Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 4/15 kur. 4-7
  • Waweza Kupata Wapi Mwongozo Wenye Kutumainika?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waweza Kupata Wapi Mwongozo Wenye Kutumainika?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Akusudiwa Kupokea Mwongozo wa Kimungu
  • Utungaji wa Biblia Kimungu
  • Yenye Manufaa—Haidhuru Kamwe
  • Wakati Ujao Salama kwa Wale Wafuatao Mwongozo wa Mungu
  • Tafuta Mwongozo wa Mungu Katika Kila Jambo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je, Kuna Mwongozo Unaotegemeka wa Kuwa na Maisha Bora ya Wakati Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Kwa Nini Utegemee Mwongozo wa Biblia?
    Amkeni!—2006
  • Unaweza Kupata Wapi Uongozi?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 4/15 kur. 4-7

Waweza Kupata Wapi Mwongozo Wenye Kutumainika?

“EE BWANA, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. Ee BWANA, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza.”—Yeremia 10:23, 24.

Mwandishi wa Biblia Yeremia aliandika maneno hayo yapata karne 25 zilizopita. Hali mbaya sana ya kuhuzunisha ya wanadamu baada ya maelfu ya miaka ya kutumia mwongozo wa kibinadamu yathibitisha ule ukweli usiokanushika wa taarifa hiyo. Lakini huenda ukauliza hivi, ‘Mwongozo wenye kutumainika waweza kupatikana wapi?’

Andiko lililonukuliwa juu laelekezea chanzo cha mwongozo na mwelekezo wenye kutegemeka ulio mkuu sana kupita binadamu—Muumba wa mwanadamu, Yehova Mungu. Kwa hakika hakuna ajuaye maumbile ya mwanadamu na mahitaji yake vema zaidi ya Muumba wetu. Hata hivyo, je, Mungu anapendezwa kutuandalia mwongozo na mwelekezo huo? Yeye hufanyaje hivyo? Je! ni wenye kutumika kwa nyakati zetu?

Akusudiwa Kupokea Mwongozo wa Kimungu

Inajulikana vema kwamba tofauti kuu inayotenga mwanadamu na wanyama ni muundo, uwezo, na utendaji wa ubongo wa kibinadamu. Katika wanyama karibu utendaji wote wa ubongo umeamriwa kimbele katika ile ambayo imekuja kuitwa hekima ya kisilika. Hali sivyo kwa habari ya wanadamu.—Mithali 30:24-28.

Tofauti na ubongo wa wanyama, sehemu kubwa ya ubongo wa kibinadamu haifanyi kazi kwa kuamriwa kimbele. Mungu aliwapa wanadamu uwezo wa hiari, ukiwawezesha kufanya maamuzi ya kiakili na kuonyesha sifa za hali ya juu zaidi, kama vile upendo, ukarimu, kutokuwa na ubinafsi, haki, na hekima.

Je! ni jambo la akili kufikiri kwamba Mungu angemuumba mwanadamu akiwa na uwezo wa akilini wa jinsi hiyo bila kuandaa aina fulani ya mwongozo kuhusu jinsi uwezavyo kutumiwa kwa njia bora zaidi? Mungu aliwapa wanadamu wa kwanza mwongozo wa moja kwa moja. (Mwanzo 2:15-17, 19; 3:8, 9) Hata baada ya mwanadamu kutumbukia katika dhambi, Yehova aliendelea kuongoza wanaume na wanawake waaminifu, hasa kupitia Neno lake mwenyewe lililopuliziwa, Biblia. (Zaburi 119:105) Hilo limewaruhusu wanadamu wakabili kwa mafanikio matatizo ya maisha ya kila siku watumiapo hiari yao kwa hekima.

Utungaji wa Biblia Kimungu

Ni nini hufanya Biblia iwe chanzo cha mwongozo wenye kutumainika? Kwanza, hiyo hutoa habari ambayo Muumba pekee angeweza kuandaa. Huorodhesha historia ya matukio yaliyotokea muda mrefu kabla ya mwanzo wa uhai wa kibinadamu. Kwa kielelezo, huandaa historia ya jinsi dunia ilivyotayarishwa katika hatua za kufuatana hadi ilipofaa kutegemeza uhai wa kibinadamu. (Mwanzo, sura 1, 2) Ingawa hii ilirekodiwa katika Biblia muda wa miaka zaidi ya 3,000 iliyopita, yapatana na mawazo ya kisayansi ya ki-siku-hizi.

Muda mrefu kabla ya wanadamu kwa ujumla kukubali kwamba dunia ni mviringo, Biblia ilijulisha hivi: “[Mungu] hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, na kuutundika ulimwengu [dunia, NW] pasipo kitu.” (Ayubu 26:7) Zaidi ya hayo, Biblia hufunua kwamba “[kuna Mmoja, New World Translation] anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi.” (Isaya 40:22) Mungu pekee, aliye Muumba, ndiye angaliweza kuandaa elezo hili.

Mwanadamu hakupewa kipawa cha kuweza kuona kimbele mambo yanayotazamiwa kuja. Badala ya hivyo, Muumba hutabiri wakati ujao kupitia kurasa za Biblia. Mungu alimpulizia nabii Isaya aandike hivi juu ya Yeye: “Mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.”—Isaya 46:9, 10.

Biblia imeonyesha kwamba yaweza kutabiri mwisho tangu mwanzo kwa usahihi wa ajabu. Kwa kielelezo, ilitabiri juu ya kuinuka, kuanguka, na tabia za serikali kuu za ulimwengu katika maelfu ya miaka ya historia ya kibinadamu. Unabii huo mwingi wenye kutokeza uliandikwa karne nyingi kabla ya utimizo wao, katika hali nyingine ikiwa maelfu ya miaka kimbele. Hivyo Biblia hutabiri kwa usahihi matukio ya ki-siku-hizi, pamoja na matokeo yayo ya mwisho. Biblia haina kifani pia kwa sababu hiyo huonyesha njia ya kupata wokovu wakati wa uharibifu wa serikali za kufanyizwa na wanadamu kwenye Har–Magedoni, “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.” Ufalme wa Mungu mikononi mwa Mwana wake, Yesu Kristo, utatimiza tendo hilo kuu.—Ufunuo 16:14, 16; 17:9-18; Danieli, sura ya 2, 8.

Yenye Manufaa—Haidhuru Kamwe

Hekima duni ya kibinadamu si kamilifu; kwa sababu hiyo, shauri la kibinadamu si lenye manufaa sikuzote, hata ingawa huenda likatolewa kwa madhumuni mazuri. Sivyo kwa habari ya shauri la Biblia. Mungu mwenyewe asema hivi: “Mimi ni BWANA, . . . nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Laiti ungalisikiliza amri zangu! ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari.”—Isaya 48:17, 18.

Mwongozo wa kimungu hutusaidia tupange mambo ya kutangulizwa na kushikamana na kanuni za juu zaidi maishani. Ingawa jamii ya ki-siku-hizi hukazia matimizo na miradi ya kimwili, Biblia hukazia jinsi lilivyo jambo lenye thamani kwetu “tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.” (2 Wakorintho 4:18) Katika njia hiyo tunatiwa moyo tuwe na miradi iliyo mizuri zaidi maishani, yaani, miradi ya kiroho kuhusiana na kufanya mapenzi ya Mungu, mradi wa mwisho ukiwa ule wa uhai wa milele katika mfumo mpya wenye haki.

Mkristo anapojikakamua ili kufuatia miradi hiyo ya hali ya juu, shauri la Biblia humsaidia kuishi maisha yaliyo bora zaidi iwezekanavyo katika mfumo huu mwovu wa mambo. Hekima ya kibinadamu ya ki-siku-hizi huelekea kuchochea ile falsafa ya kufanya kidogo iwezekanavyo kazini na kuchuma fedha nyingi iwezekanavyo. Kwa upande ule mwingine, Biblia hutuambia “atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.” Mtume Paulo aliwaandikia Wakristo Waebrania hivi: “Tunaamini kwamba tuna dhamiri njema, tukitaka kuwa na mwenendo mwema katika mambo yote.”—Mithali 10:4; Waebrania 13:18.

Biblia hutoa pia mawaidha yatumikayo kuhusu mpango wa familia. Hiyo huthibitisha kimahususi fungu la mume na la mke pia katika mpango wa ndoa, na pia njia sahihi ya kulea na kuelimisha watoto. Husema hivi: “Imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. . . . Wala mke asikose kumstahi mumewe. Enyi watoto, watiini wazazi wenu . . . Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.” Kufuata shauri la Muumba lililo bora zaidi huchangia sana uthabiti na furaha ya familia.—Waefeso 5:21–6:4.

Wakati Ujao Salama kwa Wale Wafuatao Mwongozo wa Mungu

Neno la Mungu lililoandikwa huonyesha suluhisho la Mungu kwa matatizo yote ya wanadamu. Hivi karibuni sana Yehova Mungu ataondolea mbali kabisa mfumo wa mambo uliopo, pamoja na maumivu, utovu wa haki na kuteseka kote, na ataweka mfumo wake mwadilifu mahali pao. Biblia hueleza hili kwenye 2 Petro 3:7-10, ikiongeza hivi kwenye mstari wa 13: “Kama ilivyo ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.” Hiyo ndiyo habari njema zaidi ambayo ingeweza kutolewa kwa familia ya kibinadamu. Ndio ujumbe hasa ambao Biblia hutoa na ambao Mashahidi wa Yehova huhubiri katika mabara na visiwa vya bahari zaidi ya 200.

Mapenzi ya Mungu yanapozoewa duniani pote, familia nzima ya kibinadamu itanufaika kwa kufuata ule mwongozo mzuri kabisa wa Muumba wayo, Yehova. Hakutakuwako tena matatizo, uhalifu, na madawa ya kulevya. Wanadamu hawatapatwa tena na maradhi, kuzeeka, na kifo. Familia ya kibinadamu itainuliwa hadi ukamilifu ambao wazazi wetu wa kwanza walikuwa nao kabla ya wao kuasi dhidi ya mwongozo wa Mungu.

Kitabu cha mwisho cha Biblia hujumlisha vema kama nini hali ya furaha ya wale watumainio mwongozo wa kimungu! Ufunuo 21:4, 5: “[Mungu] atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.” Muumba wetu alithibitisha hilo, akisema: “Tazama, nayafanya yote kuwa mapya.” Yeye aongeza hivi: “Maneno hayo ni amini na kweli.”

Ikiwa tutapokea baraka hizo, Mungu atazamia nini kwetu? Mtume Paulo aeleza kwamba mapenzi ya Mungu ni kwamba “watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo [ujuzi sahihi wa, NW] kweli.” (1 Timotheo 2:4) Mashahidi wa Yehova wakualika kwa uchangamfu upate ujuzi huo sahihi wa kweli kupitia funzo kamili la Biblia. Kwa kujifunza kwa bidii-nyendelevu kuhusu mapenzi ya kimungu, wewe pia waweza kujionea mwenyewe kwamba hekima ya kimungu ndio mwongozo pekee wenye kutegemeka katika nyakati hizi za hatari. Uharaka wa nyakati hizi hufanya iwe lazima tuufuate kuliko wakati mwingine wowote!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki