Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 4/15 uku. 31
  • Tangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tangazo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Usaidizi kwa Halmashauri za Baraza Linaloongoza
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Mabadiliko Katika Baraza Inayoongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Jinsi Ambavyo Baraza Linaloongoza Limepangwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Uandalizi wa Yehova Wale ‘waliopewa’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 4/15 uku. 31

Tangazo

Usaidizi kwa Halmashauri za Baraza Linaloongoza

Washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, wakiwa 12 sasa, huendelea kutumikia kwa uaminifu katika migawo yao. Wanashukuru sikuzote wale washiriki waaminifu-washikamanifu wa “mkutano mkubwa” wanaozidi kuongezeka kwa ajili ya utegemezo wao wenye bidii. (Ufunuo 7:9, 15) Kwa sababu ya ongezeko hilo kubwa ulimwenguni pote, yaonekana kwamba inafaa wakati huu kuandalia Baraza Linaloongoza usaidizi wa ziada. Kwa hiyo imeamuliwa kualika wasaidizi kadhaa, hasa kutoka miongoni mwa mkutano mkubwa, kushiriki katika mikutano ya kila moja ya Halmashauri za Baraza Linaloongoza, yaani, Halmashauri ya Wafanyi Kazi, ya Utangazaji, ya Utumishi, ya Ufundishaji, na ya Uandikaji. Hivyo, idadi ya watu watakaohudhuria mikutano ya kila moja ya halmashauri hizi itaongezeka kuwa saba au nane. Chini ya mwelekezo wa washiriki wa halmashauri za Baraza Linaloongoza, wasaidizi hao watashiriki katika mazungumzo na kutekeleza migawo mbalimbali wanayopewa na halmashauri. Mpango huo mpya waanza Mei 1, 1992.

Kwa muda wa miaka mingi sasa, idadi ya mabaki ya Mashahidi wapakwa-mafuta imeendelea kupungua, huku idadi ya mkutano mkubwa ikiongezeka kupita matazamio yetu makubwa zaidi. (Isaya 60:22) Twamshukuru Yehova kama nini kwa ajili ya upanuzi huo mzuri ajabu! Jina jipya, Mashahidi wa Yehova, lilipokubaliwa kwa shukrani katika 1931, kilele cha idadi ya wahubiri wa Ufalme kilikuwa 39,372, wengi wao wakiwa wale waliodai kuwa ndugu wa Kristo wapakwa-mafuta. (Isaya 43:10-12; Waebrania 2:11) Miaka sitini baadaye, katika 1991, kilele cha wahubiri ulimwenguni pote kilikuwa 4,278,820, ambao kati yao ni 8,850 tu waliodai kuwa mabaki ya wapakwa-mafuta. Kama ilivyotazamiwa kulingana na nuru ya Maandiko, “mkutano mkubwa” wako wengi kuliko mabaki ya “kundi dogo” kwa uwiano wa zaidi ya 480 kwa 1. (Luka 12:32; Ufunuo 7:4-9) Katika kushughulikia masilahi ya Ufalme yanayoongezeka, hakika mabaki wanahitaji na huthamini ushirikiano na utegemezo wa mkutano mkubwa.

Kama ilivyoelezwa katika toleo hili la Mnara wa Mlinzi, kuna kikundi kinachotumikia pamoja na Israeli wa kiroho kinacholingana na Wanethini na wana wa watumishi wa Sulemani waliorudi kutoka uhamisho wa Kibabuloni pamoja na mabaki Wayahudi; wasio Waisraeli hao hata walikuwa wengi kuliko Walawi waliorudi. (Ezra 2:40-58; 8:15-20) Wale “waliopewa” kutoka miongoni mwa mkutano mkubwa wa leo ni wanaume Wakristo wakomavu ambao wamekuwa na ujuzi mwingi ukiwa tokeo la kushughulikia uangalizi katika matawi, katika kazi ya kusafiri, na miongoni mwa yale makundi 66,000 yaliyosimamishwa sasa kotekote duniani.

Hivi karibuni, Shule za Huduma ya Ufalme zilifanywa ulimwenguni pote ili kuwafunza waangalizi na wasaidizi wao watumishi wa huduma. Katika United States pekee, waangalizi 59,420 walihudhuria. Hivyo “wazee” hao walitayarishwa kutimiza madaraka yao kwa mafanikio zaidi.—1 Petro 5:1-3; linganisha Waefeso 4:8, 11.

Kwenye makao makuu ya Brooklyn ya Mashahidi wa Yehova, baadhi ya wale “waliopewa” wametumikia kwa muda wa miaka mingi sana. Hao hutia ndani waangalizi wakomavu kutoka katika ule mkutano mkubwa ambao wamepata uwezo na ujuzi mwingi sana. Hivyo, Baraza Linaloongoza limeteua wachache kati ya waangalizi hao wasaidie katika mikutano ya halmashauri za Baraza Linaloongoza. Hao sio kwa lazima wanaume ambao wamekuwa na rekodi refu zaidi ya utumishi. Badala ya hivyo, wao ni wanaume wakomavu, wenye ujuzi walio na sifa ambazo huwastahilisha kutoa usaidizi katika nyanja mahususi. Kupewa kwao mgawo wa kufanya kazi pamoja na halmashauri fulani hakuwapi cheo cha kipekee. Kama Yesu alivyosema kuhusu wanafunzi wake, “nyote ni ndugu.” (Mathayo 23:8) Hata hivyo, wanaume hao watapewa vingi, na kwa hiyo “vitatakwa vingi” kutoka wao.—Luka 12:48.

Twashangilia katika mwendo wa kusonga mbele wa tengenezo la Yehova leo. Muda wa miaka kumi iliyopita, kumekuwako karibu ongezeko la asilimia 100 katika idadi ya wale wanaohudumu shambani, kwa kupatana na unabii kuhusu Daudi Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo: “Kwa habari ya ongezeko la serikali yake na amani hakutakuwa na mwisho.” (Isaya 9:7, King James Version) Katika njia ile ile ambayo Wanethini walifanya kazi pamoja na makuhani katika kutengeneza upya kuta za Yerusalemu, ndivyo ule unabii kuhusu tengenezo la Yehova unavyotimizwa leo: “Na wageni watajenga kuta zako.” (Isaya 60:10; Nehemia 3:22, 26) Wanethini wa ki-siku-hizi wapaswa kupongezwa kwa ajili ya bidii ile wanayoonyesha katika kuijenga ibada ya kweli, wakiwasaidia “makuhani wa BWANA [Yehova, NW]” katika kazi au utumishi wowote ule ambao huenda wakapewa kuwa mgawo katika tengenezo la Yehova la ulimwenguni pote.—Isaya 61:5, 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki