Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 2/1 uku. 30
  • Baraza la Dini za Ulimwengu—Je! Litafanikiwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baraza la Dini za Ulimwengu—Je! Litafanikiwa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Miaka Mia Moja Iliyopita
  • Ufalme wa Mungu—Tumaini Pekee
  • Dini ni Nyingi Sana!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Dini Zakutana Huko Assisi Kutafuta Amani
    Amkeni!—2002
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanashiriki Katika Ibada za Dini Nyingine?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je, Dini Zote Zinaelekeza Watu kwa Mungu Yuleyule?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 2/1 uku. 30

Baraza la Dini za Ulimwengu—Je! Litafanikiwa?

MAMIA ya viongozi wa kidini walikusanyika kwenye Baraza la pili la Dini za Ulimwengu lililokutana katika Chicago, Illinois, U.S.A., katika kiangazi cha 1993. Dini ya Buddha, Jumuiya ya Wakristo, Dini ya Hindu, Dini ya Kiyahudi, na Uislamu hizo zote ziliwakilishwa. Wachawi na waabudu wa vijimungu-vike waliwakilishwa pia. Walizungumzia daraka lao katika kumaliza vita. Mwenyekiti wa baraza hilo alikiri kwamba “theluthi mbili ya mapigano makuu katika ulimwengu leo yana uhusiano wa kidini.”

Miaka Mia Moja Iliyopita

Je! baraza hilo lilifanikiwa? Ona lile lililotukia miaka mia moja iliyopita kwenye Baraza la kwanza la Dini za Ulimwengu. Hilo pia lilikutana katika Chicago, katika kiangazi cha 1893, na dini zaidi ya 40 ziliwakilishwa. Halmashauri ya Baraza la Dini za Ulimwengu yakiri kwamba wale waliohudhuria katika 1893 “waliamini kwamba hilo lingekuwa la kwanza kati ya mfululizo wa makusanyiko ya kimataifa ya mchangamano wa dini ambao ungechangia uelewevu, amani na maendeleo. Haikuwa hivyo. Kutovumilia na jeuri ya kidini imekuwa sehemu ya vita vya ile miaka 100 ambayo imepita, na yaendelea kuwa hivyo leo.” Kwa nini limekosa kufaulu? Kwa sababu wazo hilo lenyewe la mchangamano wa dini halikubaliwi na Mungu. Biblia husema hivi: “Msifungwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa.”—2 Wakorintho 6:14-17.

Kwa kufaa, toleo la Septemba 1893 la Zion’s Watch Tower lilikazia ukosefu wa utegemezo wa Kimaandiko wa lile Baraza la Dini za Ulimwengu liliposema hivi, kwa ucheshi kidogo: “[Waakiolojia] wamechimbua micheduara mizuri ajabu mingi ya udongo uliookwa kutoka katika magofu ya Babuloni na majiji mengine ya kale, lakini kuna mingine ambayo haijapatikana bado. . . . Hawajapata yoyote inayosema juu ya Musa na Yoshua wakiwa wameita ‘Baraza la Dini,’ la Wamoabi na Waamoni, na Waedomi . . . Hawajapata yoyote inayosema juu ya mzee Samweli mwenye nguvu akiwa ametumana huko Gathi na Ekroni kwamba wawakilishi wa makuhani wa Dagoni waje Shilo wafanye mkutano pamoja na makuhani wa Yehova . . . Hawajapata yoyote inayosema juu ya mzee Eliya mwenye ukanda wa ngozi akiwa amependekeza ‘baraza’ pamoja na makuhani wa Baali na Moloki kuwa na mazungumzo ya juma moja kuhusu mafundisho ya imani zao mbalimbali, wakiwa na kusudi la kuendeleza kustahi kwao dini ya mmoja na mwenzake.”

Ufalme wa Mungu—Tumaini Pekee

Baraza la Dini za Ulimwengu halitafanikiwa. Magazeti ya habari na wahudhuriaji walitumia maneno kama vile “mchafuko,” “msukosuko,” na “fujo” kuhusiana na baraza hilo. Kulingana na ripoti moja, hata polisi walihusika katika kutuliza migogoro miwili iliyosababishwa na migawanyiko ya kisiasa. Katika hati moja ya 1952, baraza hilo liliorodhesha mojayapo makusudi yalo kuwa: “Kusimamisha Baraza la Ulimwengu la Dini lenye kudumu kufanya kazi pamoja na UMOJA WA MATAIFA ili kupata amani na uelewevu ulimwenguni miongoni mwa watu wote.” Tofauti na hilo, Yesu alisema kwamba Ufalme wake haukuwa sehemu ya ulimwengu huu. Biblia huelekezea Ufalme wa Mungu kuwa suluhisho pekee la matatizo ya ainabinadamu.—Danieli 2:44; Yohana 18:36. ◆

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki