Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 4/1 kur. 11-14
  • Neno la Mungu Ni Ukweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Neno la Mungu Ni Ukweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo
  • Hekima Bora ya Biblia
  • Shauri la Biblia—Lenye Hekima Isiyo na Kifani
  • Kwa Faida Yetu ya Muda Mrefu
  • Matatizo Magumu Katika Maisha
  • Chanzo cha Hali ya Juu Zaidi cha Hekima
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Biblia na Wewe
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Usidanganywe na “Hekima ya Ulimwengu Huu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Hekima ya Kweli Inapaza Sauti Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 4/1 kur. 11-14

Neno la Mungu Ni Ukweli

“Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.”—Yohana 17:17

1. Mtunga zaburi Mwebrania aliionaje Biblia, lakini wengi leo huionaje?

“NENO lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.” (Zaburi 119:105) Ndivyo alivyosema mtunga zaburi Mwebrania. Ni wachache tu leo wanaostahi hivyo Neno la Mungu. Katika karne hii ya 20, Neno la Mungu liko kwa namna ya maandishi likiwa Biblia Takatifu. Limetafsiriwa katika lugha nyingi zaidi na kugawanywa kotekote kuliko kitabu kingine chochote katika historia. Hata hivyo, walio wengi hukataa kulipokea kuwa taa kwa nyayo zao. Hata wale ambao hudai kuwa Wakristo hupendelea sana-sana kufuata mawazo yao wenyewe badala ya kuacha Biblia inurishe njia yao.—2 Timotheo 3:5.

2, 3. Mashahidi wa Yehova huionaje Biblia, na hiyo imewaletea manufaa gani?

2 Kwa utofauti mkubwa, sisi ambao ni Mashahidi wa Yehova twaafikiana na mtunga zaburi. Kwetu sisi, Biblia ni mwongozo uliotolewa na Mungu. Twajua kwamba “kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.” (2 Timotheo 3:16) Tofauti na watu wengi leo, sisi hatutaki kufanyafanya majaribio tuone ni maadili na mwenendo gani ufaao. Twajua mambo yafaayo kwa sababu Biblia yatuambia.

3 Hiyo imetuletea manufaa zilizo kubwa. Tumekuja kumjua Yehova, na tumejifunza makusudi yake matukufu kwa dunia na ainabinadamu, kwa hiyo tuna uhakika kwamba wakati ujao ulio mwangavu wawezekana kwa sisi na jamaa zetu. Sisi twaafikiana kwa moyo mzima na mtunga zaburi aliyesema hivi: “Sheria yako naipenda mno ajabu, ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa. Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, kwa maana ninayo sikuzote.”—Zaburi 119:97, 98.

Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo

4. Kutambua Biblia kuwa Neno la Mungu huweka wajibu gani juu yetu?

4 Kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuafikiana na maneno ya Yesu yaliyoelekezwa kwa Baba yake: “Neno lako ndiyo kweli.” (Yohana 17:17) Lakini kutambua uhakika huu huweka wajibu juu yetu. Ni lazima tusaidie wengine wang’amue kwamba Neno la Mungu ndio ukweli. Kwa njia hii wao pia wataweza kuonea shangwe baraka ambazo sisi hupata. Twaweza kuwasaidiaje kwa njia hiyo? Kwanza, ni lazima tufanye kila jitihada kutumia kanuni za Biblia katika maisha zetu za kila siku. Kwa njia hiyo, watu wenye mioyo ifaayo wataona kwamba kwa kweli njia ya Biblia ndiyo bora zaidi.

5. Petro alitoa shauri gani juu ya kutoa ushahidi kwa mwenendo wetu?

5 Hii ilikuwa ndiyo maana kuu ya shauri la mtume Petro kwa wanawake Wakristo ambao waume zao walikuwa wasioamini. Yeye alisema kwao hivi: “Nanyi wake, jiwekeni chini ya mamlaka ya waume zenu, ili kama wako waume wowote wasioamini neno la Mungu, wapate kuamini kwa kuuona mwenendo wenu. Haitakuwa lazima kwenu kusema neno.” (1 Petro 3:1, HNWW) Hiyo pia ilikuwa ndiyo kanuni yenye kuongoza shauri lake kwa Wakristo wote—wanaume, wanawake, na watoto—aliposema hivi: “Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.”—1 Petro 2:12; 3:16.

Hekima Bora ya Biblia

6. Petro hutusaidiaje tuone kwamba twapaswa kusaidia wengine kuithamini Biblia?

6 Zaidi ya hilo, Wakristo waweza kusaidia wengine wathamini Biblia wakifanya kama vile Petro ashauri: “Mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu. Mwe tayari sikuzote kumjibu [kutoa utetezi mbele ya, NW] kila mtu awaulizaye habari [anayedai nyinyi sababu ya, NW] za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu [staha ya kina kirefu, NW].” (1 Petro 3:15) Wahudumu Wakristo wapaswa waweze kutetea Biblia na kufafanulia wengine kwamba ni Neno la Mungu. Wao waweza kufanyaje hivyo?

7. Ni uhakika gani juu ya Biblia huonyesha kwamba ni lazima iwe ni Neno la Mungu?

7 Njia moja ya kusababu mambo kwa uvutio yapatikana katika kitabu cha Mithali, Humo twasoma: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima . . . , [utapata] kumjua Mungu. Kwa kuwa Bwana [Yehova, NW] huwapa watu hekima; kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.” (Mithali 2:1-6) Hekima ya Mungu mwenyewe hupatikana katika kurasa za Biblia. Wakati mtu mwenye moyo mweupe aonapo hekima hiyo ya kina kirefu, hawezi kushindwa kung’amua kwamba Biblia si neno la mwanadamu tu.

8, 9. Shauri la Biblia juu ya kufuliza kuwa na maoni yaliyosawazika juu ya kujipatia utajiri limeonyeshwaje kuwa sahihi?

8 Fikiria vielelezo vichache. Leo, kwa kawaida mafanikio katika maisha hupimwa kifedha. Kwa kadiri mapato ya mtu yazidivyo, ndivyo yeye hufikiriwa kuwa mwenye mafanikio zaidi. Hata hivyo, Biblia huonya dhidi ya kutia mkazo mwingi mno juu ya vitu vya kimwili. Mtume Paulo aliandika hivi: “Hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”—1 Timotheo 6:9, 10; linganisha Mathayo 6:24.

9 Yaliyoonwa yameonyesha kwamba onyo hili lafaa sana. Mwanasaikolojia wa kitiba asema hivi: “Kuwa namba 1 na tajiri hakukufanyi uhisi umetimiza lolote, umetosheka, umestahiwa au kupendwa kikweli.” Ndiyo, wale ambao hutumia nishati zao zote wakifuatia utajiri huja mwishowe kuhisi uchungu na mvurugiko wa fikira. Ingawa Maandiko hukiri kwamba pesa ni zenye thamani, huelekeza kwenye jambo lililo la maana zaidi: “Hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilivyo ulinzi, na ubora wa maarifa ni kwamba hekima humhifadhi yeye aliye nayo.”—Mhubiri 7:12.

10. Kwa nini twapaswa kutii shauri la Biblia kuangalia mashirika yetu?

10 Biblia ina miongozo mingi ya jinsi hiyo. Mwingine ni huu: “Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; bali rafiki wa wapumbavu ataumia.” (Mithali 13:20) Yaliyoonwa yamethibitisha hilo pia kuwa ukweli. Mkazo wa marika umeongoza vijana wengi katika ulevi, utumizi mbaya wa dawa za kulevya, na ukosefu wa adili. Watu wowote ambao huchangamana na wenye kutumia usemi mbaya hujikuta hatimaye wakitumia uneni kama huo wa kunyarafisha. Wengi huiba kutoka kwa waajiri wao eti kwa sababu ‘kila mtu afanya hivyo.’ Kwa kweli, kama vile Biblia isemavyo: “Mashirika mabaya yanaharibu mazoea yenye mafaa.”—1 Wakorintho 15:33, NW.

11. Uchunguzi wa kisaikolojia ulionyeshaje hekima ya kufuata Kanuni ya Kidhahabu?

11 Moja la mashauri yaliyo maarufu zaidi katika Biblia ni ile yenye kuitwa Kanuni ya Kidhahabu: “Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo.” (Mathayo 7:12) Kama ainabinadamu ingefuata kanuni hiyo, kwa wazi ulimwengu ungekuwa mahali bora. Lakini hata ikiwa wanadamu kwa ujumla hawafuati kanuni hiyo, ni afadhali wewe mtu mmoja ufanye hivyo. Kwa nini? Kwa sababu sisi tulifanyizwa ili tujali wengine na kuwahangaikia. (Matendo 20:35) Uchunguzi wa kisaikolojia ulioendeshwa katika United States ili kuona watu huitikiaje wasaidiapo wengine ulifikia umalizio huu: “Basi, yaonekana kwamba kujali wengine ni sehemu ya hali ya kibinadamu kama ilivyo kuhusu kujijali sisi wenyewe.”—Mathayo 22:39.

Shauri la Biblia—Lenye Hekima Isiyo na Kifani

12. Ni jambo gani moja linaloifanya Biblia kuwa isiyo na kifani?

12 Leo, bila shaka, kuna vyanzo vingi vya mashauri nje ya Biblia. Magazeti huwa na safu za ushauri, na maduka ya vitabu yamejaa vitabu vyenye maagizo ya kujisaidia binafsi. Tena, kuna wanasaikolojia, washauri waliosomea kazi hiyo, na wengine ambao hutoa ushauri katika nyanja tofauti. Lakini Biblia haina kifani katika angalau pande tatu. Kwanza, shauri layo ni lenye manufaa sikuzote. Haliwi kamwe nadharia tu, na halitudhuru kamwe. Mtu yeyote ambaye hufuata shauri la Biblia atalazimika kuafikiana na mtunga zaburi aliposema kwa Mungu hivi katika sala: “Shuhuda [makumbusha yako, NW] zako ni amini sana.”—Zaburi 93:5.

13. Ni nini kinachoonyesha Biblia kuwa yenye kupita sana vyanzo vya kibinadamu vya hekima?

13 Pili, Biblia imeshinda mtihani wa wakati. (1 Petro 1:25; Isaya 40:8) Shauri kutoka vyanzo vya kibinadamu ni lenye kubadilika vibaya sana, na lenye kufuatwa kwa wingi mwaka mmoja huchambuliwa mara nyingi mwaka ufuatao. Hata hivyo, ingawa Biblia ilimalizwa karibu miaka 2,000 iliyopita, ingali ndiyo yenye shauri la hekima zaidi lipatikanalo, na maneno yayo hutumika ulimwenguni pote. Hutumika kwa matokeo yale yale hata kama twaishi katika Afrika, katika Esia, katika Amerika Kusini au Kaskazini, katika Ulaya, au katika visiwa vya bahari.

14. Ni katika njia gani shauri la Neno la Mungu lapita mengine yote?

14 Mwisho, mweneo mkubwa wa shauri la Biblia haulinganiki. Mithali ya Biblia husema hivi: “Yehova mwenyewe hutoa hekima,” na hata iwe twakabili tatizo au uamuzi gani, katika Biblia mna hekima ambayo hutusaidia kulitatua. (Mithali 2:6) Watoto, matineja, wazazi, wazee-wazee, waajiriwa, waajiri, watu katika mamlaka, wote hupata kwamba hekima iliyo katika Biblia huwahusu. (Mithali 4:11) Hata tukabilipo hali ambazo hazikujulikana wakati wa Yesu na mitume wake, Biblia hutupa shauri lenye matokeo mazuri. Kwa kielelezo, huko nyuma katika karne ya kwanza, uvutaji tumbako haukujulikana katika Mashariki ya Kati. Leo, umeenea kotekote. Hata hivyo, mtu yeyote mwenye kuangalia shauri la Biblia la kuepuka ‘kuletwa chini ya mamlaka [au kudhibitiwa] na kitu chochote’ na kukaa akiwa safi na “uchafu wote wa mwili na roho” ataepuka zoea hili, ambalo ni lenye uzoelevu mbaya na haribifu kwa afya.—1 Wakorintho 6:12; 2 Wakorintho 7:1.

Kwa Faida Yetu ya Muda Mrefu

15. Kwa nini wengi hudai kwamba Biblia ni ya kizamani?

15 Ni kweli, wengi husema kwamba Biblia ni ya kizamani na isiyohusiana na hali za karne hii ya 20. Hata hivyo, yaelekea sababu ni kwamba Biblia haisemi yale watakayo kusikia. Kufuata shauri la Kimaandiko hutuletea manufaa ya muda mrefu, lakini kufanya hivyo huwa mara nyingi kwahitaji saburi, nidhamu, na kujikana—tabia ambazo hazipendwi na wengi katika ulimwengu ambao hututia moyo tutafute kutosheleza tamaa zetu papo hapo.—Mithali 1:1-3.

16, 17. Biblia huweka viwango gani vya juu vya adili ya ngono, navyo vimepuuzwaje katika nyakati za ki-siku-hizi?

16 Kielelezo ni lile jambo la adili katika ngono. Viwango vya Kimaandiko vyadai kufuatwa sana. Mahali pekee pa uhusiano wa karibu sana kingono ni ndani ya ndoa, na uhusiano wote huo wa karibu sana kingono nje ya ndoa hukatazwa. Twasoma hivi: “Waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti.” (1 Wakorintho 6:9, 10) Tena, Biblia huwataka Wakristo wawe mume na mke mmoja. (1 Timotheo 3:2) Na ingawa kuna visa vya kupita kiasi ambapo talaka au mtengano ungeweza kuruhusiwa, Biblia husema kwamba kwa ujumla kifungo cha ndoa ni cha maisha. Yesu mwenyewe alisema: “Yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja . . . Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.”—Mathayo 19:4-6, 9; 1 Wakorintho 7:12-16.

17 Leo, viwango hivi hupuuzwa kotekote, Mazoea legelege ya ngono huvumiliwa. Mahusiano ya kingono kati ya matineja wanaofanya matembezi ya wavulana na wasichana huonwa kuwa jambo la kawaida. Kuishi pamoja bila manufaa ya ndoa hukubaliwa. Miongoni mwa wenzi waliofunga ndoa, si jambo lisilo la kawaida ngono isiyo halali kufanywa na mwenzi mmojapo. Na talaka ni yenye kuenea kote sana katika ulimwengu wa ki-siku-hizi. Hata hivyo, viwango hivyo vilegevu havikuleta furaha. Matokeo mabaya yamethibitisha kwamba kumbe Biblia ilikuwa sahihi kwa kusisitizia kufuata sana viwango vya kiadili.

18, 19. Ni nini kimetokana na upuuzaji ulioenea kotekote wa viwango vya Yehova vya adili?

18 Ladies’ Home Journal lilisema hivi; “Mkazo uliotiwa juu ya ngono ambao ulikuwa alama ya miaka ya sitini na ya sabini haukuleta furaha ya kibinadamu isiyo na kikomo bali sikitiko zito la kibinadamu.” “Sikitiko zito la kibinadamu” linalorejezewa hapa latia ndani watoto wanaosumbuliwa sana moyoni na talaka za wazazi wao na watu wazima wanaotaabishwa sana na maumivu ya hisia-moyo. Latia ndani pia ongezeko katika jamaa za mzazi mmoja na mweneo mkubwa wa wasichana waseja ambao hupata watoto hali wao wenyewe wangali watoto. Tena, latia ndani magonjwa yanayopitishwa kingono yenye kuenea pote, kama vile malengelenge ya viungo vya uzazi, kisonono, kaswende, klamidia, na UKIMWI.

19 Kwa sababu ya yote haya, profesa mmoja wa sosholojia alisema hivi: “Pengine sisi ni watu wazima vya kutosha kufikiria kama haingetufaidi sisi sote kukufanya kujiepusha na ngono za kabla ya ndoa kuwe mwongozo unaotimiza zaidi mahitaji ya raia zetu na haki yao ya kupata uhuru: uhuru na magonjwa, uhuru na mimba zisizotakwa.” Biblia husema hivi kwa usahihi: “Heri [mwenye furaha ni, NW] aliyemfanya Bwana [Yehova NW] kuwa tumaini lake, wala hakuwaelekea wenye kiburi, wala hao wanaogeukia uongo.” (Zaburi 40:4) Wale ambao hutumaini hekima ya Biblia hawadanganywi na uwongo wa wale wanaokaidi Biblia na kusema kwamba sheria legevu zaidi za kiadili huleta furaha. Hata kama ni vyenye kusisitizia kufuatwa sana, viwango vyenye hekima vya Biblia huleta manufaa bora kabisa.

Matatizo Magumu Katika Maisha

20. Ni kanuni gani za Biblia ambazo zimethibitika kuwa zenye msaada kwa wale ambao hulazimika kukabiliana na umaskini katika maisha zao?

20 Hekima ya Biblia hutusaidia pia tushughulikie matatizo magumu ambayo sisi hukabili katika maisha. Kwa kielelezo, katika mabara mengi, kuna Wakristo wanaoishi katika umaskini mbaya sana, wa kupindukia. Hata hivyo wao hukabiliana na umaskini wao na bado hupata furaha. Jinsi gani? Kwa kufuata Neno la Mungu lililovuviwa. Wao huchukua kwa uzito maneno yanayofariji ya Zaburi 55:22: “Umtwike Bwana [Yehova, NW] mzigo wako naye atakutegemeza.” Wao humwegemea Mungu awape imara ya kuvumilia. Halafu hutumia kanuni za Biblia na kuepuka mazoea yenye kudhuru, ya utapanyaji mali, kama kuvuta sigareti na kulewa. Ni wenye bidii ya kufanya kazi, kama vile Biblia inavyopendekeza, na hivyo mara nyingi hupata kwamba wanaweza kulisha jamaa zao wakati watu wavivu au wale wenye kujiacha wakate tamaa wanaposhindwa. (Mithali 6:6-11; 10:26) Zaidi ya hilo, wao hutii onyo hili la Biblia: “Usiwe mwenye kuhasidi wale wanaofanya yasiyo ya uadilifu.” (Zaburi 37:1, NW) Hawaoni kwamba njia tu ni kucheza kamari wala vitendo vya uhalifu, kama vile kuuza dawa za kulevya. Huenda mambo haya yakatoa “utatuzi” wa haraka kwa matatizo yao, lakini matunda ya muda mrefu ni machungu.

21, 22. (a) Mwanamke mmoja Mkristo alichotaje msaada na faraja kutokana na Biblia? (b) Ni uhakika gani zaidi juu ya unaotusaidia sisi tung’amue kwamba hiyo ni Neno la Mungu?

21 Je! kufuata Biblia huwasaidia kweli kweli wale walio maskini sana? Ndiyo, kama vile mengi sana yaliyoonwa huthibitisha. Mjane mmoja Mkristo katika Esia aandika hivi: “Ingawa mimi naishi nikikaribia sana kuwa maskini, sina fundo wala uchungu. Kweli za Biblia hujaza mimi maoni ya kutazamia mazuri.” Yeye aripoti kwamba ahadi ya Yesu inayostahili kuangaliwa imetimizwa katika kisa chake. Yesu alisema: “Utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.” (Mathayo 6:33) Mjane huyo ashuhudia kwamba kwa kuweka utumishi wake wa Mungu kwanza katika maisha yake, sikuzote yeye hupokea mahitaji ya kimwili ya maisha. Na utumishi wake wa Kikristo humpa adhama na mradi katika maisha ambao hufanya umaskini wake uvumilike.

22 Kwa kweli, kina kirefu cha hekima ya Biblia huonyesha kikweli kwamba hiyo ni Neno la Mungu. Hakuna kitabu kilichotokezwa na wanadamu tu ambacho kingeweza kuzungumzia pande nyingi sana zilizo tofauti za maisha na kiwe na ufahamu wenye kina sana na sahihi kwa upatani sana jinsi hiyo. Lakini kuna uhakika mwingine juu ya Biblia ambao huonyesha ina asili ya kimungu. Ina nguvu ya kubadili watu wawe bora. Tutazungumzia hilo katika makala ifuatayo.

Je! Waweza Kufafanua?

◻Mashahidi wa Yehova hubarikiwaje kwa kuipokea Biblia kuwa Neno la Mungu?

◻ Sisi tukiwa waamini katika Neno la Mungu, tuna wajibu gani, na mwenendo wetu waweza kutusaidiaje tutimize wajibu huu?

◻ Ni nini hufanya shauri la Biblia lenye hekima lipite ushauri wa kibinadamu tu?

◻ Ni nini baadhi ya vielelezo vinavyoonyesha kina cha hekima ya Biblia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki