Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 6/1 kur. 15-20
  • Kimbilio Lao—Ni Uwongo!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kimbilio Lao—Ni Uwongo!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Agano na Mauti (Kifo)”
  • Kukataa “Jiwe Lililojaribiwa”
  • Matumaini ya Ubatili kwa Amani
  • ‘Mungu Ni Kimbilio Letu’
  • Jumuiya ya Wakristo “Mahali pa Kukanyaga kwa Miguu”
  • Jina la Yehova “Ngome Imara”
  • Isaya Atabiri ‘Tendo la Ajabu’ la Yehova
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Wakisema “Amani” Wakati Haipo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Endelea Kuonya Juu ya Kazi ya Ajabu ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • ‘Pata Kimbilio Katika Jina la Yehova’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 6/1 kur. 15-20

Kimbilio Lao—Ni Uwongo!

“Tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu, tumejificha chini ya maneno yasiyo kweli”.—ISAYA 28:15.

1, 2 .(a) Ni tengenezo gani leo lapasa liangalie jambo lililotukia kwa ufalme wa Yuda wa kale? (b) Yuda ilikuwa na uhakika gani uliowekwa pasipofaa?

JE! MANENO hayo yatumika kwa Jumuiya ya Wakristo leo kama yalivyotumika kwa ufalme wa Yuda wa kale wa makabila mawili? Kwa hakika, yanatumika! Na ulinganifu huo huonyesha kimbele mabaya yatakayopata Jumuiya ya Wakristo ya ki-siku-hizi. Inamaanisha kwamba msiba mkuu utafikilia karibuni tengenezo hilo lililoasi imani.

2 Kaskazini mwa Yuda ulikuwako ule ufalme wa Israeli wa makabila kumi. Israeli ulipothibitika kuwa usioaminika, Yehova aliruhusu ushindwe na Ashuru katika 740 K.W.K. Ufalme dada yake, Yuda, ulijionea ushahidi wa tukio hilo lenye kuleta msiba, lakini kwa wazi ulifikiria kwamba jambo kama hilo halingeupata kamwe. ‘Kwani,’ viongozi wake wakajigamba, ‘je! si hekalu la Yehova lingali linatenda kazi katika Yerusalemu? Je! sisi si watu wa Yehova waliopendelewa?’ Je! si makuhani na manabii wetu husema katika jina la Yehova?’ (Linganisha Yeremia 7:4, 8-11.) Viongozi hao wa kidini walikuwa na uhakika kwamba walikuwa salama. Lakini walikosea! Walikuwa bila imani kama tu ndugu zao wa kaskazini. Kwa hiyo, kilichotukia kwa Samaria kingetukia kwa Yerusalemu pia.

3. Kwa nini Jumuiya ya Wakristo ina uhakika kwa habari ya wakati ujao, lakini, je, kuna sababu nzuri kwa uhakika wayo?

3 Kwa njia inayofanana na hiyo, Jumuiya ya Wakristo hudai kuwa na uhusiano wa pekee pamoja na Mungu. ‘Kwani,’ inajigamba, ‘sisi tuna makumi ya maelfu ya makanisa, na jamii ya makasisi wa kulipwa pamoja na mamia ya mamilioni ya wafuasi. Tuna Biblia pia, nasi hutumia jina la Yesu katika ibada yetu. Hakika, tunapendelewa na Mungu!’ Hata hivyo, yale yaliyotukia kwa Yerusalemu wa kale hufanyiza onyo kali. Yajapokuwa matukio ya karibuni ya kisiasa yasiyo ya kawaida, tunajua kwamba Yehova karibuni atatenda kwa njia ya mkataa dhidi ya Jumuiya ya Wakristo na dini bandia nyingine zote.

“Agano na Mauti (Kifo)”

4. Yuda ilifikiri ilikuwa imefanya agano gani?

4 Katika nyakati za kale, Yerusalemu usio na imani ulipokea maonyo mengi kupitia manabii wa kweli wa Mungu, lakini haukuyaamini. Badala ya hivyo, ulijigamba kwamba haungechukuliwa kamwe na kifo kuingizwa ndani ya Sheoli, kaburi, kama kilivyokuwa kimechukua ufalme wa kaskazini wa Israeli. Nabii Isaya alipuliziwa roho aseme kwa Yuda hivi: “Basi, lisikieni neno la BWANA [Yehova, NW], enyi watu wenye dharau, mnaowatawala watu hawa walio ndani ya Yerusalemu. Kwa sababu mmesema, Tumefanya agano na mauti, tumepatana na kuzimu [Sheoli, NW]; pigo lifurikalo litakapopita, halitatufikia sisi; kwa maana tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu, tumejificha chini ya maneno yasiyo kweli.”—Isaya 28:14, 15.

5. (a) Agano la kudhaniwa pamoja na kifo la Yuda lilikuwa nini? (b) Yuda ilikuwa imesahau onyo gani lililopewa Mfalme Asa?

5 Ndiyo, viongozi wa Yerusalemu walifikiria kwamba walikuwa na mapatano na kifo na Sheoli, ili kwamba jiji lao lingehifadhiwa. Lakini, je, agano la kudhaniwa la Yerusalemu pamoja na kifo lilimaanisha kwamba walikuwa wametubu dhambi zao na sasa walimtumaini Yehova kwa ajili ya wokovu? (Yeremia 8:6, 7) Sivyo hata kidogo! Badala ya hilo, waligeukia watawala wa kisiasa ili kupata msaada. Lakini kutegemea kwao rafiki za kilimwengu kulikuwa madanganyo, uwongo. Watu wa kilimwengu waliowatumaini hawangeweza kuwaokoa. Na kwa kuwa waliacha Yehova, Yehova aliacha Yerusalemu. Ilitukia kama vile nabii Azaria alikuwa ameonya Mfalme Asa: “BWANA [Yehova, NW] yu pamoja nanyi, mkiwa pamoja naye; nanyi mkimtafuta ataonekana kwenu; lakini mkimwacha atawaacha ninyi.”—2 Nyakati 15:2.

6, 7. Yuda ilichukua hatua gani ili kuhakikisha usalama wayo, lakini kukiwa na tokeo gani la mwisho?

6 Wakiwa na uhakika katika mapatano yao ya kisiasa, viongozi wa Yerusalemu walikuwa na hakika kwamba hakuna ‘pigo lifurikalo lenye kupita’ la majeshi yenye kuvamia lingekuja karibu nao kusumbua amani na usalama wao. Lilipotishwa na Israeli na Siria wakiwa katika upatano, Yuda liligeukia Ashuru kwa msaada. (2 Wafalme 16:5-9) Baadaye, lilipotishwa na majeshi ya Babuloni, liliitisha msaada kwa Misri naye Farao akaitikia, akatuma jeshi likasaidie.—Yeremia 37:5-8; Ezekieli 17:11-15.

7 Lakini majeshi ya Babuloni yalikuwa yenye nguvu mno, navyo vikosi vya Misri vikalazimika kuondoka. Uhakika wa Yerusalemu katika Misri ulithibitika kuwa kosa, na katika 607 K.W.K. Yehova aliuachilia uharibiwe kama alivyokuwa ametabiri. Kwa hiyo watawala na makuhani wa Yerusalemu walikosea! Tumaini lao katika mapatano ya kilimwengu kwa ajili ya amani na usalama yalikuwa ‘uwongo’ ambao ulifagiliwa mbali na pigo la gharika ya majeshi ya Babuloni.

Kukataa “Jiwe Lililojaribiwa”

8. Jumuiya ya Wakristo imechukuaje mahali panapofanana sana na pa Yuda ya kale?

8 Je! kuna hali inayolingana leo? Hakika, iko. Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo wanahisi pia kwamba hakuna maafa yatakayowafikia. Kwa kweli, wao husema kama vile Isaya alivyotabiri: “Tumefanya agano na mauti, tumepatana na kuzimu [kaburi]; pigo lifurikalo litakapopita, halitatufikia sisi; kwa maana tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu, tumejificha chini ya maneno yasiyo kweli.” (Isaya 28:15) Kama Yerusalemu wa kale, Jumuiya ya Wakristo hutegemea mapatano ya ulimwengu kwa ajili ya usalama, na makasisi wayo hukataa kupata kimbilio katika Yehova. Kwani, hata hawatumii jina lake, nao hudhihaki na kunyanyasa wale wanaoheshimu jina hilo. Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo wamefanya kama vile makuhani wakuu Wayahudi wa karne ya kwanza walivyofanya walipomkataa Kristo. Kwa kweli, wamesema, “Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.”—Yohana 19:15.

9. (a) Ni nani wanaoonya Jumuiya ya Wakristo leo katika njia ile ile ambayo Isaya alionya Yuda? (b) Jumuiya ya Wakristo yapasa kugeukia nani?

9 Leo, Mashahidi wa Yehova huonya kwamba gharika ya majeshi yenye kufisha karibuni itafagia Jumuiya ya Wakristo. Zaidi ya hilo, wao huelekeza kwenye mahali pa kweli pa kimbilio la kuiondokea gharika hiyo. Wananukuu Isaya 28:16, inayosema: “Bwana, MUNGU [Yehova, NW], asema hivi, Tazama, naweka jiwe katika Sayuni, liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani, msingi ulio imara; yeye aaminiye hatafanya haraka.” Ni nani huyo “jiwe la pembeni lenye thamani”? Mtume Petro alinukuu maneno hayo na kuyatumia kwa Yesu Kristo. (1 Petro 2:6) Kama Jumuiya ya Wakristo ingalikuwa imetafuta amani pamoja na Mfalme wa Yehova, Yesu Kristo, basi ingaliepuka furiko kubwa la gharika ijayo.—Linganisha Luka 19:42-44.

10. Jumuiya ya Wakristo imekuza mahusiko gani?

10 Lakini haijafanya hivyo. Badala ya hivyo, katika utafutaji wayo wa amani na usalama, inajiingiza katika pendeleo la viongozi wa kisiasa wa mataifa—inafanya hivyo lijapokuwa onyo la Biblia kwamba urafiki pamoja na ulimwengu ni uadui pamoja na Mungu. (Yakobo 4:4) Zaidi ya hayo, katika 1919 ilitetea kwa imara sana Ushirika wa Mataifa kuwa ndio tumaini bora zaidi kwa wanadamu kwa ajili ya amani. Kisha, tokea 1945 na kuendelea, iliweka tumaini layo katika Umoja wa Mataifa. (Linganisha Ufunuo 17:3, 11.) Kuhusika kwayo pamoja na tengenezo hilo ni kwa kadiri gani?

11. Dini ina uwakilisho gani kwenye UM?

11 Kitabu cha karibuni kinatupa dokezo kinapotaarifu hivi: “Matengenezo ya Kikatoliki yasiyopungua ishirini na manne yanawakilishwa kwenye UM. Viongozi kadhaa wa kidini wa ulimwengu wamezuru tengenezo hilo la kimataifa. Ziara zenye kukumbukwa zaidi ni ile ya Mtakatifu Papa Paul 6 wakati wa Kusanyiko Kuu katika 1965 na ya Papa John Paul 2 katika 1979. Dini nyingi zina maombi, sala, nyimbo za dini na ibada kwa ajili ya Umoja wa Mataifa. Mifano ya maana zaidi ni ile ya imani za Kikatoliki, Yunitaria-Yunivasali, Kibaptisti na Kibahai.”

Matumaini ya Ubatili kwa Amani

12, 13. Yajapokuwa matumaini yaliyoenea sana kwamba amani inaonekana katika wakati ujao, kwa nini Mashahidi wa Yehova wana uhakika kwamba maonyo yao ni ya kweli?

12 Mojawapo wa viongozi wa kisiasa mwenye mamlaka zaidi alirudisha mwangwi wa matumaini ya walio wengi aliposema hivi: “Kizazi hiki cha watu duniani huenda kikajionea chenyewe kuja kwa kipindi cha amani kisichobadilika katika historia ya ustaarabu.” Je! alikuwa sahihi? Je! matukio ya hivi karibuni yamaanisha kwamba maonyo ambayo Mashahidi wa Yehova wametoa kuhusu tekelezo la hukumu ya Yehova juu ya mataifa hayatatimia kweli? Je! Mashahidi wa Yehova wamekosea?

13 La, hawajakosea. Wanajua wanasema kweli kwa sababu wanaweka tumaini lao katika Yehova na katika Biblia, ambayo ni Neno la kweli la Mungu mwenyewe. Tito 1:2 inasema hivi: ‘Mungu hawezi kusema uwongo.’ Kwa hiyo wana uhakika kamili kwamba wakati unabii wa Biblia unaposema kwamba jambo fulani litatukia, litatendeka bila kushindwa. Yehova mwenyewe ataarifu hivi: “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu.”—Isaya 55:11.

14, 15. (a) Viongozi wa Yuda walikuwa wakipiga mbiu ya habari gani kabla tu ya uharibifu wa Yerusalemu katika 607 K.W.K.? (b) Kabla ya uharibifu wa ghafula kuja juu ya ulimwengu huu ni habari gani iliyotabiriwa na Paulo ingepigwa mbiu? (c) Tunaweza kutarajia nini kwenye upeo wa tangazo linalotolewa unabii kwenye 1 Wathesalonike 5:3?

14 Katika miaka kabla ya uharibifu wa Yerusalemu katika 607 K.W.K., Yeremia aliripoti kwamba viongozi walikuwa wakipaaza kilio, “Kuna amani! Kuna amani!” (Yeremia 8:11, NW) Hata hivyo, huo ulikuwa uwongo. Yerusalemu uliharibiwa katika kutimiza maonyo yaliyopuliziwa roho ya manabii wa kweli wa Yehova. Mtume Paulo alionya kwamba jambo sawa na hilo lingetukia katika siku zetu. Alisema kwamba watu wangekuwa wakipaaza kilio “amani na salama!” Lakini kisha, alisema, “ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula.”—1 Wathesalonike 5:3.

15 Tulipokuwa tukiingia miaka ya 1990, karatasi-habari na magazeti kila mahali yalikuwa yakisema kwamba ile Vita Baridi imekwisha na kwamba amani ya ulimwengu yakaribia. Lakini vita ya kupiga bunduki ikatokea katika Mashariki ya Kati. Hata hivyo, hali ya ulimwengu haina budi kuendelea mpaka ifike mahali ambapo kilio cha “amani na salama” kilichotolewa unabii kwenye 1 Wathesalonike 5:2, 3 kitaongezeka kufika upeo. Matumaini yetu yakiwa yametiwa nanga thabiti katika Neno la Mungu, tunajua kwamba, upeo huo unapofikwa, hukumu za Mungu zitatekelezwa upesi na bila kukosea. Matangazo yoyote ya amani na usalama yenye kufanyizwa kwa kupachikwa viraka hayapasi kutufanya tufikirie kwamba uharibifu uliotabiriwa na Mungu hautakuja. Hukumu za Yehova zimerekodiwa katika Neno lake Biblia bila uwezekano wa kubadilishwa. Jumuiya ya Wakristo, pamoja na dini nyingine zote bandia, itaharibiwa. Na kisha hukumu za Yehova zenye kuangamiza zitaonyeshwa dhidi ya ulimwengu wa Shetani uliosalia. (2 Wathesalonike 1:6-8; 2:8; Ufunuo 18:21; 19:19-21) Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova wana uhakika kwamba Yehova atatimiza neno lake, wao huendelea kulinda chini ya mwongozo wa jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye akili na kuchunguza kwa uangalifu jinsi matukio ya ulimwengu yanavyokunjuka. (Mathayo 24:45-47) Kwa hakika, juhudi zozote za binadamu hazipasi kutufanya tufikiri kwamba Yehova ameacha kusudi lake kuleta furiko kubwa la gharika ya uharibifu juu ya Jumuiya ya Wakristo iliyojaa dhambi.

‘Mungu Ni Kimbilio Letu’

16, 17. Mashahidi wa Yehova huitikiaje kama wengine wanaudhiwa na uwazi wa ujumbe wao?

16 Wengine huenda wakaudhika na uwazi wa Mashahidi wa Yehova katika kupiga mbiu habari hiyo. Hata hivyo, wasemapo kwamba watawala wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamefanya kimbilio katika mpango unaosema uwongo, wao husimulia yale tu Biblia isemayo. Wasemapo kwamba Jumuiya ya Wakristo inastahili adhabu kwa sababu imekuwa sehemu ya ulimwengu, huwa wakiripoti tu yale ambayo Mungu mwenyewe asema katika Biblia. (Wafilipi 3:18, 19) Zaidi ya hilo, kwa sababu Jumuiya ya Wakristo imeweka tumaini layo katika mipango iliyopendekezwa na ulimwengu, inakuwa kwa kweli ikiunga mkono mungu wa ulimwengu huu, Shetani Ibilisi, ambaye Yesu alisema alikuwa ndiye baba ya uwongo.—Yohana 8:44; 2 Wakorintho 4:4.

17 Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wanajulisha wazi hivi: Kwa habari yetu, sisi hatutii moyo matumaini bandia ya amani ya ulimwengu kwa sababu ya mandhari ya kisiasa inayobadilika. Badala ya hivyo, sisi tunarudisha mwangwi wa maneno ya mtunga zaburi: “Mungu ndiye kimbilio letu. Hakika binadamu ni ubatili, na wenye cheo ni uwongo, katika mizani huinuka; wote pamoja ni hafifu kuliko ubatili [mpumuo mmoja, NW].” (Zaburi 62:8, 9) Mipango ya kibinadamu ya kueneza na kuhifadhi Jumuiya ya Wakristo na mfumo huu wa mambo uliosalia ni ubandia, uwongo! Yote ikiwekwa pamoja haina nguvu za kuzuia makusudi ya Yehova kama vile hewa yenye moto iliyojaa kinywani isivyoweza!

18. Ni onyo gani la mtunga zaburi linalofaa leo?

18 Mashahidi wa Yehova hunukuu pia Zaburi 33, mistari 17 hadi 19, ambayo hujulisha wazi hivi: “Farasi [wa Misri, kifananishi cha vita] hafai kitu kwa wokovu, wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake. Tazama, jicho la BWANA [Yehova, NW] li kwao wamchao, wazingojeao fadhili zake. Yeye huwaponya nafsi zao na mauti, na kuwahuisha wakati wa njaa.” Wakristo wa kweli leo watumaini Yehova na Ufalme wake wa kimbingu, mpango pekee unaoweza kuleta amani yenye kudumu.

Jumuiya ya Wakristo “Mahali pa Kukanyaga kwa Miguu”

19. Kwa nini kutegemea matengenezo ya kisiasa kuleta amani ya ulimwengu ni madanganyo?

19 Kutumaini vibadala vya Ufalme wa Mungu vilivyofanyizwa na binadamu hukifanya kibadala hicho kuwa sanamu, kitu cha kuabudiwa. (Ufunuo 13:14, 15) Hivyo, kutia moyo tegemeo katika mashirika ya kisiasa, kama vile Umoja wa Mataifa, kwa ajili ya amani na usalama ni udanganyo, uwongo. Kuhusu vitu kama hivyo vya matumaini ya bandia, Yeremia husema: “Sanamu yake ya kuyeyusha ni uwongo, wala hakuna pumuzi ndani yake. Ni pasipo maana tu, kazi ya udanganyifu; wakati wa kuangaliwa watapotea.” (Yeremia 10:14, 15, ZSB) Kwa hiyo, farasi wa vita wa Misri ya ufananisho, yaani, uweza wa kisiasa-kijeshi wa mataifa leo, hautakinga milki ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo katika siku yayo ya hatari. Mapatano ya dini za Jumuiya ya Wakristo na ulimwengu huu hakika yatashindwa kuzikinga.

20, 21. (a) Ni jambo gani lililotukia kwa Ushirika wa Mataifa, na kwa nini Umoja wa Mataifa hautakuwa na tokeo zuri zaidi? (b) Isaya alionyeshaje kwamba mapatano ya Jumuiya ya Wakristo pamoja na ulimwengu hayataiokoa?

20 Jumuiya ya Wakristo ilitumainia Ushirika wa Mataifa, lakini ilipinduliwa hata pasipo Har–Magedoni kuja. Sasa imehamisha mapatano yayo kwa Umoja wa Mataifa. Lakini karibuni itakabiliana na “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” nayo haitaokoka. (Ufunuo 16:14) Hata UM uliofufuka hauwezi kamwe kuleta amani na usalama. Neno la Mungu la kiunabii linaonyesha kwamba tengenezo la Umoja wa Mataifa pamoja na mataifa yaliyo washiriki walo “watafanya vita na Mwana-Kondoo [Kristo akiwa katika mamlaka ya Ufalme], na Mwana-Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana na Mfalme wa Wafalme.”—Ufunuo 17:14.

21 Mashahidi wa Yehova kwa uhakika wasema kwamba hakuna wokovu kwa Jumuiya ya Wakristo katika mapatano yayo na ulimwengu wa Shetani. Na wanaposema hivyo, wanaelekeza tu kwa yale ambayo Biblia yenyewe husema. Isaya 28:17, 18 hunukuu Yehova akiwa anasema hivi: “Nami nitafanya hukumu kuwa ndiyo kanuni, na haki kuwa ndiyo timazi; na mvua ya mawe itachukulia mbali hilo kimbilio la maneno ya uongo, na maji yatapagharikisha mahali pa kujisitiri. Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo [mtakapokuwa mahali pa kukanyaga kwa miguu, NW].”

22. Hukumu kamilifu itumiwapo kwa Jumuiya ya Wakristo, tokeo litakuwa nini?

22 Wakati Yehova asababishapo kutekelezwa kwa uamuzi wake wa hukumu, itakuwa kulingana na uadilifu na haki kamilifu. Na msingi wa Jumuiya ya Wakristo wa uhakika, ‘mapatano na kifo’ yayo, utafagiliwa mbali kabisa kama kwa pigo la gharika yenye kufurika. Isaya aendelea kusema: “Maana litapita asubuhi baada ya asubuhi, wakati wa mchana na wakati wa usiku; na kuifahamu habari ile kutakuwa kitisho tu.” (Isaya 28:19) Itatisha kama nini kwa watazamaji kujionea wenyewe nguvu kamili za hukumu ya Yehova! Itakuwa ogopesho kama nini kwa makasisi wa Jumuiya ya Wakristo na wafuasi wao kupata kujua, wakiwa wamechelewa mno, kwamba wameweka tumaini lao katika uwongo!

Jina la Yehova “Ngome Imara”

23, 24. Badala ya kutafuta usalama katika ulimwengu huu, Mashahidi wa Yehova watafanya nini?

23 Lakini namna gani Mashahidi wa Yehova? Hata waelekeanapo na chuki na mnyanyaso wa kimataifa, wao hudumu wakiwa wamejitenga na ulimwengu. Hawasahau kamwe kwamba Yesu alisema kwa habari ya wafuasi wake hivi: “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:16, NW) Muda wote wa hizi siku za mwisho, wao wameweka tumaini lao katika Ufalme wa Yehova, si katika mipango ya kibinadamu. Kwa hiyo, maafa ya Jumuiya ya Wakristo hayatawafanya watishike. Kama Isaya alivyotabiri: “Yeye aaminiye hatafanya haraka [hatababaika, NW].”—Isaya 28:16.

24 Mithali 18:10 husema: “Jina la BWANA [Yehova, NW] ni ngome imara; mwenye haki huikimbilia, akawa salama.” Kwa hiyo sisi twaalika watu wote walio mfano wa kondoo wafanye kimbilio katika Yehova na katika Ufalme wake ulio mikononi mwa Kristo. Akiwa mahali pa kujificha, Yehova si ubandia! Ufalme wake mikononi mwa Kristo si uwongo! Kimbilio la Jumuiya ya Wakristo ni uwongo, lakini kimbilio la Wakristo wa kweli ndio ukweli.

Waweza Kueleza?

◻ Yuda ya kale ilifanyaje uwongo kuwa kimbilio?

◻ Jumuiya ya Wakristo imejaribuje kujificha katika ubandia?

◻ Isaya alionyaje Yuda, na Mashahidi wa Yehova hutamkaje onyo linalofanana na hilo leo?

◻ Jumuiya ya Wakristo itapataje kwamba imeweka uhakika wayo pasipofaa?

◻ Tofauti na Jumuiya ya Wakristo, Mashahidi wa Yehova hudumisha msimamo gani?

“Kwa mara ya kwanza tangu Vita ya Ulimwengu 2 jumuiya ya kimataifa imeunganika.Uongozi wa Umoja wa Mataifa, uliokuwa wakati mmoja hali bora yenye kutumainiwa tu, sasa

unahakikisha njozi ya mwanzishaji wao. . . .Kwa hiyo ulimwengu waweza kuchukua nafasi hii kutimiza ahadi iliyoshikiliwa kwa muda mrefuya utengemano mpya wa ulimwengu.”

—Rais Bush wa United States katika ujumbe wake wa Taifa la Muungano kwa taifa hilo, Januari 29, 1991

[Sanduku katika ukurasa wa 17]

MATUMAINI YA JUU YAONWA KWA UMOJA WA MATAIFA

“Kwa mara ya kwanza tangu Vita ya Ulimwengu 2 jumuiya ya kimataifa imeunganika.Uongozi wa Umoja wa Mataifa, uliokuwa wakati mmoja hali bora yenye kutumainiwa tu, sasaunahakikisha njozi ya mwanzishaji wao. . . .Kwa hiyo ulimwengu waweza kuchukua nafasi hii kutimiza ahadi iliyoshikiliwa kwa muda mrefuya utengemano mpya wa ulimwengu.”—Rais Bush wa United States katika ujumbe wake wa Taifa la Muungano kwa taifa hilo, Januari 29, 1991

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki