Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 12/1 kur. 15-20
  • Tunaweza Kuitikiaje Upendo wa Mungu Bila Ubinafsi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunaweza Kuitikiaje Upendo wa Mungu Bila Ubinafsi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kupenda Uadilifu, Kuchukia Ukosefu wa Kutii Sheria
  • Onyesha Upendo wa Kidugu
  • Kuhudumia Wale Walio Nje
  • Endeleeni Kuitikia Upendo wa Mungu
  • Waliitikia Upendo wa Mungu Bila Ubinafsi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Mjengwe na Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • “Endeleeni Kutembea Katika Upendo”
    Mkaribie Yehova
  • Iweni na Juhudi Nyingi Katika Kupendana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 12/1 kur. 15-20

Tunaweza Kuitikiaje Upendo wa Mungu Bila Ubinafsi?

“Ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.”—1 YOHANA 4:11.

1, 2. Ni nini linalotakwa kwetu ili tuitikie maonyesho ya upendo wa Mungu bila ubinafsi?

YEHOVA ndiye ufananisho unaofaa kabisa wa upendo. Kwa kweli, katika makala iliyotangulia, tuliona jinsi maonyesho wazi ya upendo wake ni mengi sana kwa kweli. Pia tuliona jinsi Musa, Daudi, na Yesu Kristo waliitikia hayo maonyesho wazi ya upendo bila ubinafsi. Je! kila mmoja wa Mashahidi wa Yehova hapaswi kutaka kufanya ivyo hivyo? Hakika!

2 Ni nini linalotakwa ili sisi tuitikie mawonyesho ya upendo wa Mungu bila ubinafsi? Kwanza, ni lazima tumpe yeye mahali pa kwanza katika maisha zetu, kumpenda kwa moyo, nafsi, akili, na nguvu zetu zote. (Marko 12:29, 30) Hiyo inamaanisha kukaza fikira kwenye Mungu, kuwa na uhusiano mchangamfu wa kibinafsi pamoja na Yehova. Je! sisi tunatamani kuongea na Baba yetu wa kimbingu katika sala? Je! tunasali bila kukoma na kudumu katika sala? Au tunafanya haraka kupitia sala zetu, na nyakati fulani hata kuwa wenye shughuli mno kusali? (Warumi 12:12; 1 Wathesalonike 5:17) Je! sisi tunaelekeza uangalifu kwa Yehova, tukimpa yeye na tengenezo lake sifa kwa mambo ambayo huenda tukawa tumetimiza? (1 Wakorintho 3:7; 4:7) Kwa kweli, je! sisi tunajisikia kama mtunga zaburi? Kwa habari ya Mungu, alisema hivi: “Mara saba kila siku nakusifu.”—Zaburi 119:164.

3. Tunapokutana pamoja kirafiki, tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaitikia upendo wa Mungu bila ubinafsi?

3 Wakati ambao sisi tunakutana kwa mambo ya kirafiki unaweza kufunua kama tunaitikia au hatuitikii upendo wa Mungu bila ubinafsi. Je! maongezi yetu wakati huo yanategemea mambo ya kilimwengu au ya kiroho? Si kwamba tunahitaji kuwa na funzo zito la Biblia kila wakati tunapokutana pamoja na Wakristo wenzetu. Lakini kwa uhakika tunaweza kupata mambo ya namna fulani ya kiroho yaliyo ya kupendeza ili kuyatia katika maongezi yetu. Namna gani kusimulia maono ya shambani, kuzungumza andiko la Biblia tunalolipenda zaidi, kueleza jinsi tulijifunza ukweli, au kutaja shuhuda za utunzaji wenye upendo na baraka ya Mungu?

4. Tunapaswa kuonaje mambo ikiwa tunakatishwa tamaa kwa habari ya pendeleo fulani la utumishi?

4 Hali nyingine inayoweza kufunua kadiri ya uthamini wetu kwa upendo wa Mungu ni wakati tunaposahauliwa kuhusu pendeleo fulani la utumishi katika tengenezo la Yehova. Tunaitikiaje? Ikiwa tunahangaikia hasa kuheshimu Yehova, tutakubali kwamba inaelekea sana kwamba Mungu ataheshimiwa kwa usawa ule ule na yeyote yule aliye na pendeleo hilo hasa la utumishi. (Linganisha Luka 9:48.) Lakini ikiwa tuna hangaiko lisilofaa juu ya sisi wenyewe kupata faida au jina, tutasononeka kwamba tumesahauliwa, kama vile huenda tukafikiri. Inatupasa kukumbuka kwamba Yehova anatupenda na huenda hata akajua kwamba kwa sasa hatuwezi kubeba uzito wa daraka fulani la kitheokrasi. Huenda ikawa anatubariki sana kwa njia nyinginezo, na hayo maonyesho wazi ya upendo wake yanapasa kutusaidia tuendeleze usawaziko wetu wa kiroho.—Mithali 10:22.

Kupenda Uadilifu, Kuchukia Ukosefu wa Kutii Sheria

5. Maonyesho wazi ya upendo wa Mungu yanapasa kuwa na tokeo gani juu ya mwenendo wetu?

5 Maonyesho wazi ya upendo wa Mungu kuelekea sisi yanapasa kutusukuma kuiga Kristo katika kupenda uadilifu na kuchukia ukosefu wa kutii sheria. (Waebrania 1:9) Ni kweli, hatuwezi kufanya hivi kikamilifu, kama Yesu alivyofanya. Na bado, tunaweza kufanya uwe mradi wetu kuwa watakatifu, wanyoofu, na wenye kushika sheria kwa kadiri inavyowezekana katika hali yetu ya kutokamilika. Ili kufanya hivi, zaidi ya kusitawisha upendo wa uadilifu na mambo mema ni lazima pia tusitawishe chuki, machukio makubwa, karaha, kwa lililo ovu. Kama vile mtume Paulo alivyoeleza jambo hilo: “Lichukieni [kirihini, NW] lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.” (Warumi 12:9) “Kirihi” ni neno kali sana, linalomaanisha “kuona kwa mwepuko wa kuchukizwa kwa kadiri inayozidi kabisa.”—Webster’s New Collegiate Dictionary.

6. Ni nini kitatusaidia tujikinge na majaribu yanayowekwa katika njia yetu na ulimwengu, mwili wetu wenye dhambi, na Ibilisi?

6 Ni nini kitatusaidia kujikinga na majaribu yanayotupwa katika njia yetu na ulimwengu, mwili wetu wenyewe wenye dhambi, na Ibilisi? Ni uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova Mungu. Yeye anatusihi hivi: “Mwanangu, uwe na hekima na kunifurahisha moyo wangu; ili nipate kumjibu anilaumuye.” (Mithali 27:11) Ndiyo, uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova utatusukuma kufuata ule mwendo wa hekima wa kuchukia anayochukia. Zaidi ya hilo, hata ikiwa kuvunja moja ya sheria za Mungu huenda kukaonekana kuwa jambo la kufurahika au la kusisimua kadiri gani, ni lazima tuendelee kujiambia wenyewe kwamba kufanya hivyo hakufai hata kidogo. (Wagalatia 6:7, 8) Moyo wa kibinadamu ni wenye hila, wenye vipengele, wenye udanganyifu, kama vile tunavyokumbushwa kwenye Yeremia 17:9. Moyo wa Kikristo unapenda mambo mema, mazuri, yaliyo safi. Lakini nyakati fulani maelekeo yenye dhambi yanauelekeza pia utamani lililo baya. Kama vile mioyo ya Waisraeli walioabudu Yehova na bado wakabaki na “mahali pa juu” pa ibada yao ya sanamu, ndivyo moyo wetu wenyewe unaweza kuwa na ubinafsi na kufanya madanganyo. (1 Wafalme 22:43; Kumbukumbu 12:2) Huenda moyo wetu usiokamilika ukajaribu kutafuta udhuru wa kutuweka katika njia yenye jaribu. Huenda ukajaribu kupunguza uzito wa kosa tunalojaribiwa kwalo. Au huenda moyo wetu ukajaribu kutusadikisha kwamba adhabu yoyote itakuwa ya muda tu.

7. Kwa sababu gani ni lazima tujikinge tusitamani lililo baya?

7 Kwa kuthamini upendo wa Mungu, ni lazima tujikinge tusitamani lililo baya, kama vile kuegemea kuelekea ukosefu wa adili katika ngono, tuwe hatujafunga au tumefunga ndoa. Tena na tena, jambo lililoanza likiwa ni kuchezeana kirafiki tu limekuwa na tokeo la kufanya Wakristo wawili wahusiane sana katika maono ya moyoni hivi kwamba wamezoea dhambi na kutengwa na ushirika. Hata wazee, wanaopaswa kuwa mifano isiyolaumika kwa kundi la kondoo, wamepatwa na balaa katika mambo haya!—Linganisha 1 Wafalme 15:4, 5.

8. Ni mfano gani wa onyo ambao mtume Paulo anatupa sisi, na tatizo hilo linaweza kuonyeshwa kwa mfano gani?

8 Fikiria mtume Paulo, aliyebarikiwa kwa njozi na nguvu zinazozidi za asili na kwa zawadi ya uvuvio wa kimungu. Ili afanikiwe katika jitihada yake ngumu juu ya mielekeo yenye dhambi, ilikuwa lazima apigepige—ndiyo, apige vikali—mwili wake. Je! sisi tunathubutu kutosheka kufanya kwa kadiri inayopungua hiyo? (Warumi 7:15-25; 1 Wakorintho 9:27) Ni kama kwamba sisi tumo katika mashua ndogo ya kupiga makasia (vibao) katika mto unaotiririka mbio sana na ni kama tunavutwa kuelekea maporomoko yake. Ili kuepuka msiba, ni lazima tupige makasia kwa kujikaza sana kupanda juu kuelekeana na mkondo ule mkali. Huenda isionekane tunafanya maendeleo mengi, lakini ikiwa tunaendelea kujitahidi kwa nguvu nyingi, hatutaporomoka chini kwenye maanguko tukapate uharibifu. Kwa uhakika, maonyesho wazi ya upendo wa Yehova Mungu kuelekea sisi yanapasa kutufanya tujitahidi kwa nguvu nyingi tuwe waaminifu--washikamanifu kwake kwa kuchukia ukosefu wa kutii sheria na kwa kupenda uadilifu.

Onyesha Upendo wa Kidugu

9. Ni shauri gani ambalo mtume Yohana anatoa juu ya kupenda ndugu zetu?

9 Maonyesho wazi ya upendo wa Mungu yanapasa pia kutusukuma tupende ndugu zetu kama vile Yesu Kristo anavyopenda wanafunzi wake. (Yohana 13:1) Kwa kufaa sana, mtume Yohana anasema hivi: “Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. Wapenzi, ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.” (1 Yohana 4:10, 11) Kwa uhakika, Yesu alisema kwamba njia ambayo wafuasi wake wa kweli wanaweza kutambuliwa ni kwa upendo ambao wanao miongoni mwao wenyewe.—Yohana 13:34, 35.

10, 11. Ni nini nyingine za njia ambazo tunaweza kuonyesha upendo wa kidugu?

10 Tunajua kwamba Wakristo wanapaswa kuonyesha upendo wa kidugu. Lakini si jambo baya kujikumbusha wenyewe njia mbalimbali ambazo tunaweza kuonyeshana upendo huu ulio kama wa Kristo. Upendo huo utatusaidia tuachilie mbali tofauti zinazohusu rangi ya ngozi, utaifa, elimu, utamaduni, na cheo cha kiuchumi. Zaidi ya hilo, upendo wa kidugu utatusukuma tuje pamoja katika mikutano. Ikiwa kweli tunapenda ndugu zetu, hatutaacha hali mbaya ya hewa au ugonjwa mdogo tu utunyime shangwe ya kushirikiana pamoja nao na kushiriki katika badilishano la kitia-moyo. (Warumi 1:11, 12) Zaidi ya hilo, upendo wa kidugu utatufanya tujitayarishe vizuri kwa ajili ya mikutano yetu na kuishiriki kwa utendaji ili tuweze kuchocheana kwenye upendo na kazi nzuri sana.—Waebrania 10:23-25.

11 Namna gani kusaidia ndugu zetu katika huduma ya shambani? Imeonwa kwamba wazee na watumishi wa huduma wanajitia mara nyingi katika huduma ya nyumba kwa nyumba wakiwa mmoja na mwenzake au wakiwa peke yao na hali, kwa kufanya mipango kidogo tu, wangeweza kualika wahubiri wa Ufalme wanaohitaji msaada katika huduma waandamane nao. Kuonyesha upendo katika njia hii kutafanya utumishi wa shambani wa wazee na watumishi wa huduma uthawabishe maradufu. Namna gani kwenda na mhubiri mpya katika funzo la nyumbani la Biblia?—Warumi 15:1, 2.

12. Tunapaswa kuelewaje 1 Yohana 3:16-18?

12 Pia upendo utatufanya tuje kusaidia ndugu zetu ambao huenda wakawa katika uhitaji halisi wa kimwili. Mtume Yohana aliandika hivi: “Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.” (1 Yohana 3:16-18) Huenda ikawa hatutaombwa sasa kutoa nafsi zetu kwa ajili yao, lakini nyakati fulani tuna-kuwa na nafasi za kuwaonyesha upendo kwa njia nyinginezo, si kwa maneno tu au kwa ulimi bali pia kwa matendo. Hakuna ubaya wowote kupenda ndugu zetu kwa maneno, lakini hatutaki kufanya upendo wetu uishie hapo wanapokuwa katika uhitaji wa vitu vya kimwili. Usemi wa Yesu kwamba “ni heri [furaha, NW] kutoa kuliko kupokea” yanatumika kwa kuandaa msaada wa vitu vya kimwili pia.—Matendo 20:35.

13. (a) Ni nini nyingine za kweli za msingi ambazo tumejifunza kwa msaada wa tengenezo la Yehova linaloonekana? (b) Ni jambo gani halali ambalo Charles Taze Russell alitokeza?

13 Sisi tuna nafasi ya kuonyesha upendo kwa ndugu zetu wanaoongoza katika kundi au kwa ukamatano na tengenezo la Yehova linaloonekana ulimwenguni pote. Hii inatia ndani kuwa waaminifu-washikamanifu kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” (Mathayo 24:45-47) Acheni tukubali wazi uhakika wa kwamba hata iwe tumefanya kiasi gani cha usomaji wa Biblia, hatungalijifunza kamwe ukweli tukiwa peke yetu. Hatungaligundua ukweli kuhusu Yehova, makusudi na sifa zake, maana na ubora wa jina lake, Ufalme, ukombozi wa Yesu, tofauti kati ya tengenezo la Mungu na la Shetani, wala sababu ambayo Mungu ameruhusu uovu. Ni kama tu vile msimamizi wa kwanza wa Watch Tower Society, Charles Taze Russell, alivyoandika katika 1914: “Je! sisi si kikundi cha watu wenye baraka, wenye furaha? Je! Mungu wetu si mwaminifu? Ikiwa mtu yeyote anajua chochote kilicho kizuri zaidi, na akichukue. Ikiwa yeyote wa nyinyi atakuja kupata chochote kilicho kizuri zaidi, tunatumaini kwamba mtatuambia. Sisi hatujui kitu kilicho kizuri zaidi wala kilicho na nusu ya wema wa yale ambayo tumepata katika Neno la Mungu. . . . Hakuna ulimi wala kalamu inayoweza kueleza amani, shangwe na baraka ambayo maarifa ya wazi juu ya Mungu wa kweli yameingiza ndani ya moyo na maisha yetu. Ile Hadithi ya Hekima, Haki, Nguvu na Upendo wa Mungu inatosheleza kikamili matamanio ya kichwa chetu na pia moyo wetu. Sisi hatutafuti zaidi. Hakuna kitu zaidi cha kutamaniwa kuliko kupata kuifanya Hadithi hii iliyo nzuri ajabu ieleweke wazi zaidi katika akili yetu.” (The Watch Tower, Desemba  15, 1914, kurasa  377-8) Jinsi yalivyo ya kweli maneno hayo yaliyoandikwa vizuri!

Kuhudumia Wale Walio Nje

14. Maonyesho ya upendo wa Mungu yanapasa kutusukuma tutendeje kuelekea wale walio nje?

14 Maonyesho ya upendo wa Mungu ambayo tumeonea shangwe yanapasa kutusukuma tuonyeshe upendo wa jirani kwa wale walio nje ya kundi. Tunawezaje kufanya hivi? Huenda hali zikaonyesha kwamba tunaweza kusaidia jirani zetu kwa njia ya kimwili. Lakini, la maana zaidi, tunaweza kuonyesha upendo wa jirani kwa kuletea wengine habari njema za Ufalme wa Mungu na kusaidia wapendao uadilifu wawe wanafunzi wa Yesu Kristo. Je! sisi tunashiriki kwa ukawaida katika huduma hii ya peupe, au tunaiachilia? Je! imekuwa ni desturi tu au namna ya utumishi kidogo tu wa kuonyesha? Au sisi tunasukumwa kikweli na upendo wa jirani? Je! tunaonyesha wazi kuji-tia katika hali za wengine? Je! sisi ni wenye subira, tukingojea watu waitikie? Je! tunawatia moyo wenye nyumba waeleze maoni yao? Ndiyo, badala ya sisi kupiga domo juu ya kila kitu, na turuhusu upendo wa jirani utusukume kusikiliza na kuwa na mazungumzo ya Biblia yenye kuthawabisha pamoja na watu tunaokuta katika huduma yetu.

15. (a) Kwa nini “ushahidi wa vivi hivi” ni mtajo mzuri kuliko “ushahidi wa kushtukia”? (b) Kwa nini kutumia kwa faida nafasi za kutoa ushahidi wa vivi hivi?

15 Je! sisi tuko macho kwa kadiri tunavyopaswa ili kutumia kwa faida nafasi za kutoa ushahidi wa vivi hivi? Inapasa kuangaliwa kwamba huku si kutoa ushahidi wa kushtukia tu, ikitoa wazo la utendaji usiopangwa au ulio na umaana mdogo. Ushahidi wa vivi hivi ni wa maana sana, na upendo kwa wanadamu wenzetu utatusukuma kutafuta nafasi za kuushiriki. Jinsi ushahidi huo ulivyo na matokeo mara nyingi! Kwa mfano, alipokuwa akihudhuria mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Italia ya kaskazini, ndugu mmoja alienda kwenye banda la kutengenezea magari ili taa ya mbele ya motakaa yake ibadilishwe. Alipokuwa akingoja, aliwapa ushahidi wale wenye kumzunguka na kuwapa vikaratasi vya ukaribishaji kuwaalika kwenye hotuba ya Biblia ya watu wote Jumapili. Kwenye mkusanyiko mmoja wa kimataifa katika Roma mwaka mmoja baadaye, ndugu fulani ambaye yeye hakumtambua alimsalimu kwa uchangamfu. Ndugu huyu alikuwa nani? Alikuwa mmoja wa wale wanaume aliokuwa amewapa kikaratasi cha ukaribishaji kwenye banda la kutengenezea magari mwaka ule uliotangulia! Mwanamume huyo alikuwa ameenda kusikia ile hotuba ya watu wote na kutoa jina lake ili apate funzo la Biblia. Sasa yeye na mke wake pia ni Mashahidi wa Yehova waliojiweka wakfu. Hakuna shaka kwamba ushahidi wa vivi hivi unaweza kuthawabisha sana!

Endeleeni Kuitikia Upendo wa Mungu

16. Ni maswali gani ambayo ingefaa tujiulize?

16 Kwa kweli Yehova amekuwa mwingi katika kuonyesha wazi upendo kwa viumbe wake. Kama vile tumeona, Maandiko yanatupa sisi mifano mizuri sana ya wale ambao wameitikia maonyesho wazi ya upendo wa Mungu bila ubinafsi. Kwa kufaa sana, mtunga zaburi aliyevuviwa alitoa mshangao huu: “Na wamshukuru BWANA [Yehova, NW] kwa fadhili [fadhili-upendo, NW] zake, na maajabu yake kwa wanadamu.” (Zaburi 107:8, 15, 21, 31) Je! sisi tuthubutu kukubali fadhili zisizostahiliwa za Mungu na kukosa kusudi lake? Hilo lisitendeke kamwe! (2 Wakorintho 6:1) Hivyo basi acheni sisi mmoja mmoja tujiulize hivi: ‘Je! kweli mimi nathamini maonyesho ya upendo wa Mungu ambayo nimeonea shangwe tayari na ambayo natumainia kwa uhakika kuonea shangwe zaidi wakati ujao? Je! yananisukuma kupenda Yehova kwa moyo, nafsi, akili, na nguvu zangu zote? Je! kweli mimi ni mtu mwenye kukaza fikira kwa Mungu? Je! mimi napenda uadilifu na kuchukia ukosefu wa kutii sheria? Je! ninaonyesha upendo wa kidugu? Nami ninajaribu kutembea katika hatua za nyayo za Yesu kwa ukaribu wa kadiri gani kwa habari ya huduma yangu?’

17. Kutakuwa na tokeo gani tukiitikia maonyesho wazi ya upendo wa Yehova Mungu bila ubinafsi?

17 Kwa kweli, kuna njia nyingi za kuonyesha shukrani zetu za moyo mweupe kwa maonyesho yote ya wazi ya upendo wa Mungu ambayo tumeyaona. Kwa kutumia kwa faida kamili nafasi za kuonyesha uthamini huo, tutafurahisha moyo wa Baba yetu wa kimbingu, tuwe baraka kwa wengine, na kupokea shangwe, amani, na mtosheko sisi wenyewe. Kwa hiyo sisi na tuendelee kuitikia maonyesho wazi ya upendo wa Mungu bila ubinafsi.

Wewe Ungejibuje?

◻ Ni nini kinachotakwa ili kuitikia upendo wa Mungu bila ubinafsi?

◻ Sisi tunawezaje kujikinga na majaribu?

◻ Ni nini nyingine za njia za kuonyesha upendo wa kidugu?

◻ Maonyesho wazi ya upendo wa Yehova yanapasa kutusukuma tutende jinsi gani kuelekea jirani zetu?

[Picha katika ukurasa wa 17]

Ni lazima tujitahidi sana kujikinga na mielekeo yenye dhambi ili kuepuka msiba

[Picha katika ukurasa wa 18]

Wazee wanaonyesha upendo wa kidugu kwa kuandamana na wengine katika huduma ya Ufalme

[Picha katika ukurasa wa 19]

Charles Taze Russell, msimamizi wa kwanza wa Watch Tower Society, alivuta uangalifu kwenye amani, shangwe, na baraka ambayo ni Mungu peke yake anayeweza kuandaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki