Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 3/1 kur. 4-7
  • Amani ya Akili Katika Jamii Yenye Ushindani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Amani ya Akili Katika Jamii Yenye Ushindani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Chanzo cha Roho ya Ushindani
  • Kufanikiwa Bila Ushindani
  • Jinsi ya Kudumisha Amani ya Akili
  • Je! Ushindani Ndio Ufunguo wa Kufanikiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Tumeokolewa, Si Kupitia Matendo Tu, Bali Kupitia Fadhili Zisizostahiliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Roho Inayoendesha Taratibu ya Zamani Iliyopo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Je, ‘Utaendelea Kutembea Kwa Roho’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 3/1 kur. 4-7

Amani ya Akili Katika Jamii Yenye Ushindani

“MTU atakaye kuwa wa kwanza,” Yesu Kristo akawashauri mitume wake, “atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mtumishi wa wote.” Mitume walikuwa wakibishana juu ya ni nani aliyekuwa mkuu zaidi miongoni mwao. Walijua kwamba Yesu alichukia roho ya aina hiyo. Yeye hakuwashindanisha wanafunzi wake kamwe ili kuchochea maendeleo ya kiroho.—Marko 9:33-37.

Kabla ya kuja duniani, Yesu Kristo alishiriki katika kuumbwa kwa mume na mke wa kwanza wa kibinadamu na alijua jinsi walivyofanyizwa. (Wakolosai 1:15, 16) Wanadamu wa kwanza waliumbwa wakiwa na uwezo wa kufanya maendeleo bila kushindana na wengine bila huruma. Wanadamu hawakuwa na uhitaji wa kupingana miongoni mwao ili kuamua ni nani aliyekuwa kichwa chao, wala hawakushindana na wanyama katika shindano la kuendelea kuwa hai.—Mwanzo 1:26; 2:20-24; 1 Wakorintho 11:3.

Chanzo cha Roho ya Ushindani

Basi, hiyo roho ya ushindani isiyo na huruma ilikujaje kuwa kani yenye kutawala katika jamii ya kibinadamu? Kesi ya kwanza ya uuaji wa kimakusudi katika historia ya kibinadamu yatoa kidokezo. Roho ya ushindani kwa upande wa Kaini, mwana mwenye umri mkubwa zaidi wa mume na mke wa kwanza wa kibinadamu, iliongoza kwenye msiba huo. Kaini alimuua ndugu yake Abeli kwa sababu dhabihu ya Abeli ilimpendeza Mungu, ilihali ya Kaini haikumpendeza. Na Biblia yasema kwamba Kaini ‘alikuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake.’—1 Yohana 3:12; Mwanzo 4:4-8.

Ndiyo, yule mwovu, Shetani Ibilisi, ndiye mwanzilishi na mchochezi wa roho ya ushindani. Ingawa alikuwa mwana wa kimalaika wa Mungu mwenye mapendeleo ya juu, alitaka zaidi. (Linganisha Ezekieli 28:14, 15.) Alipomshawishi Hawa, alifunua tamaa yake mwenyewe. Alisema kwamba kwa kula lile tunda lililokatazwa, ‘hakika Hawa angekuwa kama Mungu.’ (Mwanzo 3:4, 5) Kwa kweli, ni Shetani aliyetaka kuwa kama Mungu, akishindana na Yehova. Roho ya kushindana dhidi ya Mungu ilimhimiza kuasi.—Yakobo 1:14, 15.

Roho hiyo inaambukiza. Chini ya uvutano wa Shetani, amani ya kupewa na Mungu ya mpango wa awali wa familia ilipotea. (Mwanzo 3:6, 16) Tangu uasi wake dhidi ya Mungu, Shetani Ibilisi ameitawala ainabinadamu, akichochea roho ya ushindani, hata akiwadanganya wanaume na wanawake waamini kwamba ushindani usio na huruma ndio ufunguo wa kufanikiwa. Hata hivyo, Biblia yaeleza hivi: “Hapo palipo wivu na ugomvi, ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya.” (Yakobo 3:14-16) Hivyo Shetani amemnyang’anya mwanadamu furaha na amani yake ya akili.

Kufanikiwa Bila Ushindani

Tofauti na uvutano wa Shetani wenye hila, Biblia yatoa vielelezo vya kufanikiwa bila ushindani. Kikuu zaidi ni kile cha Yesu Kristo. Ijapokuwa alikuwa akiwako katika umbo la Mungu, hakufikiria kamwe kuwa sawa na Mungu bali alichukua umbo la mtumwa na kuja duniani. Zaidi ya hayo, alijinyenyekeza akawa mtiifu hadi kifo juu ya mti wa mateso. Mtazamo huo mtiifu, bila roho yoyote ya ushindani, uliongoza kwenye kujishindia kwake upendeleo wa kimungu. “Kwa sababu hiihii pia Mungu alimkweza kwenye cheo cha juu zaidi na kumpa kwa fadhili jina lililo juu ya kila jina jingine.” (Wafilipi 2:5-9, NW) Ni ufanisi upi mkubwa zaidi ambao ungeweza kupatikana na kiumbe chochote kile? Alimpendeza Baba yake kwa kadiri ambavyo hakuna kiumbe kingine ambacho kingeweza, na alifanya hivyo bila roho ya kutaka kupita wote au ya ushindani.—Mithali 27:11.

Wale malaika waaminifu wengi sana mbinguni huonyesha mtazamo uo huo. Ingawa Yesu, aliyekuwa kichwa cha malaika, alikuwa chini kidogo kuliko malaika alipokuja duniani, walitumikia mahitaji yake kwa nia ya kupenda. Kwa wazi, wao hawakufikiria hata kidogo kutumia hali hiyo kwa faida yao na kujaribu kutwaa cheo chake cha Malaika Mkuu.—Mathayo 4:11; 1 Wathesalonike 4:16; Waebrania 2:7.

Kuchukia kwao sana mitazamo ya ushindani kunaonekana kwa wazi hata zaidi tufikiriapo njia ambayo wameitikia kusudi la Mungu la kukweza wanadamu fulani wasio wakamilifu kwenye uhai wa kiroho usioweza kufa, ambao wakiwa katika hali hiyo ‘watawahukumu malaika.’ (1 Wakorintho 6:3) Malaika wana maarifa mengi katika kumtumikia Yehova na wana uwezo mwingine zaidi wa kutimiza mema kuliko wanadamu wasio wakamilifu. Bado, malaika huwahudumia kwa furaha wale wapakwa walio duniani, bila wivu hata kidogo juu ya yale ambayo hao watapokea. (Waebrania 1:14) Mtazamo wao mzuri, usio na ushindani huwawezesha waendelee kutumikia wakiwa mbele ya kiti cha utawala cha Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

Kisha, fikiria wale watumishi waaminifu wa kale wa Mungu watakaofufuliwa duniani. Abrahamu alikuwa kielelezo cha imani chenye kutokeza na aliitwa “baba ya wote waaminio.” (Warumi 4:9, 11) Ayubu aliweka kielelezo bora sana cha uvumilivu. (Yakobo 5:11) Musa, aliyekuwa “mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi,” aliongoza taifa la Israeli kwenye uhuru. (Hesabu 12:3) Ni nani miongoni mwa wanadamu wasio wakamilifu aliye na kielelezo bora zaidi cha imani, uvumilivu, na upole kuliko wanaume hao? Hata hivyo, wamo katika mstari wa kurithi makao ya kidunia ya Ufalme wa Mungu. (Mathayo 25:34; Waebrania 11:13-16) Wao, kama vile Yohana Mbatizaji, watakuwa na cheo cha chini kwa “aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni.” (Mathayo 11:11) Je! watafikiria hata kidogo kulalamika wakisisitiza kwamba imani, uvumilivu, au upole wao ulikuwa sawa na au katika hali nyingine ulipita ule wa wale wanaopewa uhai mbinguni? Hasha! Watakuwa raia wa kidunia wenye furaha wa Ufalme wa Mungu.

Leo pia, watu bila mtazamo wa ushindani ni washirika wenye kupendeza. Yasuo, aliyetajwa katika makala ya kwanza, alipata madeni mengi sana kwa sababu ya kujaribu biashara ya kununua na kuuza dhahabu na kupoteza mali zake zote. “Marafiki” wake walimwacha. Kwa kuwa mke wake alikuwa ameanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, alihudhuria mikutano yao kwa sababu ya kuhisi majuto kwa ajili ya kule kuteseka alikoletea familia yake. Hatimaye, aliacha kuwa mwenye ushindani akawa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Sasa anafurahia ushirika wa marafiki Wakristo, ambao huwa tayari kumsaidia katika nyakati za msononeko.

Jinsi ya Kudumisha Amani ya Akili

Si rahisi kudumisha amani ya akili katika jamii yenye ushindani isiyo na huruma. Twafanya vema kuona kwamba Biblia hushutumu “uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda” kuwa “matendo ya mwili” yanayozuia watu wasiurithi Ufalme wa Mungu. Matendo yote hayo yahusiana sana na roho ya ushindani. Si ajabu kwamba mtume Paulo aliwatia moyo Wagalatia hivi: “Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.”—Wagalatia 5:19-21, 26.

Katika muktadha huo, barua ya Paulo ilionyesha ufunguo wa kukabiliana na ushindani wa kujisifu. Alisema hivi: “Tunda la roho ni upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujidhibiti. Dhidi ya mambo ya namna hiyo hakuna sheria yoyote.” (Wagalatia 5:22, 23, NW) Tunda la roho hutusaidia tuondoshe ushindani akilini mwetu. Kwa kielelezo, fikiria sifa ya upendo. “Upendo hauhusudu,” aeleza Paulo. “Haujigambi, haututumuki, haujiendeshi bila adabu, hautafuti masilahi yao wenyewe, haupati kuwa wenye kuchokozeka.” (1 Wakorintho 13:4-7, NW) Kwa kukuza upendo, twaweza kung’oa wivu, ambayo ndiyo kani ichocheayo roho ya ushindani. Yale matunda mengine ya roho hutusaidia pia kuondosha dalili zozote za roho ya ushindani isiyo na huruma kutoka katika mioyo na akili zetu. Kwani, kujidhibiti kukiwako, hamu yoyote ya kushindana dhidi ya wengine ili kushinda juu chini yaweza kukandamizwa upesi!—Mithali 17:27.

Hata hivyo, ili kukuza sifa hizo, ni lazima turuhusu roho ya Mungu ifanye kazi juu yetu. Twaweza kuiendeleza kazi hiyo ifaayo ya roho takatifu kwa kudumu katika sala na kuomba ili roho ya Mungu itusaidie. (Luka 11:13) Mungu atatupa sisi nini, katika kuitikia sala yetu? Biblia hujibu hivi: “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”—Wafilipi 4:6, 7.

Hiyo ilikuwa wazi kwa habari ya mitume wa Yesu. Hata baada ya Yesu kuanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana katika usiku wake wa mwisho pamoja na mitume, walikuwa bado wakizozana juu ya ni nani kati yao aliyeonekana kuwa mkuu zaidi. (Luka 22:24-27) Yesu alikuwa amejaribu katika pindi mbalimbali kuwasaidia wasahihishe fikira zao, lakini mtazamo huo wa ushindani ulikuwa umekazika kikiki ndani yao. (Marko 9:34-37; 10:35-45; Yohana 13:12-17) Hata hivyo, mara walipopokea roho takatifu siku 50 hivi baada ya mzozo huo, mtazamo wao ulibadilika. Hakukuwa na bishano juu ya ni nani angewawakilisha katika kusema na ule umati wenye udadisi uliokusanyika katika ile siku ya Pentekoste.—Matendo 2:14-21.

Hakukuwa na nafasi ya utawala wowote wa kibinadamu juu ya kutaniko la Kikristo. Walipohitaji kusuluhisha tatizo kuhusu tohara, Yakobo, ambaye hata hakuwa mwanafunzi wakati wa kifo cha Yesu, alisimamia mkutano huo wa maana. Hakuna ishara yoyote ya mzozo juu ya ni nani ambaye angeongoza katika mkutano huo wa baraza lililoongoza la kutaniko la Kikristo. Ilikuwa tofauti kama nini na wakati mitume walipotiwa waa na roho ya ushindani! Kwa msaada wa roho takatifu, walikumbuka mafundisho ya Yesu wakaanza kuelewa maana ya masomo yake.—Yohana 14:26.

Jambo hilo laweza kuwa kweli kwetu. Kwa msaada wa roho takatifu, twaweza kushinda hamu yoyote yenye kuendelea ya kushindana na wengine ili kufanya maendeleo kwa hasara yao. Badala ya hivyo, twaweza kupata amani ya akili ipitayo akili zote. Biblia hutuhakikishia kwamba hivi karibuni, chanzo cha ushindani usio na huruma, Shetani Ibilisi, atatiwa katika abiso, utendaji wake utakomeshwa. (Ufunuo 20:1-3) Ushindani kati ya majirani hautakuwako tena. Je! tokeo litakuwa jamii isiyo na maendeleo? Hasha! Wanadamu watafikia ukamilifu, si kupitia ushindani wowote kati yao, bali kupitia matumizi ya dhabihu ya fidia ya Yesu kuelekea wao.—1 Yohana 2:1, 2.

Keinosuke, aliyetajwa mapema, ambaye wakati mmoja alikuwa amejionea utukufu wa ufanisi wa kilimwengu kwa kuuza magari mengi zaidi ya yeyote, alijichosha kiakili na kimwili, lakini aliacha kazi yake hatimaye. “Sasa, maisha yangu yamejaa shangwe ya kweli,” yeye asema. Alikuja kuona ni kwa nini ufanisi wa kweli ulitia alama maisha ya Yesu. Sasa yeye hupata kiburudisho katika yoyote awezayo kufanya katika kutaniko la Mungu la ulimwenguni pote. Hivyo anatayarishwa kwa ajili ya ulimwengu mpya, ambao hautakuwa na ushindani. Wewe pia waweza kuwa na mwono wa kimbele wa jamii hiyo ya ulimwengu mpya kwa kuzuru mojayapo Majumba ya Ufalme katika eneo lako na kushirikiana na Mashahidi wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Amani na ushirikiano zitafurahiwa na jamii ya kibinadamu katika ulimwengu mpya wa Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki