Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 8/1 uku. 25
  • Kuiacha Nuru Yao Iangaze Katika India

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuiacha Nuru Yao Iangaze Katika India
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • “Acheni Nuru Yenu Iangaze” ili Yehova Atukuzwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • “Acheni Nuru Yenu Iangaze”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • “Acheni Nuru Yenu Ing’ae”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kuacha Nuru Yetu Ing’ae kwa Uendelevu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 8/1 uku. 25

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Kuiacha Nuru Yao Iangaze Katika India

Habari njema ya Ufalme inahubiriwa katika India na Mashahidi 11,524 wenye shangwe. (Mathayo 24:14) Wale 1,066 waliobatizwa katika mwaka wa utumishi wa 1991 ni wapiga mbiu ya Ufalme, wanaoiacha nuru yao iangaze kwa wengine. Wote walifurahi kama nini kuona hudhurio la 28,866 wakihudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho wa kifo cha Kristo.

◻ Wengi hujifunza juu ya tumaini la Ufalme kwa mara ya kwanza kupitia ushahidi wa vivi-hivi. Kwa mfano, Shahidi mmoja aliwaambia wafanyakazi wenzake, waliokuwa maseremala pia, kuhusu Ufalme. Mfanyakazi mmoja aliitikia akaanza kuiacha nuru yake iangaze kwa familia na marafiki wake. Hao kwa shangwe waliwapitishia wengine ujumbe huo wa Ufalme mzuri ajabu. Kulingana na ripoti, katika muda wa miaka michache tu, ‘watu zaidi ya 30 walikuwa wamejifunza kweli.’ Yehova alimbariki yeye na ndugu zake wapya wa kiroho kwa ajili ya kuiacha nuru yao iangaze.

◻ Ndugu mmoja mchanga katika kundi jingine aliiacha nuru yake iangaze kwa kuwatolea wanafunzi wenzake shuleni ushahidi wa vivi-hivi. Wengine wao walipendezwa na tumaini la Ufalme, naye mara nyingi aliwaelezea Biblia hadi baada ya usiku wa manane. Mmoja, Mkatoliki, alichukua msimamo imara kwa ajili ya kweli ijapokuwa kuonwa na padri juu ya matokeo makali ikiwa angeendelea kushirikiana na Shahidi huyo. Hata hivyo, mwanafunzi huyo alisadiki kwamba alikuwa akijifunza kweli ya Biblia kutoka kwa Mashahidi, naye akaendelea kutwaa maarifa. Hatimaye alibatizwa na sasa hutumikia akiwa mtumishi wa huduma kundini. Yeye hushangilia katika tumaini linalotokana na ile nuru nzuri ajabu ya kweli!—Warumi 12:12.

◻ Mwingine aliyemsikiliza Shahidi huyo mchanga alikuwa mwanafunzi aliyejulikana sana, ambaye hakuamini kuwako kwa Mungu, naye alikuwa akidhihaki wale waliodai kuamini katika Mungu, lakini siku moja alijiunga katika mazungumzo na kuuliza maswali mengi. Alishangaa alipopata majibu yenye kupatana na akili kwa maswali yake yote akafikia mkataa kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Alifanya maendeleo katika maarifa ya Biblia na hatimaye akabatizwa. Baba yake Mhindu alimpinga kufikia hatua ya kumfukuza kutoka nyumbani. Hata hivyo, msimamo imara wa kijana huyo kwa ajili ya kweli ulithawabishwa wakati ndugu zake wawili wa kimnofu na marafiki wake wawili walipoikubali kweli na kubatizwa. Mmoja wa ndugu zake sasa hutumikia kwenye ofisi la tawi katika India.

◻ Kiongozi mmoja wa wanafunzi alijiunga katika mazungumzo pamoja na Shahidi huyo mchanga. Alikuwa mwenye kuvuta sigareti mfululizo na mwenye kunywa vileo sana. Wakati mmoja, alikuwa ametaka kuwapiga wanafunzi wenzake wawili waliokuwa wamejifunza kweli kutoka kwa Shahidi huyo. Kwa sababu ya kuikubali kweli, walikuwa wamekataa kujiunga katika mgomo wa chuo na pia hawangetoa damu wakati wa kampeni ya ukusanyaji-damu iliyotangulizwa na kiongozi huyo wa wanafunzi. Kijana huyo sasa afurahi kuwa Shahidi mchukuaji nuru wa Yehova.

◻ Kwa ujumla, mwanafunzi yule ambaye mwanzoni aliiacha nuru yake iangaze ameweza kusaidia 15 wa marika wake wafikie wakfu na ubatizo kwa kuwatolea ushahidi vivi hivi.

Ni shangwe kuwaona wengi katika nchi hiyo pana wakilikubali tumaini la Biblia la ulimwengu mpya wa Mungu na kujiunga na udugu wa ulimwenguni pote unaokusanywa na Yehova Mungu ili kuishi milele chini ya Ufalme wake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki