‘Kutafuta Maneno Yapendezayo, Yaliyo Sahihi’
“HUYO Mhubiri [Mkutanishi, NW] akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu [maneno sahihi ya ukweli, NW].” (Mhubiri 12:10) ‘Maneno yapendezayo, yaliyo sahihi’ yenye msingi wa Maandiko yaliyovuviwa yanaweza kuwa ya thamani kama nini! Yanalinganishwa na “machungwa [matofaa ya dhahabu, NW] katika vyano vya fedha,” yakiwa ya ustadi na uvutio katika pindi yoyote na yasiyohesabika bei katika hali zenye mkazo.—Mithali 25:11.
Katika siku yetu yule Mkutanishi Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, ameandaa mali za kiroho zinazopita kwa mbali zile zilizoonewa shangwe na watu wa Mungu chini ya wafalme Waisraeli wa kale. (Mathayo 12:42) Kwa zaidi ya karne moja, maneno yapendezayo, yaliyo sahihi ya ukweli yanayohusu kila upande wa maisha yametokezwa katika vichapo vya Watch Tower Society na kuenezwa mahali pengi katika lugha nyingi. Familia nyingi na watu wengi mmoja mmoja wameweza hivyo kujaza katika nyumba zao wenyewe maktaba ya vichapo vya marejezo vyenye kutegemeka ambavyo vinakaza fikira juu ya Biblia. Kwa kuongezea, makundi yaliyo mengi ya Mashahidi wa Yehova yana maktaba nzuri sana za utumizi kwenye Majumba ya Ufalme yao.
Hata hivyo, kupata maneno yapendezayo, yaliyo sahihi yanayohitajiwa kwa ajili ya hali fulani hasa kungali kunataka uchunguzi. Kwa kutambua hilo, kuanzia mapema katika historia yake, Watch Tower Society imechapa faharisi kwa vichapo vyake.—Ona sanduku katika kurasa 28 na 29.
Mwongozo Mpya
Mwaka 1985 ulianza sura mpya katika historia ya Watch Tower Publications Indexes (Faharisi). Index tisa za mapema zaidi ziliunganishwa na kupatanishwa kuwa buku moja linalohusu 1930 mpaka 1985, mradi ambao ulitaka miaka 14 ya jitihada za kibinadamu. Manufaa za buku moja hilo la Index inayohusu miaka mingi ziliongoza kwenye mwongozo mpya katika 1986, ule wa kuchapa Index za muda baada ya muda kuanzia wakati huo. Kila mwaka, kwa kawaida katika muda wa miaka minne yenye kufuatana, broshua ya Index ya muda baada ya muda itahusisha mwaka mmoja, miaka miwili, mitatu, halafu minne. Kila miaka mitano Index yenye jalada gumu itaunganisha Index zote kuanzia 1986 na kuendelea, kama vile 1986-90, 1986-95, na hivyo hivyo. Kwa njia hiyo, haihitajiwi kuangalia zaidi ya Index tatu: Index ya 1930-1985, Index ya sasa yenye jalada gumu, na broshua ya sasa.
Index Iliyotayarishwa kwa Kukufikiria Wewe
Sehemu ya kwanza katika kila Index ni faharisi ya habari. Katika kutayarisha faharisi ya habari, maswali mawili yanatiwa akilini: (1) Ni habari gani zinazopasa kutiwa katika faharisi? (2) Ni wapi ambapo mtu angeweza kutafuta habari hizo?
Wewe uliye msomaji, ni mara chache ambapo ungependezwa na kutafuta kila elezo dogo juu ya habari fulani. Kwa kuwa kwa ujumla unatafuta habari za maana au zilizo za mafaa kweli kweli, hizo ndizo zinazochaguliwa ili zitiwe katika faharisi. Lakini habari hizo hazihitaji kuwa ndefu sana. Mwingizo katika Index ungeweza kutaja hata sentensi moja tu, kama vile usemi wa mwongozo wa Sosaiti juu ya jambo fulani. Au ungeweza kutia ndani makala nzima, hata kichapo kizima. Hata hivyo, kwa kawaida mwingizo unaongoza kwenye mafungu kadhaa ya mazungumzo.
Swali la mahali ambapo marejezo yanapasa kuonekana katika Index lina umaana pia, kwa maana wasomaji wanafikiri kwa njia tofauti na watatazama chini ya vichwa tofauti. Kwa mfano, habari juu ya Mnara wa Babeli zinazonekana chini ya MNARA WA BABELI. Lakini huenda wasomaji fulani wakatazama chini ya BABULONI (Babylon), UCHIMBUZI WA VITU VYA KALE (“Archaeology”), au LUGHA (“Language[s]”), ikitegemea upande wa habari hiyo ambao unawapendeza. Basi, jitihada zinafanywa kurudia marejezo chini ya vichwa mbalimbali vinavyofaa, kwa kukumbuka kwamba wasomaji ni wa umri na malezi mbalimbali, na wana makusudi tofauti.
Jinsi Index Inavyoweza Kukusaidia
Kama vile ramani Index inaweza kukutumikia ikiwa tu utaitumia. Unapaswa kutazamia kupata nini ama katika faharisi ya habari au katika sehemu ile ya faharisi ya Maandiko inayofuata?
Marejezo katika sehemu ya faharisi ya Maandiko yanahusu habari zinazoeleza mistari mmoja mmoja. Huenda ukapata elezo la kikao ambamo maneno ya andiko fulani yalisemwa, kwa nini yaliandikwa, yalitumika kwa nani, au maana ya maneno au vifungu kimoja kimoja vya maneno. Mfano mmoja ungeweza kuwa lile ombi katika sala ya kiolezo ya Yesu: “Usitutie majaribuni.” (Mathayo 6:13) Kwa nini ilisemwa kwa njia hiyo? Faharisi ya Maandiko itakusaidia ujue ni kwa nini.
Faharisi ya habari, kama vile jina layo linavyoonyesha, ni faharisi hasa ya habari badala ya maneno au vifungu vya maneno. Wakati wa kujaribu kupata makala kulingana na kichwa chayo, wasomaji fulani wamekuwa na ugumu wa kuipata. Huenda tatizo hili likasitawi wakati ambapo hakuna neno katika kichwa kikuu linalotambulisha kikweli habari hiyo. Mfano mmoja ungeweza kuwa ile makala “Je! Mimi Nina Kasoro Fulani?,” iliyozungumzia kuvutiwa na watu wa jinsi ile ile. Ukikumbuka yaliyomo katika makala ile, ungeweza kuelekea kwenye vichwa MAONO YA NDANI (“Feelings”) au UGONI-JINSIA-MOJA (“Homosexuality”) katika 1986-1989 Index, nawe utapata imerejezewa humo.
Index inaweza kuwa ya thamani ya pekee katika kutafuta habari juu ya matatizo ambayo huenda ukawa unakabili. Kwa mfano, ikiwa wewe ni mzazi, je! nyakati fulani unajiona umevurugika katika jitihada yako ya kuwatia nidhamu na kuwaongoza watoto wako? Chini ya WATOTO (“Children”) utapata marejezo kwenye habari nyingi inayoandaa muono-ndani katika kufikiri kwao, maono ya ndani, na mahitaji. Hata hivyo, chini ya kichwa MAZOEZI YA WATOTO (“Child Training”), ndipo utapata marejezo ya pande zote za kufundisha na kutia nidhamu.
Nyakati fulani Watch Tower Society inapata maombi yaliyoandikwa kuomba msaada kutatua matatizo ya ndoa au maswali juu ya kufaa kwa mahusiano fulani ya kindani katika ndoa. Ingawa huenda Sosaiti ikaweza kujibu, mashauri ayo hayo yenye mafaa yanayochochea maono ya ndani kwa urahisi yanaweza kupatikana kwa kufungua kwenye kichwa NDOA (“Marriage”), pamoja na vichwa vyake vidogo “matatizo” (“problems”) na “Ngono” (“sex”) au “mahusiano ya kingono” (“sex relations”), na kutafuta marejezo yaliyoorodheshwa.
Pia barua zinapokewa kutoka kwa wale wanaosumbuliwa na mshuko wa moyo au msononeko wa akili. Uhakikishio na msaada unaoandaliwa kwa barua unaweza kupatikana kwa haraka zaidi katika maktaba yako mwenyewe au ile iliyo kwenye Jumba la Ufalme kwa kuangalia vichwa MSHUKO WA MOYO (“Depression”) na UGONJWA WA AKILI (“Mental Illness”) katika Index. Makala zinazoeleza jinsi ya kukabili magonjwa ya akili, matibabu yanayopatikana, na maono yenye kugusa moyo juu ya wale ambao wamepata kuwa na mshuko wa moyo yanarejezewa.
Je! wewe ni kijana? Huenda ukawa na mahangaiko juu ya ndoa, maisha ya familia, shule, uhusiano wako na wazazi wako, na hivyo hivyo. Kichwa kikubwa VIJANA kina marejezo chini ya hivi vichwa vidogo vyote na vinginevyo. Kwa kuongezea, vichwa kama MAHUSIANO (“Relationships”), SHULE (“Schools”), KAZI-MAISHA (“Career”), na MATEMBEZI YA KUJUANA (“Courtship”) yana mengi ya kutoa. Kwa ajili ya ripoti za shule, Index inaweza kukuongoza kwenye habari nzuri juu ya asili, zile sayansi, dawa za kulevya, uchumi, na habari nyingine nyingi.
Manufaa kwa Ajili ya Marika Yote
Mwanamke wa miaka 81 aliandika hivi: “Vitabu na magazeti hayo ni mgodi wa dhahabu wa habari na imara ya kiroho—na Index inatokeza dhahabu hizo kwenye uso wa ardhi.” Mama mmoja ambaye watoto wake wana miaka minane na tisa alisema hivi: “Sasa mimi nashangaa ni jinsi gani nilivyokaa bila hiyo. Imeniongoza kwenye majibu ya mengi ya maswali ambayo yamenishangaza kwa muda mrefu na ikafanya uchunguzi wakati wa kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kundi uwe rahisi zaidi. . . . Pia ningependa kuwaambia jinsi kichapo hiki kimesaidia funzo letu la Biblia la familia. . . . Mume wangu anapowapa wasichana chaguo la kile ambacho wangependa kufanya, mara nyingi wao wanataka kufanya uchunguzi kwa kutumia Index hii. Wanafurahia kuchagua habari wanayopendezwa nayo, kama vile wanyama wawapendao au nchi tofauti-tofauti, nao wanaweza kutafuta habari hizo bila kusaidiwa sana. Hii imewafundisha pia kwamba funzo la Biblia ni kitu cha kufurahiwa.”
Utafutaji wa maneno yanayopendeza na maneno yaliyo sahihi ya ukweli una thawabu zisizohesabika bei. Jitihada za Mkutanishi ziliandaa manufaa nyingi kuliko zile alizokusudia hapo kwanza, kwa maana maneno hayo yametumika kuwatia moyo na kuwaongoza watumishi wa Yehova mpaka leo hii. Jitihada zetu kama hizo pia zinaleta baraka ya Yehova, zikiwa na matokeo yanayoweza kudumu milele.—Mithali 3:13-18, 21-26.
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 28, 29]
Faharisi za Mapema
Katika 1902 chapa ya pekee ya Chapa Sambamba ya Biblia ya Holman ilitokezwa kwa ajili ya Watch Tower Society, nayo ilikuwa na misaada yenye maelezo mengi yaliyotayarishwa na Sosaiti. Nyongeza yake ilikuwa na faharisi za habari na Maandiko pia kwa ule mfululizo wa vitabu Millenial Dawn (ambavyo baadaye vilijulikana kuwa Studies in the Scriptures), vijitabu viwili vikuu, na Zion’s Watch Tower kwa ajili ya 1879-1901.
Biblia za Berea za 1907 na baada ya hapo ziliandaa faharisi kama hizo. Hizo zilipitwa ubora katika 1922 na faharisi zenye maelezo marefu kwa vichapo vya Sosaiti. Faharisi hizi zilitokea katika buku la mwisho la mabuku saba ya chapa-upya za Watch Tower (1879-1919). Mpaka leo hii hizi za mwisho ndizo njia kuu ya kupata habari zilizotokezwa katika vichapo vya mapema vya Watch Tower Society.
Hata hivyo, kwa miaka 40 iliyofuata, uchunguzi katika vichapo vilivyotolewa baada ya 1919 ilikuwa lazima ufanywe kwa kutumia faharisi zilizotawanyika katika nyuma za vitabu na katika toleo la mwisho la magazeti kila mwaka. Lakini katika 1959 Sosaiti ilianza mradi mkubwa kuandaa faharisi ya habari na Maandiko katika buku moja kwa vichapo vyayo vya Kiingereza. Kikoa cha watu kilikusanywa kikitia ndani washiriki wa wafanya kazi wa makao makuu, wahitimu wamisionari wa Watchtower Bible School of Gilead, na hata waangalizi wanaosafiri kutoka Jiji la New York. Baada ya mwaka mmoja na nusu wa jitihada nyingi ya wafanya kazi 18 waliojitoa, Watch Tower Publications Index ya kwanza, ikiwa na sehemu za habari zilizozungumzwa na maandiko yaliyoelezwa, ikihusisha miaka 31 kuanzia 1930 mpaka 1960, ilitolewa. Ilitolewa mara ya kwanza kwa wasikilizaji wenye furaha nyingi kwenye Waabudu Wenye Umoja Makusanyiko ya 1961.
Tangu wakati huo, Watch Tower Publications Index imetokea katika Kiingereza kila mwaka, ikiwa na Index yenye jalada gumu yenye kutokea baada ya kila miaka mitano.