Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 8/1 kur. 342-344
  • Uasi Juu ya Mungu Unafunuka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uasi Juu ya Mungu Unafunuka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “SIRI YA KUASI”
  • KIZUIZI CHA KARNE YA KWANZA
  • UASI UNATOKEZA KABISA
  • Kutambulisha “Mtu wa Kuasi [Sheria]”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kifo cha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Mtu wa Uasi Sheria
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Kristo Aliuchukia Ukosefu wa Kufuata Sheria —Je! Wewe Wauchukia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 8/1 kur. 342-344

Uasi Juu ya Mungu Unafunuka

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1, 2. (a) Shetani Ibilisi ametumia nini kama njia yake kuu kujaribu kupindua kundi la kweli la Mungu? (b) Ni wakati gani uasi huu ulipofunuliwa?

TUNGEWEZA kutazamia kwamba, Mungu akiwa na adui, huyo angejaribu kupindua mpango wo wote ambao Mungu angewafanyia watu wake. Na njia yenye matokeo zaidi ingekuwa kuanzisha uasi ndani ya kundi la Mungu lenyewe, na kutokeza katika hilo ‘kundi la Mungu’ la uongo. Adui ya Mungu Shetani amefanya jambo lili hili. Jitihada hiyo ilianza karne ya kwanza, siku zile zile mitume walipokuwa hai. Ni wakati gani uasi huu ulipofunuliwa kabisa?

2 Kufunuliwa kabisa kwa uasi huu kulianza muda mfupi tu baada ya mitume kufa. Wakati huo waliokuwa Wakristo wa kweli wangeweza kuuona wazi, ingawa wachoyo wenye kujidai kuwa Wakristo walivutiwa nao wakapofushwa hasa wasione ulivyokuwa hasa na mwisho wake uliosemwa kwa unabii wasijue ungekuwaje.

“SIRI YA KUASI”

3, 4. Mtume Paulo aliyaita nini matendo ya kikundi hicho chenye uasi katika siku zake, kabla hakijatokeza kabisa, na kwa sababu gani?

3 Mtume Paulo aliyaita matendo ya kikundi hicho katika siku zake “siri ya kuasi.” Hii ni kwa sababu uasi huo usingeweza kupangwa na kujitokeza wenyewe wakati huo. Kwa sababu gani sivyo?

4 Akijibu ulizo hili, mtume Paulo aliandikia Wakristo katika mji wa Thesalonike hivi: “Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake. Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa. Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi.”​—2 The. 2:6-8.

KIZUIZI CHA KARNE YA KWANZA

5. (a) Ni nani waliokuwa kizuizi cha ukengeufu huo (kuacha imani kwa kuikana kabisa) wakati wa karne ya kwanza? (b) Inaonekanaje kwamba ‘‘yule asi au “mtu wa kuasi” si mwanamume mmoja tu?

5 Wakristo wa kwanza walijua kwamba ‘huyo azuiaye sasa’ hakuwa mtu mmoja, bali jamii ya mitume wa kweli wa Bwana Yesu Kristo, kutia na Paulo. Vivyo hivyo, “yule asi,” “mtu wa kuasi,” asingekuwa mtu mmoja, bali jamii ya watu wengi wenye kuasi. (2 The. 2:3) Maneno ya mtume katika 2 Wathesalonike 2:8 yanaonyesha kwamba “mtu” huyu angekuwa hai mpaka wakati wa kuwapo kwa Kristo. Jamii tu ya watu tofauti tofauti katika karne mbali-mbali ndiyo ingeweza kufanya hivi, kwa maana bila shaka mtu mmoja asingeweza kuishi muda mrefu hivyo.

6, 7. Mtume Yohana alionyeshaje kwamba “siri ya kuasi” ilikuwa ikiendelea wakati alipokuwa hai?

6 Kuna uhakikisho wa kutosha kwamba “siri ya kuasi” ilikuwa ikiendelea kweli katika kundi la Kikristo la karne ya kwanza na kwamba iligandamizwa au ikazuiwa na uongozi wa kiroho wenye nguvu na hatua ya haraka ya mitume. Mfano mmoja unapatikana katika aliyoyaandika mtume Yohana:

7 “Niliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe anayependa kuwa wa kwanza kati yao, hatupokei sisi. Basi, kama nikifika nitakumbuka matendo yake anayotenda, akitoa maneno mabaya yulu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na maneno haya, ila yeye mwenyewe hakaribishi hawa ndugu, na wale wanaotaka kuwakaribisha, anawazuiza, na kuwaondosha katika kanisa.”​—3 Yohana 9, 10, Swahili Congo Bible.

8, 9. Mtume Paulo alionyeshaje kwamba “siri” hiyo ilikuwa ya ujanja na udanganyifu sana, na kwamba ilihusu viongozi wa kidini?

8 Katika barua ya Paulo kwa kundi katika Korintho ambamo alisema juu ya watu wenye kujisifu waliotafuta ukuu na uwezo, udanganyifu ‘wa siri’ wa watu hawa waasi unaonyeshwa kuwa ungehusu viongozi wa kidini:

9 “Hawa ni mitume wa uwongo, wenye kutenda kazi kwa hila, wakiyigeuza kuwa kama mitume ya Kristo. Wala si ajabu; kwa sababu Satani mwenyewe anayigeuza awe malaika ya nuru. Basi si neno kubwa kama watumishi wake vilevile wanayigeuza wawe watumishi wa haki; mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.”​—2 Kor. 11;12-15, Swahili Congo Bible.

10. Toa mfano wa kuendelea kwa “siri” hii siku za mitume, na utaje mfano wa hatua aliyochukua Paulo kuizuia.

10 Paulo alifanyiwa matata na watu fulani walioendeleza mawazo ya ukengeufu (kuacha imani), lakini yeye akaonyesha wazi wao walikuwa akina nani, ikafanya wengine wao wafukuzwe kundini. Wanaume wawili, waliokuwa wakiitwa Himenayo (Himeneo) na Iskanda (Alesanduro), walikuwa wametupilia kando dhamiri njema ‘wakaharibisha imani’ yao. Paulo ‘aliwatoa kwa Satani wafundishwe wasitukane Mungu.’ (lTim. 1:19, 20, Swahili Congo Bible) Baadaye Paulo alimwandikia Timotheo hivi: “Himenayo na Fileto . . . walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama [ufufuo] imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu.”​—2 Tim. 2:17, 18.

11-13. Uasi wa kidini uliokuwako karibu na mwisho wa Karne ya kwanza ulielezwa kuwaje?

11 Uasi wa kidini uliendelea mpaka mwisho wa karne ya kwanza. Mwaka wa 96 C.E. Yesu Kristo aliyetukuzwa aliiambia hivi baraza ya wazee ya kundi la Efeso kupitia kwa mtume Yohana: “Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo.”​—Ufu. 2:1, 2.

12 Tena, Yohana aliandika akitoa ushuhuda wa wazi juu ya utendaji wa “siri ya kuasi” na kukaribia kwa kufunuliwa kwake:

13 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.”​—1 Yohana 2:18, 19.

14. Kwa sababu gani “siri ya kuasi” haikujitokeza ikiwa “mtu wa kuasi” wakati mitume walipokuwa hai?

14 Kutokana na maandiko haya ya mitume yenye kufunua hali mbaya zilizokuwa zinatokeza wazi hapa na pale kundini, tunaweza kuona kwamba mitume walifunga njia “wakati wa mwisho” wa uangalizi wa mitume duniani, wakazuia “siri ya kuasi” isitengenezwe iwe jamii ya watu, “mtu wa kuasi.”

UASI UNATOKEZA KABISA

15. Wakati ambapo uasi ungefunuliwa, ungekuwa utendaji wa namna gani?

15 Alipokuwa akizungumza juu ya kufunuliwa kwa “mtu wa kuasi” huyu mwenye watu wengi ndani yake, Paulo alisema hivi: “Yule ambaye [kuwapo] kwake ni kwa mfano wa [“kila mwujiza,” NW] kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo; na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea.”​—2 The. 2:9, 10.

16, 17. Cyclopædia ya M’Clintock na Strong inaonyeshaje kwamba Shetani aliweza kutokeza kundi la Kikristo la uongo kwa kutumia “mtu wa kuasi”?

16 “Mtu wa kuasi” alifunuliwa kabisa baada ya kufa kwa mitume. Viongozi wengine katika makundi walianza kupiga ubwana juu ya ndugu zao wakafanyia wanasiasa wa kilimwengu mambo ya kuwafurahisha. Uasi huo ulijionyesha wazi kwa njia ya aibu sana siku za Mfalme Konstantino, ambaye alifanya Ukristo dini ya Serikali. Juu ya jambo hili, Cyclopædia ya M’Clintock na Strong inaeleza hivi:

17 “Unyofu wa Injili ulipotolewa; ibada na sherehe za kujionyesha zikaingizwa; waalimu wa Ukristo walipewa madaraja ya kilimwengu na mishahara, nao ufalme wa Kristo ukageuzwa sana kuwa ufalme wa ulimwengu huu.” Vol. 2, uk. 488.

18. Matengenezo ya kanisa yalitenganisha Wakristo na “mtu wa kuasi”?

18 Kwa karne nyingi kanisa lenye kuasi lilikuwa na uwezo kwa serikali, likaleta kipindi kisicho na mwangaza wa mambo ya kiroho na mateso mengi. Baadaye, Matengenezo ya kanisa yalifuata, lakini hayakurudisha ibada ya kweli. Kulikuwa ni kujitenga tu na mamlaka ya Kanisa Katoliki na mapapa wake. Mafundisho makuu ya uongo yalichukuliwa yakaingizwa katika makanisa ya Kiprotestanti, nao mapadre wa makanisa hayo hata leo wanaonyesha wazi nia ile ile iliyoonyeshwa na wale walioanza uasi, wakijionyesha kuwa ndio peke yao wamewekwa wafanye huduma ya Neno la Mungu, wakiwa na uwezo mbalimbali wa pekee, mapendeleo, haki, uhuru mbalimbali, madaraja na vyeo visivyoshirikiwa na “watu wa kawaida” wasio na maana sana.

19. “Mtu wa kuasi” anatimizaje maneno ya mtume Paulo katika 2 Wathesalonike 2:9, 10?

19 Kulingana na mtume, “kuwapo kwake mtu wa kuasi ni kwa mfano wa [“kila mwujiza,” NW] kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo; na katika madanganyo yote ya udhalimu.” Tunaona haya kati ya mapadre wa Jumuiya ya Wakristo leo. (2 The. 2:9, 10) Wanadai waheshimiwe sana na kustahiwa. Mara nyingi wanavaa mavazi ya fahari yenye kung’aa, wanaitwa kwa vyeo vya kuwasifu sana, wanafurahi wakiwa katika majengo ya makanisa yenye fahari na kuendesha ibada zenye kuvutia, kama vile kule wanakodai ni kugeuka kwa mkate na divai kuwa mwili halisi na damu halisi ya Yesu katika “Misa.” Wanajivunia elimu ya kilimwengu, cheo chao na maongozi kwa Serikali ya kisiasa na jeshi.

20, 21. (a) Ni mambo gani mengine yaliyomo kati ya ‘miujiza’ ya “mtu wa kuasi”? (b) Mhudumu wa Kimethodist Gabriel Setiloane alisema nini kwa wengine waliomo kati ya ‘miujiza’ hii?

20 Kwa habari ya ‘kufanya kwao miujiza,’ ‘wameongoa’ (wamegeuza) idadi kubwa sana za watu kwa kutumia nguvu. Wamejenga mahospitali na shule za kanisa, na wamepeleka wamisionari-madaktari kwenye nchi ‘za kipagani.’ Ndiyo, ‘wamejigeuza kuwa watumishi wa haki.’ (2 Kor. 11:15) Wakati ule ule wanaruhusu ‘waongofu’ wao waendeleze mazoea yao mengi ya kipagani, wakiyaunganisha na unaoitwa “Ukristo.” Kwa kweli, Kanisa limesaidia serikali za Jumuiya ya Wakristo zitawale nchi hizo, utawala huo ukiwa wenye nguvu zaidi kwa sababu ya uwezo ambao viongozi wa kidini wametumia juu ya watu. Sasa fikiria maneno yaliyosemwa na mhudumu wa Kimethodist Fabriel Setiloane katika mkutano uliojulikana kama All-Africa Church Conference uliofanyiwa Uganda mwaka wa 1963:

21 “Maendeleo ya Kanisa katika Afrika yamesonga pamoja na Mjasiri, Mvumbua nchi, Mkoloni na hata Mweneza utawala. Mkono uliosimamisha Msalaba . . . katika bara hii haukuwa wa padre wala wa mtume. Ulikuwa mkono wenye madoa ya damu wa askari. . . . Hata kufikia karne hii Kanisa katika bara hii halikuweza kujitoa katika utawala wa Kaisari, ijapokuwa limeonywa lifanye hivyo.”

22. “Mtu wa kuasi” amepanuka kuwa mkubwa zaidi, na je! ameufaidi ulimwengu?

22 Jamii ya mapadre ya “mtu wa kuasi” imekua kadiri gani? Mwaka wa 1971 C.E. tarakimu zilizoandikwa za Kanisa Katoliki la Kirumi zilionyesha kulikuwa na mapadre 419,611 kwa wanakanisa Wakatoliki 566,771,600 ulimwenguni pote. Yote haya yakiwapo, je! ulimwengu ni bora, kwa adili na kwa kiroho? Je! kuna upendo, amani, umoja na furaha zaidi katika ulimwengu leo na katika Jumuiya ya Wakristo yenyewe?

23. Watu mmoja mmoja waliomo katika makanisa ya Kristendomu wamepaswa wafanye nini wanapomjua “mtu wa kuasi”?

23 Wale wanaoichunguza Biblia kwa unyofu wa moyo wanaona kwa vyepesi kwamba jamii ya “mtu wa kuasi” imesitawi kweli kweli kulingana na maneno ya unabii ya mtume Paulo. “Mtu” huyu mwenye watu wengi ndani yake anajulikana wazi-wazi kama mapadre wa Jumuiya ya Wakristo. Wanaoshirikiana na jamii hiyo kama watu wa kawaida tu au pengine kama mapadre wenye mioyo minyofu, wanaonywa na Biblia wajitenge na jamii hii ya Ibilisi yenye udanganyifu yenye kusudi la kupindua kundi la Mungu la kweli na kuificha kweli. (2 Tim. 3:1-5; Ufu. 18:4) Mpango wa Shetani hautakuwa na matokeo mazuri, kama vile maneno ya mtume yanavyoonyesha katika 2 Wathesalonike 2:8, nayo maneno hayo yataangaliwa katika toleo lifuatalo la Mnara wa Mlinzi.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki