Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 11/1 kur. 5-7
  • Siku ya Kisasi cha Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Siku ya Kisasi cha Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Sababu Gani Siku ya Kisasi?
  • Siku ya Kisasi cha Mungu Itatimiza Nini?
  • Utafanya Nini?
  • Sababu gani Mungu wa upendo atalipa kisasi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Je! Kisasi Ni Kibaya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je! Siku ya Mungu ya Kisasi Inakaribia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 11/1 kur. 5-7

Siku ya Kisasi cha Mungu

KAMA tulivyoona katika makala iliyotangulia, kuna sababu kadhaa kwa nini ni vibaya kwetu kutafuta kulipa kisasi. Ni kosa kwa sababu mwishowe, hakusuluhishi jambo lolote. Ni kosa kwa sababu kunafanya uadui uwe wa daima badala ya kujenga vifungo vya kuunganisha vya urafiki. Na ni kosa kwa sababu kunaumiza mwenye kuweka mawazo ya kulipa kisasi.

Hata hivyo, sababu yenye umaana zaidi, kwa nini kisasi cha kibinadamu ni kibaya inaonwa katika maneno ya Musa kwa Israeli: “BWANA [Yehova, NW], Mungu wako, ni Mungu wa rehema.” (Kumbukumbu la Torati 4:31) Kwa kuwa Mungu ni mwenye rehema, twapaswa tuwe wenye rehema kama yeye. Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: “Iweni na huruma [rehema, NW], kama Baba yenu alivyo na huruma [rehema, NW].”—Luka 6:36.

Hata hivyo, Biblia pia humweleza Mungu kuwa “Mungu wa [vitendo vya, NW] kisasi.” (Zaburi 94:1) Nabii Isaya alisema juu ya “mwaka wa BWANA [Yehova, NW] uliokubaliwa” na pia “siku ya kisasi cha Mungu wetu.” (Isaya 61:2) Mungu anaweza kuwaje mwenye rehema na mwenye kulipa kisasi pia? Na ikiwa tutaiga rehema ya Mungu, kwa nini tusimwige katika kulipa kisasi?

Kujibu swali la kwanza, Mungu ni mwenye rehema kwa sababu aipenda ainabinadamu, na yeye husamehe kadiri awezavyo kwa muda mrefu awezavyo ili awape wanadamu nafasi ya kurekebisha njia zao. Wengi, kama vile mtume Paulo, wametumia vizuri rehema hiyo. Lakini Mungu ni mwenye kulipa kisasi pia—kwa maana ya kutekeleza haki—kwa sababu rehema kama hiyo yaweza kuendelea kwa kiasi fulani tu cha wakati. Wengine wanapoonyesha kwamba hawatabadili kamwe njia zao, Mungu atatekeleza hukumu katika ile iitwayo siku ya kisasi chake.

Katika kujibu swali la pili, la, hatuna haki ya kuwa wenye kulipa kisasi kwa sababu Mungu hulipa kisasi. Yehova ni mkamilifu katika haki. Wanadamu hawako hivyo. Mungu huona pande zote za jambo naye sikuzote hufanya uamuzi wenye uadilifu. Hatuwezi kutegemewa tufanye vivyo hivyo. Ndiyo sababu Paulo alishauri hivi: “Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana [Yehova, NW].” (Warumi 12:19) Kwa ajili yetu wenyewe, ni lazima tuache kisasi mikononi mwa Yehova.

Kwa Sababu Gani Siku ya Kisasi?

Hata hivyo, katika mahali pengi Biblia hukiri uhitaji wa kupasishwa adhabu kwa watenda mabaya wasiotubu. Kwa mfano, mtume Paulo alitabiri kwamba Mungu, kupitia Yesu, ‘angewalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu.’ (2 Wathesalonike 1:8) Tuna sababu nzuri za kuchukua maneno hayo kwa uzito. Kwa nini?

Kwanza, kwa sababu walio wengi leo huendelea kukaidi enzi kuu ya Muumba, wao hupuuza sheria zake zenye uadilifu. Wadai wasidai kumwamini Mungu, mwenendo wao huonyesha kwa wazi kwamba hawahisi kuwa watapasishwa adhabu na Mungu. Maneno ya mtunga zaburi hutumika kwa wote kama hao: “Kwani mdhalimu kumdharau Mungu, akisema moyoni mwake, Hutapatiliza?” (Zaburi 10:13) Kwa hakika, Yehova hatajiruhusu afanyiwe mzaha kwa njia hiyo milele. Ingawa yeye ni Mungu wa upendo, yeye ni Mungu wa haki pia. Yeye atasikia vilio vya wale wanaohangaikia haki kweli kweli: “BWANA [Yehova, NW], uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako, usiwasahau wanyonge.”—Zaburi 10:12.

Zaidi ya hayo, watu wenye kukaidi sheria wanaiharibu dunia yenyewe tunamoishi. Wanachafua hewa, ardhi, maji; wanajaza dunia ukosefu wa haki na ukatili. Na wamerundika silaha za kutosha za kemikali, za nyukilia na nyingine hatari sana zinazotisha kuwako kwa ainabinadamu. Kujiingiza kwa kimungu ni kwa lazima ili kuhakikisha wakati ujao salama kwa ainabinadamu yenye utiifu. (Ufunuo 11:18) Kujiingiza huko ndiko Isaya alikorejezea kuwa siku ya kisasi.

Siku ya Kisasi cha Mungu Itatimiza Nini?

Kulingana na Vine’s Expository Dictionary of Old and New Testament Words, katika Maandiko ya Kigiriki, neno la kusema kisasi, linapotumiwa kumhusu Mungu, humaanisha kihalisi “‘kile kitokanacho na haki,’ si, kama ilivyo mara nyingi kwa kisasi cha kibinadamu, kitokanacho na kuhisi umizo au kwa sababu tu ya hisia ya uchungu.” Hivyo basi, kisasi cha Mungu dhidi ya adui zake hautakuwa wakati wa umwagaji damu usiozuiwa, kama kilivyo kisasi cha kibinafsi. “Bwana [Yehova, NW] ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu,” Biblia yatuambia.—2 Petro 2:9.

Watumishi wa Mungu hutazamia siku ya kisasi cha Mungu kuwa wakati ambao mwe-nendo mwema utatetewa na waadilifu kukombolewa katika uonevu wa waovu. Hilo halimaanishi kwamba wao ni wenye nia ya kudhuru au wenye kulipa kisasi. “Aufurahiaye msiba [wa mwingine, NW] hatakosa adhabu,” Biblia huonya. (Mithali 17:5) Tofauti na hilo, wanasitawisha rehema na huruma, wakimwachia Mungu maamuzi yoyote kuhusu kisasi.

Ni kweli, si rahisi kwa watu wenye kukasirika kutenda kwa njia hiyo. Lakini inawezekana, na wengi wamefanya hivyo. Kwa mfano, Pedro alikuwa na wakati wa utotoni usio wa furaha na mara nyingi alipigwa na ndugu yake mwenye umri mkubwa zaidi. Kwa hiyo akakua akiwa mtu mzima mwenye jeuri, akiwatatiza polisi daima na hasira aliyohisi kuelekea ndugu yake aliifungulia juu ya mke na watoto wake. Mwishowe, alimsikiliza mmoja wa Mashahidi wa Yehova na baadaye akaanza kujifunza Biblia. “Kwa msaada wa Yehova,” yeye asimulia, “Nilibadilika, na sasa, badala ya kupiga watu, ninawasaidia nikiwa mzee Mkristo.” Kwa msaada wa Biblia na roho takatifu, wengine wasiohesabika wamebadilika vivyo hivyo wakaacha kuwa wenye chuki au wenye kulipa kisasi wakawa wenye kuonyesha upendo na saburi kuelekea wengine.

Utafanya Nini?

Kukumbuka siku ya kisasi cha Mungu inayokuja kutatusaidia tufaidike na saburi ya Yehova. Lakini nafasi ya kufanya hivyo ina kikomo. Siku hiyo itafika karibuni. Mtume Petro alionyesha kwa nini haijaja bado: “Bwana [Yehova, NW] hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.”—2 Petro 3:9.

Basi, ni muhimu kujitayarisha sasa kwa ajili ya siku ya Mungu ya kupasisha adhabu kwa kujifunza Maandiko na kutumia shauri layo. Hilo litatusaidia kufuata maneno ya mtunga zaburi: “Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya. Maana watenda mabaya wataharibiwa, bali wamngojao BWANA [Yehova, NW] ndio watakaoirithi nchi [dunia, NW].”—Zaburi 37:8, 9.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Baada ya siku ya kisasi cha Mungu, ‘wale wamngojao Yehova watairithi dunia’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki