Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 9/1 kur. 29-31
  • Thamini Utumishi Wako Mtakatifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thamini Utumishi Wako Mtakatifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tujifunzapo Kwanza Kuhusu Mungu
  • Je, Kweli Hizo Ni Dhabihu?
  • Fikiria Thawabu
  • Hatua ya Kujiweka Wakfu
  • Thawabu Nyinginezo za Utumishi Mwaminifu
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Kwa Nini Kuishi Maisha ya Kimungu Huleta Furaha
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • ‘Jiokoe Wewe Mwenyewe na Wale Wakusikilizao’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 9/1 kur. 29-31

Thamini Utumishi Wako Mtakatifu

ILI kutimiza mradi wowote mzuri, ni lazima tuwe tayari kulipa gharama. Kuwa daktari huchukua miaka mingi ya funzo na bidii, na vilevile fedha. Mwanariadha wa mazoezi wa viungo vya mwili mwenye mafanikio ametumia muda mwingi wa ujana wake akifanya kwa utaratibu mazoezi magumu zaidi akitafuta kabisa ukamilifu. Mcheza piano mwenye ustadi vilevile aweza kutazama nyuma kwa miaka mingi ya mazoezi ya kujitoa sana.

Hata hivyo, kuna mradi mmoja uletao faida kuliko gharama yoyote tuwezayo kulipa. Huo ni nini? Ni pendeleo la kuwa mtumishi wa Aliye Juu Zaidi Sana, Yehova Mungu. Dhabihu zozote tufanyazo kwa njia ya wakati, fedha, au nishati, pendeleo la kumtolea Muumba wetu utumishi mtakatifu huleta thawabu zisizo na kifani. Maneno ya mtume Paulo ni kweli: “Utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” (1 Timotheo 4:8) Ebu tuone jinsi jambo hilo lilivyo kweli.

Tujifunzapo Kwanza Kuhusu Mungu

Wengi wa watu ambao huitikia vizuri habari njema na kuanza funzo la Biblia yaelekea hawatambui kadiri ya mabadiliko yatakayotokea maishani mwao. Kwanza, mwanafunzi mpya wa Biblia aweza kupoteza marafiki fulani wasioelewa sababu inayomfanya asishirikiane nao tena katika mambo ambayo sasa yeye aona kuwa hayamheshimu Mungu. (1 Petro 4:4) Wengine waweza kupatwa na upinzani katika familia nao waweza kuhuzunika kuona wale wawapendao wakionyesha kutompenda, au hata kumchukia Yehova. (Mathayo 10:36) Hilo laweza kuwa gharama kubwa kulipa.

Kazini au shuleni, pia kutakuwa na gharama ya kulipa. Baada ya muda fulani mwanafunzi mpya wa Biblia ataacha kushiriki katika karamu na sherehe nyinginezo za kilimwengu. Hatasikiliza tena misemo michafu ya wafanyakazi wenzi au wanafunzi wenzi, wala hatashiriki nao maneno machafu ya ucheshi. Badala ya hivyo, atajaribu kutumia himizo linalopatikana kwenye Waefeso 5:3, 4: “Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wala kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu; wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali afadhali kushukuru.”

Mabadiliko kama hayo yanaweza kufanya mwanafunzi wa Biblia awe tofauti. Hilo laweza kuwa jambo gumu, hasa kwa kijana ambaye angali shuleni bado. Akiwajibika kukabili sikukuu moja baada ya nyingine, na vilevile mafundisho yapingayo mafundisho ya Mungu, kama vile mageuzi, na mkazo wa daima wa kufuatana na umati, ni lazima vijana Wakristo wapige vita nyakati zote kwa ajili ya imani. Kufuata njia za Mungu kutawafanya wawe tofauti na kwaweza kutokeza dhihaka kutoka kwa wanadarasa wenzi na walimu. Hilo ni jambo gumu kukubali hasa katika miaka ya utineja yenye hisia nyingi, lakini kupata kibali cha Mungu lastahili hayo.

Je, Kweli Hizo Ni Dhabihu?

Mambo mengine ambayo kwanza huonekana kuwa dhabihu hugeuka kuwa baraka. Wengine hulazimika kuacha tabia ya kutumia tumbaku. (2 Wakorintho 7:1) Hilo laweza kuwa jitihada, lakini waweza kupata baraka kama nini ushindapo hatimaye kitendo hicho chenye kukirihi! Jambo lilo hilo laweza kusemwa kuhusu kushinda uraibu wa dawa nyinginezo za kulevya au wa kileo. Maisha ni mazuri kama nini bila tabia hizo zenye kudhuru! Ni lazima wengine warekebishe hali yao ya ndoa. Watu wanaoishi pamoja bila kufunga ndoa ni lazima wafunge ndoa au kuacha kuishi pamoja. (Waebrania 13:4) Wale wanaoishi na wake wengi ni lazima wabaki na mke wa ujana wao pekee. (Mithali 5:18) Mabadiliko kama hayo hutokeza huhusisha dhabihu, lakini hayo huleta amani nyumbani.

Fikiria Thawabu

Kwa kweli, mtu yeyote atiiye sheria za Yehova hunufaika kikweli. Kwa mara ya kwanza kabisa maishani mwake, mwanafunzi wa Biblia huanza kumwendea Muumba wake kwa jina Lake, Yehova. (Zaburi 83:18) Mwanafunzi huyo huja kumpenda Yehova ajifunzapo juu ya mambo ya ajabu ambayo Yeye amefanya na ambayo angali atafanyia wanadamu. Katika nchi ambazo hofu ya wafu imeenea, yeye huacha hofu hiyo ya kishirikina, akijua kwamba wafu wamelala, wakingojea ufufuo. (Mhubiri 9:5, 10) Na inafariji kama nini kujua kwamba Yehova hatesi watu milele katika helo! Naam, kwa hakika ile kweli humweka huru.—Yohana 8:32.

Mwanafunzi apatanishapo maisha yake zaidi na zaidi na viwango vya Yehova, yeye hupata dhamiri safi na kujistahi. Kujifunza kuishi kama Mkristo wa kweli humsaidia kushughulikia familia yake kwa njia bora zaidi, jambo ambalo hutokeza uradhi mkubwa na shangwe. Kisha kuna kuhudhuria mikutano katika Jumba la Ufalme. Hilo ni ono lenye kufurahisha kama nini! Hapo pana watu wanaoonyesha upendo mchangamfu ambao Biblia yasema kuwa utambulisho wa watu wa Mungu. (Zaburi 133:1; Yohana 13:35) Usemi wao ni safi na wenye kujenga wakiyasema “matendo makuu ya Mungu.” (Matendo 2:11) Naam, kukutana na “ushirika wote wa akina ndugu” hutokeza furaha. (1 Petro 2:17, NW) Ushirika mzuri kama huo humsaidia mwanafunzi wa Biblia ‘akavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.’—Waefeso 4:24.

Hatua ya Kujiweka Wakfu

Mtu huyo aendeleapo kupata ujuzi, hatimaye yeye husukumwa na upendo wake kwa Yehova aweke maisha yake wakfu kwake na aonyeshe wakfu huo kwa ubatizo wa maji. (Mathayo 28:19, 20) Shauri la Yesu ni kwamba kabla ya kuchukua hatua hiyo, wanafunzi wake wahesabu gharama. (Luka 14:28) Kumbuka kwamba Mkristo aliyejiweka wakfu hutanguliza mapenzi ya Yehova na kuacha kabisa mambo ya mwili. Yeye hufanya bidii aache “matendo ya mwili” na kusitawisha ‘tunda la roho.’ (Wagalatia 5:19-24) Shauri linalopatikana kwenye Warumi 12:2 sasa hutimiza fungu kubwa zaidi maishani mwake: “Msifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” Kwa hiyo, Mkristo aliyejiweka wakfu huishi maisha yake akiwa na kusudi jipya.

Lakini, ebu fikiria yale ambayo yeye hupokea. Kwanza, sasa ana uhusiano wa kibinafsi pamoja na Muumba wa ulimwengu wote mzima. Yeye hutangazwa kuwa mwadilifu ili awe rafiki ya Mungu! (Yakobo 2:23) Kwa umaana mzito zaidi, yeye humtaja Mungu “Baba yetu uliye mbinguni.” (Mathayo 6:9) Baraka nyingine kwa wale waliojiweka wakfu karibuni ni kujua kwamba kwa kweli uhai una kusudi, na kwamba anaishi kwa kupatana na kusudi hilo. (Mhubiri 12:13) Kwa kufuata uongozi wa Yesu, yeye aweza kumthibitisha Ibilisi kuwa mwongo kwa kubaki mwaminifu. Jambo hilo huleta shangwe kama nini moyoni mwa Yehova!—Mithali 27:11.

Bila shaka, Mkristo avumiliapo katika njia ya uaminifu, kuna dhabihu nyinginezo za kufanywa. Kuwa na funzo la Neno la Mungu la kibinafsi na la mikutano. (Zaburi 1:1-3; Waebrania 10:25) Wakati wa huduma ya shambani ni lazima ununuliwe kutoka kwa utendaji mwingine. (Waefeso 5:16) Wakati na jitihada pia zinahitajika kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na kusafiri kwenda makusanyiko na mikusanyiko yao. Yaweza kuwa kujidhabihu katika kushiriki kusaidia kifedha Jumba la Ufalme na kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Hata hivyo, kama mamilioni ya Wakristo wawezavyo kutoa ushuhuda, kushiriki katika mambo hayo kwa moyo wote huleta furaha. Yesu alisema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko kulivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35, NW.

Thawabu za kutegemeza kazi ya Yehova huzishinda gharama tunazotumia kwa mbali. Tunapoendelea kukomaa, huduma yetu huja kutokeza matunda na kuwa yenye shangwe zaidi. Kwa kweli, hakuna chochote kiwezacho kutuletea uradhi zaidi kama kumfunza mtu mwingine kweli ya Biblia na kumwona akichukua ibada ya Yehova. Na kama mwabudu huyo ni mshiriki wa familia, labda akiwa mtoto aliyezoezwa “katika adabu na maonyo ya Bwana,” hilo huleta shangwe ya pekee. (Waefeso 6:4) Sisi huona baraka nyingi za Mungu katika jitihada zetu za kuwa ‘wafanya kazi pamoja naye.’—1 Wakorintho 3:9.

Thawabu Nyinginezo za Utumishi Mwaminifu

Ni kweli kwamba tutakuwa na matatizo maadamu mfumo huu wa mambo waendelea kuwapo. Yaelekea kwamba matatizo yatakuwa mabaya zaidi kadiri muda wa Ibilisi uzidivyo kuwa mfupi. Huenda tutalazimika kupatwa na mnyanyaso au kuvumilia kishawishi. Lakini kujua kwetu kwamba Mungu yu pamoja nasi hutufariji na kutupa nguvu za kuvumilia. (1 Wakorintho 10:13; 2 Timotheo 3:12) Baadhi ya Wakristo wenzetu wamevumilia miaka mingi ya kutendwa kikatili, lakini wao huvumilia kwa sababu ya upendo wao kwa Mungu. Wale ambao huvumilia kwa mafanikio majaribu ya aina mbalimbali huhisi kama mitume walivyohisi walipochapwa na kuachiliwa. Matendo 5:41 yasimulia: “Nao wakatoka katika ile baraza, wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuaibishwa kwa ajili ya Jina hilo.”

Thawabu ya kuvumilia hushinda kwa mbali gharama tunazopata hata sasa. Lakini kumbuka kwamba ujitoaji kimungu ‘unayo ahadi’ si ya “uzima wa sasa” tu bali pia ya “ule utakaokuwapo baadaye.” (1 Timotheo 4:8) Ni mazuri kama nini matarajio ya yule avumiliaye! Ukiwa mwaminifu, utaokoka dhiki imalizayo mfumo huu wa mambo. Au ukifa kabla ya tukio hilo kubwa sana, utafufuliwa katika ulimwengu mpya utakaofuata. (Danieli 12:1; Yohana 11:23-25) Ebu wazia ile hisia ya kushangilia utakayokuwa nayo wakati huo ambapo utaweza kusema: “Kwa msaada wa Yehova, nimefaulu!” Inasisimua kama nini kurithi fungu katika dunia hiyo, ambayo “itajawa na kumjua BWANA, kama vile maji yanavyoifunika bahari.”—Isaya 11:9.

Naam, kuna gharama katika kumtumikia Mungu. Lakini kwa kulinganishwa na thawabu, gharama hiyo ni ndogo sana. (Wafilipi 3:7, 8) Kwa kufikiria yale yote ambayo Mungu anafanyia watumishi wake sasa na yale atakayofanya katika wakati ujao, twarudia maneno ya mtunga-zaburi: “Nimrudishie BWANA nini kwa ukarimu wake wote alionitendea?”—Zaburi 116:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki