33 Pazeni sauti kwa shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+
Ni jambo linalofaa kwa wanyoofu kumsifu yeye.
 2 Mshukuruni Yehova kwa kinubi;
Mwimbieni sifa kwa kinanda chenye nyuzi kumi.
 3 Mwimbieni wimbo mpya;+
Pigeni nyuzi kwa ustadi, na kupaza sauti kwa shangwe.
 4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+
Na kila jambo analofanya linategemeka.
 5 Anapenda uadilifu na haki.+
Dunia imejaa upendo mshikamanifu wa Yehova.+
 6 Kwa neno la Yehova mbingu ziliumbwa,+
Na kwa roho ya kinywa chake kila kitu kilichomo kiliumbwa.
 7 Huyakusanya maji ya bahari kana kwamba ni bwawa;+
Huyaweka mawimbi makubwa ya maji katika maghala.
 8 Dunia yote na imwogope Yehova.+
Wakaaji wa nchi na wamhofu.
 9 Kwa maana alisema, ikawa;+
Aliamuru, ikasimama imara.+
10 Yehova amevuruga njama za mataifa;+
Ameharibu mipango ya mataifa.+
11 Lakini maamuzi ya Yehova yatasimama milele;+
Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi baada ya kizazi.
12 Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+
Watu ambao amewachagua kuwa miliki yake mwenyewe.+
13 Yehova anatazama chini kutoka mbinguni;
Anawaona wanadamu wote.+
14 Kutoka katika makao yake,
Anawakazia macho wakaaji wa dunia.
15 Yeye ndiye anayeumba mioyo ya wote;
Huchunguza kazi zao zote.+
16 Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa;+
Mtu hodari haokolewi na nguvu zake nyingi.+
17 Farasi ni tumaini la uwongo la wokovu;+
Nguvu zake nyingi hazimhakikishii mtu kwamba ataponyoka.
18 Tazama! Jicho la Yehova linawalinda wale wanaomwogopa,+
Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu,
19 Ili awaokoe kutoka katika kifo
Na kuwahifadhi hai wakati wa njaa kali.+
20 Tunamtarajia Yehova.
Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+
21 Mioyo yetu hushangilia kwa sababu yake,
Kwa maana tunalitumaini jina lake takatifu.+
22 Upendo wako mshikamanifu na ukae juu yetu, Ee Yehova,+
Tunapoendelea kukungojea.+