfupi baada ya hapo akalazimika kuondoka nyumbani kwa sababu baba yake alimtongoza-tongoza kinyume cha adili, naye akiri hivi: “Nilihisi nikiwa mtu asiye wa kikawaida, na nikapoteza kabisa hali ya kujiamini.” Ndivyo likaanza poromoko lake la kuingia ndani ya mshuko mzito wa moyo.

Siku moja Marie alipokuwa ameshuka moyo vibaya mno, Mashahidi wa Yehova wawili walimtembelea nyumbani kwake. Mara hiyo akaonyesha upendezi mkubwa katika ujumbe wao wa Biblia wenye uchangamfu. “Hapo kwanza, mimi niliuona ubure mtupu tu wa maisha na mambo mengi sana ya kuchukiza, lakini sasa nikapata kusadiki kwamba ningeweza kuishi katika ulimwengu mpya ambamo Mungu angesahihisha mambo yote haya ya ukosefu wa haki. Kwa msaada wa Mungu ningeweza kustahili kupata baraka hiyo; hivyo, maisha yangu yakaanza kuwa na umaana halisi.” Alipokuwa akihudhuria mikutano ya Mashahidi, alipata upendo halisi na tegemezo la hisia-moyo. (Yohana 13:34, 35) Ushauri stadi wa wazee wa kundi ulimsaidia pia aanze kubadili fikira zake za mwelekeo hasi. (Yakobo 5:14) Mshuko wake wa moyo ulianza kupungua. Umati wa watu wengine ambao, kama Marie, wameshushwa moyo na hali za ulimwengu umeipata “shangwe ya Yehova” kwa kuja kwenye maarifa sahihi ya ukweli wa Biblia.—Nehemia 8:10; 1 Timotheo 2:4, NW.

Hata hivyo, je! mshuko wa moyo wa Marie uliondoka papo hapo? Je! tuchukulie kwamba Wakristo wamekingika kabisa wasiweze kupata mshuko wa moyo? Ili kujibu maswali haya, ni lazima tuwe na maoni yasiyo ya kijuujuu ya . mchafuko huu na visababishi vyayo vyenye kutatanika. Kujua mizizi halisi ya mshuko wa moyo kwaweza kukufanikisha zaidi katika kushughulika nao ndani yako mwenyewe au katika kusaidia mtu fulani mwenye kusumbuliwa nao.

Mizizi ya Mshuko Mkali wa Moyo

Katika visa fulani mshuko wa moyo una visababishi vya kimwili, kama ugonjwa, mapungukio ya vilisha mwili, na matatizo ya hormoni. Huenda pia ukawa ni tendomwitikio lenye kusababishwa na visumusumu fulani-fulani, vichafuzi, matibabu, na vitu fulani visivyopatana na mwili wa mtu.a Hata hivyo, Biblia yafunua kwamba “fikira za mtu zenye kumwondolea utulivu” huenda pia zikawa kisababishi.—Zaburi 94:19, NW.

Watu walio wengi ambao hushuka moyo, kama Marie, wamepatwa na maumizo kadhaa yasiyofurahisha au hali zenye mikazo. Wengi huhisi kama mtunga zaburi: “Nafsi yangu imekuwa na mabalaa ya kutosha . . . Yamenisonga yote kwa wakati mmoja. Wewe [Yehova] umeweka rafiki na mwandamani wakawa mbali sana na mimi; wajuani wangu ni mahali penye giza.” (Zaburi 88:3, 17, 18, NW) Kwa hiyo kama mtunga zaburi, wao huhisi wamelemewa na matatizo au hasara mbalimbali na huyaona maisha yao kwa ujumla yakiwa bila tumaini. Huenda wakahisi kana kwamba wako peke yao mahali penye giza na kwamba hata Mungu amewatupilia mbali.

Kwa nini wao hufikia kukata shauri hilo lenye kuvunja moyo, hivyo wakisitawisha roho iliyopigwa? Si kwa sababu ya matatizo yao ya nje tu; pia ni kwa sababu ya hisia zenye maumivu au za kujishuku-shuku. Wao huhisi hawana utoshelevu wa kushughulika na tatizo au hasara. “Kwa sababu ya umivu la moyo kuna roho iliyopigwa,” yafafanua Mithali 15:13, NW. Umivu hilo la moyo lingehusisha kuhisi kwamba mtu ni mshindwa au kwamba wengine wamfikiria hivyo. Hata Mkristo wa karne ya kwanza Epafrodito, alipokwisha kupata nafuu ya ugonjwa mzito wakati wa utume mmoja uliopangwa na kundi la nyumbani kwao, ‘alishuka moyo kwa sababu kundi hilo lilisikia alikuwa amekuwa mgonjwa.’—Wafilipi 2:25-30, NW.

Kwa kuwa ‘roho iliyopigwa hukausha mifupa,’ au hufukua uwepo halisi wa mtu, mara nyingi mzizi wa mshuko mzito wa moyo huwa ni hisia za kujishushia staha. (Mithali 17:22 Pia umivu la moyo lingeweza kuletwa na hangaiko kubwa mno kuhusu jinsi wengine watuonavyo, kutaka ukamilifu, kuwa na kasirani isiyotatuliwa, udhia, magongano yasiyotatuliwa pamoja na wengine, au hatia (iliyo halisi au ya kutiliwa chumvi).

Kwa hiyo visababishi vya mshuko mzito wa moyo ni vingi. Hata hivyo, Marie alipata shangwe halisi baada ya kuwa Mkristo. “Ndipo nikawa na tumaini,” yeye akasema. Lakini kwa muda fulani bado alilazimika kuvumilia mshuko wa moyo. Watu wa jinsi hiyo waweza kuushindaje hatimaye?

[Maelezo ya Chini]

a Ona “Mshuko wa Moyo: Je! Yote Ni Katika Kichwa cha Mtu?” katika toleo la Oktoba 8, 1988 la Amkeni!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki