Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 8/15 uku. 30
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Sehemu 4: “Sisi Watu”
    Amkeni!—1991
  • Je! Umeipata Dini ya Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Je! Maskani Yako Ni Mahali pa Pumziko na Amani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Waweza Kupata Wapi Mwongozo Wenye Kutumainika?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 8/15 uku. 30

Je! Wakumbuka?

Je! umefikiria kwa uangalifu matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, utaiona kuwa jambo lenye kupendeza kukumbuka yafuatayo:

▫ Ni nini tofauti kuu kati ya watu na wanyama?

Tofauti kuu yakazia muundo, uwezo, na kazi za ubongo. Katika wanyama karibu kazi zote za ubongo zimeamriwa katika ile ambayo imekuja kuitwa hekima ya kisilika. Sivyo kwa habari ya wanadamu. Mungu aliwapa wanadamu uwezo wa hiari. (Mithali 30:24-28)—4/15, ukurasa 5.

▫ Kuimba kulikuwa na sehemu gani katika ibada ya hekalu ya Waisraeli?

Muziki, hasa waimbaji, walikuwa na mahali pa maana katika ibada, si kwa lazima ili kukazia kikiki mambo mazito zaidi ya Sheria, bali ili kuandaa roho ifaayo kwa ajili ya ibada. Uliwasaidia Waisraeli wamwabudu Yehova kwa idili. (1 Mambo ya Nyakati 23:4, 5; 25:7)—5/1, kurasa 10, 11.

▫ Watoto wanahitaji uangalifu wa aina gani tangu utoto?

Ni lazima wazazi watoe karibu uangalifu wa daima kwa mtoto aliyezaliwa karibuni. Paulo aliandika hivi: “Tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu.” (2 Timotheo 3:15) Kwa hiyo uangalifu wa wazazi ambao Timotheo alipokea, hata kutoka utoto, ulikuwa wa aina ya kiroho pia.—5/15, ukurasa 11.

▫ Ni nini mambo manne yanayothibitisha kwamba Biblia ina ujumbe wa Mungu kwa wanadamu wote?

(1) Kupatikana. Biblia inapatikana kwa asilimia 98 hivi ya idadi ya watu ulimwenguni. (2) Uhistoria. Biblia ina mambo ya hakika ya kihistoria, badala ya hekaya zisizothibitishika. (3) Utumikaji. Amri na kanuni zayo huonyesha njia ya maisha iletayo manufaa kwa wale washikamanao nazo. (4) Unabii. Ni kitabu kisimuliacho kinagaubaga kuhusu yale yatakayotukia wakati ujao.—6/1, kurasa 8, 9.

▫ Ni daraka jipi liandamanalo na kuijua dini ya kweli?

Mara tumetambulisha dini ya kweli, ni lazima tutegemeze maisha zetu juu yayo. Hiyo ni njia ya maisha. (Zaburi 119:105; Isaya 2:3)—6/1, ukurasa 13.

▫ Kwa nini funzo la kibinafsi la Biblia ni muhimu sana?

Watumishi wote wa Mungu huhitaji shangwe na nguvu zao zifanywe upya kila siku kwa kupata mambo mapya au yenye kina zaidi ya ile kweli ya Neno la Mungu. Kwa njia hii wao hujiweka wakiwa wamechochewa kiroho.—6/15, ukurasa 8.

▫ Ni nini kimaanishwacho na neno “dhambi” kama litumiwavyo katika Biblia?

Katika hali zayo za kitenzi, maneno ya Kiebrania na Kigiriki yatumiwayo kwa kawaida katika Biblia kuonyesha “dhambi” humaanisha “kukosa,” kwa maana ya kukosa au kutofikia mradi, alama, au shabaha. Wanadamu wawili wa kwanza walipungukiwa na utukufu wa Mungu, wakakosa kusudi la kuumbwa kwao kwa mfano wa Mungu. Yaani, walitenda dhambi. (Mwanzo 2:17; 3:6)—6/15, ukurasa 12.

▫ Kwa nini si jambo la hekima hata kidogo kusoma fasihi za uasi-imani?

Baadhi ya fasihi za uasi-imani hutoa ubandia mbalimbali kupitia “maneno laini” na “maneno yaliyotungwa.” (Warumi 16:17, 18; 2 Petro 2:3) Maandishi yote ya uasi-imani huchambua na kuvunja tu. Hakuna lolote linalojenga.—7/1, ukurasa 12.

▫ Je! Ugiriki ilikuwa chanzo cha demokrasi?

Katika Ugiriki ya kale, demokrasi ilifuatwa katika majiji machache tu yaliyojitawala, na hata katika majiji haya ni wanaume pekee waliopiga kura. Hilo lilimaanisha kwamba sehemu nne kati ya tano ya idadi ya watu haikutiwa ndani. Bila shaka huo haukuwa utawala uliopendwa na wengi au demokrasi!—7/1, ukurasa 16.

▫ Ni nini kifanyacho ndoa ya Kikristo isitawi?

Wakati mume na mke wanapostahi maoni ya Mungu juu ya ndoa na kujitahidi kuishi kulingana na kanuni za Neno lake. (Waefeso 5:21-33)—7/15, ukurasa 10.

▫ Funzo lenu la familia linaweza kuwaje lenye kufurahisha?

Jaribu kuwahusisha watoto wote. Uwe mwenye mtazamo chanya na mwenye kujenga, ukiwapongeza watoto wako kwa uchangamfu kwa ajili ya kushiriki kwao. Usipitie habari tu bali ujaribu kuifikia mioyo ya watoto wako.—7/15, ukurasa 18.

▫ Ni nini kimaanishwacho na maneno: “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama.” (1 Wathesalonike 5:3)

Ona kwamba Biblia haisemi kwamba mataifa yatapata “amani na salama.” Lakini angalau watakuwa wakisema kuzihusu kwa njia ya kipekee sana, inayoonyesha matazamio mazuri na usadikisho ambao haujapata kuonekana hapo awali. Uwezekano wa kupata amani na salama utaonekana kuwa karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote.—8/1, ukurasa 6.

▫ Taja njia tatu ambazo katika hizo Yehova huonyesha kwamba yeye ni mwenye kukubali sababu.

Yehova ameonyesha kuwa kwake tayari kusamehe. (Zaburi 86:5) Amekuwa tayari kubadili tendo lililokusudiwa wakati hali mpya zimetokea. (Ona Yona, sura ya 3.) Pia, Yehova amejionyesha kuwa mwenye kukubali sababu katika utumiaji wa mamlaka. (1 Wafalme 22:19-22)—8/1, kurasa 12-14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki