Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 8/1 kur. 23-25
  • Waroma Wapata Habari Bora Kabisa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waroma Wapata Habari Bora Kabisa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • PAULO NA WAROMA
  • IMANI NA SHERIA
  • UADILIFU
  • KUJIBU VIPINGAMIZI
  • UADILIFU NA WAYAHUDI WA KIMNOFU
  • KANUNI ZA
  • KWA AJILI YA WAPAKWA-MAFUTA
  • Kinachokaziwa Ni Imani Yako—Katika Warumi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kitabu Cha Biblia Namb 45—Warumi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Wanatangazwa Kuwa Waadilifu “Ili Wapate Uzima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Waroma 5:8—“Kristo Alikufa kwa Ajili Yetu, Tulipokuwa Tungali Wenye Dhambi”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 8/1 kur. 23-25

Waroma Wapata Habari Bora Kabisa

BINADAMU mwenye dhambi aweza kuwaje mwadilifu machoni pa Mungu na hivyo apate uhai wa milele? Swali hilo lilisababisha mazungumzo motomoto katika karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu. Je! wewe walijua jibu? Uwe walijua au hulijui, una deni lako mwenyewe la kusoma mazungumzo stadi ya mtume Paulo juu ya tatizo hilo katika kitabu cha Biblia cha Waroma. Kufanya hivyo kutakusaidia uelewe uhusiano muhimu uliopo kati ya imani, kazi, uadilifu, na uhai.

PAULO NA WAROMA

Kitabu cha Waroma ni barua iliyoandikwa na Paulo karibu 56 W.K. kwa Wakristo katika Roma. Kwa nini yeye aliandika barua hiyo? Ingawa katika 56 W.K. Paulo hakuwa amezuru Roma, yaonekana wazi alijua Wakristo wengi huko, kwa kuwa katika barua yake aliwataja watu kadhaa kwa majina. Kwa kuongezea, Paulo alitaka sana kwenda Roma ili kuwapa kitia-moyo ndugu zake Wakristo huko, na pia alikuwa amepanga kufanya Roma iwe kituo cha muda akiwa katika safari yake ya kimisionari aliyokusudia ya kwenda Hispania.—Waroma 1:11, 12; 15:22-24, NW.

Hata hivyo, kusudi kubwa la Paulo katika kuandika barua hiyo lilikuwa kujibu swali hili: Watu waweza kupataje uadilifu uongozao kwenye uhai? Jibu lageuka kuwa habari bora kabisa. Uadilifu huhesabiwa kwa msingi wa imani. Paulo ajulisha jambo hilo na kuweka msingi wa kichwa cha barua yake aandikapo hivi: “Mimi sioni aibu juu ya habari njema; hizo, kwa uhakika, ni nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu kwa kila mtu mwenye imani, kwa Myahudi kwanza na pia kwa Mgiriki; kwa maana katika uadilifu wa Mungu zinafunuliwa kwa sababu ya imani na kuelekea imani, kama vile ilivyoandikwa: ‘Lakini mwadilifu—kwa njia ya imani ataishi.’”—Waroma 1:16, 17, NW.

IMANI NA SHERIA

Katika karne ya kwanza, si kila mtu aliyekubali kwamba uadilifu ulihesabiwa kwa msingi wa imani. Wachache wenye sauti nyingi walisisitiza kwamba mengi zaidi yalihitajiwa. Kwani si Yehova aliyekuwa ameandaa Sheria ya Kimusa? Angewezaje kuwa mwadilifu mtu yeyote asiyejitiisha kwa uandalizi huo uliovuviwa? (Ona Wagalatia 4:9-11, 21; 5:2.) Katika mwaka 49 W.K., swali la kuifuatilia sana Sheria lilizungumzwa na baraza lenye kuongoza katika Yerusalemu, nao wakakata shauri kwamba Wasio Wayahudi waliozikubali habari njema hawakuhitaji kutahiriwa wala kujitiisha kwenye virekebi vya Sheria ya Kiyahudi.—Matendo 15:1, 2, 28, 29.

Karibu miaka saba baadaye, Paulo aliandika barua yake kwa Waroma akiunga mkono uamuzi huo uliokuwa alama ya badiliko kubwa. Kwa kweli, alisonga mbele zaidi ya hapo. Si kwamba tu Sheria haikuhitajika kabisa kwa Wakristo Wasio Wayahudi bali pia Wayahudi waliotegemea kuitii hawangejulishwa rasmi kuwa ni waadilifu ili wapate uhai.

UADILIFU

KUPITIA IMANI

Usomapo kupitia kitabu cha Waroma, utaona jinsi Paulo asitawishavyo utetezi wa kisa chake kwa uangalifu mwingi, akiunga mkono taarifa zake kwa manukuu mengi kutokana na Maandiko ya Kiebrania. Anaposema na Wayahudi, ambao huenda wakawa na ugumu wa kukubali fundisho lake lililovuviwa, aonyesha shauku na hangaikio. (Waroma 3:1, 2; 9:1-3) Hata hivyo, yeye atokeza kisa chake kwa uwazi mwingi na sababu nzuri zisizoweza kufanyiwa ubishi.

Katika Waroma sura ya 1 hadi sura ya 4, Paulo aanza kwa ukweli wa kwamba kila mtu ana hatia ya dhambi. Hivyo, njia pekee ambayo wanadamu waweza kujulishwa rasmi kuwa waadilifu ni kwa msingi wa imani. Ni kweli kwamba Wayahudi walijaribu kuwa waadilifu kwa kushika Sheria ya Kimusa. Lakini walishindwa. Hivyo, Paulo asema hivi kwa ujasiri: “Wayahudi na vilevile Wagiriki wako chini ya dhambi wote.” Athibitisha ukweli huu usiopendwa na wengi kwa manukuu kadhaa ya Maandiko.—Waroma 3:9, NW.

Kwa kuwa “kwa kazi za sheria hakuna mnofu ambao utajulishwa rasmi kuwa mwadilifu,” kuna tumaini gani? Mungu atawajulisha rasmi wanadamu kuwa ni waadilifu hiyo ikiwa ni zawadi ya bure kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. (Waroma 3:20, 24, NW) Ili wajifaidi na hilo, ni lazima wawe na imani katika dhabihu hiyo. Je! fundisho hilo ni kwamba wanadamu hujulishwa rasmi kuwa waadilifu kwa msingi wa imani ni jambo jipya? Sivyo hata kidogo. Abrahamu mwenyewe alijulishwa rasmi kuwa mwadilifu kwa sababu ya imani yake kabla Sheria hata haijaanzishwa.—Waroma 4:3, NW.

Akiisha kuthibitisha umaana wa imani, katika sura ya 5 Paulo azungumza juu ya msingi wa imani ya Kikristo. Msingi huo ni Yesu, ambaye mwendo wake wa uadilifu hutangua matokeo mabaya ya dhambi ya Adamu kwa wale walio na imani katika Yeye. Hivyo, “kupitia kitendo kimoja cha kutetewa haki,” si kwa kutii Sheria ya Kimusa, “tokeo kwa watu wa namna zote ni kujulishwa rasmi kwao kuwa waadilifu kwa ajili ya uhai.”—Waroma 5:18, NW.

KUJIBU VIPINGAMIZI

Ingawa hivyo, ikiwa Wakristo hawako chini ya Sheria, sasa basi ni nini kitawazuia kusonga mbele watende dhambi na hata hivyo wategemee kujulishwa rasmi kuwa waadilifu, kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu? Paulo ajibu kipingamizi hicho katika Waroma sura ya 6. Wakristo wamefia mwendo wao uliopita wenye dhambi. Maisha yao mapya katika Yesu huwashurutisha wapigane na udhaifu wao mbalimbali wa kimnofu. Yeye ahimiza hivi: “Msiache dhambi iendelee kutawala kama mfalme katika miili yenu yenye kufa.”—Waroma 6:12, NW.

Lakini je! haiwapasi Wayahudi, angalau, washikamane bado na Sheria ya Kimusa? Katika sura ya 7, Paulo aeleza kwa uangalifu kwamba sivyo ilivyo. Kama vile mwanamke aliyefunga ndoa alivyo huru na sheria ya mume wake wakati mume afapo, ndivyo kifo cha Yesu kilivyowaweka huru Wayahudi kutoka ujitiisho kwa Sheria. Paulo asema hivi: “Nyinyi pia mlifanywa wafu kwa Sheria kupitia mwili wa Kristo.”—Waroma 7:4, NW.

Je! hiyo yamaanisha kwamba Sheria ilikuwa na kasoro? Sivyo kwa vyovyote. Sheria ilikuwa kamilifu. Tatizo lilikuwa kwamba watu wasiokamilika hawangeweza kuitii Sheria. “Sisi twajua kwamba Sheria ni ya kiroho,” akaandika Paulo, “lakini mimi ni wa kimnofu, nikauzwa chini ya dhambi.” Binadamu asiyekamilika hawezi kushika Sheria kamilifu ya Mungu na kwa hiyo yeye hulaaniwa vikali nayo. Basi, ni vizuri kama nini kwamba “wale walio katika mwungano pamoja na Kristo Yesu hawana laana kali”! Wakristo wapakwa-mafuta wamechukuliwa ili walelewe na roho wawe wana wa Mungu. Roho ya Yehova huwasaidia wapigane mweleka na hali za kutokamilika za mnofu. “Nani ataandikisha shtaka dhidi ya wachaguliwa wa Mungu? Mungu ndiye huwajulisha rasmi kuwa waadilifu.” (Waroma 7:14; 8:1, 33, NW) Hakuna kiwezacho kuwatenganisha na upendo wa Mungu.

UADILIFU NA WAYAHUDI WA KIMNOFU

Ikiwa Sheria haihitajiwi tena, jambo hilo laliacha wapi taifa la Israeli? Na namna gani maandiko yote yale yanayoahidi kurudishwa kwa Israeli? Maswali haya yazungumzwa katika Waroma sura ya 9 hadi ya 11. Maandiko ya Kiebrania yalitabiri kwamba ni wachache tu wa Waisraeli ambao wangeokolewa na kwamba Mungu angegeuza uangalifu wake kuelekea mataifa. Kupatana na hilo, unabii mbalimbali juu ya wokovu wa Israeli hautimizwi na Israeli wa kimnofu bali na kundi la Kikristo, ambalo lajumlika kuwa hivyo kutokana na kiini cha Wayahudi wa kimnofu wanaoamini na kujaziwa kabisa na Wasio Wayahudi wenye mioyo ifaayo.—Waroma 10:19-21; 11:1, 5, 17-24.

KANUNI ZA

UADILIFU

Katika Waroma sura ya 12 hadi ya 15, Paulo aendelea kueleza njia fulani zifaazo ambamo Wakristo wapakwa-mafuta waweza kuishi kupatana na kujulishwa rasmi kwao kuwa waadilifu. Kwa kielelezo, asema hivi: “Mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri. Na mwache kufanyizwa kulingana na mtindo wa huu mfumo wa mambo, bali mgeuzwe kwa kubadili akili zenu.” (Waroma 12:1, 2, NW) Twapaswa kutumaini katika nguvu ya wema wala tusipigane na uovu kwa kutumia uovu. “Usijiache ushindwe na uovu,” akaandika mtume, “bali endelea kuushinda uovu kwa wema.”—Waroma 12:21, NW.

Roma kilikuwa kitovu cha nguvu za kisiasa katika siku ya Paulo. Hivyo, kwa hekima Paulo aliwashauri hivi Wakristo: “Acheni kila nafsi iwe katika kutii mamlaka za juu zaidi, kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa njia ya Mungu.” (Waroma 13:1, NW) Mishughulikiano ya Wakristo ni sehemu pia ya kuishi kupatana na uadilifu. “Nyinyi watu msiwe mnawiwa na mtu yeyote hata kitu kimoja,” asema Paulo, “isipokuwa kupendana mmoja na mwenzake; kwa maana yeye ape-ndaye binadamu mwenzake ameitimiza sheria.”—Waroma 13:8, NW.

Zaidi ya hilo, Wakristo wapaswa wawe wenye kufikiria dhamiri ya mmoja na mwingine na wasiwe wakihukumu-hukumu. Paulo ahimiza hivi: “Acheni tufuatie mambo yanayofanyiza amani na mambo yaliyo ya kujenga mmoja na mwenzake.” (Waroma 14:19, NW) Lo, hilo ni shauri zuri kama nini la kutumia katika kila jambo la maisha ya Mkristo! Halafu, katika sura ya 16, Paulo amalizia kwa salamu za kibinafsi na maneno ya mwisho ya kitia-moyo na shauri.

KWA AJILI YA WAPAKWA-MAFUTA

NA KONDOO WENGINE

Kichwa kilichozungumzwa katika Waroma kilikuwa cha maana katika karne ya kwanza na kingali chapasa kupewa umuhimu leo. Uadilifu na uhai wa milele ni lazima vipendeze watumishi wote wa Yehova. Ni kweli kwamba Waroma kiliandikwa kwa kundi la Wakristo wapakwa-mafuta, hali leo walio wengi sana wa Mashahidi wa Yehova ni wa “umati mkubwa” na wana tumaini la kidunia. (Ufunuo 7:9, NW) Hata hivyo, barua hii ina ujumbe muhimu kwa hao pia. Ujumbe gani?

Kitabu cha Waroma huthibitisha kwamba Wakristo hujulishwa rasmi kuwa waadilifu kwa njia ya imani. Kwa wapakwa-mafuta, hiyo ni kwa tazamio la kuwa watawala-wenzi pamoja na Yesu katika Ufalme wa kimbingu. Hata hivyo, washiriki wa umati mkubwa hujulishwa rasmi pia kuwa waadilifu, lakini wakiwa ‘rafiki za Mungu,’ kama alivyokuwa Abrahamu mzee wa ukoo. (Yakobo 2:21-23) Uadilifu wao ni kwa tazamio la kuokoka dhiki kubwa, na msingi wao ni damu ya Yesu, kama vile ilivyo kwa habari ya wapakwa-mafuta. (Zaburi 37:11; Yohana 10:16; Ufunuo 7:9, 14) Hivyo, njia ya Paulo ya kusababu mambo katika Waroma ni ya kuhangaikiwa sana na kondoo wengine na pia wapakwa-mafuta. Na shauri zuri la kitabu hicho la kuishi kupatana na kujulishwa kwetu rasmi kwamba sisi ni waadilifu ni muhimu kwa Wakristo wote.

The Book of Life, kilichohaririwa na Madaktari Newton Marshall Hall na Irving Francis Wood, chataarifu hivi: “Kwa kuzungumzia juu ya upande ule wenye kubishaniwa na wa kimafundisho, [Waroma] chafikia kilele cha fundisho la Paulo lililovuviwa. Ni chenye hisani, busara, hata hivyo chenye mamlaka. . . . Kujifunza waraka huu kuna thawabu zao zilizo nyingi na tele.” Kwa nini usijisomee mwenyewe kitabu hicho na ushangilie katika “habari njema” zilizomo, ambazo ni “nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu.”—Waroma 1:16, NW.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 24]

“Hakuna mamlaka [ya kilimwengu] isipokuwa kwa njia ya Mungu.” Hii haimaanishi kwamba Mungu ndiye huweka kila mtawala mmoja mmoja mahali atakapokuwa. Bali, watawala wa kilimwengu wapo kwa ruhusa tu ya Mungu. Katika visa vingi, watawala wa kibinadamu walitangulia kuonwa na kutabiriwa na Mungu na hivyo ‘waliwekwa na Mungu katika vyeo vyao vinavyohusu.’—Waroma 13:1, NW.

[Hisani]

Museo della Civiltà Romana, Roma

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 25]

Wakristo waambiwa hivi: “Vaeni Bwana Yesu Kristo.” Hii yamaanisha kwamba wao wapaswa kufuata hatua za nyayo za Yesu kwa ukaribu, wakimwiga kwa kutanguliza katika maisha zao masilahi ya kiroho kuliko ya kimnofu, hivyo, ‘si kupangia mapema tamaa za mnofu.’—Waroma 13:14, NW.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 25]

Paulo aliwaambia Waroma ‘wasalimiane mmoja na mwenzake kwa busu takatifu.’ Hata hivyo, hapo hakuwa akiweka imara desturi mpya ya Kikristo wala kawaida ya kidini. Katika siku ya Paulo, mara nyingi busu juu ya kipaji cha uso, midomo, au mkono lilifanywa kuwa ishara ya salamu, shauku, au staha. Hivyo, Paulo alikuwa akirejezea desturi iliyokuwa ya kawaida katika siku yake.—Waroma 16:16, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki