Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Endeleeni ‘Kumsikiliza’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Ufalme wa Mungu—Je, Unapata Maana Yao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Njia Iliyo Pana na Rahisi”
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Je! yatupasa tukate shauri kutokana na Mathayo 7:13, 14 na Luka 13:24 kwamba hata katika ufufuo, wanadamu walio wengi watakataa ibada ya kweli?

Sivyo, mistari hii haiungi mkono kukata shauri jinsi hiyo. Bali, yahusu hasa kupata uhai katika Ufalme wa kimbingu.

Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 7:13, 14 ni sehemu ya Mahubiri ya Mlimani. Yeye alisema: “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.”

Mengi ya yale ambayo Yesu alisema katika pindi hii yalihusu hasa Ufalme wa kimbingu. Kwa kielelezo, yeye alianza kwa maneno haya: “Wenye furaha ni wale wenye kujua uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbingu ni wao.” Alisema kwamba wenye kutakata katika moyo ‘wangeona Mungu’ na kwamba “ufalme wa mbingu” ni wa wale “wenye kunyanyaswa kwa ajili ya uadilifu.” (Mathayo 5:3, 8, 10, NW) Baadaye katika hotuba iyo hiyo, Yesu alinena juu ya barabara pana inayoongoza kuingia katika uharibifu na barabara iliyosonga inayoongoza kwenye uhai. Kwa sehemu, aliongezea hivi: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”—Mathayo 7:13, 14, 21.

Maana ya Luka 13:24 yafanana na hiyo, kama ionyeshwavyo na habari zenye kuzunguka. Yesu alitoa vielezi viwili juu ya “ufalme wa Mungu.” Baadaye, aliulizwa hivi: “Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache?” Yesu alijibu: “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.” “Wengi” yarejezea watu walioomba sana waruhusiwe kuingia baada ya mlango kufungwa na kutiwa kufuli. Hawa walikuwa “wafanyaji wa udhalimu” ambao hawakustahili kuwa na ‘Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu.’ “Wengi” hao walikuwa wamefikiri wangekuwa wa kwanza “katika ufalme wa Mungu,” lakini kwa kweli wangekuwa ndio wa mwisho, kwa wazi ikimaanisha kwamba hawangekuwa humo hata kidogo.—Luka 13:18-30.

Habari zenye kuzunguka zaonyesha kwamba Yesu alikuwa akishughulikia kuingia ndani ya Ufalme wa kimbingu wa Mungu. Viongozi wa Kiyahudi huko nyuma walikuwa wameonea shangwe cheo chenye pendeleo, wakiwa na fursa ya kuwa na Neno la Mungu. Walihisi kwamba walikuwa matajiri kiroho na waadilifu machoni pa Mungu, tofauti na watu wa kawaida, ambao wao waliwadharau. (Yohana 9:24-34) Hata hivyo, Yesu alisema kwamba wakusanya kodi na makahaba waliokubali ujumbe wake na kutubu wangeweza kuwa na kibali cha Mungu.—Linganisha Mathayo 21:23-32; Luka 16:14-31.

Watu wa kawaida waliokuja kuwa wanafunzi wa Yesu walikuwa katika mstari wa kukubaliwa kuwa wana wa kiroho wakati wito wa kimbingu ulipofunguka wazi kwenye Pentekoste 33 W.K. (Waebrania 10:19, 20) Ingawa umati wa watu wengi sana ulisikia Yesu, wale waliomkubali na baadaye wakapata tumaini la kimbingu walikuwa wachache. Lakini kundi dogo la wanadamu waliozaliwa kwa roho wenye kupokea thawabu hiyo wangeweza kulinganishwa na Yakobo akiegemea mezani akiwa mbinguni pamoja na Yehova (Abrahamu Mkubwa Zaidi) na Mwana wake (aliyefananishwa na Isaka). Kwa uhakika hilo ni jambo lililostahiki kujitahidi kisulubu, lakini walio wengi wa wale waliosikia Yesu hawakufanya hivyo.

Kwa hiyo, twaweza kuona kutokana na habari zenye kuzunguka vituko vyote viwili kwamba maelezo ya Yesu (juu ya kuwa kwa wachache katika barabara iliyosonga inayoongoza kwenye uhai na kuokolewa kwao) yalihusu hasa kuwa na kibali cha Mungu wakati huo ambapo Yeye alikuwa akitoa tumaini la uhai wa kimbingu. Waliosikia ujumbe wa ukweli na kujifunza yaliyotakwa na kuitikia wakathibitika kuwa waaminifu ni wachache kwa ulinganisho.— Mathayo 22:14; 24:13; Yohana 6:60-66.

Inapendeza kwamba hata leo, wakati ambapo Biblia nzima yapatikana na kuna utimizo mwingi sana wa unabii wa kimungu juu ya siku za mwisho, kwa ulinganisho ni wachache huitikia ujumbe wa Kikristo na kuvumilia katika kutumikia Yehova. Hii yapatana na kielezi cha Yesu juu ya udongo tofauti-tofauti. Alisema kwamba watu fulani wangesikia “neno la ufalme,” lakini Shetani angenyakua kilichopandwa. Wengine wangelikubali neno kwa shangwe lakini baada ya muda wangeshindwa kwa sababu ya dhiki au mnyanyaso. Hata hivyo wengine wangethibitika kuwa wasiozaa matunda kwa sababu ya “wasiwasi wa mfumo huu wa mambo na nguvu yenye udanganyifu ya mali.”—Mathayo 13:18-23, NW.

Twaweza kuwa na uhakika kwamba mambo yatakuwa tofauti sana wakati mamilioni kwa mamilioni watakapofufuliwa wakati wa Siku ya Hukumu. Wakati huo Shetani hatakuwa huru kunyakua mbegu za ukweli zilizopandwa katika mioyo yao. Hawatalazimika kukabiliana na mnyanyaso au wasiwasi wa mfumo mwovu uliopo. Watafundishwa wakiwa katika mazingira ya uadilifu, wakiwa wamezungukwa na kazi ya kimuujiza ya Mungu, kutia na ufufuo wa wafu na kuponywa kwa mataifa. Ni kweli, watu fulani hawataitikia hata wakati huo. (Linganisha Yohana 11:45-53.) Lakini kuna sababu njema ya kufikiri kwamba walio wengi wataelewa maana ya lile neno, waliitikie, na kuokolewa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki