Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 3/15 kur. 123-126
  • Umoja wa Mataifa—Rafiki au Adui ya Dini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Umoja wa Mataifa—Rafiki au Adui ya Dini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KRISTENDOMU NI KAMA YERUSALEMU WA KARNE YA KWANZA
  • UASHERATI WA KIROHO WA DINI YA UONGO
  • UHARIBIFU WA DINI YA UONGO
  • WAKATI WA KUCHUKUA HATUA
  • Kufisha Babuloni Mkubwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Amani, Usalama, na Ile ‘Sanamu ya Mnyama’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Huu Ndio Wakati wa Kukimbia!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • N’nini Kinachozuia Amani ya Ulimwengu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 3/15 kur. 123-126

Umoja wa Mataifa​—Rafiki au Adui ya Dini?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. Mara nyingi Yesu alijibuje maulizo ya wanafunzi wake?

YESU Kristo alipokuwa duniani, wanafunzi wake walimwuliza maulizo mengi. Mara nyingi alijibu kulingana na hali mara hiyo kwanza, kisha akatoa jibu kamili zaidi la unabii lenye mfiko wa mbali isilolifahamu wakati huo. Baada ya Pentekoste, mwaka wa 33 C.E., walipata fahamu. Mambo mengine yalipaswa yafahamiwe baadaye. Mojawapo la haya ni juu ya tengenezo la ulimwengu la amani usalama tulijualo leo kama Umoja wa Mataifa.

2. Yesu alifuataje njia hii katika kujibu ulizo la mitume lililomo katika Mathayo 24:3?

2 Habari inayohusika ni ulizo la wanafunzi walilouliza siku chache kabla ya kifo cha Kristo: “Mambo haya [yanayohusu hukumu juu ya Yerusalemu na uharibifu wa hekalu] yatakuwa lini, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya mwisho wa taratibu ya mambo?” (Mt. 24:3 NW) Yesu alitoa maelezo mengi juu ya uharibifu uliokuwa unakuja wa Yerusalemu. Ndipo alipoendelea kutoa habari zaidi, kionyesha kwamba jibu lake lilikuwa na matumizi ya unabii ya baadaye kwa mwisho wa taratibu ya mambo ya siku zetu. Unabii huu ulikaza fikira hasa juu ya uharibifu wa taratibu za dini ya uongo za Kristendomu. Je! Umoja wa Mataifa utaziona dini za ulimwengu kama msaada au kizuizi katika kujaribu kuleta usalama wa ulimwengu?

3. Sehemu ya unabii wa Yesu katika Mathayo 24:15, 16 ilitimizwaje juu ya Yerusalemu?

3 Sehemu ya kutokeza ya jibu la Yesu ilikuwa mtajo wake wa unabii wa Danieli juu ya “chukizo la uharibifu” ambalo ‘lingesimama katika patakatifu.’ (Mt. 24:15, 16) Unabii huu ulikuwa na utimizo katika karne ya kwanza majeshi ya Rumi ya kipagani yalipoingia Yerusalemu, hata wakaufukua ukuta wa hekalu chini wakitaka kuuangusha. Muda wa miaka inayopungua minne baadaye mwishowe waliuharibu mji kabisa. Ni nini utimizo wa baadaye ulio mkubwa zaidi?

KRISTENDOMU NI KAMA YERUSALEMU WA KARNE YA KWANZA

4. Ni haraka gani za pekee ulizokuwa umefurahia Yerusalemu, lakini je! wao walizithamini kweli?

4 Ili kuufahamu utimizo wa kisasa, ni lazima kwanza kuona ulinganifu kati ya Yerusalemu wa kale na Kristendomu ya kisasa. Yerusalemu ulijidai kuwa mji wa Mungu. Kweli, kiti cha enzi cha Daudi, kilichoitwa ‘kiti cha enzi cha Yehova,’ kilikuwa kimewekwa huko. (1 Nya. (Sik.) 29:23) Hekalu lake liliitwa ‘nyumba ya Yehova.’ (Zab. 27:4) Lakini Israeli walikuwa wamekuwa waasi sana hata hakukuwa na mfalme wa ukoo wa Daudi juu ya kiti cha enzi tena. Nayo ibada ya kweli ya Mungu ilikuwa imechafuliwa sana na mapokeo ya waandishi na Mafarisayo hata Mungu akawa karibu kuiacha ‘nyumba’ yake milele.​—Mt. 23:38; 15:1-9.

5-7. Ni katika njia gani Kristendomu imekuwa sawa na Yerusalemu wa kale?

5 Vivyo hivyo, Kristendomu imejitokeza kama yenye kumwakilisha Mungu. Yajihesabu kama ‘takatifu’ nayo imebariki vita zake kama takatifu, hata Vita vya Ulimwengu vya Kwanza na vya Pili. Kwa hiyo imo katika hali inayofanana katika mambo mengi na ile ya Yerusalemu, ingawa Kristendomu haikukubaliwa na Mungu kama yake mwenyewe wakati wo wote.

6 Katika kujibu ulizo la wanafunzi wake, Yesu alisema kwamba “upendo wa wengi [wa watumishi wa kujidai wa Mungu] utapoa.” (Mt. 24:12) Ndivyo ilivyokuwa kati ya Wayahudi kabla ya uharibifu wa Yerusalemu. Na bila shaka hali hiyo imo katika mataifa yaitwayo ‘ya Kikristo’ ya kizazi hiki. Wakristo wa kujidai, hata viongozi wa dini, wamefanya kazi kwa nguvu siasani, badala ya kuutangaza ufalme wa Mungu. Kwa hiyo, ni nini lipaswalo kuzipata dini za Kristendomu?

7 Ingefaa kabisa kitu kile kile ambacho Kristendomu amekitumainia, badala ya kumtumainia Mungu, kilete maangamizi yake. Na tuone namna unabii katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo uonyeshavyo hili.

UASHERATI WA KIROHO WA DINI YA UONGO

8. Dunia yatawaliwa na mamlaka gani ya ulimwengu leo, na unabii wafunua nini pia kilipaswa kije?

8 Leo tamasha ya ulimwengu imetawaliwa na Mamlaka ya Saba ya Ulimwengu ya historia ya Biblia, Mamlaka ya Ulimwengu ya Mwungano wa Waingereza na Waamerika. Walakini, Biblia yafunua MAMLAKA YA NANE YA ULIMWENGU. Kama ilivyofananishwa katika Ufunuo 17:9-11, mnyama-mwitu mwekundu sana alionyeshwa kwa mtume Yohana katika njozi. Mgongoni pa mnyama huyo alikuwako mwanamke kahaba, ‘Babeli Mkuu.’

9. Biblia yamwelezaje “mnyama” huyu?

9 Twasoma hivi juu ya “mnyama” huyu wa mfano: “Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo. Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache. Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu.”

10. (a) Eleza Ufunuo 17:9-11 kwa habari ya “wafalme saba.” (b) “Kahaba” ampandaye mnyama ni nani, naye amefanya nini?

10 Wakati njozi hii ya Biblia ilipotolewa, katika karne ya kwanza Mamlaka ya Sita ya Ulimwengu, Rumi, ndiyo ilitawala. Ya saba haikuwa imefika. Mamlaka tano zilizotangulia za ulimwengu, ambazo ‘zilikuwa zimekwisha kuanguka’ zilikuwa, kwa kufuatana, Misri, Ashuru, Babeli, Umedi-Uajemi na Ugiriki. ‘Babeli Mkuu’ imekuwa na shughuli na mamlaka zote hizi za ulimwengu, ikijitia katika siasa na kuwa na maongozi makuu humo. Kwa sababu hiyo aitwa “kahaba,” mwenye kufanya uasherati wa kiroho. Aitwa pia “mji ule mkubwa, wenye ufalme juu ya wafalme wa nchi.” (Ufu. 17:18) Kwa hiyo, yeye ni milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, ambamo iitwayo dini ‘ya Kikristo’ imeshiriki sehemu iliyo kubwa. Kama nguvu kubwa katika kupigana na kufanya mamlaka za ulimwengu ziwapige Wakristo wa kweli, yeye “amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu.”​—Ufu. 17:6.

11. Twawezaje kuwaza kwamba “mnyama mwekundu sana” siyo jamii ya mataifa ya Kikomunisti?

11 Huyu “mnyama mwekundu sana” ni “mfalme” wa nane, mamlaka ya nane ya ulimwengu. Kwa kuwa “atoka kwa wale saba,” (NW) siyo jamii ya Kikomunisti ya mataifa. Pia, tofauti na jamii ya Kikomunisti, ‘alikuwako (kwa muda), kisha hakuwako; apanda kutoka shimo refu lisilopimika (la kutotenda) na kuelekea uharibifuni (NW).’

12, 13. (a) Ni kwa njia gani “mnyama” ‘alikuwako,’ ‘hakuwako,’ na ‘alipanda’ kutoka shimo refu lisilopimika? (b) Kwa sababu gani “mnyama” ni “chukizo” machoni pa Mungu? (c) Je! mataifa yote mashirika ya Umoja wa Mataifa yajidai kuupendelea Ukristo?

12 Tengenezo la ulimwengu la amani na usalama, lililojulikana kwanza (‘lilipokuwako’) kama Ushirika wa Mataifa, lilitengenezwa baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Liliingia katika shimo refu lisilopimika mwaka wa 1939, lilipoonyeshwa kuwa hoi kutoweza kukomesha Vita ya Ulimwengu ya Pili (hivyo ‘halikuwako’). Halafu, katika mwaka wa 1945, ‘lilipanda’ likiwa na jina jipya, Umoja wa Mataifa. Ni “chukizo” machoni pa Mungu namna gani? Wa kukumbukwa sana ni uhakika wa kwamba limepandwa na kahaba wa mfano, mwanamke mchafu. Pia, ni “rafiki wa ulimwengu,” hii ikilifanya “adui wa Mungu” kwa kuwa limetengenezwa na mamlaka za kilimwengu na kuinuliwa, hasa na Kristendomu na dini zake, mahali pa ufalme wa Mungu kama tumaini la amani na usalama wa ulimwengu.​—Yak. 4:4; Yohana 18:36.

13 Sasa nusu ya mataifa mashirika ya Umoja wa Mataifa hata hayajidai kuwa Kikristo.

14. Twaweza kusema nini juu ya ubishi wa kwamba Umoja wa Mataifa umefanya mema fulani ulimwenguni?

14 Lakini je! Umoja wa Mataifa haukufanya mema fulani? Wengine wasema, ‘Sababu gani kuukomesha? Huo ni jaribio la kudumisha amani.’ Lakini je! Milki ya Kirumi ilikuwa ‘njema’? Ilijaribu kudumisha Pax Romana, amani ya Kirumi, katika ulimwengu mzima, lakini hata hivyo, ilikuwa ya kipagani nayo ndiyo iliyoharibu Yerusalemu wa kidini na hekalu. Baadaye ilitesa Wakristo wa kweli.

UHARIBIFU WA DINI YA UONGO

15, 16. Biblia yaelezaje uharibifu wa ‘Babeli Mkuu’?

15 Biblia yaonyesha nini yatimizwayo na Umoja wa Mataifa kabla ‘haujaelekea uharibifuni’? Ndio unaoharibu ‘Babeli Mkuu.’

16 Masimulizi yaeleza uharibifu huu wa dini ya uongo: “Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na kutano na mataifa na lugha. Na zile pembe kumi ulizoziona, na huyo mnyama, hao watamchukia yule kahaba, nao watafanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.”​—Ufu. 17:15, 16.

17. Umoja wa Mataifa unageuka kuwa nini kwa dini za Kristendomu?

17 Majeshi ya Kirumi yalileta uharibifu kwa mji mtakatifu Yerusalemu na hekalu lake. Vivyo hivyo, majeshi yaliyo chini ya uongozi wa Umoja wa Mataifa yanapata kuwa mwenye kuharibu uitwao uwanja “mtakatifu” wa michezo wa utawala wa Kristendomu​—⁠dini zake za uongo ‘za Kikristo.’

18-20. (a) Ni nini kwa kweli kiletacho uharibifu huu? (b) Biblia yampaje Yehova sifa kwa uharibifu wa dini ya uongo?

18 Ni nini hasa kiletacho uharibifu huu? ni wazo tu la Umoja wa Mataifa? Ni hukumu ya Mungu juu ya matengenezo ‘ya kikahaba’ ya dini za uongo ambazo zimeonea watu kwa muda mrefu na kufanya hivyo kwa kujisingizia kama dini, zikimwakilisha Mungu vibaya na kuliletea jina lake suto. Hivi ndivyo ilivyo hasa na kwa wazi juu ya dini za Kristendomu. Masimulizi yafunua hasa anayefanyizisha ‘Babeli Mkuu’ kazi ya kuharibu yanaposema:

19 “Maana Mungu ametia mioyoni mwao [mioyoni mwa watawala wa dunia] kufanya shauri lake, na kufanya shauri moja, na kumpa yule mnyama ufalme wao hata maneno ya Mungu yatimizwe.”​—Ufu 17:17.

20 Kwa sababu hiyo Yehova Mungu ndiye apataye sifa kwa kuondolea mbali dini ya uongo. Yeye apewa sifa ya hili katika sura ifuatayo ya Ufunuo, katika kelele hii: “Furahini juu yake [Babeli Mkuu], . . . kwa maana Mungu amehukumu hukumu yenu juu yake.”​—Ufu. 18:20.

21. Baada ya “mnyama mwekundu sana” kuharibu dini ya uongo, atakuwa rafiki ya Wakristo wa kweli?

21 Basi “mnyama” wa rangi nyekundu atakuwa rafiki ya Wakristo wa kweli? Sivyo kama vile Milki ya Kirumi isivyokuwa. Kama adui, lazima “mnyama” huyo ‘aelekee uharibifuni’ mikononi mwa Yesu Kristo. Wafalme wanaofananishwa na pembe kumi za mnyama ‘watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana-Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme.’ (Ufu. 17:14) “Chukizo” litaangamia wakati huo, lisitokee tena kamwe.

WAKATI WA KUCHUKUA HATUA

22, 23. Ni hatua gani ya haraka ipendekezayo Biblia kwa watu walio washirika wa matengenezo ya ‘Babeli Mkuu’?

22 Sura ya “chukizo” sasa juu ya tamasha ya ulimwengu ni sehemu ya “ishara” ya kuwapo kwa Kristo na kukaribia kwa shambulio lake juu ya Mwana-Kondoo. Kwa hiyo, unaokaribia hata zaidi ni uharibifu wa ‘Babeli Mkuu.’ Hii ina maana gani kwa wale ambao huenda wanahusika na matengenezo haya ya kilimwengu?

23 Neno la Mungu lasihi: “Tokeni kwake [Babeli Mkuu], enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.”​—Ufu. 18:4.

24. Kwa sababu gani inastahili jitihada zote kufuata onyo la Biblia kutoka katika ‘Babeli Mkuu’?

24 Mtu aweza kuokoka kwa kujifunza Biblia aone kwamba wakati huu wa hukumu umetufikia, na kwa kutofautisha tu kati ya dini ya kweli na uongo. Lakini inastahili jitihada yo yote inayohitajiwa. Kwa maana uzima utafurahisha duniani baada ya uharibifu wa matengenezo yote yenye udhalimu na yenye kumdharau Mungu. Kisha, watu watapata mapozo na afya ya sikuzote. Mamilioni ambao wamepoteza maisha zao kwa sababu ya utawala wa udanganyifu wenye kumwaga damu wa ‘Babeli Mkuu’ watafufuliwa wajiunge na wale watakaokuwa duniani waufurahie uharibifu wa dini ya uongo.​—Ufu. 20:11-13; 21:1-4.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki