Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 3/1 kur. 5-7
  • Je! Mipango kwa Ajili ya Usalama wa Kimataifa Itafanikiwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Mipango kwa Ajili ya Usalama wa Kimataifa Itafanikiwa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Yasema Nini?
  • Usalama wa Kweli Duniani
  • Amani na Usalama wa Kweli Ni Karibu!
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Amani na Usalama Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Amani Kutoka kwa Mungu Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kutazama Mbele ya “Amani na Usalama” Wenye Kufanyizwa na Binadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 3/1 kur. 5-7

Je! Mipango kwa Ajili ya Usalama wa Kimataifa Itafanikiwa?

“VITA baridi, ambayo imekumba ulimwengu kwa miaka zaidi ya 40 yaonekana imeisha kwa rehema ya Mungu,” lataarifu One World, gazeti la WCC (Baraza la Makanisa Ulimwenguni). “Matokeo ya maana katika Ulaya ya Kati na Mashariki . . . yaonekana kuwa ishara nzuri kwa amani na usalama katika Ulaya na sehemu nyinginezo za ulimwengu,” aongeza mwandikaji Mwanglikana John Pobee, wa Programu juu ya Elimu ya Kitheolojia ya WCC.

Si wawakilishi wa WCC peke yao wanaohusisha Mungu na mipango ya mwanadamu kwa ajili ya usalama wa kimataifa. Katika Aprili 1991, muda mfupi baada ya vita ya Ghuba ya Ajemi, Papa John Paul alimpelekea ujumbe katibu mkuu wa UM wa wakati huo Havie Peres di Kweya ambao katika huo alisema: “Maaskofu wa Makanisa Katoliki ya Mashariki ya Kati na Magharibi wana uhakika katika kazi ya Umoja wa Mataifa . . . Wanatumaini kwamba, kupitia Umoja wa Mataifa na mashirika yayo yenye kufanya kazi maalum, wale walio katika hali ya uhitaji mwingi kwa sababu ya vita hiyo ya karibuni hawatakosa kuhurumiwa na kuungwa mkono kimataifa.”

Zaidi ya hayo, Vatikani ilikuwa mojawapo ya zile nchi 35 zilizofanyiza na kutia sahihi ule Mwafaka wa Helsinki wa 1975 na pia ile Hati ya Stockholm ya 1986. Wakati Umoja wa Mataifa ulipotangaza 1986 kuwa “Mwaka wa Kimataifa wa Amani,” papa aliitikia kwa kualika wawakilishi wa dini kubwa kubwa za ulimwengu washiriki katika mwadhimisho wa “Siku ya Ulimwengu ya Sala kwa Ajili ya Amani.” Katika Oktoba 1986, wawakilishi wa imani za Kibuddha, Kihindu, Kiislamu, Kishinto, Kianglikana, Kilutheri, Orthodoksi ya Kigiriki, Kiyahudi, na imani nyinginezo waliketi pamoja katika Assisi, Italia, na kusali kwa zamu kwa ajili ya amani ya ulimwengu.

Miaka kadhaa baadaye, katika hotuba aliyotoa Roma, Askofu Mkuu wa Kantabari wa Anglikana alikumbuka pindi hiyo iliyo juu. “Katika Assisi,” akasema, “tuliona kwamba Askofu wa Roma [papa] alikuwa ameweza kukusanya Makanisa ya Kikristo pamoja. Tuliweza kusali pamoja, kuongea pamoja na kutenda kazi pamoja kwa ajili ya amani na hali njema ya aina ya kibinadamu . . . Katika hatua hiyo ya kwanza ya sala kwa ajili ya amani ya ulimwengu nilihisi nikiwa mbele ya Mungu aliyesema ‘Tazama nafanya jambo jipya.’”

Dini nyinginezo, ingawa hazikuwakilishwa katika Assisi, zina matazamio mazuri pia kuhusu mipango ya mwanadamu kwa ajili ya usalama wa kimataifa. Uhariri katika Die Kerkbode jarida rasmi la Dutch Reformed Church la Afrika Kusini, ulisema hivi: “Tunaona badiliko la kuingia utaratibu wa ulimwengu mpya. Jambo lililoonekana kutowezekana miaka michache iliyopita latukia leo mbele ya macho yetu. Upatano unaotukia katika sehemu kuu zaidi ya ulimwengu kati ya Urusi na Magharibi unaathiri maeneo makubwa. Katika sehemu yetu ya ulimwengu, watu wanaopingana kwa kawaida na maadui wa mwisho wanasemezana, na himizo kuelekea ‘amani’ linatokea kila mahali . . . Kulingana na maoni ya Kikristo, jitihada zote za kuleta amani kati ya watu zapasa kukaribishwa. Twaweza kusali kwa ajili ya amani katika wakati wetu.”

Je! Mungu anabariki mipango ya mwanadamu kwa ajili ya usalama wa kimataifa?

Biblia Yasema Nini?

Kuhusu habari ya kutegemea jitihada za kibinadamu, Biblia hutoa onyo la moja kwa moja: “Msiwatumainie wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.” (Zaburi 146:3, 4) Maendeleo ya siku hizi kuelekea amani yaweza kuonekana kuwa yenye kutia moyo. Lakini ni lazima tuyaone mambo kihalisi. Uwezo wa wanadamu umepungukiwa. Mara nyingi, matukio ni makubwa kuliko wanadamu. Mara nyingi hawawezi kutambua visababishi, mambo yaliyofichika, yanayoharibu mipango yao iliyofikiriwa sana.

Miaka 700 kabla ya wakati wa Yesu, katika siku za nabii Isaya, viongozi Wayahudi walikuwa wakipangia usalama kupitia mikataba ya kimataifa pamoja na nchi za jirani katika njia inayofanana na yale yanayotukia leo. Katika siku hizo pia, viongozi wa kidini waliunga mkono yale ambayo wanasiasa walikuwa wanafanya. Lakini Isaya alionya hivi: “Fanyeni shauri [mpango, NW] pamoja, nalo litabatilika; semeni neno, lakini halitasimama.” (Isaya 8:10) Mpango wao ukawa wenye maafa. Je! jambo kama hilo laweza kutukia leo?

Naam, laweza, kwa kuwa kupitia nabii huyo huyo, Mungu alitangaza kwamba Yeye ana njia Yake mwenyewe ya kuleta usalama duniani. Itakuwa, si kupitia tengenezo lolote la kibinadamu, bali kupitia mzao wa mfalme Mwisraeli Daudi. (Isaya 9:6, 7) Mrithi huyo wa Mfalme Daudi ni Yesu Kristo, ambaye, alipohojiwa na Pontio Pilato, alikiri kwamba alikuwa Mfalme lakini alisema hivi: “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu.” (Yohana 18:36; Luka 1:32) Kwa kweli, Ufalme wa Yesu ungekuwa wa kimbingu. Nao—si Umoja wa Mataifa wala taifa lolote la kisiasa la kidunia—ndio ungeleta usalama wa kudumu, wenye kutegemeka, kwenye dunia hii.—Danieli 2:44.

Yesu Kristo alitabiri kwamba Ufalme wake ungeanza kutawala kutoka mbingu wakati kungekuwa “habari za vita na matetesi ya vita,” kukiwa na ‘taifa likiondoka kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.’ Utimizo wa unabii watia alama 1914 kuwa ndio wakati ambao hayo yalitukia na hutambulisha miaka tangu wakati huo kuwa “umalizio wa mfumo wa mambo.”—Mathayo 24:3, NW, 6-8.

Hilo lamaanisha nini? Kwamba wakati unaobaki wa mfumo wa ulimwengu uliopo sasa ni mfupi, na hivi karibuni utaisha. Je! hiyo ni sababu ya hangaiko au huzuni? Sivyo tukikumbuka ule ukatili, ukosefu wa haki, uonevu, vita, na kuteseka kote ambako kumetia alama mfumo huu wa mambo. Kwa hakika kutakuwako kitulizo chini ya mtawala ambaye Neno la Mungu, Biblia, husema hivi juu yake: “Na roho ya BWANA [Yehova, NW] atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na kumcha BWANA [Yehova, NW].”—Isaya 11:2.

Usalama wa Kweli Duniani

Kwa kweli, hakutakuwako kamwe usalama wa kweli duniani mpaka ule unabii wa Isaya utimizwe ulimwenguni pote, chini ya Ufalme wa Mungu: “Mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.” (Isaya 65:17) Hata iwe ni sala ngapi ambazo viongozi wa kidini wanatoa kwa ajili ya ulimwengu huu, mipango ya kibinadamu kwa ajili ya usalama wa kimataifa haiwezi kuchukua mahali pa njia ya Mungu ya kuleta amani na usalama.

Usalama wa kudumu wa ulimwenguni pote ambao Ufalme wa Mungu unaleta utakuwa mtukufu. Hapa ni mojawapo tu ya maelezo yanayopatikana katika Biblia: “Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe. Bali wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu; kwa kuwa kinywa cha BWANA [Yehova, NW] wa majeshi kimesema hivi.”—Mika 4:3, 4.

Ni usalama uliohakikishiwa na Mungu mwenyewe tu ndio waweza kuwa wenye kudumu na wenye kutegemeka. Hivyo, badala ya kuweka tumaini lako kwa wakuu, kwa nini usiweke tumaini lako kwake? Ndipo utakapopata kwamba maneno ya mtunga zaburi ni ya kweli: “Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, na tumaini lake ni kwa BWANA [Yehova, NW], Mungu wake. Aliyezifanya mbingu na nchi, bahari na vitu vyote vilivyomo. Huishika kweli milele.”—Zaburi 146:5, 6.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Kanisa Katoliki na Siasa za Kimataifa

“Ingawa Kristo alisema kwamba ufalme wake ‘sio wa ulimwengu huu,’ makasisi wenye vyeo vya juu na upapa ukiwa shirika umeshiriki kwa bidii katika mapambano ya kisiasa ya kimataifa na kitaifa tangu wakati wa Konstantino.” —“The Catholic Church in World Politics,” cha Profesa Eric Hanson wa Chuo Kikuu cha Santa Clara cha Kiyesuiti.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki