Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 4/15 kur. 26-27
  • “Siku Ya Bwana”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Siku Ya Bwana”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Siku ya Bwana
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Siku ya Yehova
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • “Yesu Kristo Ni Bwana”—Jinsi Gani na Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kitabu cha Ufunuo—Kinamaanisha Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 4/15 kur. 26-27

“Siku Ya Bwana”

“KWA kuvuviwa [kupuliziwa roho] mimi nilikuja kuwa katika ile siku ya Bwana.” (Ufunuo 1:10, NW) Ndivyo alivyosema mtume Yohana aliyezeeka, anayeonyeshwa juu, katika sura ya kwanza ya kitabu cha Biblia cha Ufunuo. Maneno yake yanatusaidia kutambua wakati wa utimizo wa njozi tukufu ambazo aendelea kueleza.

Hata hivyo, si wote wanaokubali fasiri hiyo ya Ufunuo 1:10. Kwa mfano, mtafsiri Mjerumani Jörg Zink analifasiri hivi: “Nilijazwa kwa roho takatifu—ilikuwa Jumapili.” Hata hivyo, tafsiri za Biblia nyingi hutafsiri fungu la maneno ya Kigiriki teiʹ ky·ri·a·keiʹ he·meʹrai kuwa “siku ya Bwana.” Lakini katika kielezi-chini wengi hudai kwamba linarejezea Jumapili. Je, hilo ni sawa?

Herders Bibelkommentar, cha Kijerumani, kitabu cha marejezo cha Kikatoliki, kinaeleza sababu za kufikiri huku kinaposema hivi: “Rejezo linafanywa hapa [katika Ufunuo 1:10] si kwenye Siku ya Hukumu ya Mwisho, ambayo inajulikana pia kuwa ‘Siku ya Bwana,’ bali kwenye siku hususa ya juma. Wakristo wa mapema walianza kuadhimisha siku ya kwanza ya juma kuwa siku ya ibada zao za kanisa zenye maana mapema tangu katikati ya karne ya kwanza. (Mdo. 20:7; 1 Kor. 16:2)” Hata hivyo, maandiko hayo mawili yaliyonukuliwa na kitabu hicho cha marejezo hayathibitishi kwa njia yoyote kwamba Wakristo wa karne ya kwanza waliona siku ya kwanza ya juma kuwa “siku ya ibada zao za kanisa zenye maana.”

Andiko la kwanza, Matendo 20:7, linare-kodi tu kwamba Paulo, wenzi wake wa kusafiri, na Wakristo kutoka Troa walikusanyika pamoja siku ya kwanza ya juma kwa ajili ya mlo. Kwa kuwa Paulo alikuwa aondoke siku ya pili na hangewaona tena kwa muda mrefu, alitumia nafasi hiyo kusema nao kwa urefu.

Andiko la pili, 1 Wakorintho 16:2, liliwatia moyo Wakristo katika Korintho kuweka pesa kando “siku ya kwanza ya juma” ili kuwa na kitu cha kuchanga kwa wale wenye uhitaji katika Yudea. Mwanachuo Adolf Deissmann adokeza kwamba siku hiyo huenda ilikuwa siku ya malipo. Kwa vyovyote, dokezo la Paulo lilikuwa lenye kutumika, kwa kuwa pesa zingeisha katika juma.

Haijasemwa popote katika Biblia kwamba Wakristo katika wakati wa kimitume waliona siku ya kwanza ya juma, inayoitwa Jumapili sasa, kuwa namna fulani ya sabato ya Kikristo, siku iliyowekwa kwa ajili ya mikutano yao ya kawaida ya ibada. Ilikuwa baada ya kifo cha mitume tu kwamba Jumapili ilikuja kuonwa katika njia hiyo na ikaja kuitwa “Siku ya Bwana.” Hiyo ilikuwa sehemu ya ule uasi-imani uliotabiriwa na Yesu na mitume wenyewe.—Mathayo 13:36-43; Matendo 20:29, 30; 1 Yohana 2:18.

Kwa hiyo, basi “siku ya Bwana” ni nini? Maneno yanayotangulia na kufuata ya Ufunuo 1:10 yanaelekezea Yesu kuwa Bwana ambaye hiyo ni siku yake. Neno la Mungu linatambulisha usemi kama “siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo” na wakati wa hukumu kwa ainabinadamu na kurudishwa kwa Paradiso.—1 Wakorintho 1:8; 15:24-26; Wafilipi 1:6, 10; 2:16.

Kwa hiyo, Hans Bruns, katika tafsiri yake iliyo na maelezo, Das Neue Testament (Agano Jipya), yuko sahihi anaposema hivi: “Wengine hushikilia kwamba yeye [Yohana] anaongea juu ya Jumapili hapa, lakini inaelekea zaidi kwamba anarejezea ile Siku tukufu ya Bwana, ambayo kwa kweli hasa maelezo yake yote yanaihusu.” W. E. Vine asema hivi: “‘Siku ya Bwana’ . . . ni ile Siku ya wonyesho Wake wa hukumu juu ya ulimwengu.” Lexikon zur Bibel (Kamusi ya Biblia) ya Fritz Rienecker inasema kwamba kwa wazi “siku ya Bwana” inarejezea “siku ya hukumu.”

Ufahamu unaofaa wa huo usemi “siku ya Bwana” unatusaidia kufahamu kitabu chote cha Ufunuo. Tena, ushuhuda ni kwamba ile siku imeanza tayari. Kwa hiyo, inafaa kama nini kwamba ‘tuyasikie maneno ya unabii wa Ufunuo na kuyashika yaliyoandikwa humo’!—Ufunuo 1:3, 19.

[Picha katika ukurasa wa 27]

Elezo lililo wazi na la ki-siku-hizi la kila mstari katika kitabu cha Ufunuo linatolewa katika “Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!” Msaada huu wenye kuvutia unapatikana kutoka kwa Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki