Wao Hufanya Lile Wawezalo
Ingawa hawawezi kumlipa Yehova kwa faida zake zote kwao, wengi hufanya lile wawezalo kuitegemeza kazi ya kuhubiri ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wake. (Mathayo 24:14; linganisha Marko 14:3-9.) Yenye kupendeza kuhusu jambo hilo ni barua hii kutoka kwa familia huko Minnesota (U.S.A.):
“Ndugu Wapendwa,
“Tunapeleka upaji wa kiasi cha dola _._. Tunaomba kwamba utumiwe kwa kulipa gharama za kazi ya ulimwenguni pote au uwekwe katika Hazina ya Kujenga Majumba ya Ufalme, au kwa uhitaji mwingine wowote ambao huenda tengenezo likawa nao. . . .
“Tuna uhakika kwamba pesa hizo zitatumiwa kwa kupatana na mapenzi ya [Yehova]. Tungependa kuchukua nafasi hii kuwatolea kitia-moyo chetu kuendelea na kazi nzuri, na hasa kuwashukuru kwa ajili ya tepu ya video ya utendaji wa ulimwenguni pote wa Sosaiti ya [Watch Tower]. Tepu hiyo ndiyo iliyotuarifu juu ya ukubwa wa kazi hiyo, nayo ilikazia juu yetu kwamba michango yetu ya hiari inahitajiwa. Mbeleni, tulikuwa tumeacha kundi, mzunguko, na wilaya ishughulike na kuwapelekea michango, lakini sasa tunamshukuru Yehova kwa ajili ya kuwa mwenye saburi nasi katika ukosefu wetu wa busara na kutuonyesha kwa upendo uhitaji wetu wa kusaidia kibinafsi katika kulipa gharama ya kazi hii yenye kuokoa uhai, kuongezea zile namna nyingine za michango. Tumenuia kupeleka, tukiwa familia, kiasi kisichopungua dola _._ kwa mwezi . . . moja kwa moja hadi New York.
“Asanteni tena, kwa utumishi wenu mzuri ambao mmetupa na kwa uaminifu kwa Yehova ambao mmeonyesha.”