Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 8/1 uku. 3
  • Dini ni Nyingi Sana!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dini ni Nyingi Sana!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Asili Yake ni Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Dini Ilianzaje?
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
  • Je, Dini Zote Zinaelekeza Watu kwa Mungu Yuleyule?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Dini Zote Ni Barabara Mbalimbali Zinazoongoza kwa Mungu?
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 8/1 uku. 3

Dini ni Nyingi Sana!

IKIWA kuna Mungu mmoja tu, kwa sababu gani kuna dini nyingi sana? Je! umepata kutaka kujua jambo hilo? Watu wengi wenye kufikiri wametaka kujua. Na jibu lake si rahisi kupata. Hali ya kidini katika ulimwengu imevurugika sana. Ebu chunguza mambo fulani ya hakika.

Kuna Dini Ngapi? Ni vigumu kusema. Walakini kuna za namna mbali-mbali. Makabila fulani yanaabudu miungu ya mahali pao. Watu wengi wa nchi za Mashariki wanaabudu mababu zao waliokufa. Wengine wana mungu mmoja tu; Wahindu wana mamilioni ya miungu. Watu wengi katika Jumuiya ya Wakristo wanauamini utatu wa miungu—nafsi tatu katika mungu mmoja. Watu wengine wanafuata dini bila kuwa na imani katika mungu ye yote.

Je! Dini Zote ni Njia Tofauti-Tofauti za Kumwabudu Mungu Mmoja? Ndivyo watu wengi wanavyoamini. Walakini kama ambavyo mambo ya hakika yametoka kuonyesha, hiyo haiwezi kuwa kweli. Licha ya hayo, hata nyutu za miungu wanaoabudiwa ni tofauti. Dini nyingine zina miungu inayoaminiwa kuwa ni yenye ubaridi kuwaelekea wanadamu. Nyingine zina miungu yenye kutaka kulipa kisasi, na bado nyingine zinaiona miungu yao kuwa yenye fadhili. Kwa wazi, dini hizo zote hazizungumzi juu ya mu-ngu yule yule.

Je! Kuna Mambo Yanayofanana Kati ya Dini Zote? Zijapokuwa tofauti hizo, kuna mifanano iliyoenea sana ambayo tutazungumza juu yayo baadaye. Hata hivyo, kwa wakati huu, na tuseme hivi tu: Dini nyingi zinafundisha kwamba kuna mamlaka iliyo juu ya ile ya wanadamu (ingawa hazikubaliani mamlaka hiyo ni nini). Dini nyingi zinatoa uongozi juu ya namna ya kujiendesha katika maisha ya sasa (ijapokuwa uongozi huo unatofautiana katika dini hii na hii). Dini nyingi zinafundisha juu ya “wokovu” wa namna fulani, au tumaini la uzima ambao katika huo taabu zetu za wakati huu hazitakuwapo tena (ingawa zinatofautiana juu ya “wokovu” huo ni wa aina gani).

Je! Tunaweza Kujifunza Lo Lote Kutokana na Hayo? Kwa wazi, kwa ujumla wanadamu wanafahamu juu ya uwezekano wa kufurahia aina bora ya maisha kuliko ile waliyo nayo sasa. Hata hivyo, watu mmoja mmoja wanajiona wana upungufu kuweza kukabili matatizo hayo yaliyo mbele yao na wanaona uhitaji wa kusaidiwa na mamlaka iliyo juu zaidi.

Walakini kukiwa na dini nyingi sana hivyo zenye kutoa mashauri yanayopingana, mtu anapaswa kwenda wapi apate msaada huo ambao bila shaka anauhitaji? Ingawaje, dini hizo zote zenye kupingana zilitoka wapi? Je! kuna njia yo yote ya kutambua ni ipi ya haki?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki