Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 12/15 kur. 25-28
  • Ni Huduma kwa Ajili Yako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Huduma kwa Ajili Yako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uhitaji wa Wahudumu
  • Huduma ya Kikristo
  • Je! Yapasa Iwe Kazi-Maisha Yako?
  • Fikilia Kuwa na Huduma Kamili Zaidi
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Wahudumu wa Mungu Ni Akina Nani Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Ni Lazima Wakristo wa Kweli Wote Wawe Wahudumu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Ni Nani Walio Wahudumu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 12/15 kur. 25-28

Ni Huduma kwa Ajili Yako?

YEHOVA ameonyesha ukarimu wake kwa kuiandaa dunia kikamili ili sisi tuonee uhai shangwe. Kwa ukarimu alikubali maandalizi hayo yabaki hata baada ya Adamu na Hawa kuasi. Zaidi ya hayo, ameonyesha upendo wake unaozidi wote kwa kumtuma Mwana wake kuwaokoa wanadamu wenye kuamini kutokana na msiba wa dhambi.—Mathayo 5:45; Yohana 3:16.

Tunaweza kuitikiaje upendo wa jinsi hiyo? Yesu alisema kwamba ni lazima tumpende Yehova Mungu wetu kwa moyo, nafsi, akili na nguvu zetu zote. Hilo ladokeza kwamba tunawiwa naye ibada na uaminifu-mshikamanifu wetu na kwamba twapaswa kuishi maisha zetu kulingana na mapenzi yake.—Marko 12:30; 1 Petro 4:2.

Lakini ni nini kinachotiwa ndani katika kufanya mapenzi ya Mungu? Je! kuna utumishi ambao twaweza kumtolea—huduma ambayo twapaswa kushiriki?

Uhitaji wa Wahudumu

Makanisa yamewavuruga watu kuhusu jinsi ya kumwabudu na kutumikia Mungu. Hata hivyo, Biblia huonyesha kwamba kuna dini moja tu ya kweli, “Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote.” Yesu alisema hivi: “Waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli.” Kwa hiyo wanashauriwa hivi: “Nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka.”—Waefeso 4:3-6; Yohana 4:23; 1 Wakorintho 1:10.

Mvurugo kuhusu ni gani iliyo dini ya kweli ulianza Edeni wakati Shetani alipopinga haki ya enzi kuu ya Yehova kwa kushuku njia ya Mungu ya kutawala. (Mwanzo 3:1-6, 13) Shetani sasa hutegemeza upinzani huo dhidi ya Mungu kwa mafundisho bandia yanayoenezwa na wahudumu wadanganyifu wa kidini ambao ‘hujigeuza wawe mfano wa malaika wa nuru.’ Kwa hiyo Biblia husema hivi: “Wapenzi, msiiamini kila roho . . . kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.”—2 Wakorintho 11:14, 15; 1 Yohana 4:1.

Kwa furaha, Mungu amechukua hatua za kusuluhisha swala hilo la utawala. Akiwa amemtuma Mwana wake kuikomboa ainabinadamu, sasa amemfanya Yesu kuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu wa kimbingu, akiwa na mamlaka ya kumharibu Shetani na manabii, au wahudumu wake. Hilo litahakikisha kwamba mapenzi ya Mungu yanafanywa duniani, kwa baraka ya milele ya watu watiifu.—Danieli 7:13, 14; Waebrania 2:9.

Shetani amezificha kweli hizo. (2 Wakorintho 4:4) Hivyo, tunahitajiwa kutumikia tukiwa wahudumu wa Mungu, tukifichua mambo bandia ya Shetani na kuitolea kweli ushahidi. Yehova hatulazimishi tuingie katika utumishi huo. Anatutaka, kama Yesu, tuwe na nia ya kujitoa wenyewe kwa sababu ya kumthamini yeye na yale ambayo ametufanyia.—Zaburi 110:3; Waebrania 12:1-3.

Huduma ya Kikristo

Yesu “alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu.” (Luka 8:1) Pia yeye aliwazoeza wanafunzi wake kuwa wahudumu kama yeye na akawatuma waende kuhubiri. (Mathayo 10:1-14, 27) Baadaye, aliwapa utume wa kuendeleza huduma hiyo hadi mifikio ya mbali ya dunia.—Mathayo 28:19, 20; Matendo 1:8.

Utume huo ni wajibu wa Wakristo wa kweli, na roho ya Mungu huwachochea wahubiri. Kama ilivyotukia Pentekoste 33 W.K., wote wanaokubali habari njema huchukua daraka la kufanya tangazo la peupe la imani yao.—Matendo 2:1-4, 16-21; Warumi 10:9, 13-15.

Lakini, watu wengi hawawezi kujiona wenyewe wakiwa wahudumu. Peter, mmoja wa Mashahidi wa Yehova, asema hivi: “Wanaume katika Ujerumani mara nyingi huliona kuwa jambo la kushusha cheo kuongea juu ya dini. ‘Hilo lapasa kufanywa na makasisi,’ wao husema.” Kulingana na Tony, ambaye amekuwa misionari kwa miongo mingi, watu katika Uingereza wamesema hivi: “Lile mnalosema ni zuri, na mimi nafikiri kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wema. Lakini kwenda nyumba kwa nyumba nikihubiri—nisingeweza kufanya hivyo hata kidogo.” Ben alijifunza Biblia kwa kitambo fulani pamoja na mwanamume wa Naijeria aliyemwambia hivi: “Siwezi kujionyesha mwenyewe nikihubiri peupe kutoka nyumba kwa nyumba; lakini ningeweza kutolea kundi lenu pesa za kuwasaidia wale walio na nia ya kufanya hivyo.” Naam, watu wengi hukosa imani na usadikisho unaohitajiwa kwa ajili ya huduma ya Kikristo.

Hata hivyo, kuhubiri peupe ni daraka la wote katika kundi la Kikristo, haidhuru umri wala jinsia yao. Si kwa wazee na watumishi wa huduma tu, ‘wanaoongoza,’ bali pia ni kwa Wakristo kwa ujumla. Wote wanahimizwa hivi: “Na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake. . . . Watiini wenye kuwaongoza.”—Waebrania 13:15, 17.

Akihutubia umati wa mchanganyiko katika Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu alisema hivi: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.” Katika pindi nyingine alionyesha kwamba kufanya mapenzi ya Mungu kwatia ndani kuhubiri wasioamini. Wanafunzi wake walikuwa wakimsihi aache kuwahubiri Wasamaria fulani ili ale, lakini alisema hivi: “Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.”—Mathayo 7:21; Yohana 4:27-38.

Je! Yapasa Iwe Kazi-Maisha Yako?

Kwa kawaida watu hupendelea kufuatia chakula cha kimwili na mali. Lakini mapema katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu aliwashauri wasikilizaji wake dhidi ya kufuatia mambo kama hayo kwa wasiwasi. “Bali,” akasema, “jiwekeeni hazina mbinguni . . . Utafuteni kwanza ufalme wake, na haki [ya Mungu].”—Mathayo 6:20, 33.

Kuutafuta kwanza Ufalme unamaanisha kutokubali mapendezi mengine yapunguze umaana wa huduma yetu. Hata hivyo, kufanya hivyo hakumaanishi kuondolea mbali mambo mengine yote. Kwa mfano, Biblia hututia moyo tusikose kutunza wajibu mbalimbali wa familia ulio halisi. Sisi tuna wajibu huo mbalimbali kama wanadamu wengine wote. Kukosa kuutunza ni kutenda katika njia iliyo kinyume na imani ya Kikristo. (1 Timotheo 5:8) Hata hivyo, twapaswa kufanya yote tuwezayo kufanya kwa kufaa katika huduma huku tukishughulikia madaraka mengine katika njia iliyosawazika.

Yesu alisema hivi: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa . . . kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Muktadha wa unabii huo huuweka utimizo wao katika siku yetu. Tangu 1914 habari njema ni kwamba Ufalme umepewa uwezo wa kutenda kwa kuunga mkono enzi kuu ya Yehova na dhidi ya Shetani na ulimwengu wake. (Ufunuo 11:15-18) Twapaswa kufikiria kwa uzito maana ya hilo. Mwisho utakuja, na ni lazima tutimize kazi ya kuhubiri kabla ya wakati huo. Maisha yamo hatarini; twaweza kusaidia kuokoa mengi yayo.

Fikilia Kuwa na Huduma Kamili Zaidi

Mashahidi wa Yehova walio wengi hutoa muda wa saa kumi au zaidi kila mwezi kushiriki habari njema pamoja na wengine. Maelfu hutumia muda wa saa mbili au zaidi kila siku katika kuhubiri wakiwa mapainia wasaidizi, na wengine hutumikia daima wakiwa mapainia wa kawaida na wa pekee. Wanathamini uharaka wa kazi hiyo na hutaka kushiriki kikamili wawezavyo ili waitimize kabla ya kuja kwa mwisho wa ulimwengu huu usio na furaha.

Je! wewe tayari ni Shahidi wa Yehova mwenye kutenda? Basi fikilia uwe na ushiriki kamili zaidi katika utumishi. Fanyia maendeleo ustadi wako katika kuhubiri na kufundisha, ukijaribu kuwa na matokeo zaidi katika huduma. Ikiwa una uwezo wa kuwa painia, fanya hivyo. Ikiwa hali zako kwa kweli hazikuruhusu ufanye hivyo, basi watie moyo wale wawezao wafikilie utumishi huo.

Ikiwa wewe si Shahidi wa Yehova aliyejiweka wakfu, usiseme kwamba huduma si kwa ajili yako. Mwanamume mwingine aitwaye Peter, mhandisi wa mashine, alikataa kwa uthabiti mke wake asishiriki habari njema pamoja na wengine. “Naweza kuruhusuje mke wangu ahubiri kutoka nyumba kwa nyumba?” alikuwa akiuliza. Baada ya miaka ya kuchunguza usadikisho imara wa mke wake kuhusu kweli ya Neno la Mungu, aliamua kujifunza Biblia pia. Sasa, kama mke wake, yeye ni mhudumu wa habari njema aliyejiweka wakfu na kubatizwa.

Basi usijizuie mwenyewe usiwe na pendeleo la kumtumikia Yehova. Tunakutia moyo ujifunze Biblia na kushirikiana na Wakristo wa kweli kwenye mikutano yao. Hilo litakusaidia ufinyange maisha yako kupatana na uadilifu wa Mungu na kujenga imani imara katika makusudi yake. Ukifanya maendeleo katika hilo, wewe pia utastahili kuwa mhudumu wa Mungu. Kisha utakuwa na pendeleo la kushiriki katika kutekeleza amri hii ya Yesu: “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi . . . kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi.”—Mathayo 28:19, 20.

Naam, kuna huduma ambayo wewe waweza kuishiriki, na ni jambo la uharaka zaidi ya wakati mwingine wowote ufanye hivyo.

[Picha katika ukurasa wa 25]

Mwuguzi mmoja aliye na familia ya kutunza asema hivi: “Mimi husafiri zaidi ya muda wa saa moja kila siku kwenda hospitali ninakofanya kazi, kwa hiyo nilifikiri singeweza kufanya upainia msaidizi. Lakini nilipanga shughuli zangu kwa uangalifu ili kushiriki katika utumishi wa shambani mapema kila asubuhi kabla ya kwenda kazini, wakati wa vipindi vya mapumziko, na katika siku za kupumzika. Waweza kuwazia shangwe yangu wakati, kufikia mwisho wa mwezi mmoja, nilikuwa nimetumia saa 117 katika kuhubiri! Niliangusha magazeti 263, maandikisho 22 kwa magazeti, na kuweza kuanzisha mafunzo ya Biblia 3.”

[Picha katika ukurasa wa 27]

Michael ana watoto wachanga saba, naye ana kazi yenye madaraka katika chuo cha Naijeria. Yeye pia ni mzee katika kundi la Kikristo. Yeye hushiriki maoni ya maelfu ya Mashahidi:

“Mimi huona huduma kuwa kazi-maisha yangu na hukumbuka sikuzote kwamba Paulo alisema: ‘Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.’ Mke wangu na mimi ‘hupanda’ katika mazungumzo mafupi ya habari njema nyumba kwa nyumba. ‘Tunatia maji’ kwa kurudia wale waonyeshao kupendezwa ili kuwafundisha kutoka Biblia, kama Yesu alivyosema twapaswa kufanya. Mafunzo ya Biblia nyumbani ya kila juma yamesaidia hesabu kubwa ya watu—katika visa fulani familia nzima-nzima—wapate maarifa ya kweli.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki