Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 1/15 kur. 24-29
  • Lugha Iliyo Safi Yaunganisha Umati Mkubwa wa Waabudu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lugha Iliyo Safi Yaunganisha Umati Mkubwa wa Waabudu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Lugha Iliyo Safi kwa Ajili ya Mataifa Yote”
  • Kujifunza Lugha Iliyo Safi
  • Chakula Kigumu cha Kiroho
  • Kusema Lugha Iliyo Safi Kwamaanisha Kuonyesha Upendo wa Kidugu
  • Kusema Lugha Iliyo Safi Kwamaanisha Kuchunga Mwenendo Wetu
  • Shauri la Lugha Iliyo Safi kwa Familia
  • Kusema Lugha Iliyo Safi kwa Wengine
  • Vitolewa vya Mkusanyiko
  • Hotuba ya Watu Wote na Maelezo ya Kumalizia
  • Semeni Lugha Iliyo Safi Mkaishi Milele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Lugha Safi Kwa Ajili Ya Mataifa Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Unazungumza Ile “Lugha Safi” kwa Ufasaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Unganishweni Na Lugha Iliyo Safi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 1/15 kur. 24-29

Lugha Iliyo Safi Yaunganisha Umati Mkubwa wa Waabudu

LUGHA iliyo safi ya kupewa na Mungu ni kani yenye kuleta umoja wa Kikristo. Uthibitisho wa hilo ulionekana kwa wote waliohudhuria mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova uliofanywa katika Berlin Magharibi kuanzia Jumanne mpaka Ijumaa, Julai 24 mpaka 27, 1990, kwa kuwa Mashahidi wa kutoka nchi tofauti-tofauti 64 walikuwako.

Wakati “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya ilipofanywa katika Polandi katika kiangazi cha 1989, maelfu ya wajumbe walikuja kutoka Urusi na Chekoslovakia, lakini ni mamia machache tu waliokuwako kutoka Ujerumani Mashariki. Lo, hali ya ulimwengu imebadilika kama nini kisiasa tangu wakati huo! Wakati huu, wajumbe wenye kukadiriwa kuwa 30,000 kutoka Ujerumani Mashariki walikutana na Mashahidi katika Stediamu Olympia katika Berlin Magharibi. Mkusanyiko huo ulikuwa kawaida ya mamia yaliyofanywa katika sehemu nyingine za ulimwengu, kwa ujumla Alhamisi mpaka Jumapili.

Jumanne, katika hotuba yake ya kufungua ya ukaribishaji mwenyekiti alisimulia daraka ambalo mikusanyiko ilikuwa imetimiza tangu 1919 katika kusaidia Mashahidi wa Yehova kufanya maendeleo katika kusema lugha iliyo safi. Vivyo hivyo mkusanyiko huu ungesaidia wote wenye kuhudhuria kuendeleza uwezo wao wa kusema lugha iliyo safi na kuishi kulingana nayo. Aliwakumbusha wajumbe kwamba kwa kujipamba vizuri na mwenendo wao wenyewe, watu wa Yehova wanadhihirisha maendeleo ambayo wamefanya katika kusema lugha iliyo safi.

“Lugha Iliyo Safi kwa Ajili ya Mataifa Yote”

Kwa kufaa, hotuba ya msingi ya mkusanyiko ilikazia kichwa kilichotangulia. Kilikuwa juu ya msingi wa Sefania 3:9, ambapo Mungu aliahidi hivi: “Hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la BWANA [Yehova, NW], wamtumikie kwa nia moja.” Lugha iliyo safi inahusisha uelewevu ufaao na uthamini wa ukweli juu ya Mungu na makusudi yake. Ni Yehova pekee awezaye kuandaa hilo kwa njia ya roho takatifu yake. Ni lazima kupenda ukweli kuwe ndicho kichocheo cha kujifunza lugha iliyo safi, ambayo haina ukosefu wote wa usafi wa kiadili.

Zaidi ya hilo, kusema lugha iliyo safi si shauri la kutumia msamiati fulani tu. Bali, njia yetu ya maisha ni lazima iafikiane na yale yatokayo katika midomo yetu. Kwa uhakika, hali ya sauti yetu, hali ya uso, na ishara ni za maana pia, kwani zinaonyesha tulivyo kwa ndani. Ili kuendelea vizuri na lugha iliyo safi, ni lazima tuwe na programu isiyogeukageuka ya kujifunza na kuhudhuria kwa ukawaida mikutano yote ya kundi.

Kujifunza Lugha Iliyo Safi

Kama vile hotuba moja alasiri ya Jumanne ilivyokazia, kujifunza lugha iliyo safi kwamaanisha “Kuendelea Kutoka Kwenye Mambo ya Msingi na Kufikia Ukomavu.” Ukuzi wahitajiwa sana ndipo tuendelee kusitawi kiroho. Hiyo yamaanisha kujifaidi na maandalizi yote ya mwendeleo wa kiroho na kutumia kanuni za Biblia kila siku.

Ili kuwa mahiri katika lugha iliyo safi, ni lazima kuwa “Waliofunzwa na Yehova,” kichwa cha mfululizo wa asubuhi ya Jumamosi. Msemaji wa kwanza alionyesha jambo hili ‘Kama Lilivyotolewa Kielelezo na Yesu.’ Kwamba Yesu alifundishwa na Yehova ilionekana wazi kutokana na maneno na vitendo vyake. Hivyo basi sisi twataka kumwiga katika jinsi alivyofundisha. Na kama vile Yesu alivyonyenyekea sikuzote mapenzi ya Baba yake, ndivyo ilivyo lazima kwa sisi.

Wasemaji watatu waliofuata walionyesha jinsi Yehova hufundisha kwa njia ya mikutano na makusanyiko. Sisi hunufaika kutokana na mikutano yote mitano ya kundi na hatupaswi kupuuza wowote wayo. Kila mkutano ni muhimu kwa mwendeleo wetu wa kiroho. Pia Yehova hutufundisha kwa njia ya programu za kusanyiko la mzunguko, mkusanyiko wa wilaya, na siku ya kusanyiko la pekee. Ili kunufaika kutokana na zote hizi, ni lazima tusikilize kwa makini halafu tuzoee mambo tujifunzayo.

Mfululizo huu ulifuatwa na ile hotuba “Kudhabihu kwa Ajili ya Funzo la Binafsi.” Ili kupata wakati kwa ajili yalo, ni lazima tutii shauri kwenye Waefeso 5:15, 16 kununua wakati kutoka kwenye mambo yasiyo ya maana sana.

Mradi unaofaa wa kujifunza kwetu lugha iliyo safi ni wakfu na ubatizo. Ukweli huu ulikaziwa katika ile hotuba “Ubatizo wa Wale Wanaojifunza Lugha Iliyo Safi.” Lugha hii inaongoza wengi kwenye wakfu na ubatizo. Hata hivyo, ni lazima mtu baada ya hapo aendelee kufuata kigezo cha Yesu kwa kuzihubiri kwa bidii habari njema, kuuvaa utu mpya, na kuendelea kujitenga na ulimwengu.

Chakula Kigumu cha Kiroho

Pia wakusanyikaji walipendezwa sana kupokea chakula kigumu cha kiroho chenye msingi wa utimizo wa drama za kiunabii. Alasiri ya Alhamisi, hotuba mbili zilikuwa na msingi wa vichwa vilivyochukuliwa kutoka unabii wa Ezekieli. Ya kwanza, “Gari la Yehova la Kimbingu Liko Katika Mwendo,” ilieleza juu ya kichukuzi cha kimbingu chenye kutia hofu kikienda kasi kama umeme. Chafananisha tengenezo la kimbingu la Yehova, ambalo Mungu aelekeza kila hatua yalo kwa upendo, akilitumia kutekeleza makusudi yake. Ezekieli afananisha mabaki wapakwa-mafuta, hasa tangu 1919. Hasa tangu 1935 wameungwa na “umati mkubwa.”—Ufunuo 7:9, NW.

Hotuba iliyofuata ilikuwa na kichwa “Enda Sambamba na Tengenezo Lionekanalo.” Hakuna shaka kwamba tengenezo lionekanalo la Mungu linaenda sambamba na tengenezo lake la kimbingu lililo kama gari. Kama Ezekieli alivyofanya, watumishi wa Yehova leo ni lazima watimize kwa utii utume wao wa kiunabii kujapokuwa na kutojali, dhihaka, au hata upinzani. Kwenda sambamba huongoza kwenye baraka nyingi sasa na uhai wa milele katika ulimwengu mpya wa Mungu unaokaribia upesi-upesi.

Asubuhi ya Ijumaa, chakula kigumu cha kiroho kiliandaliwa pia kwa njia ya hotuba tatu zenye msingi wa Isaya sura ya 28. Ya kwanza ya hizi ilionyesha kwa maneno yenye kani kwamba walevi wa kiroho wa Israeli na Yuda za kale walifananisha walevi wa Jumuiya ya Wakristo. Na kama vile wale wa kwanza walivyopatwa na hukumu kali za Yehova, ndivyo na zile za Jumuiya ya Wakristo.

Hotuba iliyofuata, yenye kichwa “Kimbilio Lao Ni Uwongo!,” ilikuwa na onyo hili kali: Kama vile kutumaini kwa Yuda ya kale katika Misri kulivyothibitika kuwa kimbilio la ubatili, ndivyo na upatano wa Jumuiya ya Wakristo na serikali za kisiasa za siku yetu zitakuwa. Hotuba ya tatu juu ya Isaya sura ya 28, “Endelea Kuonya Juu ya Kazi ya Ajabu ya Yehova,” ilielekezwa kwa watu wa Mungu. Lile ambalo Yehova ataitenda Jumuiya ya Wakristo kwa kufaa laitwa la ajabu, kwa maana litakuja kama mshangao kamili kwake. Leo, Yehova ni taji la utukufu kwa kile kikundi kidogo cha Wakristo wapakwa mafuta na kwa wale “kondoo wengine” zaidi ya milioni nne. (Yohana 10:16) Msemaji alimalizia kwa maneno haya yenye kuchochea: “Bidii yetu, azimio, na uaminifu-mshikamanifu na vichangie sifa ya milele ya Mungu wetu mweza yote, Yehova!”

Kusema Lugha Iliyo Safi Kwamaanisha Kuonyesha Upendo wa Kidugu

Alasiri ya Jumatano wakusanyikaji walikaziwa kwamba kusema lugha iliyo safi kwamaanisha “Fikiria Mayatima na Wajane Katika Dhiki Yao.” Wavulana wasio na akina baba waweza kusaidiwa kwa kupokea mazoezi ya kibinafsi. Twaweza kuonyesha ufikirio kwa wajane kwa maneno yenye fadhili ya kitia-moyo, kwa kuwahusisha ndani ya utendaji wetu mbalimbali wa Kikristo na vikusanyiko vya kirafiki, na kwa kuwapa usaidizi wa kimwili ikiwa wanastahili na wamo kikweli katika uhitaji. Mahoji yalionyesha jinsi mambo haya yalivyokuwa yakifanywa.

Alasiri ya Alhamisi, hotuba nyingine yenye kuchangamsha moyo ilionyesha “Jinsi Wakristo Hujali Mmoja na Mwenzake.” Mashahidi wa Yehova wana rekodi nzuri ya kutunzana mmoja na mwenzake, hasa wakati misiba kama tufani na matetemeko yatokeapo, wakati ambapo kuna uhitaji wa kuandikia maofisa, au wakati kuna mahitaji ya mahali. Lakini wakati magumu yatokeapo kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu, twapaswa kutumia kanuni zenye kuhusika katika shauri la Yesu kwenye Mathayo 5:23, 24 na 18:15-17. Hasa wakati mipango ya kibiashara ihusikapo kati ya akina ndugu kuna uhitaji wa kuheshimiana na kujizoeza uangalifu ili wala mwajiri wala mwajiriwa asitumie uhusiano wa kiroho kujifaidi kwa ubinafsi.

Kusema Lugha Iliyo Safi Kwamaanisha Kuchunga Mwenendo Wetu

Uhitaji wa kuchunga mwenendo wetu ulikaziwa-kaziwa. Hivyo, msemaji wa kwanza alasiri ya Jumanne alihutubu juu ya kichwa “Kusikia na Kushika Neno la Mungu.” Alionyesha kwamba kuna sababu mbili kubwa za kuja kwetu kwenye mikusanyiko: kutwaa maarifa sahihi na kuchochewa kutenda kwa kutegemea maarif hayo.

Hotuba ya kwanza asubuhi ya Jumatano ilitokeza lile swali lenye kupekua moyo “Kristo ‘Alichukia Uvunjaji-Sheria’—Vipi Wewe?” Haitoshi kupenda uadilifu. Ni lazima pia tuchukie kutotii sheria ili tuwe na dhamiri njema, kudumisha uhusiano mwema na Yehova, kuepuka kuleta suto juu ya jina lake, na kuepuka kuvuna matunda ya kutotii sheria—ufisadi na kifo.

Yenye kuhusiana kwa ukaribu na kichwa hicho ilikuwa hotuba iliyofuata, yenye kichwa “Kataa Mawazio ya Kilimwengu, Fuatia Uhalisi wa Ufalme.” Shetani, Hawa, na malaika walioanguka wote walifuatia mawazio kwa angamio lao. Mawazio ya kilimwengu, yenye ndoto za kufuatia vitu vya kimwili au yale yenye kushughulika na mambo haramu, hutokeza mzinduko ikiwa pia si utendaji kosa zito. Ili kukinza mawazio haya, ni lazima tufuatie mambo halisi ya Ufalme kwa njia ya funzo, sala, hudhurio la mikutano, na huduma ya peupe.

Ili kuishi maisha za Kikristo zenye unyoofu, ni lazima pia tutii shauri lililotolewa alasiri Jumatano katika hotuba “Wakristo—Ishini Kulingana na Uwezo Wenu wa Kifedha.” Kutofanya hivi bila shaka kutakuwa na matokeo yenye madhara kimwili na kiroho pia. Mwendo wa hekima ni mtu kuzuia tamaa zake za ubinafsi kwa kutoingia bila sababu katika deni la bure na kwa kupanga matumizi yawezekanayo ya fedha halafu kushikamana nayo. Nyakati zote twahitaji kusitawisha ujitoaji kimungu. Pamoja na kuridhika, hii ni njia ya pato kubwa.—1 Timotheo 6:6-8.

Umaana wa kuangalia mashirika yetu ulikaziwa katika hotuba ya Jumanne “Je! Marafiki Wako Ni Marafiki wa Yehova?” Marafiki zetu wapaswa kuwa Wakristo ambao wamevaa utu ulio kama wa Kristo na ni wenye bidii katika kazi ya kuhubiri. Wajuani wa kilimwengu si rafiki za Mungu, nasi hatuwezi kufanya urafiki nao bila kujidhuru sisi wenyewe. Hata ndani ya kundi, ni lazima tuwe wachaguzi ikiwa mashirika yetu yatakuwa yenye kujenga kikweli.

Shauri lililotangulia kuhusu mwenendo lilikaziwa wazi sana na drama ya ki-siku-hizi. Ilikuwa na kichwa “Kukabiliana Na Vitendo vya Kiufundi vya Ibilisi.”

Shauri la Lugha Iliyo Safi kwa Familia

Yenye kuhitajiwa sana ilikuwa hotuba ya Jumatano “Wazazi—Timizeni Wajibu Wenu!” Ni lazima wazazi wenyewe wajue mapenzi ya Mungu na kuwa wakiyafanya kwa kadiri ya uwezo wao. Ni lazima pia wakazie Neno la Mungu katika watoto wao. Zaidi ya hilo, haitoshi kupeleka watoto kwenye mikutano ya Kikristo tu na nje katika huduma ya shambani. Ni lazima wafundishwe kumpenda Yehova na kuiona hekima yenye mafaa ya kufanya mambo ya kimungu.

Ndipo ukaja mfululizo juu ya “Familia Katika Siku Yetu.” Msemaji wa kwanza alionyesha kwamba familia ilianza na Mungu. Ni lazima akina baba wawasiliane vizuri kuhusu mambo ya kiroho. Ni lazima akina mama wawe wapamba nyumba wazuri, na ni lazima watoto waonyeshe staha kwa Yehova kwa kushirikiana na wazazi wao.

Msemaji aliyefuata alionyesha kwamba familia iko “Chini ya Shambulio la Washindani.” Mikazo ya kiuchumi inaleta hasara zayo. Mahali pa kazi pana wingi wa majaribu ya kufanya kosa, na mambo yenye kuonyeshwa katika vyombo vya habari yamejaa jeuri, ngono haramu, na huvutia ufuatiaji wa vitu vya kimwili. Ni lazima mafundisho yaanze mapema, na bidii kubwa ya uendelevu inatakiwa ili kushinda mavutano ya kilimwengu. Ni lazima utumizi mzuri ufanywe wa vyombo vya kitheokrasi ambavyo huandaliwa na Watch Tower Society.

Hotuba iliyofuata, yenye kushughulika na “Kuhifadhiwa Kwayo [Familia] Kuingia Katika Ulimwengu Mpya,” ilikazia lile daraka zito ambalo wazazi wanalo. Kuzoeza watoto ni lazima kufanywe kwa bidii kubwa kabisa. Shauri zuri lilitolewa kuhusu mafunzo ya Biblia ya kifamilia na mambo gani ya kujifunza, yote haya kwa kusudi la kufikia mioyo ya watoto. Hapo tu ndipo wazazi na watoto waweza kutumainia kuhifadhiwa ndani ya ulimwengu mpya wakiwa familia.

Kutoa shauri zuri kwa hali ya familia ambamo Mashahidi wengi hujikuta ilikuwa ndiyo hotuba “Kuiweza Hali Katika Nyumba Iliyogawanyika.” Wale walio katika hali za jinsi hiyo walishauriwa wasikate tumaini kamwe la kwamba huenda siku fulani asiye mwamini akawa mwamini. Tumia wakati na mwenzi asiyeamini na uhakikishe kwamba wayatimiza yote yatakiwayo na mwenzi Mkristo. Waweza kupata msaada kutoka kwa wazee au labda kutoka kwa wengine katika nyumba zilizogawanyika.

Kusema Lugha Iliyo Safi kwa Wengine

Kwa kufaa sana, uangalifu mwingi ulielekezwa kwenye kutumia kwetu fursa za kufundisha wengine lugha iliyo safi. Hivyo, asubuhi ya Jumatano wakusanyikaji waliisikia hotuba “Tumia Wakati Wako Wenye Thamani kwa Hekima.” Ili kufanya hivyo ni lazima tuweke mambo ya kutangulizwa kwanza, kupatana na Mathayo 6:33, NW, ambayo yasema hivi: “Endeleeni, basi, kutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.” Hiyo yatia ndani kuweka kando wakati wa funzo la Biblia la kibinafsi, kuhudhuria mikutano yote, na kuwa wa kawaida katika huduma ya shambani. Hii yataka kwamba tununue wakati kutoka kwenye utendaji usio wa maana sana ingawa ni wenye kufurahisha. Mahoji fulani yalionyesha jinsi watu fulani walivyokuwa wakifanya jambo hili.

Ni lazima tusisahau kamwe kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova. Alasiri ya Alhamisi, maonyesho kadhaa yalikazia umaana wa jambo hilo chini ya kichwa “Fuliza Kunena Lugha Iliyo Safi Kwenye Kila Pindi.” Maonyesho haya yalionyesha jinsi hili laweza kufanywa katika kutoa ushahidi barabarani, katika kutoa ushahidi vivi hivi, na kwa utumizi wa simu. Upendo usio na ubinafsi kwa Yehova Mungu na jirani yetu utatuchochea tuseme lugha iliyo safi kwenye kila fursa.

Wenye kuhusiana kwa ukaribu na kichwa hiki ulikuwa utoaji uliofuata, “Mibaraka ya Wale Wasiotoa Udhuru wa Kuacha.” Kwa utofautiano mkubwa na Jumuiya ya Wakristo lipo tengenezo la ufundishaji la Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Mmoja mmoja, ni lazima tukinze misongo yote, kama upinzani wa kiserikali, ubaridi wenye kuenea sana, na matatizo ya kiuchumi. Maonyesho yenye msingi wa kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko yalionyesha jinsi mikazo hii yaweza kushindwa.

Pia yenye kutia moyo kuhubiri kwa bidii ilikuwa ile drama ya Biblia Kufanya Mapenzi ya Mungu kwa Bidii. Ilionyesha jinsi Yehu mwenye bidii alivyokuwa upande wa jina la Yehova na jinsi lilivyo jambo la maana kwetu kuonyesha moyo mkuu kama huo na bidii kwa ajili ya kazi ya Mungu.

Vitolewa vya Mkusanyiko

Kulikuwako vitolewa viwili vya kutokeza katika Kiingereza na Kijerumani wakati wa mkusanyiko. Cha kwanza cha vichapo hivi kilitolewa pamoja na ile hotuba yenye kichwa “Kuokoa Uhai Wako kwa Damu—Jinsi Gani?” Kwanza msemaji alieleza hatari zenye kushirikishwa na kutiwa damu mishipani. Alionyesha kwamba kuna njia nyingi za kutumiwa badala ya damu katika kujazia potezo la damu. Lakini Mashahidi wa Yehova hushika mwiko wa damu si kwa sababu ni isiyo ya kiafya bali kwa sababu si jambo takatifu kuikubali. Wao huepuka, si kwa sababu huenda damu ikawa ina uchafuzi, bali kwa sababu ni ya thamani kwa Mungu. Damu yenye kuokoa uhai kweli kweli ni ile damu ya ukombozi ya Yesu Kristo. Kwa kumalizia msemaji alipendeza wasikilizaji wake wote kwa kutoa ile broshua ya kurasa 32 Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako?

Kitolewa cha pili chenye thamani kilikuwa kuhusiana na ile hotuba “Mtafuteni-Tafuteni Yehova, Enyi Watu.” Sana-sana, watu hawamtafuti-tafuti Mungu. Kuwako kwa dini tofauti nyingi kwaonyesha jinsi binadamu ametafuta-tafuta Mungu mahali pasipofaa kwa sababu amepuuza Neno la Mungu. Kama ionwavyo kulingana na ripoti zetu za Ukumbusho kila mwaka, mamilioni wahitaji kusaidiwa kuchukua msimamo wao kwa ajili ya Yehova. Isaya 55:6, 7 yaonyesha kwamba kwa kweli Yehova ni Mungu mwenye upendo na mwenye rehema, aliye tayari ‘kusamehe kabisa.’ Tukiwa Mashahidi, tumepewa lugha iliyo safi ili tuweze kusaidia wengine wajiunge nasi katika kumtumikia Yehova bega kwa bega.

Leo, watu wa Yehova waelekewa na tatizo kwa sababu ya harakati za ujumla ya idadi za watu. Tokeo ni kwamba, dini za aina zote huenda zikadaiwa kufuatwa na watu katika eneo letu. Ili tuweze kusaidia Wahindu, Wabuddha, Washinto, na wale wa dini nyingine nyingi, Sosaiti imeandaa kile kitabu kizuri cha kurasa 384 Mankind’s Search for God (Jitihada ya Ainabinadamu Kutafuta-tafuta Mungu). Hicho hutokeza kimamlaka mafundisho ya msingi ya dini kubwa-kubwa zilizo nje ya Jumuiya ya Wakristo. Lakini pia chafuatia rekodi ya dini bandia ndani ya Jumuiya ya Wakristo. Kitabu hiki chaweza kufungua njia ya kuanzisha mafunzo ya Biblia na watu wa dini nyingi tofauti.

Hotuba ya Watu Wote na Maelezo ya Kumalizia

“Unganishweni na Lugha Iliyo Safi” kilikuwa ndicho kichwa cha hotuba ya watu wote. Msemaji alionyesha kwamba ingawa lugha elfu tatu sasa zatenda kuwa kizuizi cha umoja, lugha iliyo safi ni kani hodari ya kuunganisha. Imelinda Mashahidi wa Yehova dhidi ya makosa ya Kibabuloni, imewafundisha kustahi utakato wa uhai na damu, na imewasaidia kuishi kulingana na kanuni za Biblia ambazo huwanufaisha kiroho na kimwili. Wote wahitaji kuhangaikia kujifunza na kusema lugha iliyo safi, kwa maana ni wale tu wanaofanya hivyo watakaookoka Har–Magedoni. Hakuna wakati wa kupoteza katika kutii shauri lililo kwenye Sefania 2:1-3.

Baada ya shauri fulani zuri la Kimaandiko juu ya uhitaji wa “Kuwa Wenye Kukesha kwa Habari ya Sala,” yakaja maelezo ya kumalizia msingi wayo ukiwa ni kichwa “Kutembea kwa Kupatana na Lugha Iliyo Safi.” Idadi ya wale ambao sasa wanatembea kulingana na lugha iliyo safi inaongezeka kikweli. Na staha kwa lugha iliyo safi ilionyeshwa na wale wenye kuhudhuria mikusanyiko hii kwa usafi wao, utaratibu, na upatano wa kitengenezo. Vichapo vipya vilivyotolewa vitasaidia Mashahidi wa Yehova wote waeneze lugha iliyo safi kwa matokeo zaidi.

Msemaji wa mwisho wa mkusanyiko alikumbusha wote juu ya uhitaji wa uvumilivu. Alionyesha kwamba kama tokeo la mkusanyiko huu, wote wapaswa kuimarishwa katika azimio lao la kusonga mbele. Ndipo akamalizia kwa maneno: “Na tuendelee kutembea kupatana na lugha iliyo safi iliyotolewa na Mungu ili tuweze kutukuza Baba yetu mwenye upendo wa kimbingu, Yehova Mungu, sasa na hata milele!”

[Sanduku katika ukurasa wa 26]

Hudhurio la kilele kwenye mkusanyiko katika Berlin Magharibi lilikuwa 44,532, na 1,018 walibatizwa. Iliwachukua wabatizwa dakika 19 kumiminika wakitoka katika Stediamu Olympia, na katika wakati huo kulikuwa na makofi yenye kuendelea. Kulikuwa na sehemu ya pekee kwa ajili ya wajumbe wenye kusema Kiingereza. Wapatao 6,000 kati yao walisikia programu nzima katika lugha yao. Kwenye mkusanyiko huu, kulikuwako pia 4,500 kutoka Polandi; wakati wa saa mbili za mchana-kati, washiriki wa Baraza Linaloongoza walitoa hotuba fupi kwa manufaa yao.

[Picha katika ukurasa wa 24]

1. Stediamu Olympia, Berlin Magharibi

2. Programu iliyochapwa ya mkusanyiko

3. Basi mia mbili zilileta wajumbe kutoka Ujerumani Mashariki

4. Wakusanyikaji Wapolandi walifurahi kupokea vitolewa vilivyochapwa

5. Mapambo ya maua yalitia upendezi katika tamasha

6. A. D. Schroeder, mmoja wa washiriki wa Baraza Linaloongoza akiwa katika programu katika Berlin Magharibi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki