Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 1/1 kur. 9-18
  • Kushangilia Katika Muumba Wetu Mtukufu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushangilia Katika Muumba Wetu Mtukufu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kuyahimiza’
  • Kutunza Upanuzi Zaidi
  • Muda wa Saa Bilioni Moja!
  • Programu ya Ujenzi Iliyo Kubwa Sana
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Kujenga kwa Ajili ya Wakati Ujao wa Milele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 1/1 kur. 9-18

Kushangilia Katika Muumba Wetu Mtukufu

“Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya [Mfanyi mtukufu wake, “NW”], wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.”—ZABURI 149:2.

1. Vijapokuwa vilio vya “kupata uhuru hatimaye,” hali ya kweli ya ainabinadamu ni nini?

ULIMWENGU wa leo umekumbwa na “maumivu ya ghafula ya taabu.” Huo ndio usemi ambao Yesu alitumia katika unabii wake kuhusu “umalizio wa mfumo wa mambo,” enzi yenye msiba mkuu iliyoanza na vita ya ulimwengu ya kwanza katika 1914. (Mathayo 24:3-8, NW) Wanasiasa wengi hawaoni lolote ila huzuni kwa wakati ujao. Vijapokuwa vilio vya “kupata uhuru hatimaye” katika Ulaya ya Mashariki, mmoja aliyekuwa rais wakati mmoja katika eneo hilo alitoa muhtasari wa hali hiyo aliposema hivi: “Ongezeko kubwa mno la idadi ya watu na ongezeko la halijoto katika angahewa ya dunia, mashimo katika tabaka la ozoni na UKIMWI, tisho la ugaidi wa kinyukilia na pengo lenye kupanuka kwa njia yenye kutokeza kati ya nchi za kaskazini zenye utajiri na nchi za kusini zenye umaskini, hatari ya njaa kuu, kumalizika kwa mazingira yenye kutegemeza uhai na nyenzo za madini za sayari hii, kupanuka kwa jamii inayoongozwa na maonyesho ya televisheni na tisho lenye kuongezeka la vita vya kieneo—yote hayo, pamoja na maelfu ya mambo mengine, huwakilisha tisho la ujumla kwa ainabinadamu.” Hakuna utawala wowote wa kibinadamu uwezao kuondoa tisho hilo litakaloishia katika msiba.—Yeremia 10:23.

2. Ni nani aliye na suluhisho la kudumu kwa matatizo ya ainabinadamu, na yeye amechukua hatua gani tayari?

2 Hata hivyo, tunaweza kushangilia kwamba Muumba wetu Mtukufu ana suluhisho la kudumu. Katika unabii wa Yesu “umalizio wa mfumo wa mambo” unalingana na “kuwapo” kwake kusikoonekana. (Mathayo 24:3, 37-39, NW) Ili kuiumba “mbingu mpya,” Yehova alimweka Yesu kwenye kiti chake cha utawala akiwa Mfalme wa Kimesiya, uthibitisho wa kiunabii ukionyesha kwamba jambo hilo la kihistoria lilitukia mbinguni katika mwaka 1914.a (2 Petro 3:13) Yesu, akiwa mtawala mshiriki pamoja na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, sasa amepewa utume wa kuhukumu mataifa na kuwatenganisha wasikivu, watu wa dunia wenye mfano wa kondoo kutoka kwa wale wenye mfano wa mbuzi walio washupavu. “Mbuzi” wasiomcha Mungu wanatiwa alama kwa ajili ya “kukatiliwa mbali kwa milele” na “kondoo” wanatiwa alama kwa ajili ya uhai wa milele katika makao ya kidunia ya Ufalme.—Mathayo 25:31-34, 46, NW.

3. Wakristo wa kweli wana sababu gani ya kushangilia?

3 Mabaki ya Israeli wa kiroho duniani, ambao sasa umati mkubwa wa kondoo hao watiifu umejiunga nao, wana kila sababu ya kuwa na shangwe katika Yehova, Mfalme wa umilele, anapoleta makusudi yake matukufu kwenye upeo kupitia Ufalme wa Mwana wake. Wanaweza kusema hivi: “Nitafurahi sana katika BWANA [Yehova, NW] nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu . . . Kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU [Yehova, NW] atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.” (Isaya 61:10, 11) “Machipuko” hayo yanathibitishwa katika wale mamilioni wanaokusanywa sasa kutoka kwa mataifa ili waimbe sifa za Yehova.

‘Kuyahimiza’

4, 5. (a) Kukusanywa kwa watu wa Mungu kulitabiriwaje? (b) Ni ongezeko gani lenye kutokeza lililoonwa wakati wa mwaka wa utumishi wa 1992?

4 Kukusanya huko kunaongeza mwendo huku mwisho wa mfumo wa Shetani unapokaribia. Muumba wetu Mtukufu ajulisha rasmi hivi: “Watu wako nao watakuwa wenye haki wote . . . , Chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe, kazi ya mikono yangu mwenyewe, ili mimi nitukuzwe. Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa hodari; Mimi BWANA [Yehova, NW], nitayahimiza hayo wakati wake.” (Isaya 60:21, 22) Kuhimiza huko kunaonyeshwa vizuri ajabu katika Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 1992 ya Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote, ambayo imetangazwa kwenye kurasa 12 hadi 15 za gazeti hili.

5 Lenye kutokeza katika ripoti hiyo ni kilele kipya cha wapiga mbiu ya Ufalme 4,472,787, ongezeko la 193,967—asilimia 4.5 zaidi ya mwaka jana. Kilele cha 301,002 waliobatizwa katika 1992 huonyesha pia jambo la kwamba wengi sana wanaikubali kweli ya Biblia. Tunashangilia kama nini kwamba katika hii “siku ya giza na weusi, . . . [kuna watu] wakuu, tena wenye nguvu,” ambao kama bumba la nzige, wanaeneza ushahidi wa Ufalme “mpaka kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia”! (Yoeli 2:2, 25; Matendo 1:8, NW) Kutoka Alaska yenye barafu—ambako ndege ya Watch Tower Society imefanya ziara zaidi ya 50 kwenye maeneo yenye kujaa theluji—hadi majangwa makavu ya Mali na Burkina Faso na visiwa vilivyotawanyika vya Maikronesia, watumishi wa Yehova wanamulika wakiwa “nuru ya mataifa, ili wokovu [wake] upate kuwa kwenye upembe wa dunia.”—Isaya 49:6, NW.

6, 7. Ni badiliko gani la matukio lililoshuhudiwa katika miaka ya karibuni, na watumishi wa Yehova wameliitikiaje?

6 Yehova amekuwa kama ngome na mnara imara katika kuwalinda na kuwategemeza watu wake. Katika sehemu nyingi za dunia, Mashahidi wa Yehova wamelazimika kuvumilia miongo kadhaa ya uonevu na mnyanyaso mkatili. (Zaburi 37:39, 40; 61:3, 4) Lakini hivi karibuni, kana kwamba kwa muujiza, vizuizi na vipingamizi vimeondolewa katika mabara yapata 21, hivi kwamba sasa watu wa Mungu wanaweza kupiga mbiu kwa uhuru kwamba Muumba wetu Mtukufu amemtawaza Kristo kuwa Mfalme juu ya dunia.—Zaburi 2:6-12.

7 Je! watu wa Yehova wanatumia vizuri uhuru wao uliopatikana hivi karibuni? Ona katika chati maongezeko ya Bulgaria, Romania, na Muungano wa Sovieti wa zamani katika Ulaya ya Mashariki na ya Angola, Benin, na Msumbiji katika Afrika. Hata katika Zaire, upanuzi ni wa ajabu sana. Wakiwa na shangwe mioyoni mwao, ndugu zetu waliowekwa huru wanajibu ule mwito: “Mshukuruni BWANA [Yehova, NW] kwa kuwa ni mwema . . . , yeye peke yake afanya maajabu makuu; kwa maana fadhili [fadhili-upendo, NW] zake ni za milele.” (Zaburi 136:1, 4) Shukrani hizo zinaonyeshwa kwa utumishi wenye bidii katika kukusanya watu wengine wenye mfano wa kondoo kwenye upande wa Ufalme.

8. Wasifaji wapya wa Yehova wamekujaje kama “warukao kama wingu” katika Ulaya ya Mashariki? katika Afrika?

8 Wakati wa kiangazi cha Ulaya kilichopita, mikusanyiko ya watu wa Yehova iliyofanywa katika mabara yaliyokuwa ya Kikomunisti zamani imekuwa na mahudhurio yenye kustaajabisha. Yenye kustaajabisha hata zaidi ni idadi ya wale wanaobatizwa, kama vile chati yenye kuandama inavyoonyesha. Vivyo hivyo, katika Togo, Afrika, marufuku iliondolewa katika Desemba 10, 1991. Mwezi uliofuata mkusanyiko wa kitaifa ulifanywa. Kwa kulinganishwa na wastani wa kila mwezi wa wahubiri walio shambani 6,443, hudhurio katika mikusanyiko hiyo lilipanda hadi 25,467, watu 556 wakibatizwa—asilimia 8.6 ya idadi ya wahubiri. Kama vile Isaya 60:8 linavyoonyesha, wasifaji wapya wa Mungu “[wanaruka] kama wingu, na kama njiwa waendao madirishani kwao” katika makundi ya watu wa Yehova.

9. Ni maandalizi gani ambayo yamefanywa ili Wakristo katika nchi zilizowekwa huru hivi karibuni waweze ‘kula na kushiba’?

9 Njaa ya kupata chakula cha kiroho katika Ulaya ya Mashariki na Afrika inatulizwa pia. Viwanda vya Watch Tower Society katika Ujerumani, Italia, na Afrika Kusini vimepeleka lori baada ya lori zilizojaa fasihi katika lugha kadhaa, hadi kwenye nchi zenye njaa kubwa ya kiroho. Hapo mbeleni, Mashahidi wengi walilazimika kupitishiana magazeti yaliyochakaa kwa kutumiwa sana, lakini sasa wanapokea chakula cha kiroho kwa wingi. Wanashangilia kushiriki katika utimizo wa unabii huu: “Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la BWANA [Yehova, NW], Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu.”—Yoeli 2:26.

Kutunza Upanuzi Zaidi

10. Kwa sababu ya hudhurio la juu kwenye Ukumbusho, ni mwaliko gani unaotolewa kwa wote wanaopendezwa?

10 Tarakimu ya hudhurio la ulimwenguni pote la Ukumbusho wa kifo cha Yesu ni ya ajabu kwelikweli, 11,431,171, ongezeko la 781,013, au asilimia 7.3 zaidi ya mwaka jana. Karibuni, enyi wapya wote! Lingekuwa jambo zuri kama nini ikiwa hao wenye kupendezwa karibuni wangefurahia faida ya kuwa na funzo la Biblia nyumbani pamoja na mmoja wa Mashahidi wa Yehova! (Ona Isaya 48:17.) Ripoti ya Mwaka wa Utumishi inaonyesha mafunzo ya jinsi hiyo 4,278,068 yakiongozwa kila mwezi, ongezeko zuri la asilimia 8.4. Hata hivyo, wengi zaidi wangeweza kufanya wapatikane kwa utumishi huo. Mashahidi wa Yehova wanafurahia kutembelea kwa kawaida wale wenye kupendezwa ili kuongoza funzo la Biblia nyumbani bila malipo, hivyo wakiwasaidia hao waweke imara miguu yao kwenye barabara inayoongoza kwenye uhai wa milele. (Yohana 3:16, 36) Kwa nini usiombe funzo la jinsi hiyo? Na ukumbuke, unakaribishwa kwa uchangamfu sikuzote kwenye Jumba la Ufalme!—Zaburi 122:1; Warumi 15:7.

11, 12. (a) Ni matatizo gani yanayokabiliwa katika mabara mengine? (b) “Kusawazisha” kunatukia katika njia gani kati ya mabara yenye utajiri zaidi na yale yenye umaskini zaidi?

11 Yale makundi yenye Majumba ya Ufalme mazuri yamebarikiwa sana. Hali ni tofauti katika mabara ambako Mashahidi waaminifu-washikamanifu wamevumilia miaka mingi chini ya marufuku, wakikutana kisiri katika vikundi vidogo. Katika sehemu hizo, sasa wako huru lakini wana Majumba ya Ufalme machache. Kwa kielelezo, katika nchi moja ya Afrika, makundi 93 yanatumikiwa na Majumba ya Ufalme matatu tu. Kwa hiyo mikutano kwa kawaida hufanywa kwenye mashamba makubwa yaliyo tupu. Kundi la watu 150 laweza kuwa na watu wafikao 450 wakihudhuria mikutano hiyo kwa ukawaida.

12 Mara nyingi katika Ulaya ya Mashariki ni vigumu kununua jengo au kujenga, lakini kuna kadiri fulani ya maendeleo. Kuwekwa wakfu kwa majengo mapya mazuri ya tawi kuliratibiwa Novemba 28, 1992 katika Polandi. Michango yenye ukarimu kwa kazi ya Mashahidi wa Yehova ya ulimwenguni pote inatumiwa ili kusaidia ujenzi wa majumba na majengo mengine. Hivyo, “kusawazisha” kunatukia kwa kuwa ukarimu wa ndugu wanaochanga kutoka kwa “wingi” wao wa kimwili unasaidia kuandalia mahitaji ya kiroho ya makundi katika mabara yaliyo na upungufu.—2 Wakorintho 8:13, 14, NW.

Muda wa Saa Bilioni Moja!

13. Ni muda wa saa ngapi uliotumiwa katika kuhubiri na kufundisha katika 1992, na ni jitihada za nani zinazoonyeshwa katika tarakimu hiyo?

13 Ungefanya nini na muda wa saa bilioni moja? Wote wanaopata uhai wa milele wataweza kutumia muda wa saa hizo nyingi, na hata zaidi, katika utumishi kwa Yehova wenye matokeo na wenye kuridhisha. Lakini ebu wazia kupakia muda wa saa hizo nyingi katika mwaka mmoja! Hilo ndilo watu wa Yehova walilotimiza katika 1992. Tukijumlisha pamoja ripoti moja moja za wahubiri wa Ufalme wote, tunapata kilele kipya cha muda wa saa 1,024,910,434 zilizotumiwa katika njia bora zaidi ambayo saa zaweza kutumiwa—kumsifu Muumba wetu Mtukufu, “[ku]fundisha . . . waziwazi, na nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20) Kwa wastani, Mashahidi 4,290,057 walikuwa wakiripoti kila mwezi. Wanatoka matabaka yote ya maisha. Baadhi yao hawawezi kuchanga wakati mwingi sana kwa kazi ya Ufalme. Hao wanatia ndani vichwa vya familia, ambao ni lazima waandalie watu wa nyumbani; wazee-wazee; na wengi wenye matatizo ya afya; pamoja na watoto walio shuleni bado. Hata hivyo, ripoti iliyotolewa na kila mmoja ni wonyesho unaothaminiwa wa upendo kwa Yehova.—Linganisha Luka 21:2-4.

14. Vijana ‘wanamkumbukaje Muumba wao Mtukufu’?

14 Kizazi kichanga zaidi kinakulia katika utumishi wa Yehova, na kwa furaha wengi wao wanatumia maneno ya Sulemani kwenye Mhubiri 12:1: “Mkumbuke Muumba wako [Mtukufu, NW] siku za ujana wako.” Wanajitahidi katika kazi yao ya shule, pamoja na kuzoezwa katika mambo ya kiroho na wazazi wenye kujitoa. Imekuwa shangwe kuona idadi kubwa ya vijana matineja wakisimama kwenye mikusanyiko ya hivi karibuni, wakijitoa wenyewe kwa ajili ya ubatizo. Ni shangwe pia kujua kwamba wengi, kwa kujifunza ufundi au stadi fulani, wanafanya matayarisho yafaayo ili kupainia wanapohitimu shule. Hivyo, wataweza kujitegemeza wenyewe, kama vile mtume Paulo alivyofanya mara kwa mara kwa kutengeneza hema.—Matendo 18:1-4.

15, 16. Mapainia na watumishi wengine wa wakati wote wamechangiaje maendeleo ya kazi ya Ufalme, na baadhi yao wamefurahia baraka zipi?

15 Mapainia na watumishi wengine wa wakati wote wanashiriki sehemu kubwa kama nini kwa maendeleo ya kazi ya Ufalme! Idadi ya mapainia imeongezeka kufikia kilele cha 931,521 mwaka ambao umepita. Hao wanapohubiri kila siku kutoka nyumba hadi nyumba na kuongoza mafunzo ya Biblia katika nyumba za watu, wanakuja kuwa wenye mafanikio sana katika kujieleza kwa Maandiko. Isitoshe, wengi wamestahili kuhudhuria Shule ya Utumishi wa Painia ya majuma mawili, inayowasaidia kusitawisha uwezo na shangwe kubwa zaidi katika kufanya kazi ya Mungu.

16 Kila mmoja wa mapainia hao waaminifu wanaweza kukubaliana na maneno kwenye Isaya 50:4: “Bwana MUNGU [Yehova, NW] amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka.” Kuna watu wengine mmoja mmoja leo waliochoka na ulimwengu wenye ufisadi unaowazunguka lakini wanaopata burudisho kupitia neno linalosemwa na mapainia wetu waaminifu.—Linganisha Mithali 15:23; Ezekieli 9:4.

Programu ya Ujenzi Iliyo Kubwa Sana

17. Kuongezea ujenzi wa kiroho, ni ujenzi gani wa vitu vya kimwili ambao umeshuhudiwa katika miaka ya karibuni?

17 Ufanisi wa kiroho wa ulimwenguni pote wa Mashahidi wa Yehova hutaka pia ukuzi wa vitu vya kimwili. Upanuzi wa vifaa vya kuchapishia, ofisi, makao ya Betheli na ujenzi wa Majumba ya Ufalme na Majumba ya Kusanyiko yanahitajika. Kwa hiyo Mashahidi wa Yehova wanatakwa wawe wajenzi katika njia ya kimwili. Ujenzi kama huo ulitukia katika siku ya Mfalme Sulemani. Sulemani alijenga hekalu kwa ajili ya ibada ya Yehova kulingana na “mpango wa ujenzi . . . uliokuja kuwa na yeye kwa kupuliziwa,” Yehova akiwa ameiandaa kwa baba yake, Mfalme Daudi. (1 Mambo ya Nyakati 28:11, 12, NW) Hivyo Sulemani hakuwajenga wasikilizaji wake tu kwa maneno ya hekima yenye thamani kubwa bali pia alielekeza ujenzi wa vitu vya kimwili wenye ubora usiopata kamwe kufanywa na walimwengu.—1 Wafalme 6:1; 9:15, 17-19.

18, 19. (a) Ni miradi gani ya ujenzi yenye kuendelea kwa kasi inayofanywa na tengenezo la Yehova? (b) Roho ya Yehova imedhihirikaje katika ujenzi wa vitu vya kimwili na wa kiroho pia?

18 Leo, Mashahidi wa Yehova hawajengi kwa kutumia mipango ya ujenzi yenye kupuliziwa kimungu, lakini wana roho ya Mungu. Kama vile katika siku za Israeli, roho hiyo huwachochea wajenge katika njia inayowastaajabisha watu wa ulimwengu. (Zekaria 4:6) Wakati ni mfupi. Majumba ya Ufalme na majengo mengine yanahitajiwa bila kukawia. Katika nchi nyinginezo Majumba ya Ufalme yenye kujengwa upesi ni ya kawaida. Kwa kielelezo, katika miaka 10 ambayo imepita, Kanada inaripoti ujenzi wa majumba 306, kila moja katika muda wa siku zinazopungua mbili. Kwa sababu ya upanuzi wenye kasi wa kazi ya Yehova ulimwenguni pote, jumla ya majengo mapya ya tawi au upanuzi mbalimbali wa tawi 43 yanajengwa au yanapangwa sasa kujengwa. Isitoshe, jengo la makao lenye orofa 30, lililo na vyumba vya kulala vya wanabetheli waliojitolea wapatao elfu moja hivi, linakaribia kumalizika katika Brooklyn. Pia katika New York State, huko Patterson, ujenzi wa kitovu cha elimu ya Biblia, mradi mkubwa zaidi ambao Watch Tower Society imepata kuanzisha, unasonga mbele zaidi ya vile ulivyoratibiwa.

19 Miradi hiyo inaendelea vema na kwa ubora wa kazi unaoshangaza kampuni za ujenzi za ulimwengu zenye ujuzi mwingi. Kwa nini? Kwa sababu ya ule mchango mkubwa mno unaofanywa na Mashahidi wa Yehova waliojiweka wakfu. Roho yake huwasukuma si kuandaa tu utegemezo wa kimwili bali pia kutoa kwa moyo wote wakati na nishati zao. Mahali pa ujenzi husongamana na wafanyakazi waliozoezwa vizuri na wenye kujitoa. Hakuna migomo ya wafanyakazi, na hakuna kutangatanga kazini. Roho ya Yehova huandaa kichocheo, kama vile ilivyowachochea wajenzi wa tabenakulo katika wakati wa Musa na wale waliolijenga hekalu katika siku za Sulemani. Hali ya kiroho ndiyo sifa yenye kutokeza inayotakwa kwa wafanyakazi hao.—Linganisha Kutoka 35:30-35; 36:1-3; 39:42, 43; 1 Wafalme 6:11-14.

20. (a) Habari njema zitahubiriwa kwa kadiri gani bado? (b) Ni taraja gani lenye kubarikiwa linalowangojea watu wa Yehova?

20 Sulemani aliendelea na programu yake ya ujenzi baada ya kumaliza hekalu. (2 Mambo ya Nyakati 8:1-6) Hatujui ni kwa kadiri gani ambayo kwayo kutoa ushahidi kwa ki-siku-hizi kutakavyopanuka bado—pamoja na uhitaji unaolingana wa ujenzi wa majumba na majengo mengine. Hata hivyo, twajua kwamba wakati habari hizi njema za Ufalme zitakapohubiriwa kwa kadiri ambayo Yehova aamuru, ndipo mwisho, ile “dhiki kubwa” itakuja. (Mathayo 24:14, 21) Katika dunia ambayo haitakuwa imeharibiwa tena na watu wenye pupa, mpango wa Yehova wa “mbingu mpya na nchi [dunia, NW] mpya” ndipo utailetea ainabinadamu baraka zisizoweza kusimuliwa. Kwa hiyo na ‘tushangilie daima, kwa ajili ya hivi ambavyo Mungu anaumba,’ tukimpa Muumba wetu Mtukufu sifa zote!—Isaya 65:17-19, 21, 25.

[Maelezo ya Chini]

a Ona “Ufalme Wako Uje,” kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., kurasa 105-16, 186-9.

Je! Waweza Kueleza?

◻ Tuna sababu zipi za kushangilia katika Muumba wetu Mtukufu?

◻ Ni maongezeko gani yaliyoripotiwa wakati wa mwaka wa utumishi wa 1992?

◻ Katika nchi ambako kutoa ushahidi kulikuwa kumepigwa marufuku zamani, ni baraka zipi nyingi ambazo zimeripotiwa?

◻ Vijana na mapainia wamechangiaje kwenye ongezeko katika tengenezo la Yehova?

◻ Watu wa Yehova wamekuwaje wenye shughuli nyingi katika kazi za ujenzi wa vitu vya kimwili na wa kiroho pia?

[Sanduku katika ukurasa wa 17]

Mwaka jana muda wa saa zaidi ya bilioni moja zilitumiwa katika kazi ya kuhubiri na kufundisha

[Chati katika ukurasa wa 12-15]

1992 SERVICE YEAR REPORT OF JEHOVAH’S WITNESSES WORLDWIDE

(Ona buku lililojalidiwa)

[Picha katika ukurasa wa 10]

Mamia ya maelfu ya wale waliotaka kubatizwa mwaka jana huonyesha baraka ya Yehova juu ya kazi ya kuhubiri na kufundisha

[Picha katika ukurasa wa 16]

Idadi kubwa za vijana ‘wanamkumbuka Muumba wao Mtukufu’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki