Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 8/15 kur. 28-29
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Tembea Kama Ufundishwavyo na Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Unaweza Kumsaidiaje Mtoto “Mpotevu”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Thamini Ifaavyo Zawadi Yako ya Uhai
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Heshimu Zawadi ya Uhai
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 8/15 kur. 28-29

Je! Wakumbuka?

Je! wewe umethamini kusoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Basi, ona kama waweza kuyajibu maswali yafuatayo:

◻ Wachungaji Wakristo wana msingi gani kutangulia kushugulika na watu fulani waliotengwa na ushirika kuona ikiwa huenda wakaongozwa watubu?

Hata wakati Waisraeli walipokuwa uhamishoni na kuwa bado wasiotubu, Yehova, akiwa mchungaji, alitangulia kuwatafuta, akituma manabii wake kwao. Wachungaji Wakristo wanapendezwa kusaidia wowote wenye kutubu ambao huenda wakawa kama kondoo waliopotea. (Linganisha Luka 15:4-7.)—4/15, kurasa 21-23.

◻ Kielezi cha Yesu cha mwana mpotevu kinaonyeshaje hisia na vitendo tunavyopaswa kuwa navyo wakati mtu fulani anaporudishwa katika kundi la Kikristo? (Luka 15:22-23)

Mradi wetu wapaswa kuwa kumwiga baba aliyeonyesha furaha wakati mwana wake mpotevu aliporudi. Hivyo, twapaswa kusema kwa uhuru na ndugu aliyerudishwa na kumtia moyo kutoka sasa na kuendelea kufanya maendeleo katika kweli.—4/15, ukurasa 25.

◻ Ni hadhari zipi zenye kutumika zinazoweza kuchukuliwa ili kuepuka kupatwa na uhalifu?

Inapowezekana, epuka kuwa nje katika maeneo yenye hatari wakati wa usiku. Ficha vito vyako, na kubeba vitu kama kamera katika mfuko wa kununulia vitu dukani. Jihadhari kuhusu kutembea karibu na ukingo wa barabara, hasa ikiwa unabeba mkoba au mfuko fulani wa mkono. (Ona Mithali 3:21-23.)—5/1, kurasa 5-6.

◻ Kwa sababu gani unabii kwenye Sefania 2:3 unasema: “Huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya BWANA [Yehova, NW]”?

Wokovu kwenye uhai unategemea uaminifu na uvumilivu. (Mathayo 24:13) Hivyo, wale tu wanaopatana na viwango vyenye uadilifu vya Mungu na ambao huendelea kusema lugha iliyo safi ndio watakaofichwa katika siku ya hasira ya Yehova. (Sefania 2:1, 2)—5/1, ukurasa 14.

◻ Ni nini kinachohusika katika kutanguliza Mungu katika familia?

Ni lazima wazazi na watoto wamwabudu Yehova na kufikia viwango vyake kama vilivyopangiliwa katika Biblia.—5/15, ukurasa 5.

◻ Kwa nini Yehova hajaadhibu watenda dhambi mara hiyo?

Sababu moja ni kwamba ni lazima jina la Mungu lijulishwe duniani pote. (Linganisha Warumi 9:17.) Nyingine ni ili kuruhusu wakati wa kujibu masuala ya enzi kuu ya Mungu na ukamilifu wa maadili wa mwanadamu, yaliyokuwa tokeo la uasi katika Edeni. Pia ustahimilivu wa Mungu unatolea wenye kufanya makosa nafasi ya kutubu na kurekebisha njia zao. (2 Petro 3:9)—5/15, kurasa 11-12.

◻ Ni mambo gani ya hakika yanayoshuhudia kwamba Biblia ina chanzo kinachopita uwezo wa kibinadamu?

Biblia iliandikwa na waandishi tofauti-tofauti 40 hivi, waliokuwa wa kutoka aina zote za kibinadamu na walioishi kipindi cha muda wa miaka 1,600; hata hivyo waandishi hao wote walifuata kichwa kimoja cha msingi. Upatano huo wa kindani wa Biblia haungewezekana ikiwa ungeachwa utukie wenyewe au kwa mwelekezo wa kibinadamu.—6/1, kurasa 5.

◻ Ni tendo gani geni na kazi gani isiyo ya kawaida iliyotabiriwa katika Isaya 28:21, ambayo Yehova atafanya katika siku yetu?

Lile onyo kwenye Ufunuo 17:16 linaonyesha kwamba siku moja rafiki za kisiasa za Babuloni Mkubwa watamgeukia. Tokeo litakuwa kwamba, Jumuiya ya Wakristo itaharibiwa kabisa pamoja na dini bandia nyingine zote. Hilo ndilo litakalokuwa tendo geni la Yehova na kazi yake isiyo ya kawaida kwa siku yetu.—6/1, kurasa 22-3.

◻ Wanawake Wakristo wapaswa wakumbuke nini kuhusu utumizi wa vito na rangi za uso?

Biblia haikatazi kutumia misaada ya urembo kama hiyo. (Kutoka 32:2, 3; Esta 2:7, 12, 15) Lakini kiasi lazima kiwepo sikuzote. Mwanamke angeweza kuja kuiga kwa urahisi mitindo ya kilimwengu, akitumia kwa wingi rangi ya mdomo, rangi ya mashavu, au rangi ya makope, kama vile Yezebeli alivyofanya. (2 Wafalme 9:30) Uangalifu unahitajiwa ili kuhakikisha kwamba virembeshi havitumiwi kwa wingi na vito vinavyotumiwa si vya fahari mno.—6/1, kurasa 30-31.

◻ Waisraeli waliponyokaje ‘maradhi yote mabaya ya Misri’ yaliyoenea sana nyakati za mapema? (Kumbukumbu 7:15)

Yaonekana kwamba waliyaponyoka maradhi kama hayo hasa kwa sababu ya kufuata mazoea ya kiafya yenye kuendelea yaliyoamriwa katika agano la Sheria.—6/15, ukurasa 4.

◻ Kwa nini Mungu ameamuru kwamba ni lazima wanadamu wasile damu? (Mwanzo 9:3, 4; Walawi 17:10, 11; Matendo 15:22-29)

Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu na uhai wa kibinadamu unategemea tishu yenye majimaji inayoendeleza uhai iitwayo damu. (Zaburi 36:9) Kwa kuheshimu damu kuwa kitu cha pekee, wanadamu huonyesha kutegemea kwao Mungu kwa ajili ya uhai. Kwa hiyo, sababu kuu ya amri ya Mungu kuhusu damu, ilikuwa si kwamba kutumia damu kungeweza kudhuru, bali kwamba damu ilikuwa na maana ya pekee kwa Mungu.—6/15, kurasa 8-9.

◻ Wazazi na vijana Wakristo wanaweza kuimarishaje uwezekano wa kwamba katao la damu la mtoto litaheshimiwa?

Ingawa si mtu mzima kisheria, kijana Mkristo apaswa kuweza kueleza kwa uwazi na kwa uthabiti katao lake la kidini lenye nguvu la kutotumia damu. Wazazi waweza kuwa na vipindi vya mazoezi pamoja na watoto wao ili kwamba watoto wapate ujuzi wa kueleza masadikisho yao wenyewe.—6/15, ukurasa 18.

◻ Wanawake walibarikiwaje sana wakati wa hudumu ya Yesu ya kidunia?

Yesu alianza kazi iliyoleta faraja, tumaini, na heshima mpya kwa wanawake wa jamii zote. Alifunza wanawake kweli za kiroho zenye kina kirefu. (Yohana 4:7, 24-26) Wakati wa huduma yake, yeye alikubali utumishi wa wanawake alipokuwa akisafiri kotekote nchini. (Marko 15:40, 41)—7/1, kurasa 14-15.

◻ Wazazi wameona njia zipi za Yesu za kufundisha kuwa zenye matokeo kwa watoto wao?

Wazazi hufanya vizuri kutumia vielezi ili kufanya kweli za Kikristo zivutie mioyo ya watoto wao wachanga, nao waweza kutumia maswali yaliyofikiriwa vizuri ili kutambua yale ambayo watoto wao wenye umri mkubwa zaidi wanafikiria. (Linganisha Mathayo 17:24-27.)—7/1, ukurasa 26.

◻ Kwa nini ni jambo linalowezekana Mkristo kuongozwa vibaya katika habari ya ushirika? (1 Wakorintho 15:33)

Huenda mtu akaonekana kuwa mwenye urafiki na mwenye kupendeza, lakini ikiwa hashiriki kupendezwa kwa Kikristo na utumishi wa Yehova au hata haamini Biblia, yeye ni mshirika mbaya. Kwa nini? Kwa sababu maisha yake yanategemea kanuni tofauti, na mambo yaliyo yenye umaana kwa Mkristo huenda yasiwe yenye umaana sana kwake.—7/15, ukurasa 23.

◻ Kwa nini twapaswa tufuatie fadhili-upendo?

Sifa ya fadhili-upendo inafanya tupendezeke kwa Mungu na kwa wengine. Inakuza ukaribishaji-wageni na kutufanya kuwa wenye ufikirio zaidi. Inaimarisha vifungo katika familia na katika kundi la Kikristo. Juu ya hayo yote, fadhili-upendo zinaleta utukufu kwa Yehova.—7/15, ukurasa 22.

◻ Kwa sababu gani Siku ya Hukumu ni wakati wa tumaini?

Siku ya Hukumu ni kipindi cha miaka elfu. Itasimamiwa na Mungu mwenyewe pamoja na Mwana wake, Yesu Kristo, ambaye amewekwa na Mungu kutenda akiwa Hakimu. Huo utakuwa wakati wa kurudishia ainabinadamu uhai mkamilifu wa kibinadamu ambao Adamu alipotezea wazao wake. (1 Wakorintho 15:21, 22)—8/1, kurasa 5-7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki