Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 1/1 kur. 18-23
  • Kuchunga Pamoja na Muumba Wetu Mtukufu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuchunga Pamoja na Muumba Wetu Mtukufu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mchungaji Mshiriki wa Yehova
  • Kuonea Shangwe “Amani ya Mungu”
  • Wachungaji wa Chini Waongoza!
  • Uchungaji wa Kitheokrasi
  • Wazee, Chukueni kwa Uzito Madaraka Yenu ya Uchungaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Tii Wachungaji Waliowekwa na Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kuchunga kwa Wororo Kondoo za Yehova Wenye Thamani Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Wachungaji, Waigeni Wale Wachungaji Wakuu Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 1/1 kur. 18-23

Kuchunga Pamoja na Muumba Wetu Mtukufu

“BWANA [Yehova, “NW”] ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.”—ZABURI 23:1, 3.

1. Yehova huandaa kiburudisho gani chenye upendo?

ZABURI ya 23, “melodia ya Daudi, NW” imeleta kiburudisho kwa nafsi nyingi zilizochoka. Imewatia moyo wawe na uhakika unaoonyeshwa katika mstari wa 6: “Hakika wema na fadhili [fadhili-upendo, NW] zitanifuata siku zote za maisha yangu; nami nitakaa nyumbani mwa BWANA [Yehova, NW] milele.” Je! hiyo ni tamaa yako, kukaa milele katika nyumba ya Yehova ya ibada, ukiwa na umoja na watu wake wanaokusanywa sasa kutoka mataifa yote ya dunia? “Mchungaji na Mwangalizi wa roho [nafsi, NW] zenu,” Muumba wetu Mtukufu, Yehova Mungu, atakusaidia kutimiza lengo hilo.—1 Petro 2:25.

2, 3. (a) Yehova huwachungaje watu wake kwa upendo? (b) “Kundi” la Yehova limeongezekaje kwa njia yenye kutokeza?

2 Muumba wa “mbingu mpya na dunia mpya” pia ndiye Mtengenezaji na Mwangalizi Mkuu Zaidi wa kundi ya Kikristo, “nyumba ya Mungu.” (2 Petro 3:13, HNWW; 1 Timotheo 3:15) Anapendezwa sana na kuwachunga watu wake, kama vile Isaya 40:10, 11 linavyotaarifu kwa wazi: “Tazameni, Bwana Mungu [Yehova, NW] atakuja kama shujaa, na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, na ijara yake i mbele zake. Atalilisha kundi lake kama mchungaji, atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; na kuwachukua kifuani mwake, nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.”

3 Katika maana iliyorefushwa, “kundi” hilo latia ndani wale ambao wametembea katika kweli ya Kikristo kwa muda mrefu na “wana-kondoo” ambao wamekusanywa katika nyakati za karibuni sana—kama zile idadi kubwa za wanaobatizwa katika Afrika na Ulaya ya Mashariki. Mkono imara wa Yehova, wenye kulinda unawakusanya kifuani mwake. Ingawa wamekuwa kama kondoo waliopotea, sasa wameingia katika uhusiano wa karibu sana na Mungu na Mchungaji wao mpendwa.

Mchungaji Mshiriki wa Yehova

4, 5. (a) “Mchungaji mwema” ni nani, na unabii ulielekezaje kwake? (b) Yesu anasimamia kazi gani ya kutenganisha, kukiwa na tokeo gani lenye kutokeza?

4 Akitumikia kwenye mkono wa kuume wa Baba yake mbinguni “mchungaji mwema,” Yesu Kristo, hutoa pia uangalifu wenye huruma kwa “kondoo.” Alisalimisha uhai wake ili kunufaisha kwanza lile “kundi dogo” la wapakwa-mafuta na kisha, leo, ule umati mkubwa wa “kondoo wengine” wake. (Luka 12:32; Yohana 10:14, 16) Mchungaji Mkuu, Yehova Mungu, awaelekezea kondoo hao wote, akisema hivi: “Mimi, naam, mimi, nitahukumu . . . kati ya mnyama na mnyama [kondoo na kondoo, NW]. Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao. Na mimi, BWANA [Yehova, NW], nitakuwa Mungu wao, na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mkuu kati yao; mimi BWANA [Yehova, NW] nimesema haya.”—Ezekieli 34:20-24.

5 Mtajo “mtumishi wangu, Daudi” unaelekeza kiunabii kwa Kristo Yesu, yule “mbegu” anayerithi kiti cha utawala cha Daudi. (Zaburi 89:35, 36, NW) Katika siku hiyo ya hukumu ya mataifa, Mchungaji na Mfalme mshiriki wa Yehova, Yesu Kristo, Mwana wa Daudi, anaendelea kuwatenganisha “kondoo” wa ainabinadamu na wale ambao huenda wakadai kuwa “kondoo” lakini kwa kweli ni “mbuzi.” (Mathayo 25:31-33) “Mchungaji mmoja” huyo ainuliwa pia ili kuwalisha kondoo. Tunaona utimizo mtukufu kama nini wa unabii huo leo! Huku wanasiasa wakiongea juu ya kuiunganisha ainabinadamu kupitia utaratibu wa ulimwengu mpya, yule Mchungaji mmoja anawaunganisha kikweli kondoo wa mataifa yote kupitia kampeni ya kutoa ushahidi katika lugha nyingi, iwezayo kushughulikiwa na tengenezo la Mungu tu wala si jingine.

6, 7. “Mtumwa mwaminifu mwenye akili” amehakikishaje kwamba “chakula kwa wakati wake” kinapatikana kwa kondoo?

6 Ujumbe wa Ufalme unapoenea daima katika maeneo mapya, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wa Wakristo wapakwa-mafuta, kama alivyopewa utume na yule Mchungaji mmoja, huhakikisha kwamba kila uandalizi unafanywa ili kupeleka “chakula kwa wakati wake.” (Mathayo 24:45) Mengi kati ya yale matawi yenye kuchapisha 33 ya Watch Tower Society kotekote duniani yanaongeza mazao yao ili kutosheleza ule uhitaji wenye kuongezeka wa vitabu vya mafundisho ya Biblia na magazeti mengi zaidi na yaliyo bora zaidi.

7 Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova linafanya kila jambo liwezalo ili kufanyia maendeleo ubora wa tafsiri katika lugha 200 hivi na kuanzisha tafsiri katika lugha nyinginezo kama inavyohitajiwa ili kueneza shamba zima la ulimwengu. Hilo ni kwa kuunga mkono ule utume ambao Yesu aliwapa wanafunzi wake kwenye Matendo 1:8, NW: “Ninyi mtapokea nguvu wakati roho takatifu itafika juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu mimi . . . mpaka kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” Isitoshe, New World Translation of the Holy Scriptures, ambayo tayari imechapishwa nzima au kwa sehemu katika lugha 14, sasa inatafsiriwa katika lugha nyinginezo 16 za Ulaya, Afrika, na nchi za Mashariki.

Kuonea Shangwe “Amani ya Mungu”

8. Kondoo wamebarikiwaje sana na lile agano la amani ambalo Yehova amefanya nao?

8 Kupitia Yesu Kristo, Mchungaji wake mmoja, Yehova afanya “agano la amani” pamoja na kondoo Wake wenye kulishwa vizuri. (Isaya 54:10) Kwa kuzoea imani katika damu ya Yesu iliyomwagwa, kondoo wanasaidiwa watembee katika nuru. (1 Yohana 1:7) Wanafurahia ‘amani ya Mungu, ipitayo akili zote, inayohifadhi mioyo yao na nia zao katika Kristo Yesu.’ (Wafilipi 4:7) Kama vile Ezekieli 34:25-28 linavyoendelea kusimulia, Yehova huwachunga kondoo zake waingie katika paradiso ya kiroho, hali ya usalama yenye kupendeza, ufanisi wenye kuburudisha, na wenye matokeo mengi. Mchungaji huyo mwenye upendo asema hivi juu ya kondoo zake: “Nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA [Yehova, NW], nitakapovunja vifungo vya kongwa lao, na kuwaokoa katika mikono ya watu wale waliowatumikisha. Hawatakuwa mateka ya makafiri tena, . . . bali watakaa salama salimini, wala hapana mtu atakayewatia hofu.”

9. Ni nafasi gani ambazo zimefunguliwa kwa watu wa Mungu kwa ‘kuvunjwa kwa vifungo’?

9 Tayari, katika miaka ya karibuni, Mashahidi wa Yehova katika nchi nyingi wamejionea kuvunjwa kwa “vifungo vya kongwa lao.” Wako huru kuhubiri zaidi ya wakati mwingine wowote. Sote, katika kila bara, na tutumie vizuri usalama ambao Yehova huandaa tunapoendelea kwa bidii kuitimiza kazi. Yehova hutoa uhakikisho ulioje tunapokaribia wakati wa dhiki kubwa zaidi ambayo ainabinadamu itapata kuona!—Danieli 12:1; Mathayo 24:21, 22.

10. Yehova ameandaa nani kumsaidia Mchungaji Mwema, Kristo Yesu, na baadhi yao waliambiwa nini na mtume Paulo?

10 Katika kutayarishia siku hiyo ya kisasi chake dhidi ya waovu, Yehova ameandaa wachungaji wa chini wamsaidie Mchungaji Mwema, Kristo Yesu, katika kulitunza kundi la kondoo. Hao wanasimuliwa kwenye Ufunuo 1:16 wakiwa idadi kamili ya “nyota saba” katika mkono wa kuume wa Yesu. Katika karne ya kwanza, mtume Paulo alielekezea baraza lenye kuwakilisha la wachungaji hao wa chini, akisema hivi: “Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW] [i]mewaweka nyinyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa [kundi, NW] lake Mungu, alilolinunua kwa damu [ya Mwana, NW] [w]ake mwenyewe.” (Matendo 20:28) Leo kuna wachungaji wa chini wapatao makumi ya maelfu wanaotumikia katika makundi 69,557 kotekote duniani.

Wachungaji wa Chini Waongoza!

11. Baadhi ya wachungaji wameongozaje kwa mafanikio katika maeneo yanayoenezwa mara nyingi?

11 Katika sehemu nyingi ni lazima wachungaji hao waongoze katika maeneo ambayo yameenezwa kwa kurudia-rudia katika siku hizi za mwisho. Wanaweza kuendelezaje idili ya kundi la kondoo ikiwa kwenye kiwango cha juu? Wachungaji hao wamekuwa wakifanya vema sana, na njia moja ambayo kwayo wamekuwa wenye mafanikio zaidi ni kwa kuchochea kazi ya upainia msaidizi na wa kawaida. Wachungaji wengi wenyewe wameshiriki katika utumishi huo, na hata wale wahubiri wasioweza kufanya hivyo wameonyesha roho ya upainia, wakitumikia kwa shangwe inayosaidia katika kushinda ubaridi katika eneo. (Zaburi 100:2; 104:33, 34; Wafilipi 4:4, 5) Hivyo, uovu na hali inayokaribia kuwa yenye mchafuko vinapoikumba ulimwengu, watu wengi wenye mfano wa kondoo wanaamshwa kwenye tumaini la Ufalme.—Mathayo 12:18, 21; Warumi 15:12.

12. Ni tatizo gani zito lililomo katika mashamba yenye kukua kwa haraka, na hilo hushughulikiwaje mara nyingine?

12 Tatizo jingine ni kwamba mara nyingi hakuna wachungaji wenye kustahili wanaotosha ili kutunza kundi la kondoo. Mahali ambapo kuna ukuzi wa haraka, kama vile katika Ulaya ya Mashariki, kuna makundi mengi mpya bila wazee wowote waliowekwa rasmi. Kondoo wenye nia ndio wanaochukua mzigo, lakini hawana ujuzi wowote, na msaada unahitajiwa ili kuwazoeza kondoo wanaomiminika ndani ya makundi. Katika mabara kama vile Brazili, Meksiko, na Zaire, ambako ukuzi ni wa haraka sana, ni lazima Mashahidi wachanga kwa kulinganishwa watumiwe kupanga utumishi na kuzoeza wapya wengine. Mapainia wanatoa msaada mzuri sana, na hii ni sehemu ambayo akina dada wanaweza kuwazoeza dada wapya. Yehova hubariki matokeo kwa roho yake. Ongezeko laendelea kuja.—Isaya 54:2, 3.

13. (a) Kwa kuwa mavuno ni mengi sana, Mashahidi wote wanapaswa wasali wakiomba nini? (b) Sala za watu wa Mungu zilijibiwaje kabla na wakati wa vita ya ulimwengu ya pili?

13 Katika mabara ambako kazi ya kuhubiri imesitawishwa vizuri, katika mabara ambako vizuizi vimeondolewa hivi karibuni, na katika maeneo yaliyofunguliwa mara ya kwanza, maneno ya Yesu kwenye Mathayo 9:37, 38 bado yanayahusu: “Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.” Tunahitaji kuomba pia, kwamba Yehova atainua wachungaji zaidi. Ameonyesha kwamba anaweza kufanya hivyo. Kabla na wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, watawala wakatili kama Waashuri walijaribu kuwaharibu Mashahidi wa Yehova. Lakini katika kujibu sala za Mashahidi, Yehova alisafisha tengenezo lao, akilifanya liwe la kitheokrasi kikweli, na akaandaa “wachungaji” waliohitajiwa.a Hilo lilipatana na unabii huu: “Wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo tutaondokesha wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane”—hata kadiri kubwa zaidi ya wazee waliojiweka wakfu wa kuongoza.—Mika 5:5.

14. Ni uhitaji gani wenye kutokeza uliomo katika tengenezo, na ni kitia-moyo gani kinachotolewa kwa akina ndugu?

14 Kuna uhitaji wenye kutokeza kwa Mashahidi wote wanaume waliobatizwa kufikilia mapendeleo zaidi. (1 Timotheo 3:1) Hali ni yenye uharaka. Mwisho wa mfumo huu unakaribia kwa kasi. Habakuki 2:3 hutaarifu hivi: “Njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo . . . haina budi kuja, haitakawia.” Je! akina ndugu, mwaweza kufikilia ili kustahili kwa ajili ya mapendeleo zaidi katika kazi hiyo ya uchungaji—kabla ya mwisho kuja?—Tito 1:6-9.

Uchungaji wa Kitheokrasi

15. Watu wa Yehova ni theokrasi katika njia gani?

15 Ili kushiriki kikamili katika upanuzi wa tengenezo la Yehova, watu wake wanahitaji kuwa na mtazamo wa kitheokrasi. Wanaweza kutimizaje hilo? Ni nini maana ya neno “kitheokrasi”? Webster’s New Twentieth Century Dictionary hufasili “theokrasi” kuwa “kutawalwa kwa taifa na Mungu.” “Taifa takatifu” la watu wa Yehova ni theokrasi katika maana hiyo. (1 Petro 2:9; Isaya 33:22) Wakiwa washiriki wa taifa hilo la kitheokrasi, ni lazima Wakristo wa kweli waishi na kutumikia kwa kutii Neno la Mungu na kanuni zalo.

16. Kwa msingi, tunaweza kujionyeshaje wenyewe kuwa wa kitheokrasi?

16 Mtume Paulo aeleza kwa wazi jinsi Wakristo wanavyopaswa kuwa watu wa kitheokrasi. Kwanza, yeye asema kwamba wanapaswa “[wa]vae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.” Utu wa Kikristo unapasa ufinyangwe kulingana na kanuni za Mungu zenye uadilifu zilizoandikwa katika Neno lake. Ni lazima awe mwaminifu-mshikamanifu kwa Yehova na kwa sheria Zake. Baada ya kuonyesha jinsi hilo linavyoweza kufanywa, Paulo ahimiza hivi: “Mfuateni [mwe waigaji wa, NW] Mungu, kama watoto wanaopendwa.” (Waefeso 4:24–5:1) Kama watoto watiifu, ni lazima tumwige Mungu. Hiyo ni theokrasi ya kweli katika tendo, kuonyesha kwamba kwa kweli tunaongozwa na Mungu!—Ona pia Wakolosai 3:10, 12-14.

17, 18. (a) Wakristo wa kitheokrasi huiga sifa gani ya Mungu yenye kutokeza? (b) Katika maneno yake kwa Musa, Yehova alikaziaje sifa Yake kuu, lakini Yeye aliongeza onyo gani?

17 Ni nini iliyo sifa kuu ya Mungu tunayopaswa kuiga? Mtume Yohana ajibu kwenye 1 Yohana 4:8 anaposema hivi: “Mungu ni upendo.” Mistari minane baadaye, katika mstari wa 16, yeye arudia kanuni hiyo ya muhimu: “Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.” Mchungaji Mkuu, Yehova, ni ufananisho wa upendo. Wachungaji wa kitheokrasi humwiga kwa kuwaonyesha kondoo wa Yehova upendo mwingi.—Linganisha 1 Yohana 3:16, 18; 4:7-11.

18 Mtawala Mkuu wa Kitheokrasi alijifunua mwenyewe kwa Musa kuwa “BWANA [Yehova, NW], BWANA [Yehova, NW], Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.” (Kutoka 34:6, 7) Hivyo Yehova akazia sehemu mbalimbali za sifa yake ya kitheokrasi yenye kutokeza, upendo, akionya kwa uthabiti kwamba ataadhibu makosa inapostahiliwa.

19. Tofauti na Mafarisayo, wachungaji Wakristo wanapaswa watendeje katika njia ya kitheokrasi?

19 Kwa wale wenye madaraka katika tengenezo, ni nini maana ya kuwa wa kitheokrasi? Yesu alisema hivi juu ya waandishi na Mafarisayo wa siku yake: “Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.” (Mathayo 23:4) Huo ni uonevu na kukosa upendo kama nini! Theokrasi ya kweli, au utawala wa Mungu, hutaka kundi la kondoo lichungwe kwa kutumia kanuni za Biblia zenye upendo, si kwa kuwalemeza kondoo kwa kanuni zisizokoma zenye kufanywa na mwanadamu. (Linganisha Mathayo 15:1-9.) Wakati huohuo, ni lazima wachungaji wa kitheokrasi wamwige Mungu kwa kuongezea upendo wao uthabiti wa kudumisha usafi wa kundi.—Linganisha Warumi 2:11; 1 Petro 1:17.

20. Wachungaji wa kitheokrasi hutambua mipango gani ya kitengenezo?

20 Wachungaji wa kweli hutambua kwamba katika siku hizi za mwisho, Yesu amemweka mtumwa wake mwaminifu mwenye akili juu ya vitu vyake vyote na kwamba roho takatifu imemwelekeza mtumwa huyo katika kuweka rasmi wazee ili wachunge kondoo. (Mathayo 24:3, 47; Matendo 20:28) Kwa hiyo, kuwa wa kitheokrasi kunahusisha kuwa na staha nyingi kwa ajili ya mtumwa huyo, kwa ajili ya mipango ya kitengenezo ambayo mtumwa huyo ameweka, na kwa ajili ya mpango wa wazee ndani ya kundi.—Waebrania 13:7, 17.

21. Yesu aliwawekea wachungaji wa chini mfano gani mzuri?

21 Yesu mwenyewe aliweka mfano mzuri, kwa kumtegemea Yehova na Neno Lake daima ili kupata mwongozo. Alisema hivi: “Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.” (Yohana 5:30) Wachungaji wa chini wa Bwana Yesu Kristo wanapaswa wasitawishe mtazamo mnyenyekevu kama huo. Mzee akiendea Neno la Mungu sikuzote ili kupata mwelekezo, kama Yesu alivyofanya, basi yeye kwa kweli ni wa kitheokrasi.—Mathayo 4:1-11; Yohana 6:38.

22. (a) Wote wanapaswa wajitahidi katika njia gani kuwa wa kitheokrasi? (b) Yesu huwapa kondoo mwaliko gani wenye fadhili?

22 Wanaume mliobatizwa, fikilieni ili mstahili mapendeleo kundini! Enyi kondoo wote wapendwa, iweni na lengo la kuwa wa kitheokrasi, mkimwiga Mungu na Kristo katika kuonyesha upendo! Vilevile wachungaji na kundi la kondoo na washangilie kwa sababu wameitikia mwaliko huu wa Yesu: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”—Mathayo 11:28-30.

[Maelezo ya Chini]

a Ona makala za Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) zenye kichwa “Tengenezo,” katika matoleo ya Juni 1 na 15, 1938.

Je! Waweza Kueleza?

◻ “Kundi” la Yehova ni nini, na linatia ndani nani?

◻ Yesu alitendaje akiwa “mchungaji mwema” katika karne ya kwanza, na leo?

◻ Wachungaji wa chini wana daraka gani kuu katika kulitunza kundi la kondoo?

◻ Ni nini maana ya msingi ya neno “theokrasi”?

◻ Mkristo—hasa mchungaji wa chini—anapaswa atendeje ili awe wa kitheokrasi?

[Picha katika ukurasa wa 20]

Kama mchungaji mwenye kujitoa, Yehova hulitunza kundi lake la kondoo

[Picha katika ukurasa wa 23]

Kuiga sifa ya Yehova Mungu ya upendo ni theokrasi katika tendo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki