Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 7/1 kur. 4-7
  • Kanisa Lililogawanyika Je! Laweza Kudumu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kanisa Lililogawanyika Je! Laweza Kudumu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Yule Mtu wa Kuasi”
  • Ngano na Magugu
  • Migawanyiko Mipya
  • “Tokeni Kwake, Enyi Watu Wangu”
  • Kuna Dini Moja Tu ya Kweli ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kuna Tumaini Gani kwa Ukristo?
    Amkeni!—2007
  • Uasi Juu ya Mungu Unafunuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Shamba Lenye Kuzaa Ngano na Magugu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 7/1 kur. 4-7

Kanisa Lililogawanyika Je! Laweza Kudumu?

“WATU wote wanaodai kukubali kweli yenye kuokoa ya Kristo ni wa Kanisa linaloonekana. Migawanyiko ya Jumuiya ya Wakristo—kati ya Mashariki na Magharibi, na kati ya Roma [Kanisa Katoliki ya Roma] na makanisa ya Mapinduzi—ni migawanyiko iliyo katika Kanisa moja.” (Christians in Communion) Hivyo ndivyo mwandikaji mmoja wa vitabu aonavyo Ukristo—kama familia zilizotawanyika sana za dini, zote zikidai kuwa na imani ya aina fulani kwa Yesu Kristo.

Hata hivyo, hiyo ni familia iliyogawanyika, yenye itikadi na viwango vinavyopingana. “Ukristo wa siku-hizi . . . unaweka viwango vya chini kwa mshiriki kuliko viwango viwekewavyo mtu apandaye basi,” asema mtoa-maoni mmoja. Basi, tutapimaje hali yao ya kiroho? Askofu wa Katoliki Basil Butler akata kauli hivi: “Ukristo uliogawanyika ni mgonjwa mahututi.” (The Church and Unity) Ugonjwa huo ulianzaje? Je! kuna matumaini ya kwamba utapata nafuu?

“Yule Mtu wa Kuasi”

Mtume Paulo alionya kwamba ukosefu wa muungano ungesitawi. Yeye aliandikia Wakristo hivi katika Thesalonike waliofikiri kwamba kuwapo kwa Kristo kulikuwa kumefika: “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji [siku ya Yehova], usipokuja kwanza ule ukengeufu [uasi-imani, NW]; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu.”—2 Wathesalonike 2:3.

Huyu “mtu wa kuasi” alianzisha uasi-imani na maasi katika kutaniko la Kikristo. Yeye ni nani? Si mtu fulani mmoja, bali, ni jamii ya makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. Upesi baada ya vifo vya mitume wa Yesu, jamii hiyo ilijikweza juu ya kutaniko lililoasi imani na hatimaye ikaja kufundisha falsafa za kipagani, kama vile Utatu na kutokufa kwa nafsi ya binadamu. (Matendo 20:29, 30; 2 Petro 2:1-3) Kama virusi ziwezavyo kuua, jamii hiyo iliambukiza kutaniko lililodai kuwa la Kikristo kwa mawazo yaliyotokana na roho waovu ambayo bila shaka yangetokeza mgawanyiko.—Wagalatia 5:7-10.

Ambukizo hilo tayari lilikuwa limeanza katika siku ya mtume Paulo. Yeye aliandika hivi: “Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.” (2 Wathesalonike 2:7) Mitume walitumika wakiwa vizuizi dhidi ya sumu ya uasi-imani. Uvutano wao wenye kuunganisha ulipoondolewa, uasi-imani usiozuiliwa ulienea kama donda-ndugu.—1 Timotheo 4:1-3; 2 Timotheo 2:16-18.

Utendaji wa huyu “mtu wa kuasi” waendelea bila kukoma. Katika ripoti moja ya hivi karibuni juu ya “kanisa katika mashaka ya kingono na kitheolojia,” shemase mmoja mkuu wa Kanisa la Uingereza anukuliwa akilalamika hivi: “Mapendekezo kwamba makasisi wasiingilie ngono nje ya ndoa hutupiliwa mbali. Watu wanaoendelea kufanya ugoni wa jinsia-moja hutawazwa. Wamefanya wema kuwa uovu na uovu kuwa wema.”—The Sunday Times Magazine, London, Novemba 22, 1992.

Ngano na Magugu

Yesu Kristo mwenyewe alifundisha kwamba Ukristo wa kweli ungepotea usionekane kwa muda. Alisema kwamba kuanzishwa kwa kutaniko la Kikristo kumefanana na mtu anayepanda mbegu nzuri katika shamba lake. Lakini, Yesu akasema, “akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano.” Watumwa wake walipouliza kama wanaweza kujaribu kung’oa magugu, mwenye shamba alijibu hivi: “La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.” Mchanganyiko huo wa ngano na magugu ungeendelea kwa muda gani? Mwenye shamba akasema: “Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno.”—Mathayo 13:25, 29, 30.

Mpaka “wakati wa mavuno,” au wakati wa kutenganishwa katika siku za mwisho za “mfumo wa mambo,” Wakristo bandia wangekua wakati mmoja na Wakristo wa kweli. (Mathayo 28:20) Shetani Ibilisi alitumia waasi-imani kutokeza kutaniko bandia la Kikristo lililogawanyika na lenye ufisadi. (Mathayo 13:36-39) Wao walitokeza Ukristo bandia wenye aibu kutoka kwa Ukristo wa kweli. (2 Wakorintho 11:3, 13-15; Wakolosai 2:8) Kadiri kanisa lilivyovunjika vipande-vipande kwa muda wa karne hizo, ndivyo ilizidi kuwa vigumu zaidi kutambua Wakristo wa kweli.

Migawanyiko Mipya

Katika nyakati za kisasa, chasema kitabu The Testing of the Churches—1932-1982, “migawanyiko [m]ipya imetokea, hasa dini ya roho, inayokazia kwamba mtu awe na imani ya kibinafsi na maono.” Kwa kupendeza, wengine huona dini za kuzaliwa mara ya pili, za roho, kuwa ishara za mvuvumko wa kiroho badala ya kuwa migawanyiko mipya. Kwa kielelezo, Ireland Kaskazini ilipatwa na mvuvumko kama huo katika miaka ya 1850. Kulikuwa na matumaini makubwa. Ripoti moja ilieleza juu ya “muungano wa wahudumu . . . miongoni mwa [dini za] Presbiteri, Wesley, na Independent” na ikasema kwamba “kila siku kulikuwa na ripoti mpya za ruya, usingizi, njozi, ndoto, na miujiza.”—Religious Revivals.

Wengi waliona maonyesho hayo ya kutazamisha kuwa uthibitisho wa roho ya Mungu ikifanya kazi kufufua kanisa lake. “Kanisa la Mungu,” akasema mtoa-maoni mmoja, “limevuvumka kabisa katika maeneo hayo.” Lakini, ingawa mvuvumko huo hasa ulitangazwa kuwa “muhula mtukufu na usio na kifani katika historia ya kidini ya Ulster,” huo pamoja na mivuvumko mingine kama huo haujatokeza muungano wa kidini miongoni mwa wale wanaodai kurudi kwa hali ya kiroho.

Watu kama hao watabisha kwamba wao wameungana kwa mambo ya msingi. Lakini hiyo ndiyo hoja inayotumiwa na Jumuiya ya Wakristo yote, wanaoona kwamba “kile kinachowaunganisha Wakristo tayari ni muhimu zaidi kuliko mambo ambayo yangali yanawagawanya.” (The Church and Unity) Jumuiya ya Wakristo yadai hivi: “Muungano wetu wa msingi kati yetu na pamoja na Wakristo wenzetu wote unategemea ubatizo wetu katika Kristo.” (Christians in Communion) Lakini kusema kwamba migawanyiko si muhimu kwa sababu ya imani moja kwa Yesu ni kama kusema kwamba kansa si hatari maadamu moyo wako ni wenye nguvu.

Ukweli ni kwamba dini kama hizo za kisasa zimeongezea mchafuko na kutokeza mvurugo wa kiroho huku walimu wenye kushawishi wakijikusanyia wafuasi. Jim Jones na David Koresh ni vielelezo vya karibuni zaidi vya wale waliopotosha maelfu ya watu. (Mathayo 15:14) Mhudumu mmoja wa Baptisti ni mshiriki mashuhuri wa kikundi cha Ku Klux Klan. Yeye alinganisha jitihada zake za ukuu wa watu weupe na mvuvumko wa kidini na asema kwamba wale wanaoshiriki katika kikundi hicho “watapewa nguvu ya kuongozwa kimungu, wapewe moyo-mkuu wa Yeye aliyekufa Kalvari [Yesu Kristo].”

Vipi juu ya zile zinazosemekana kuwa miujiza, kazi zenye nguvu, na ishara zinazotolewa kwa jina la Yesu? Kumbuka onyo kali la Yesu Kristo kwamba si wale wanaosema tu “Bwana, Bwana” ndio wanaopata kibali chake, bali, ni ‘wale wafanyao mapenzi ya Baba yake.’ Watu wengi leo hata hawajui jina la Baba yake, Yehova. Yesu aliwaonya wale ambao ‘wangetoa pepo kwa jina lake, na kufanya miujiza mingi kwa jina lake’ huku wakiwa ‘watendao maovu.’—Mathayo 7:21-23.

“Tokeni Kwake, Enyi Watu Wangu”

Kuna matazamio gani kwa Jumuiya ya Wakristo yenye ugonjwa? Ni matazamio mabaya sana. Basi, je, tutii lile shauri la Butler, ambaye ni askofu wa Katoliki, la “kujiunga [na kanisa] bila kufuatia mambo mengi na kulisaidia liendelee ‘kujitakasa’ ndani yalo lenyewe”? La! Jumuiya ya Wakristo iliyogawanyika na yenye kutokeza migawanyiko haitadumu. (Marko 3:24, 25) Yeye ni sehemu ya milki ya ulimwengu ya dini bandia inayoitwa Babiloni Mkubwa. (Ufunuo 18:2, 3) Mfumo huo wa kidini wenye hatia ya damu wakabili uharibifu unaokaribia sana unaoletwa na Mungu.

Biblia haidokezi kwamba Wakristo wa kweli wabaki ndani ya tengenezo hilo la kidini lenye ufisadi na kujaribu kulirekebisha kutoka ndani. Badala ya hivyo, inatia moyo hivi: “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.”—Ufunuo 18:4, 5.

‘Mtoke’ mkienda wapi? Kumbuka, Yesu aliahidi kwamba wakati wa mavuno, Wakristo wa kweli wangekusanywa pamoja tena katika muungano wa ulimwenguni pote. Nabii Mika pia alitabiri juu ya mkusanyo huo tena kwa maneno haya: “Nitawaweka pamoja kama [kundi katika zizi, NW].” (Mika 2:12) Je! jambo hilo limetukia?

Ndiyo! Wakristo wa kweli sasa wanakusanywa katika udugu wa duniani kote wenye muungano. Wao ni akina nani? Wao ni kutaniko la Kikristo la Mashahidi wa Yehova, ambao kwa muungano wanatangaza habari njema juu ya Ufalme wa Mungu katika nchi 231. Wao wamekataa mafundisho ya Jumuiya ya Wakristo yenye kuleta migawanyiko nao watafuta kumwabudu Mungu kwa kupatana na kweli ya Neno lake.—Yohana 8:31, 32; 17:17.

Unakaribishwa kwa uchangamfu kusema nao. Kama ungependa kujua mengi zaidi kuhusu Mashahidi wa Yehova, tafadhali wasialiana nao mahali penu au kupitia anwani ifaayo kwenye ukurasa 2 wa gazeti hili.

[Picha katika ukurasa wa 7]

“Mungu amekumbuka maovu yake”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki