Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 11/1 kur. 21-22
  • Mwanamume Mwenye Elimu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwanamume Mwenye Elimu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mwenyeji wa Tarso
  • Raia Mroma
  • Maoni Yafaayo
  • ‘Kufuatia Mradi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Unaweza Kupata Baraka za Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • “Nisikilizeni Ninapojitetea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Kitabu Cha Biblia Namba 50—Wafilipi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 11/1 kur. 21-22

Mwanamume Mwenye Elimu

“NDUGU zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa.” (1 Wakorintho 1:26) Kama maneno hayo yanavyoonyesha, kuna hatari ya kuingilia sana hekima ya kilimwengu au kuwa na cheo cha juu cha kijamii. Mambo kama hayo yaweza kuwa kizuizi kwa mtu kukubali habari njema.—Mithali 16:5; Marko 10:25.

Hata hivyo, katika siku ya Paulo baadhi ya wale waliokuwa wenye hekima katika njia ya kimwili walikubali kweli, na mmoja wao alikuwa Paulo mwenyewe. Akiwa ameelimishwa vizuri na yaonekana akiwa ametoka kwa familia mashuhuri, Paulo alikuwa mweneza evanjeli mwenye bidii. Hivyo alionyesha kwamba wale wenye mapendeleo katika ulimwengu huu wanaweza kumtumikia Yehova ikiwa moyo wao unafaa. Wanaweza kutumia uwezo wao mbalimbali wa kilimwengu katika utumishi wa Yehova.—Luka 16:9.

Mwenyeji wa Tarso

Paulo alizaliwa Tarso, “mji usiokuwa mnyonge,” kama alivyoufafanua baadaye. (Matendo 21:39) Labda ilikuwa ni huko alikopatia maarifa ya lugha mbalimbali—hasa ujuzi mwingi katika Ugiriki—jambo lililokuwa lenye thamani kubwa katika kazi yake ya umishonari. Maisha katika Tarso yangemfunua Paulo si kwa njia za Kiyahudi tu bali pia kwa utamaduni wa Wasio Wayahudi, ukawa ujuzi aliotumia katika miaka ya baadaye akiwa mtume kwa mataifa. Alijua jinsi ya kuieleza kweli katika njia ambayo wangeweza kuelewa. (1 Wakorintho 9:21) Kwa kielelezo, fikiria hotuba yake kwa Waathene inayoripotiwa katika Matendo sura 17. Huko, katika utoaji wake wa kweli, aliingiza kwa ustadi marejezo kwa dini ya Athene na hata nukuu kutoka mmoja wa washairi wao.

Raia Mroma

Paulo alikuwa na faida nyingine ya kilimwengu. Alikuwa raia Mroma, na alitumia hilo pia ili kuendeleza habari njema. Katika Filipi, yeye na wenzake walipigwa na kufungwa jela bila kujaribiwa kihukumu. Ilikuwa haramu kumfanyia raia Mroma hivyo, na Paulo alipowajulisha wenye mamlaka jambo hilo, walimruhusu abaki na kuhudumia kundi kabla ya yeye kuondoka kwenda kwenye kituo chake kilichofuata.—Matendo 16:37-40.

Baadaye, alipotokea mbele ya Gavana Festo, Paulo alitumia kwa faida yake uraia wake wa Kiroma kukata rufani kesi yake kwa Kaisari. Hivyo, alitetea habari njema mbele ya wenye mamlaka ya juu zaidi ya Milki ya Roma.—Matendo 25:11, 12; Wafilipi 1:7.

Paulo alipokea mazoezi katika njia itumikiayo iliyothibitika baadaye kuwa yenye mafaa. Alifundishwa kutengeneza mahema, yaelekea na baba yake. Kwa sababu hiyo, aliweza kujitegemeza mwenyewe hudumani wakati pesa zilipokuwa chache. (Matendo 18:1-3) Alipokea pia elimu nyingi ya kidini. Alilelewa akiwa “Farisayo, mwana wa Farisayo.” (Matendo 23:6) Kwa kweli, alijifunza miguuni pa Gamalieli, mmoja wa walimu Wayahudi maarufu zaidi. (Matendo 22:3) Elimu hiyo, iwezayo labda kulinganishwa na elimu bora ya chuo kikuu leo, yadokeza kwamba familia yake ilikuwa mashuhuri sana.

Maoni Yafaayo

Malezi na mazoezi ya Paulo yalitoa wakati ujao mwangavu katika Dini ya Kiyahudi. Yeye angalifanikiwa sana. Hata hivyo, mara alipokubali kwamba Yesu alikuwa ndiye Mesiya, miradi ya Paulo ilibadilika. Alipokuwa akiwaandikia Wafilipi, aliorodhesha baadhi ya faida zake za zamani za kilimwengu na kusema hivi: “Mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu.”—Wafilipi 3:7, 8.

Mwanamume huyo mwenye elimu hakutazama nyuma akitamani lile ambalo angalifanya na elimu yake ya kilimwengu; wala hakutumia ‘kusoma kwake kwingi’ kuwastaajabisha wengine sana. (Matendo 26:24; 1 Wakorintho 2:1-4) Bali, akiweka imani kamili katika Yehova Mungu, alirejezea matarajio yake ya nyuma, akisema: “Nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.” (Wafilipi 3:13, 14) Paulo alithamini mambo ya kiroho.

Hata hivyo, Paulo alitumia mazoezi hayo ya nyuma katika utumishi wa Yehova. Aliposema hivi kuhusu Wayahudi, “Nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu,” alisema hivyo kutokana na yale aliyojionea mwenyewe. (Warumi 10:2) Akiwa Farisayo mwenye kutenda, kwa hakika alikuwa na juhudi kwa ajili ya Mungu na kwa ajili ya Maandiko. Baada ya Paulo kuwa Mkristo, juhudi yake ilisawazishwa na maarifa sahihi, na angeweza kutumia elimu yake ya mapema kwa ajili ya kusudi lenye uadilifu. Kwa kielelezo katika kitabu cha Waebrania, alitumia maarifa yake yenye kina ya historia ya Kiisraeli na ibada ya hekalu kuonyesha ubora mkubwa wa mfumo wa Kikristo.

Leo wengine walio na hekima katika njia ya kimwili huitikia habari njema. Watu wenye aina zote za sifa za kustahilisha kielimu, pamoja na washiriki wa aina zote za kazi na ufundi, wameikubali kweli na kutumia mazoezi yao ya nyuma katika utumishi wa Yehova. Hata hivyo, hata elimu yao ya kilimwengu iwe ni nini, Wakristo hawasahau kamwe jambo la kwamba sifa muhimu za kustahilisha ni zile za kiroho. Hayo ndiyo “mambo yaliyo ya maana zaidi” kwa sababu yanaweza kutuongoza kwenye uhai wa milele.—Wafilipi 1:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki