Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 9/15 kur. 7-8
  • Papias Alizithamini Semi za Bwana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Papias Alizithamini Semi za Bwana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Njia Yenye Uangalifu
  • Kitabu Chake
  • Maelezo juu ya Gospeli
  • Kufahamu Uhitaji Wake wa Kiroho
  • Apokalipsi—Je, Tuiogope Au Tuitumainie?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Mababa wa Kimitume—Je, Kweli Walifuata Mafundisho ya Mitume?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • ‘Dhidi ya Maarifa—Yaitwayo Hivyo kwa Ubandia’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Sehemu 2-Je, Mababu wa Kimitume Walifundisha Fundisho la Utatu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 9/15 kur. 7-8

Papias Alizithamini Semi za Bwana

“SIKUFURAHIA . . . [ushirika wa] wale walio na mengi ya kusema, bali [nilifurahia ule wa] wale waliofundisha yale yaliyokuwa ya kweli.” Ndivyo alivyoandika Papias, aliyedai kuwa Mkristo wa karne ya pili ya Wakati wa Kawaida wetu.

Papias aliishi katika kile kipindi cha baada tu ya kifo cha mitume wa Yesu Kristo. Kwa kweli, alikuwa mshiriki wa Polycarp, ambaye yaripotiwa kwamba alijifunza kutoka kwa mtume Yohana. Sifa hizo, pamoja na njia ya Papias ya kupata ujuzi, yafanya ielekee kwamba alikuwa amearifiwa vizuri.

Njia Yenye Uangalifu

Hamu ya Papias ya kupata kweli yaonekana wazi katika vile vitabu vitano vinavyofanyiza buku lake juu ya semi za Bwana. Katika miaka yake ya mapema zaidi, hakuna shaka kwamba Papias alikariri semi nyingi za kweli alizokuwa amesikia. Baadaye, kutoka makao yake katika jiji la Kifrigia la Hierapoli, katika Esia Ndogo, Papias aliwahoji wazee-wazee ili kuhakikisha ikiwa walipata wakati wowote kuona au kusikia yeyote kati ya mitume wa Yesu. Aliwasaili kwa bidii, akaandika yale waliyosema.

Papias aeleza hivi: “Sitasita kuandika . . . yoyote niliyojifunza kwa uangalifu kwa wakati wowote kutoka kwa wazee, na kuyakumbuka kwa uangalifu, nikiwahakikishia kweli yayo. Kwani, sikufurahia, kama watu wengi, [ushirika wa] wale walio na mengi ya kusema, bali [nilifurahia ule wa] wale waliofundisha yale yaliyokuwa ya kweli; wala [sikufurahia] wale wanaosimulia amri za wengine, bali [nilifurahia] wale wanaoripoti zile [amri] zilizotolewa na Bwana kwa imani na kutokana na kweli yenyewe. Na nilipokutana na mtu yeyote aliyekuwa amekuwa mfuasi wa wazee, nilikuwa nikimwomba masimulizi yaliyotolewa na wazee—yale ambayo Andrea au Petro alisema, au yale ambayo Filipo au yale ambayo Tomaso au Yakobo, au yale ambayo Yohana au Mathayo alisema, au wanafunzi wa Bwana wengine wowote.”

Kitabu Chake

Bila shaka Papias aliweza kupata ujuzi mwingi wa kiroho. Twaweza kuwazia tu jinsi ambavyo ni lazima iwe alisikiliza kwa uangalifu yale mambo madogo-madogo yaliyozunguka maisha ya kibinafsi na huduma ya kila mmoja wa mitume. Yapata 135 W.K., Papias aliandika yale aliyotaka kujulisha katika kitabu chake mwenyewe. Kwa kusikitisha, kitabu hicho kimetoweka. Kilinukuliwa na Irenaeus, aliyedai kuwa Mkristo wa karne ya pili W.K., na Eusebio, yule mwanahistoria wa karne ya nne. Kwa kweli, kiliendelea kusomwa katika karne ya 9 W.K. na huenda ikawa kilikuwako mpaka karne ya 14.

Papias aliamini katika kuja kwa Utawala wa Mileani (Miaka Elfu) wa Kristo. (Ufunuo 20:2-7) Kulingana na Irenaeus, aliandika juu ya wakati ambapo “vitu vilivyoumbwa, vikiwa vimefanyizwa upya na kuwekwa huru, vitatokeza wingi wa aina zote za chakula, kutokana na umande wa mbinguni na hali yenye rutuba ya dunia, kama vile wazee, waliomwona Yohana, mwanafunzi wa Bwana, walivyosimulia kwamba walikuwa wamesikia jinsi ambavyo Bwana alikuwa akifundisha juu ya nyakati hizo.” Papias aliendelea kuandika hivi: “Kwa wale wenye imani mambo hayo yanaaminika. Na wakati Yuda, yule msaliti, alipokataa kuamini, akauliza, ‘Jambo hilo litaweza kutimizwaje na Bwana?’ Bwana alisema, ‘Wale watakaofikia nyakati hizo wataona.’”

Papias aliandika katika wakati ambapo Ugnosti [ujuzi wa ujumla] ulikuwa umeenea sana. Waagnosti walichanganya falsafa, mawazio, na mafumbo ya kipagani pamoja na uasi-imani wa Ukristo. Kwa kweli, maelezo ya Papias juu ya maneno, au semi za Bwana, lilikuwa jaribio la kukomesha mweneo wa Ugnosti. Baada yake, Irenaeus aliendelea kukinza ile hali bandia ya kiroho na yenye kutokezwa kupita kiasi ya Waagnosti. Ni lazima iwe fasihi ya Kiagnosti ilikuwa na habari nyingi mno, jambo hilo likichochea ule mtajo wa Papias wenye kukejeli juu ya “wale walio na mengi ya kusema.” Mradi wake ulikuwa wazi—kupinga uwongo kwa kutumia kweli.—1 Timotheo 6:4; Wafilipi 4:5.

Maelezo juu ya Gospeli

Katika vijipande vya maandishi ya Papias yaliyoko bado, twapata mtajo wa masimulizi yaliyoandikwa na Mathayo na Marko. Kwa mfano, Papias asema hivi juu ya hati ya Marko: “Marko, akiwa amekuwa mkalimani wa Petro, aliandika kwa usahihi kila jambo alilokumbuka.” Akithibitisha zaidi usahihi wa Gospeli hiyo, Papias aendelea hivi: “Kwa hiyo basi Marko hakukosea, alipoandika mambo fulani hivyo kadiri alivyoyakumbuka; kwani alihangaika sana kutokosa [kuandika] jambo lolote alilosikia, au kuandika humo taarifa yoyote bandia.”

Papias aandaa uthibitisho wa nje kwamba mwanzoni Mathayo aliandika Gospeli yake katika lugha ya Kiebrania. Papias asema hivi: “Aliandika semi hizo katika lugha ya Kiebrania, na kila mmoja aliyafasiri vizuri iwezekanavyo.” Yaelekea kwamba Papias aliyataja masimulizi ya Gospeli ya Luka na Yohana, pamoja na maandishi mengine ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Ikiwa ndivyo, angekuwa mmoja wa mashahidi wa mapema zaidi wanaothibitisha uasilia wayo na kupuliziwa kwayo kimungu. Lakini, kwa kusikitisha, ni vijipande vichache tu vya maandishi ya Papias ambavyo vimebaki.

Kufahamu Uhitaji Wake wa Kiroho

Akiwa mwangalizi katika kutaniko huko Hierapoli, Papias alikuwa mchunguzi asiyelegea. Kwa kuongezea kuwa mtafiti mwenye bidii, aliyathamini sana Maandiko. Papias aliamua kwa usahihi kwamba taarifa yoyote ya kimafundisho ya Yesu Kristo au ya mitume Wake ingekuwa ya thamani zaidi kueleza kuliko zile taarifa zenye geugeu zilizopatikana katika fasihi ya siku yake.—Yuda 17.

Yaripotiwa kwamba Papias alipatwa na kifo cha shahidi-mfia-imani huko Pargamamu katika 161 au 165 W.K. Kadiri hasa mafundisho ya Yesu Kristo yalivyoathiri maisha na mwenendo wa Papias haiwezi kusemwa kwa hakika. Lakini, alitamani sana kujifunza na kuzungumzia Maandiko. Ndivyo Wakristo wa kweli walivyo leo, kwani wanafahamu uhitaji wao wa kiroho. (Mathayo 5:3) Na kama vile Papias wanazithamini semi za Bwana.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki