Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 1/15 kur. 3-4
  • Je! Wewe Utanyakuliwa Ili Kwenda Mbinguni?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Utanyakuliwa Ili Kwenda Mbinguni?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maoni Tofauti-Tofauti Juu ya Kuchukuliwa Kimwili Kutoka Duniani
  • Kunyakuliwa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • ‘Kunyakuliwa Ili Kumlaki Bwana’—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Ukombozi Wenu Unakaribia”!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kuutazama Ulimwengu
    Amkeni!—1993
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 1/15 kur. 3-4

Je! Wewe Utanyakuliwa Ili Kwenda Mbinguni?

WATU wengi huamini kwamba wataenda mbinguni wanapokufa. Lakini wengine hufikiri kwamba watanyakuliwa ili kwenda mbinguni katika kule kunakoitwa kuchukuliwa kimwili kutoka duniani. Je! hilo ni tazamio lako?

Kuchukuliwa kimwili kutoka duniani ni kule “kutoweka kwa ghafula kwa mamilioni na mamilioni ya watu bila hata kidokezo chochote juu ya walikokwenda!” Ndivyo alivyosema mwevanjeli mmoja Mprotestanti. Kulingana na Evangelical Dictionary of Theology, neno la Kiingereza “rapture” (kuchukuliwa kimwili kutoka duniani) linarejezea “kuunganishwa kwa kanisa pamoja na Kristo kwenye kuja kwake kwa pili.”

Wengine husumbuliwa na wazo la kuwaacha nyuma marafiki na washiriki wa familia ili kumlaki Yesu Kristo. Ingawa hivyo, wengi huamini kwamba ni lazima kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kutukie. Je! hilo litatukia? Ikiwa ndivyo, wakati gani?

Maoni Tofauti-Tofauti Juu ya Kuchukuliwa Kimwili Kutoka Duniani

Biblia huonyesha kwamba kabla ya mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu ulioahidiwa, kutakuwako kipindi kiitwacho “dhiki kubwa.” Yesu alisema hivi: “Wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.” (Mathayo 24:21; Ufunuo 20:6) Wengine hufikiri kwamba kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kutatukia kabla ya dhiki kubwa. Wengine hukutazamia kutukie wakati wa dhiki kubwa. Wengine bado hufikiri kwamba kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kutakuja baada ya dhiki hiyo isiyo na kifani.

Maoni ya kwamba kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kungetukia baada ya dhiki kubwa yalienea sana mpaka mwanzo-mwanzo wa karne ya 19. Halafu, katika Uingereza harakati ikaanza iliyoongozwa na aliyekuwa kasisi wa Kanisa ya Ailandi, John Nelson Darby. Yeye na Waanglikana wenye maoni ayo hayo wakaja kujulikana kama Akina Ndugu. Kutoka kanisa lake katika Plymouth, Darby alisafiri kuhubiri katika Uswisi na kwingineko katika Ulaya. Alidai kwamba kurudi kwa Kristo kungetukia katika hatua mbili. Kungeanza na kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kisiri, ambamo “watakatifu” wangenyakuliwa kabla ya kipindi cha dhiki cha miaka saba kiiteketeze dunia. Kisha Kristo angetokea kwa njia ya kuonekana kwa macho, akiandamana na “watakatifu” hao, na pamoja wangetawala duniani kwa miaka elfu moja.

Darby alikazia uhitaji wa kujitenganisha na ulimwengu, na mwishowe wale walioshiriki maoni yake walikuja kujulikana kama Akina Ndugu wa Pekee. B. W. Newton aliongoza farakano tofauti lililoamini katika kuchukuliwa kimwili kutoka duniani lakini si kabla ya dhiki. Alexander Reese aliyetetea kuchukuliwa kimwili kutoka duniani baada ya dhiki alishikilia kwamba “nadharia za Kuchukuliwa Kimwili Kutoka Duniani Kisiri hutokeza hatari kubwa kwa tumaini la Kuja kwa Kristo.”

Wenye kuamini juu ya kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kabla ya dhiki huamini kwamba tofauti hiyo ya maoni ni yenye uzito vya kutosha kuathiri “asili ya tumaini [lao] kuhusiana na kuja kwa Kristo.” Wengine huweka tumaini lao katika “nadharia ya kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kwa sehemu,” wakiamini kwamba wale walio waaminifu-washikamanifu zaidi kwa Kristo watachukuliwa kimwili kutoka duniani kwanza na walio wa kilimwengu zaidi watachukuliwa baadaye.

Vikundi vingi vya kievanjeli hupiga mbiu kwamba kuchukuliwa kimwili kutoka duniani kwa Wakristo waaminifu kutatukia karibuni sana. Hata hivyo, kwa sababu ya maoni tofauti-tofauti, kijitabu kinachotangazwa na Kanisa la Kipentekoste la Elim la Uingereza chasema hivi: “Ingawa tunaamini orodha pana ya matukio yanayohusiana na kurudi kwa Bwana Yesu . . . , kuna uhuru katika ufasiri wa unabii kulingana na usadikisho wa mtu mmoja mmoja. Wengi hukubali msimamo wa kutokushikilia maoni sana, wakingojea kwa saburi matukio yenyewe yafunue programu ya kiunabii.”

Neno la Mungu lililopuliziwa, Biblia, ndicho kiwango ambacho twahitaji kupimia ukweli wa imani zote. (2 Timotheo 1:13; 3:16, 17) Kwa hiyo, linasema nini juu ya kuchukuliwa kimwili kutoka duniani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki