Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 7/1 kur. 9-15
  • Je! Siku ya Mungu ya Kisasi Inakaribia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Siku ya Mungu ya Kisasi Inakaribia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NDIYO! TUNAIONA BILA SHAKAI
  • KISASI CHA MUNGU​—JE! KINASTAHILI?
  • HUZUNI ZAONGEZEKA
  • KUTAMBUA “KAHABA MWENYE KUJULIKANA SANA”
  • “TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU”
  • Mfalme Apigana Penye Har-Magedoni
    “Ufalme Wako Uje”
  • Sababu gani Mungu wa upendo atalipa kisasi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Siku ya Kisasi cha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Umoja wa Mataifa—Rafiki au Adui ya Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 7/1 kur. 9-15

Je! Siku ya Mungu ya Kisasi Inakaribia?

“Yehova ana siku ya kisasi.”​— Isa. 34:8, NW

1. Je! Luka 21:25, 26 linatumika leo?

YESU KRISTO alisema wakati huu ungejulikana kwa sababu ya “huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea” kwa sababu ya matatizo yanayovuruga jamii ya kibinadamu, “huku wanadamu wakizimia mioyo kwa sababu ya hofu na kutazamiwa kwa mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.” (Luka 21:25, 26, NW) Je! sisi twaiona hali hiyo katika mwaka huu wa 1981?

NDIYO! TUNAIONA BILA SHAKAI

2. (a) Ni Jambo gani linaloonyesha kwamba Ufunuo 11:15, 18 ilianza kutimia katika mwaka 1914? (b) Matukio hayo ni utangulizi wa nini?

2 Hatari iliyopo ya ulimwengu ni matokeo ya taabu ambazo zimeongezeka kati ya wanadamu tangu mataifa yalipoingia kwa mara ya kwanza katika vita ya jumla katika mwaka 1914. Kulingana na unabii wa Ufunuo sura ya 11, mwaka huo wakati mataifa walipokasirika’​—1914—​ulionyesha pia wakati ambapo kwa haki ‘ufalme wa dunia ulipata kuwa ufalme wa Bwana wetu [Yehova] na wa Kristo wake.’ (Ufu. 11:15, 18) Huku kumtawaza Kristo akiwa na mamlaka apate kutawala ni hatua ya kujitayarisha kuweka njia ya kulipa kisasi.

3. Makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yanasimama upande gani kwa habari ya ujumbe wa Mungu wa kisasi na faraja?

3 Leo, kuna ye yote aliyeagizwa na roho ya Mungu na atangaze siku ya kisasi cha Mungu na kufariji wote waombolezao? Ndiyo, walakini si makanisa ya Jumuiya ya Wakristo. Wao hawana ujumbe wo wote wa faraja ya kweli wala hawamtaki Yehova kuwa Mungu wao. Si kwamba tu wanaepuka kutumia jina la Yehova, bali pia wanatesa Wakristo wa kweli wanaoliheshimu jina lake.

4. Sisi tuna sababu gani za kufurahi?

4 Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova wanafurahia kulichukua jina la Mungu, lililo kuu zaidi katika ulimwengu wote! Wao wanafurahia kuitwa Mashahidi wa Yehova. Wana furaha nyingi kwamba, tangu kusimamishwa Ufalme katika mwaka ule wenye maana sana wa 1914, wamekuwa na pendeleo la kutangaza “siku ya kisasi” ya Yehova katika dunia yote. Kwa hakika wao wameazimia, kama vile linavyosema Mika 4:5, kwamba “sisi tutakwenda kwa jina la [Yehova], Mungu wetu, milele na milele”! Nao wanafurahia kuona kwamba mamilioni mengi ya wenye kuomboleza wamesikiliza ujumbe wao, wakafarijiwa na kuja kwa wingi sana kwenye upande wa ufalme wa Mungu unaokuja.

KISASI CHA MUNGU​—JE! KINASTAHILI?

5. (a) Hizi “nyakati za hatari” ni zao la mwisho la kitu gani? (b) Ni hali gani tunazoziona katika Jumuiya ya Wakristo zikitimiza unabii wa Paulo kuhusu “siku za mwisho”?

5 Walakini je! leo ulimwengu ni mbaya sana kweli kweli hata kwamba una lazima ya kukutana na kisasi cha Mungu? Ebu yasikilize maneno haya ya mtume Paulo yaliyoongozwa na Mungu. Yeye alisema hivi: “Ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.” Hizi siku za hatari ni matokeo ya mwisho ya watu kukataa kuitikia kweli inayohubiriwa. (2 Tim. 2:23-26) Hata katika Jumuiya ya Wakristo twaona sasa ongezeko lenye kuogopesha la uhalifu na jeuri, kuharibika kwa jamaa, kutoheshimu mamlaka na kukosa adili. Vyanzo vya yote hayo ni choyo, pupa, kukosa upendo wa kweli. Paulo anaendelea kusema hivi: “Watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, . . . wasiopenda mema, . . . wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.” (2 Tim. 3:1-5) Je! tunaona unabii huu ukitimizwa duniani pote leo? Hakika, ndiyo. Unatimizwa barabara.

6. Ni hali gani ambayo imetokea katika kutimiza Mathayo 24:12?

6 Yesu mwenyewe, akitoa unabii juu ya “ishara . . . ya mwisho wa taratibu ya mambo,” alisema hivi: “Kwa sababu ya kuongezeka kwa kutokutii sheria upendo wa wengi zaidi utapoa.” (Mt. 24:3, 12, NW) Hiyo ni kweli kama nini katika Jumuiya ya Wakristo, na vilevile ulimwengu wote! Kila wakati wa Krismas unapokuja, katika Jumuiya ya Wakristo wanasema mengi juu ya upendo, juu ya amani na nia njema miongoni mwa watu, walakini je! mataifa ya Jumuiya ya Wakristo wanafanya mambo hayo? Maneno ya waziri mkuu wa Uingereza, yaliyosemwa juma moja tu kabla ya Krismas ya 1979 ni yenye maana. Yeye alisema: “Twakabiliana na kipindi kipya cha miaka kumi—nimekiita ‘miaka kumi ya hatari’—ambayo katika hiyo mambo yanayohatirisha usalama wetu na maisha yetu yanaweza kuwa mabaya zaidi kuliko katika miaka ya kuanzia na wa 1970.”

7, 8. (a) Ni hali gani kama ile ya siku ya maangamizi tunayoiona sasa? (b) Yehova anatoa mahakikisho gani nayo hayo yanahusianaje na “upendo” na “kisasi”?

7 Mataifa yanapambanje na mambo hayo? Kwa kuzidisha matayarisho yao ya vita! Ebu fikiria hili! Ulimwengu huu usio na upendo unatumia zaidi ya shilingi 7,000,000 (Z1,400,000) kila dakika kwa silaha, zaidi ya shilingi bilioni 3500 (Z700) kila mwaka! Yote hayo yanaharakisha sana hali kama ya siku ya maangamizi ambayo ulimwengu hauwezi kupata suluhisho. Kulingana na habari iliyochapishwa na kikundi cha madaktari, wanasayansi na wengine katika gazeti New York Times la Machi 2, 1980, kama vita ya makombora ya nuklea ingetokea kesho, ingeweza kwa saa moja tu, kuharibu sehemu kubwa ya uhai duniani—watu maelfu ya mamilioni. Hata hivyo, mataifa yanafanya kazi kwa kukazana ili kutokeza silaha kubwa zenye kuleta mauaji makubwa zaidi!

8 Sasa, basi, je! Mungu wetu mwenye upendo, muumba wa dunia hii yenye kupendeza, ataruhusu mataifa maovu yaiteketeze iwe makaa. Hata! Kwa maana yeye asema hivi wazi katika Neno lake: “[Yehova], aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuimba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni [Yehova], wala hapana mwingine.” Jina lake Yehova lisilolinganika ni uhakikisho wa kwamba Yeye, akiwa Muumba mwenye upendo na Bwana Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote, hataruhusu dunia ifanywe ukiwa. Upendo wa kimungu unamtaka yeye alipe kisasi juu ya wale wanaochafua dunia yetu na ambao wanaweza kufutilia mbali kuumba kwake kwa kibinadamu.​—Isa. 45:18; Yer. 10:10-12.

9. Kwa kuwa mataifa yamekataa kuacha kuunda silaha, sasa Yehova amekusudia kufanya nini, na kwa sababu gani?

9 Tangu itokee vita ya ulimwengu ya kwanza katika mwaka 1914, dunia hii imeloweshwa damu ya makumi ya mamilioni ya watu wasio na hatia. Kwani, Vita ya Ulimwengu ya Pili peke yake iliangamiza uhai wa watu milioni 55! Na sasa taraja la mauaji makubwa yenye kuletwa na silaha ni lenye kuogopesha zaidi. Kwa hiyo, kwa kuwa mataifa wanakataa kuacha kuunda silaha, basi Mungu wetu mwenye upendo anatangaza kwamba karibuni yeye atawaachisha kuunda silaha, katika njia yake mwenyewe yenye kuleta matokeo na yenye kudumu. Asema hivi: “Njoni, enyi watu, utazameni utendaji wa Yehova, jinsi alivyofanya matukio yenye kushtua duniani. Yeye anafanya vita vikome mpaka mwisho wa dunia.” (Zab. 46:8, 9, NW ) Ndiyo, ni kusudi la Yehova lenye upendo kufanya jambo ambalo mataifa hawatafanya kamwe​—kuharibu kabisa silaha zao zote, hata kuharibu mizinga yao yote ya nuklea. Kama vile Yehova aemavyo: “Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa.” (Rum. 12:19; Sef. 3:8, 9) Je! Ahadi ya Mungu wetu mwenye upendo kwamba atalipa kisasi haitufuahishi? Inapaswa kutufurahisha!

HUZUNI ZAONGEZEKA

10. Vita vya karne hii vimeleta matokeo gani yenye kuogopesha?

10 Vita vilivyopiganwa tangu mwaka 1914 vimeleta matokeo mabaya sana. Kati ya hayo ni kujitia katika kufanya ngono pasipo kujizuia kukitokeza magonjwa yenye kuenea ya kaswende na kisonono, na mimba zisizotakikana. Mimba hizo zisizotakikana zikaleta pamoja nazo ongezeko kubwa la kutoa mimba. Inakadiriwa kwamba sasa, ulimwenguni pote, mimba za watoto wasiozaliwa kama milioni 30 mpaka 40 hutolewa, wanauawa, kila mwaka! Huo ndio uuaji ulio mkubwa zaidi wa wasio na hatia ambao ulimwengu umepata kuona, ukipita sana vifo katika mwaka uliokuwa na vifo vingi zaidi katika vita yo yote katika historia.

11. Ni katika njia gani ‘watu waovu wanazidi kuwa wabaya’?

11 Vilevile, katika nyakati za karibuni, tumeona yakiongezeka kwa kadiri yenye kuogopesha sana mambo kama vile kutumia vibaya dawa za kulevya, talaka, uhalifu wa vijana, na uasi wa sheria wa kila namna. Leo, jamii ya watu wa namna moja wenye kulalana (wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake) inajidai kuwa na wafuasi milioni 20 katika United States peke yake. Hivi karibuni, mlawiti (mwanamume mwenye kuwalala wanaume) aliweka rekodi ya kisasa yenye kuogopesha kwa kuwaua vijana 33 aliokuwa amelala nao. Hata hivyo, kulalana kwa watu wa namna moja ni mojayapo tu ya namna za uasherati unaofanywa katika Jumuiya ya Wakristo na duniani pote. Ni kama vile tu Timotheo wa pili sura ya 3 inavyosema kuhusu hizi “siku za mwisho,” kwamba “watu wabaya . . . wataendelea, na kuzidi kuwa waovu.”​—Mst. 13.

12. Tuna vionyesho gani vinavyoonyesha kwamba ulimwengu huu umefikia mwisho wake?

12 Kwa kuutazama ulimwengu mwasherati unaotuzunguka, tunalazimika kupaza sauti hivi: Loo! jinsi ilivyo kama siku za Noa! Loo! jinsi ilivyo kama wakati wa Sodoma na Gomora! Loo! jinsi walivyo kama Wakanaani wapotovu na kama Waisraeli wenye kurudi nyuma! Ulimwengu huu uliopo uendeleapo kuzama zaidi na zaidi katika uchafu wa uasherati, twakumbushwa juu ya onyo la mtume Paulo, kwamba ‘watendao hayo wanastahili kifo.’ (Rum. 1:18, 26-32) Hasha, Mungu mwenye upendo hatavumilia zaidi uovu wenye kutisha wa hii taratibu ya mambo. Badala yake yeye atawaharibu wanaoichafua dunia yake.​—Ufu. 11:18.

KUTAMBUA “KAHABA MWENYE KUJULIKANA SANA”

13. Ni nini maana ya ‘uzinzi wa kiroho’?

13 Hata hivyo, vilevile Biblia inazungumza juu ya uasherati wa kiroho. Huo unafanywa na wale wanaodai kwamba wanaizoea dini safi, walakini wanaojitia katika mambo ya ulimwengu wa Shetani. Biblia yasema hivi: “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa [ulimwengu] ni kuwa adui wa Mungu? basi kila atakaye kuwa rafiki wa [ulimwengu] hujifanya kuwa adui wa Mungu.” (Yak. 4:4) Urafiki wa namna hiyo​—uzinzi wa kiroho—​kwa upande wa wale wanaodai kuwa watumishi wa Mungu hutoa sababu nyingine kubwa ya Yehova kulipa kisasi. Sababu gani twasema hivyo?

14. Yule “malaya mwenye kujulikana sana” ni nani, nayo yale “maji mengi” anayokaa juu yake ni nini?

14 Ni kwa sababu ya yale yanayosemwa katika Ufunuo sura ya 17. Hapo twasoma juu ya “kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi.” Hiyo yamaanisha nini? “Maji” hayo yanatambulishwa waziwazi kwa ajili yetu katika mstari wa 15 kuwa yamaanisha “jamaa na makutano na mataifa na lugha.” Lakini ni nani huyu “kahaba mkuu” anayewatawala watu? The Jerusalem Bible, tafsiri ya Kikatoliki, humtaja kuwa “malaya mwenye kujulikana sana.” Yeye amefanya nini hata apate kujulikana sana hivyo? Ufunuo 17:5 hutusaidia kujua, ikisema hivi: ‘Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, Babeli Mkuu, mama wa makahaba na machukizo ya nchi.’

15. Ni jambo gani lililoupata Babeli, lakini uliacha urithi gani?

15 ‵Kwa hiyo “malaya anayejulikana sana” ana jina, “Babeli Mkuu.” Jambo hilo linamshirikisha na Babeli wa historia ya kale, wakati wa Mfalme Nebukadreza, historia inayofunua kwamba ulijaa ibada yenye kutumia ngono zilizopotoka sana na ufisadi. (Dan. 4:28-30) Leo, Babeli wa siku za Nebukadreza haupo tena. Mahali ulipokuwa katika Iraq ya kisasa ni mahame, “kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.” (Isa. 13:19-22) Hata hivyo, Babeli wa kale uliachia wanadamu urithi fulani. Nao urithi huo ni nini? Ni ibada yake ya sanamu​—dini yake!

16. (a) Milki ya dini ya uongo ya ulimwenguni pote ilitokeaje? (b) Yehova ametoa hukumu gani juu ya Babeli Mkuu, na sababu gani?

16 Tangu nyakati za mapema zaidi baada ya Gharika, Babeli ulitambulishwa na dini ya uongo. Ilikuwa katika Babeli kwamba watu, katika kumkaidi Yehova, walianza kujenga mji na mnara wa kidini ukiwa na kilele chake katika mbingu. Na wakati Yehova alipoichafua lugha yao, ni kutoka Babeli walipotawanyika katika dunia yote, wakiichukua dini yao ya uongo. Katika karne ya nne, Wakristo waasi imani waliingiza wakaichanganya na mafundisho ya kidini na kawaida za ibada zilizozoewa Babeli taratibu ya kidini inayoendelea mpaka siku ya leo katika madhehebu mbalimbali ya Ukatoliki na Uprotestanti. Hivyo, ikatokea milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, “Babeli Mkuu,” ikitia ndani dini za “Kikristo” na zisizo za Kikristo. Kwa sababu “Babeli Mkuu” ameshiriki katika kutesa, kufanya jeuri, na hata katika vita vya historia ya ulimwengu, Mungu amepitisha hukumu yake juu yake, akisema hivi: “Na ndani yake ilionekana damu ya manabii, na ya watakatifu, na ya wale wote waliouawa juu ya nchi.”​—Ufu. 17:5, 6; 18: 24; Mwa. 10:8-10, NW; 11:1-9.

17. Ni nini yule “mnyama mwekundu sana,” naye ametimizaje unabii?

17 ‘Urafiki na ulimwengu’ wa uzinzi wa Babeli Mkuu unazidi hapo. Unatia ndani uhusiano wake wa kumtawala “mnyama” wa mfano. Kwa maana anasimuliwa pia katika Ufunuo 17:3 kuwa ameketi “juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru.” Katika Biblia, mara nyingi “wanyama” wanatumiwa kufananisha mataifa ya kisiasa. (Dan. 7:2-8; 8:5-8, 20, 21; Ufu. 13:1-18) Walakini hapa unabii unazungumza juu ya “mnyama” mwenye maumbo ya kiajabu na yasiyo ya kawaida, naye, ana “vichwa saba na pembe kumi.” Historia ya kisasa inaonyesha kwamba “mnyama” huyo alitokea kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 1920. Ulikuwa mwungano wa mataifa—ule Ushirika wa Mataifa. Ulitumbukia katika hali ya kutotenda kwa muda mfupi katika wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili. Lakini—katika kuutimiza unabii—ulitokea tena ukiwa Umoja wa Mataifa. Karibuni, ‘utaingia kwenye uharibifu.’​—Ufu. 17:8-11.

18. Uhusiano wa karibu sana wa kidini na kisiasa wa Babeli Mkuu utakomaje?

18 Dini ya uongo, “Babeli Mkuu,” imejaribu kuuongoza Ushirika wa Mataifa na Umoja wa Mataifa pia. Hata hivyo Neno la Mungu laonyesha kwamba urafiki wa karibu wa kidini na kisiasa wa namna hiyo wa mapapa na viongozi wengine wa kidini utakoma karibuni. Wakati ambapo huyo “malaya mwenye kujulikana anafikiri ameketi vizuri sana, Mungu atafanya zile “pembe kumi” za mfano za“mnyama,” ule Umoja wa Mataifa, zielekeze nguvu zao za kijeshi juu yake. Zitamwangusha kutoka mgongoni mwao, zimharibu, zimwangamize kabisa, kana kwamba kwa moto.​—Ufu. 17:16, 17,

“TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU”

19. Mungu anaonyeshaje upendo wake sasa kwa watu wote wa dini wenye mioyo minyofu?

19 Saa hiyo ya hukumu ikaribiapo, Mungu anaonyeshaje upendo wake? Katika njia hii: Kwa Wakatoliki wote, Waprotestanti, Wabuddha, Mabanyani wenye moyo mnyofu—kwa watu wote wa dini uongo wanaotaka kuwa watu wa Mungu—Mungu anawatolea mwaliko huu wenye uharaka ulioandikwa katika Ufunuo 18:4, 5: “Tokeni kwake [Babeli Mkuu], enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.”

20. Kwa sababu gani hasa huu ndio wakati wa kuondoka na kukaa mbali na Babeli Mkuu?

20 Pasipo shaka lo lote, kufikilizwa kwa hukumu ya Mungu kunakaribia zaidi na zaidi! Mataifa yanayopinga dini tayari yana uwezo mwingi katika Umoja wa Mataifa, nayo mataifa yenye majeshi yenye nguvu ambayo yanahitaji sana mafuta yanatisha nchi za Waislamu pamoja na mataifa ambayo kwa muda mrefu yalionwa kuwa kinga ya dini ya Jumuiya ya Wakristo. Huu ndio wakati hasa wa wote wanaopenda kweli na haki kuondoka kwake huyo “malaya anayejulikana sana,” ndiyo, kuukimbilia ufalme wa Mungu.

21. Har–Magedoni ni nini, nayo mataifa yatajikuta hapo wakati gani?

21 Ni jambo gani linalofuata kuharibiwa kwa “Babeli Mkuu,” milki ya ulimwengu ya dini ya uongo? Maandiko yanaonyesha kwamba zile “pembe kumi” za yule “mnyama” zitageukia dini ya kweli, inayowakilishwa na Mashahidi wa Yehova duniani. Walakini jambo hilo litokeapo mataifa hayo yatajikuta yakipigana na Mungu katika Har–Magedoni! Wala Har–Magedoni si pembe ndogo tu katika nchi ya Palestina. Badala yake, Har–Magedoni ni hali ya ulimwenguni pote inayomhitaji Mungu alipe kisasi katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” pigano lililo kubwa zaidi kupita mengine yote!​—Ufu. 16:14, 16; 17:12-14.

22. Maandiko yanaonyeshaje kwamba Har–Magedoni ni vita ya haki?

22 Biblia yasema kwamba Mungu amtumia Kristo Yesu akiwa pamoja na majeshi ya mbinguni ‘ahukumu na kupiga vita katika haki.’ Ndiyo, Har–Magedoni itakuwa vita ya haki. Ya haki? Namna gani hivyo? Kwa kuwa italeta kisasi kinachostahili juu ya mataifa na watu wa dunia ambao wamechagua kutokumjua Mungu na wanaopinga haki yake ya kutawala. Itakuwa yenye kuchagua katika kuharibu kwake. Itawaharibu waovu, na kuleta wokovu kwa wale wote ‘wanaotii Injili ya Bwana wetu Yesu,’ ndivyo asemavyo mtume Paulo. Hivyo, Har–Magedoni itasawazisha kisasi cha Mungu na upendo wa Mungu.​—2 The. 1:8; Zab. 145:20; Ufu. 19:11-21.

23. (a) Yehova ni Mungu wa namna gani, kama vile anavyoonyeshwa na Zaburi 145:17-21? (b) Ni kwa sababu gani, basi, ‘Mungu huyu wa upendo’ analipa kisasi? (c) Inatupasa kuchukua hatua gani kwa habari ya“siku ya kisasi “inayokaribia?

23 Basi, je! hatuthamini kwa nini ‘Mungu wa upendo’ lazima pia awe Mungu wa kisasi? Ni kwa sababu anapenda haki na kuchukia uovu. (Zab. 145:17-21) Ni jambo la lazima kama nini kwamba Jina lake kuu na makusudi yake yatetewe! Ni jambo la lazima kama nini dunia yetu isafishwe na kuondolewa hatia yote ya damu, upotovu na uasherati, matendo ambayo yametia madoa uumbaji huu wa Mungu ulio mzuri kwa muda wa mileani zilizopita! Ndipo tu dunia yetu itakapokuwa paradiso ya duniani pote ambayo Mungu alikusudia kwa ajili ya wanadamu. Kwa hiyo, kwanza, ‘Mungu wa upendo’ asiyelinganika lazima atayarishe njia kwa kulipa kisasi juu ya adui zake. Je! sisi hatuna furaha kwamba siku yake ya kisasi imekaribia sasa? Acheni, basi, tujiunge na wale wanaokubali mwaliko huu wa Yehova wenye upendo: “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake, kwa kuwa atalipa kisasi . . . juu ya adui zake.”​—Kum. 32:43, NW.

[Sanduku katika ukurasa wa 10]

HALI YA MAMBO KATIKA ULIMWENGU

“KUELEKEA MGONGANO: ULIMWENGU. Matumizi [ya fedha kwa ajili ya mipango] ya kijeshi yazidi kuongezeka katika njia yenye kuogopesha . . . sasa ni . . . maradufu ya hesabu ya miaka kumi iliyopita. . . . Kiasi [cha fedha] kilichotumiwa na ulimwengu kumpa vifaa kila askari katika [mwaka] 1966 kilikuwa mara 60 [zaidi ya] kiasi kilichotumiwa kumwelimisha kila mtoto.”—“To the Point,” Novemba 3, 1978

“. . . WAFARANSA WATANGULIA KUONA MSIBA. Hali ya taabu na woga juu ya wakati ujao ni halisi. Watu fulani wamefikia mahali pa kusema kwa sauti ndogo kwamba kuanguka kwa uchumi au vita au vyote viwili vitatokea kweli kweli, nao wanaelekea kupata faraja kutokana na wazo la kwamba hakuna la kufanya ila kungojea msiba huo unaokuja.”—New York “Times,” Novemba 17, 1979

‘WAJEREMANI WA MAGHARIBI WAHOFU HAR-MAGEDONI. Hali yenye woga ya vita imerudi kusumbua Ujeremani wa Magharibi kadiri hali katika mataifa yote inavyoelekea kuzidi kutozuilika. . . . Karibu asilimia 60 ya watu, kulingana na uchunguzi wa karibuni, yaamini vita yaelekea au hata yaweza kutokea katika miaka mitatu inayokuja.​’—“The Times,” London, Aprili 23, 1980

“Ulimwengu unatumia zaidi ya [shilingi bilioni 3,500 (Z700)] kila mwaka katika utendaji wa kijeshi, au [shilingi milioni 7 (Z1.4)] hivi kila dakika. [Na] kana kwamba hesabu hiyo kubwa inakuwa haitoshi, tunakariba kuona ongezeko la ghafula katika matumizi [kwa ajili] ya jeshi.”—“World Press Review,” Agosti, 1980

[Sanduku katika ukurasa wa 13]

TUNDA LA “SIKU ZA MWISHO”

“Idara ya Polisi ya Los Angeles iliripoti kwamba vijana 25,000 wenye umri wa miaka 17 au wachanga zaidi katika mji huo peke yake walikuwa wameingizwa kwenye kikundi cha wanaume wenye kulalana ili wawe wakifanya ngono na watu wazima wa kiume wenye kuwalipa. Kivulana mmoja, wa miaka 12 tu, alielezwa kuwa malaya anayepata [shilingi 7,000 (Z1,400)] kila siku.”​—“lndianapolis Sunday Star,” Juni 17, 1979

“Kulikuwako malaya karibu 1,000 walioshikwa huko Denver mwaka uliopita, na 400 wa hao walikuwa wanaume. Huenda mwaka huu [hesabu] ilizidi hiyo na kwa mara ya kwanza hesabu ya malaya wanaume waliokamatwa huenda ikazidi hesabu ya wanawake.”—“Rocky Mountain News,” Julai 8, 1979

“Mahakma kuu zaidi ya Kanisa la Mwungano la Methodisti limetoa hukumu kwamba [mwanamume] aliyekiri kuwa anafanya ngono na wanaume wenzake . . . aweza kuendelea kuwa mchungaji wa Kanisa la Washington Square katika Mji wa New York.”​—The New York “Times,” Novemba 3, 1979

[Sanduku katika ukurasa wa 14]

UMOJA WA MATAIFA AU UFALME WA MUNGU​—JIPI?

Bado dini inajaribu kuukalia Umoja wa Mataifa na kutoa uongozi juu ya maongozi yake. Hatua ya karibuni ni ile ya Papa John Paul wa Pili, ambaye alisimama mbele ya Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Oktoba 2, 1979, jambo hilo likiwa linatangazwa kwa wingi sana. Papa huyo alitangaza hivi: “Sababu yangu ya kujiingiza leo bila shaka ni kile kifungo cha pekee cha ushirikiano kinachounganisha Uongozi wa kimtume pamoja na Tengenezo la Umoja wa Mataifa. . . Natumaini kwamba Umoja wa Mataifa utaendelea kuwa baraza kuu zaidi ya amani na haki, makao ya kweli ya uhuru wa vikundi vya watu na watu mmoja mmoja wanapotumaini kupata wakati ujao ulio bora zaidi.” Walakini Papa hakuona inafaa hata kutaja chombo cha Mungu cha kuleta amani, haki na uhuru—Ufalme ambao Yesu aliomba Baba yake hivi: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mt. 6:9, 10; Ufu. 11:15) Kutokea kwa mataifa yenye nguvu yenye kupinga dini katika Umoja wa Mataifa hakumaanishi mema kwa wakati ujao wa ‘milki ya ulimwengu ya dini ya uongo.’​—Ufu. 17:16, 17.

[Picha katika ukurasa wa 12]

Ili iweko nafasi ya Taratibu Mpya ile ya kale lazima iondolewa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki