Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 4/1 kur. 20-25
  • Lugha Safi Kwa Ajili Ya Mataifa Yote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lugha Safi Kwa Ajili Ya Mataifa Yote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Zawadi ya Usemi
  • Uhitaji wa Lugha Safi
  • Wale Wenye Kupewa Lugha Iliyo Safi
  • Yanayotakwa Kwetu kwa Kujifunza Lugha Hiyo
  • Unganishweni Na Lugha Iliyo Safi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Unazungumza Ile “Lugha Safi” kwa Ufasaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Semeni Lugha Iliyo Safi Mkaishi Milele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Lugha ya Watu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 4/1 kur. 20-25

Lugha Safi Kwa Ajili Ya Mataifa Yote

“Hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la BWANA [Yehova, NW], wamtumikie kwa nia moja [bega kwa bega, NW].”—SEFANIA 3:9.

1, 2. (a) Kwa utimizo wa Sefania 3:9, Yehova anafanya nini katika siku yetu? (b) Ili kuelewa jinsi unabii wa Sefania hutuathiri, ni maswali gani yahitaji kujibiwa?

YEHOVA MUNGU anatimiza katika siku yetu kazi iliyo nzuri kweli kweli. Anaunganisha watu kutoka mataifa yote. Kama vile alivyotabiri zamani za kale katika Neno Takatifu lake, anafanya hivyo kwa kuwafundisha lugha safi.—Sefania 3:9.

2 Ni nini lugha hiyo? Kwa nini yahitajiwa kabisa? Kujifunza hiyo kwataka nini kwa sisi binafsi?

Zawadi ya Usemi

3. (a) Adamu alijaliwa zawadi gani nzuri sana? (b) Ni lugha gani ambayo Adamu alisema?

3 Uwezo wa kuwasiliana kwa njia ya usemi ni zawadi ya kimungu ambayo huweka aina ya kibinadamu wakiwa tofauti na uumbaji wote wa wanyama. Mwanadamu wa kwanza, Adamu, aliumbwa akiwa na akili yenye uwezo wa kufikiri mambo ya utimamu. Alijaliwa na viungo vya kufanyiza sauti, ulimi, na midomo ambayo ingeweza kutumiwa kwa usemi, na pia msamiati na uwezo wa kuunga maneno mapya. Adamu angeweza kufahamu wakati Yehova aliposema naye, na Adamu, kwa zamu yake, angeweza kueleza mawazo yake kwa maneno. (Mwanzo 1:28-30; 2:16, 17, 19-23) Lugha aliyopewa Adamu kwa wazi ilikuwa ile ambayo baadaye ilikuja kujulikana kuwa Kiebrania. Kwa angalau miaka ya kwanza 1,757 ya kuwako kwa binadamu, kwa wazi, ainabinadamu wote waliendelea kusema lugha moja hiyo.—Mwanzo 11:1.

4. Matukio katika siku za Nimrodi yaliathirije lugha ya kibinadamu?

4 Halafu, katika siku za Nimrodi, ili avuruge jitihada za wanadamu waovu, Yehova alivuruga lugha ya wote waliokuwa wamejiruhusu waundwe kuwa kikundi cha kushiriki katika kujenga mnara wa Babeli. (Mwanzo 11:3-9) Yaonekana kwamba kwanza Yehova alifutilia mbali kumbukumbu lote la lugha yao moja ya hapo awali halafu akaanzisha lugha mpya-mpya katika akili zao. Hiyo ilihusisha si misamiati mipya tu bali pia sarufi zilizo mpya na vigezo vipya vya mawazo. Kutokana na lugha ambazo Yehova alianzisha huko Babeli, nyingine zilisitawi hatua kwa hatua mpaka ikawa kwamba leo, kulingana na vyuo vya lugha, ndimi kama elfu tatu husemwa kotekote duniani.

5. Twaweza kujuaje yahusikayo katika badiliko la ‘kurudishiwa lugha safi’?

5 Kwa watu wanaosema lugha zote hizi, je! badiliko la ‘kurudishiwa lugha safi’ lingetaka kwamba waache ulimi wao wa kienyeji na kujifunza ile lugha ya asili ambayo Mungu alimpa Adamu? Hali zilizozunguka kutolewa kwa unabii huo zasaidia kujibu swali hilo.

Uhitaji wa Lugha Safi

6-8. (a) Ni hali gani ya kidini iliyokuwa imesitawi katika Yuda kabla ya kutolewa kwa unabii wa Sefania 3:9? (b) Katika mataifa yenye kuzunguka Yuda, ni maoni gani yaliyokuwapo sana?

6 Ufalme wa Yuda ulikuwa hivi majuzi umetawalwa kwanza na Manase halafu na Amoni, ambao walikuwa wameweka madhabahu kwa Baali, wakatumia uaguzi, na kuendeleza mazoea ya kuwasiliana na roho waovu. (2 Wafalme 21:1-6; 2 Nyakati 33:21-23) Kutokana na hilo, wakati wa utawala wa mwana na mwandamizi wa Amoni, Yosia, Yehova alimpa nabii wake Sefania utume wa kuonya kwamba hukumu ya kimungu ingefikilizwa juu ya bara hilo.—Sefania 1:1, 2.

7 Hata ingawa Wayudea walijua kutokana na historia yao wenyewe na kutokana na Maandiko yaliyopuliziwa roho kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli, walikuwa wakijitia katika desturi za ukosefu wa adili za ibada ya Baali. Waliinamia jua na mwezi na vikundi vya nyota za zodiaki, jambo ambalo lilivunja moja kwa moja sheria ya Mungu. (Kumbukumbu 4:19; 2 Wafalme 23:5) Juu ya yote haya, walikuwa wakishiriki katika namna fulani ya kuchanganya imani, kutenda kana kwamba dini yote ilikuwa sawa, kwa kufanya viapo kwa Yehova na pia kwa jina la mungu bandia Malkamu. Maoni yao yalikuwa kwamba “BWANA [Yehova, NW] hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.” (Sefania 1:4-6, 12) Kwa habari ya mataifa yenye kuzunguka Yuda, wote walikuwa na kumbukumbu la kupinga Yehova na watu wake, basi wao pia walikuwa katika mstari wa kufikiliziwa haki ya kimungu.—Sefania 2:4-15.

8 Ni dhidi ya hali ya matukio ya jinsi hiyo kwamba Yehova alitabiri kwamba ‘angewarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la Yehova, wamtumikie kwa nia moja [bega kwa bega, NW].’ (Sefania 3:9) Basi, ni nini lugha safi hiyo?

9. (a) Kwa nini lugha iliyo safi si Kiebrania wala Neno la Mungu lililoandikwa tu? (b) Ni nini lugha safi hiyo, nayo yaathirije maisha za wale waisemao?

9 Je! ni lugha ya Kiebrania? Sivyo; watu wa Yuda tayari walikuwa nacho, lakini mambo waliyokuwa wakisema na kutenda kwa wazi hayakuwa safi na manyoofu katika macho ya Yehova. Na lugha iliyo safi si Neno la Mungu tu. Wao walikuwa na hilo pia. Lakini walichohitaji kilikuwa ni uelewevu ufaao wa ukweli juu ya Mungu na makusudi yake, na ni Yehova peke yake ambaye angeweza kuuandaa kwa njia ya roho yake. Walipojifunza kusema lugha safi hiyo, kufikiri kwao, usemi wao, mwenendo wao, yote hayo yangetegemea hasa utambuzi wa uhakika wa kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli mmoja tu. (Sefania 2:3) Wao wangeweka tumaini lao katika yeye na kuipa enzi kuu yake utegemezo kamili. Hilo ni jambo la upendezi wa pekee kwetu leo. Kwa nini?

Wale Wenye Kupewa Lugha Iliyo Safi

10. Ni katika kipindi gani unabii wa Sefania 3:9 ulikuwa ukija kutimizwa?

10 Ikielekeza kwenye utimizo wa unabii wakati wa kipindi fulani hususa, Sefania 3:9 yasema hivi: “Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi.” Hapo lini? Mstari wa 8 wajibu kwamba ni katika wakati ambapo Yehova ‘anawakusanya mataifa,’ kabla ‘hajawamwagia ukali wa hasira yake,’ kwamba yeye awapa wasikivu wa dunia badiliko la kuja kwenye lugha safi.

11. (a) Ni matimizo gani mawili ambayo Sefania 3:9 ilikuwa nayo kabla ya nyakati za ki-siku-hizi? (b) Ni jinsi gani utimizo wao leo ulivyo tofauti?

11 Katika siku za Mfalme Yosia, kabla Yehova hajaruhusu majeshi ya Kibabuloni yafikilize hukumu, wengi waliacha ibada bandia na, badala yayo, wakatumikia Yehova. (2 Nyakati 34:3-33) Tena, katika karne ya kwanza W.K., kabla Yerusalemu halijaharibiwa na Waroma, maelfu ya watu walijifunza ukweli juu ya Mungu na kusudi lake wakaunganika katika utumishi wake. Wakati huo lugha ya ukweli ilitajirishwa sana na mambo ambayo Yesu Kristo alifanya kwa utimizo wa kusudi la Yehova. Lakini ni katika siku yetu wenyewe kwamba unabii wa Sefania unatimizwa katika tufe lote. Mataifa yote sasa yanakusanywa kwenye vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Mkusanyo huo umekuwa ukiendelea tangu kuzaliwa kwa Ufalme katika 1914. Na ni katika kipindi hiki hiki kwamba Yehova amekuwa akizipa jamii za watu ulimwenguni pote badiliko la lugha safi kwa utimizo wa unabii huu. Kujifunza lugha hiyo ni jambo la muhimu sana kwa sababu waokokaji wa dhiki kubwa inayokuja watakuwa watu ambao wamefanya kweli kweli lugha safi hiyo iwe lugha yao.—Yoeli 2:32.

12. (a) Njozi iliyoandikwa kwenye Isaya 6 ina uhusiano gani na unabii unaohusu lugha safi? (b) Kwa nini mabaki wapakwa-mafuta walihitaji msaada ikiwa wangeendelea kukubalika kwa ajili ya utumishi wa Yehova?

12 Kupatana na hilo, ilikuwa mapema katika kipindi kilichofuata Vita ya Ulimwengu ya 1 kwamba Yehova akaanza kufungua macho ya uelewevu ya watumishi wake wapakwa-mafuta yaone ile njozi nzuri sana iliyoandikwa kwenye Isaya sura ya 6. (Mistari 1-4) Njozi hiyo yakazia umaana wa kuwa kwetu na midomo safi ili tumtumikie Yehova kwa kukubalika. Yaonyesha kwamba, katika maana bora kabisa, Yehova ni mtakatifu. Ni lazima watumishi wake pia waonyeshe sifa hiyo. (1 Petro 1:15, 16) Lakini mabaki wapakwa-mafuta walihitaji msaada katika jambo hilo. Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya 1, kwa kadiri fulani walikuwa wamejiruhusu watiwe madoa kwa kuhusika katika mambo ya ulimwengu. “Kicho cha BWANA [Yehova, NW] ni kitakatifu,” au safi, lakini wao walikuwa wameacha hofu ya binadamu na matengenezo ya kibinadamu iathiri midomo yao, ikinyamazisha kupiga kwao mbiu ya Neno la Mungu kwa kadiri kubwa. (Zaburi 19:9) Kwa kupashana habari na Jumuiya ya Wakristo, mabaki walikuwa bado wametiwa uchafu na mengine ya mapokeo na mazoea yake.

13, 14. (a) Mabaki walionyeshaje maoni yafaayo, na ni kitendo gani ambacho Yehova alichukua kwa ajili yao? (b) Ni kwa njia gani Yehova aliwapa mabaki lugha safi?

13 Wakitambua hali yao, mabaki walisema, kama alivyosema nabii Isaya: “Ole wangu! kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, BWANA [Yehova, NW] wa majeshi.” (Isaya 6:5) Walitambua kwamba hali yao ilikuwa isiyokubalika. Hawakudumu kwa unyonge katika mwendo wenye makosa wala hawakukataa kwa shingo ngumu kukubali karipio la Yehova. Hawakujiunga na makasisi wakati hawa walipotoa utumishi wa mdomo tu kwa Ufalme wa Mungu halafu wakaunga mkono Ushirika wa Mataifa kana kwamba ulikuwa ndio Ufalme huo.

14 Kwa sababu ya mtazamo wa kutubu wa mabaki wanyenyekevu hao, Yehova kwa fadhili zisizostahiliwa zake aliendelea na kutakasa midomo yao. Isaya 6:6, 7 yatuambia hivi: “Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.” Ujumbe wenye kusafisha kutokana na Neno la Mungu ndio ulioyaharibu kama kwa moto mapokeo na mafundisho ya wanadamu. Uliondosha katika mioyo yao uchafu wa hofu ya binadamu na kuweka mahali payo bidii yenye kuwaka ili watumie midomo yao kumheshimu Yehova. Hivyo Yehova alikuwa akitimiza ahadi yake ‘kuwarudishia mataifa lugha iliyo safi [kwa uhalisi, mdomo safi], wapate kuliitia jina la Yehova.’—Sefania 3:9.

15. Itikio la mabaki lilikuwaje kupatana na sababu ambayo Yehova aliwapa lugha iliyo safi?

15 Basi wakati jamii ya Isaya katika nyakati za ki-siku-hizi ilipoanza kusikia sauti ya Yehova ikiuliza, kama ilivyoandikwa kwenye Isaya 6:8: “Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” waliitikia kwa mteremo hivi: “Mimi hapa, nitume mimi.” Haikuwa rahisi kwa wote kuanza kazi katika huduma ya peupe, lakini walitaka kutumiwa na Mungu wakiwa jamii ya watu iliyo kwa ajili ya jina lake. Roho yake iliwaimarisha. Idadi zao ziliongezeka.

16. (a) Kuhubiri kwa mabaki kulizaa matokeo gani yasiyokuwa yametarajiwa? (b) Umati mkubwa hutoaje ushuhuda kwamba sasa wao pia wanena lugha iliyo safi?

16 Baada ya muda ikawa wazi kwamba kuhubiri kwao kulikuwa kukizaa matokeo yasiyotazamiwa. Kupitia wao, Yehova alikuwa akisaidia kikundi kingine kujifunza lugha iliyo safi. (Isaya 55:5) Hawa hawakushiriki tumaini la uhai wa kimbingu, lakini walihesabu kuwa pendeleo kuwa waandamani wa mabaki ya warithi wa Ufalme na kutumikia bega kwa bega pamoja nao wakiwa wapiga mbiu wa Ufalme wa Mungu. Hatua kwa hatua, hawa wametoka katika “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi,” mpaka sasa wanajumlika kuwa “umati mkubwa” ambao hesabu yao yafika mamilioni. Usemi wenye kutoka katika vinywa vyao si namna ile ambayo ingewatambulisha na chochote cha viasili vyenye mgawanyiko vya ulimwengu. Wao hawakazi matumaini yao juu ya binadamu yeyote wala tengenezo lolote la kibinadamu. Badala ya hivyo, wao “hufuliza kulia kwa sauti kubwa, kusema: ‘Wokovu wetu ni kwa Mungu wetu, ambaye ameketi juu ya kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.’”—Ufunuo 7:9, 10, NW.

Yanayotakwa Kwetu kwa Kujifunza Lugha Hiyo

17. Kwa nini ni jambo la maana tujifunze vema lugha iliyo safi na kufanya maendeleo katika uwezo wetu wa kuitumia?

17 Hata iwe ni muda gani ambao sisi tumekuwa pamoja na tengenezo la Yehova, kuna mengi tuwezayo kufanya tufanyie maendeleo maarifa yetu ya lugha iliyo safi na uwezo wetu wa kuyatumia vema. Ni jambo la maana kutia jitihada ya kufanya hivyo. Kwa nini? Kwa sababu huu ni wonyesho wa upendo wetu kwa ajili ya ukweli.

18, 19. (a) Tangu pale pale mwanzoni, kwa nini ni jambo la maana kusitawisha upendo imara kwa ajili ya ukweli? (b) Kwa nini ni jambo la maana kuendelea kukuza upendo huo?

18 Pale mwanzoni, upendo huo hutusaidia kufungua akili na moyo wa mtu hivi kwamba aweza kuelewa maandiko aonyeshwayo; humsukuma kumkaribia Yehova na kuthamini tengenezo Lake. Hivyo, kupenda ukweli ni ufunguo wa kujiweka huru na minyororo ya dini bandia. Watu fulani hudai kuwa na upendezi katika ujumbe wa Biblia lakini kwa kweli hawaachi mahusiano yote ya dini bandia na njia yayo ya maisha yenye uendekevu. Kwa nini sivyo? Kama ilivyoelezwa kwenye 2 Wathesalonike 2:10, wao ‘hawakubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.’ Ni jambo muhimu kama nini tuwe na upendo huo!

19 Tukiisha kuukubali ukweli kwa moyo, kusitawisha kwetu upendo huo ni jambo kubwa lenye kusaidia ukuzi wetu wa kiroho. Zingatia akilini kwamba Yehova hurejezea ukweli kuwa “lugha.” Mtu ajifunzapo lugha mpya, huwa ni lazima atie jitihada ya bidii nyendelevu kujenga msamiati wake, kutamka maneno kwa usahihi, kujifunza hata mambo yaliyo madogo-madogo ya sarufi, na kadhalika. Kupenda ile lugha mpya na watu waisemao kutamsaidia azidi kufanya maendeleo. Huenda akaweza kusema lugha hiyo kwa kadiri fulani katika muda wa miezi michache, lakini huchukua miaka mingi ya jitihada ya kudhamiria ili aiseme kama mwenyeji. Jitihada ya namna hiyo hiyo yahitajiwa ili kumudu lugha iliyo safi.

20. (a) Ni nini hufanya lugha iliyo safi iwe safi kweli kweli? (b) Kwa nini uangalifu mkubwa wahitajiwa kwa upande wa kila mmoja wetu?

20 Hasa yastahili kuangaliwa kwamba lugha ambayo Mungu huwapa watumishi wake yasemwa kuwa safi. Hiyo ni kweli, si kwa sababu ya muundo wa kisarufi, bali kwa sababu hiyo hutoa ushuhuda wa kuwa na usafi wa kiadili na wa kiroho. Katika lugha hiyo hamna ruhusa ya kusema uwongo, udanganyifu, wala ulimi wenye hila. Wale wasemao lugha hiyo ni lazima waseme ukweli sikuzote. (Sefania 3:13; Waefeso 4:25) Ni lazima usemi wao vilevile uonyeshe viwango vya juu vya Yehova kuhusu adili ya ngono. (Waefeso 5:3, 4) Maandiko yatupasha habari pia kwamba kila kitu chenye kuhusiana na Babuloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini bandia, si safi. (Ufunuo 18:2-4) Ile mifano ya miungu yayo huitwa “vinyago” (sanamu-mavi, NW). (Yeremia 50:2, NW) Basi, kwa kufaa wale wajifunzao lugha iliyo safi ni lazima waondolee mbali vitu vyenye kuonekana vinavyohusiana na ibada bandia, wakatae mafundisho yayo, wajiweke huru na miadhimisho yayo, na pia waondoe kabisa katika usemi wao maneno yaonyeshayo fikira yayo yenye makosa. Zaidi ya hilo, kwenye Ufunuo 16:13-16, twafahamishwa kwamba propaganda inayokusanya mataifa katika upinzani na Ufalme wa Mungu si safi pia, kwa kuwa inapuliziwa roho na mashetani. Basi sisi twahitaji kuwa chonjo tusiache lolote la mambo haya yasiyo safi yaambukize usemi wetu.

21. Kuna nini kwenye lugha iliyo safi kuongezea maneno yasemwayo?

21 Ile tunayojifunza inaitwa lugha, na yaitwa hivyo kwa kufaa, lakini hiyo haimaanishi kwamba wale waisemao hujifunza tu jinsi ya kutumia semi zilizo kawaida kwa watu wa Yehova. Hali ya sauti, ishara za uso, na ishara za mwili ni za maana pia. Hizi huenda zikatoa ujumbe ambao maneno tu hayatoi. Mara nyingi hayo huonyesha kikweli jinsi tulivyo kwa ndani. Yaweza kuonyesha kama tumeng’oa wivu, magomvi, na mifoko ya hasira, zote hizo zikiwa ni kazi za mnofu wenye dhambi. Wakati roho ya Mungu ifanyapo kazi katika maisha zetu, tunda layo huwa wazi katika njia ambayo twawasiliana na wengine.—Wagalatia 5:19-23; Waefeso 4:31, 32.

22. Tujifunzapo vema lugha iliyo safi, hiyo huathirije kufanya kwetu maamuzi?

22 Yeyote ambaye amejifunza lugha mpya ajua kwamba hatua ya maendeleo halisi huwa imefikiwa wakati ajikutapo akifikiri kikweli katika lugha mpya hiyo, badala ya kutafsiri kutokana na ulimi wake wa kienyeji. Basi, pia, wakati sisi tujifunzapo ukweli, kutia jitihada ya bidii ya moyoni ili tuutumie katika maisha zetu, na kuushiriki kwa ukawaida pamoja na wengine, sisi hujikuta hatua kwa hatua tukifiri kupatana na ukweli. Hatuwi tukilinganisha milele yaliyo ya zamani na yaliyo mapya na kung’ang’ania kufanya uamuzi. Hata katika mambo madogo, kanuni za Biblia huja akilini kuandaa mwelekezo ambao wahitajiwa.—Mithali 4:1-12.

23. Hata ulimi wao wa kienyeji uwe nini, ni nini huonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova wote husema lugha iliyo safi duniani pote?

23 Ni kweli kwamba kuna maelfu ya lugha zitumiwazo na ainabinadamu, lakini lugha iliyo safi yaweza kuelezwa katika zote hizo. Kwa mwungamano, duniani pote, Mashahidi wa Yehova wanafanya utumizi mwema wa lugha iliyo safi watumikiapo bega kwa bega wakitoa ushahidi wa peupe ambao humletea heshima Yehova, Mungu wetu mwenye upendo.

Maswali ya Kupitia

◻ Ni nini ambacho chatiwa ndani ya zawadi ya usemi?

◻ Ni nini lugha iliyo safi?

◻ Ni kuelekea nani Sefania 3:9 imetimizwa?

◻ Twaweza kutoaje ushuhuda wa kwamba twapenda kweli kweli lugha iliyo safi?

[Picha katika ukurasa wa 23]

Wale wajuao lugha iliyo safi huishiriki pamoja na wengine

[Picha katika ukurasa wa 25]

Hata ulimi wao wa kienyeji uwe ni nini, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote husema lugha iliyo safi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki