Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 10/1 kur. 30-31
  • Je! Wewe Hufuata Maagizo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Hufuata Maagizo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ndani ya Familia
  • Katika Kundi
  • Matokeo Yenye Shangwe
  • Kufanikisha Maisha ya Jamaa
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je, Uko Tayari Kwa Ajili ya Wokovu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Musa Alifuata Maagizo kwa Makini
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 10/1 kur. 30-31

Je! Wewe Hufuata Maagizo?

BABA mwenye upendo ataagiza watoto wake ili wapate kufanikiwa maishani na wawe wenye furaha wawapo watu wazima. Na watoto wawapendao na kuwastahi wazazi wao watakubali maagizo hayo kwa sababu wao wajua ni kwa manufaa yao wenyewe. Vilevile, Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo, Yehova, huandalia watumishi wake mwongozo ambao huwaletea mafanikio na shangwe katika maisha zao. Kwa hiyo, ni jambo la maana sisi tufuate maagizo ambayo Mungu hutupa kupitia Neno lake, Biblia, na tengenezo lake la kidunia.

Ndani ya Familia

Kuna maeneo mbalimbali ambayo kwayo sisi hupewa maagizo. Moja ni ndani ya mzingo wa familia. Ndoa na familia zina asili ya kimungu. Biblia husema kwamba Mungu aliwafungisha ndoa wanadamu wawili wa kwanza na kuwaambia wawe na watoto. (Mwanzo 1:27, 28; 2:22-24) Muumba ameandalia washiriki wote wa familia maagizo kuhusu wajibu wa kila mmoja. Kwa kielelezo, mume na baba ndiye kichwa cha nyumba, jambo ambalo lamaanisha kwamba ndiye mwenye daraka la kuandaa maagizo, chakula, nguo, makao, ulinzi, na nidhamu. Pia yeye hufanya maamuzi ya familia yaliyo ya maana. Akiwa mume, apaswa kuonyesha ufikirio kwa mke wake na kumgawia heshima kama chombo dhaifu zaidi. (Waefeso 5:22, 23; 1 Timotheo 5:8; 1 Petro 3:7) Mke apaswa kuwa katika unyenyekeo kwa mume wake, amwonyeshe staha ya kina kirefu, na awe msaidiaji na kikamilisho chake. Na Maandiko huonyesha wazi kwamba ni lazima watoto wawe watiifu kwa wazazi wao.—Mwanzo 2:18; Waefeso 6:1-3; 1 Petro 3:1, 2.

Ni nini hutukia maagizo haya yakiachiliwa? Kutoafikiana na magombano hutukia wakati waume wakosapo ufikirio kwa wake zao, na wake waonyeshapo staha kidogo kwa ukichwa wa mume. Kwa uhakika, mambo hayo yamesababisha mvunjiko wa ndoa nyingi. Ukosefu wa utii na uasi wa watoto umeleta majonzi makubwa kwa wazazi wengi. Mara nyingi, wazazi ni wa kulaumiwa sana kwa kutolea watoto wao kulingana na nidhamu ifaayo, hivyo wakiwaudhi-udhi.—Waefeso 6:4, NW.

Ingawa wafanya kazi wa kijamii, wanasaikolojia, na wengine wametoa unamna-namna wa madokezo mengi sana juu ya jinsi ya kushughulika na matatizo ya familia, hakuna shauri lenye matokeo kuliko maagizo yaliyoandaliwa katika Biblia na Muumba wa familia. Kuyafuata huleta furaha na uradhi wa kweli.—Zaburi 19:7-9.

Katika Kundi

Twapaswa kufuata maagizo ambayo Kichwa cha kundi la Kikristo, Yesu Kristo, hutoa kupitia “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” kipitio kilichowekwa cha tengenezo la Mungu hapa duniani. (Mathayo 24:45-47; Waefeso 5:23) Ili kuwe na amani na mwungamano katika kundi, washirika walo wote ni lazima watende kupatana na mwongozo utolewao. Mathalani, wale wanaoongoza katika kufundisha kundi na katika kusaidia wengine huhitaji kushikamana na mielekezo wapokeayo kutoka kwenye tengenezo la Yehova. Hiyo itachangia matokeo mazuri ya kazi yao. Huenda maagizo hayo yakawa juu ya jinsi ya kushiriki katika utendaji wa kuhubiri, jinsi ya kushughulika na matatizo katika kundi, jinsi ya kutoa shauri na kitia-moyo, jinsi ya kufariji wenye shida, na kadhalika. Pia kuna mielekezo rasmi juu ya jinsi ya kutayarisha mikutano yenye kufundisha na kujenga wote ambao hushirikiana na kundi la Kikristo.—Matendo 20:20; Warumi 12:6-8; Wagalatia 6:1; 1 Wathesalonike 3:1-3.

Wazee, au waangalizi wa kundi, hasa wapaswa kuweka kielelezo chema katika habari hii. Baraza Linaloongoza hupeleka maagizo ambayo wazee wapaswa kufuata kwa uangalifu na kwa uaminifu. Wapaswa kurekebisha na kutumia maagizo kulingana na hali za kwao. Ni lazima sisi tukumbuke kwamba mmoja ambaye huelekeza kundi la Kikristo ni Yesu Kristo. Yeye afahamu kikamilifu mahitaji ya makundi yote kuzunguka ulimwengu, naye huandaa kitia-moyo na usaidizi uhitajiwao. Kwa hiyo, wazee hawapaswi kusita kutumia mielekezo yoyote wapokeayo kutoka kwenye tengenezo la kitheokrasi la Mungu. Hii itatumika kuwa kielelezo kizuri kwa wote katika kila kundi na itawasaidia wawe na mwungamano miongoni mwao wenyewe na pamoja na sehemu nyingine yote ya udugu wa Kikristo kuzunguka dunia.—Matendo 15:1-31; Waebrania 13:7; Ufunuo 5:6.

Matokeo Yenye Shangwe

Mjenzi asimamishapo jengo kubwa, yeye hufuata kwa uangalifu ramani za wachora ramani ili ajengacho kidumu. Katika zile siku zenye jeuri kabla ya Gharika, Noa alipewa utume wa kujenga safina. Aliambiwa jinsi ya kuijenga na ni wanadamu na wanyama wepi wa kuingiza humo ili kuokoka kupita Gharika inayokuja. Noa aliitikiaje? Biblia yasema hivi: “Noa akafanya hivi; sawasawa na maneno yote Mungu aliyomwagiza, akafanya hivi.” Ni Noa na wale tu waliokuwa naye katika safina walioiokoka Gharika. (Mwanzo 6:5, 13-22; 7:23, ZSB) Leo, tunaishi katika nyakati ambazo zafanana sana na siku ya Noa, na kwa sababu hii Mungu atafutilia mbali waovu wote. Biblia yatuambia hatua ambazo ni lazima tuchukue ikiwa twataka kuwa miongoni mwa waokokaji.—Mathayo 24:37-39; 2 Petro 3:5-7, 11.

Kwa hiyo, acheni tuyapokee kwa uthamini na kuzoea kutenda maagizo ambayo Yehova atupa kupitia Neno lake lililoandikwa na tengenezo lake la kidunia. Kufanya hivi kutatuletea mafanikio na shangwe na kutaokoa uhai wetu pia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki