Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 10/1 kur. 4-8
  • Biblia—Kitabu Kilichokusudiwa Kueleweka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia—Kitabu Kilichokusudiwa Kueleweka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Biblia Iliandikwa?
  • Je, Biblia Ni Ngumu Sana Kueleweka?
  • Biblia na Wafuasi wa Yesu
  • Ni Msaada Gani Upatikanao?
  • Kwa Nini Biblia Ni Muhimu?
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je! Tunahitaji Msaada Kuielewa Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kuchunguza Ndani ya “Mambo Mazito ya Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Soma Neno la Mungu na Umtumikie Katika Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 10/1 kur. 4-8

Biblia—Kitabu Kilichokusudiwa Kueleweka

WATU fulani huamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililo dhahiri linalopaswa kufuatwa kihalisi. Kwa wengine, “ujumbe wa Biblia ni wenye utata sana.” Ndivyo wasemavyo washiriki 12 wa halmashauri ya imani na theolojia ya dini kubwa zaidi ya Kiprotestanti katika Kanada. Kasisi Clifford Elliott, wa United Church, ahisi kwamba kwa wengine “Biblia inakuwa ngumu, isiyo dhahiri na isiyofaa.”

Maoni kama hayo huzusha maswali yenye mafaa yanayostahili majibu. Yaliyo ya maana kati ya hayo ni, Kwa nini Biblia iliandikwa? Je, ni ya kifumbo na ngumu kufahamika? Je, mtu wa kawaida aweza kuielewa? Ni msaada gani wahitajiwa ili mtu afahamu maana ya Maandiko? Na kwa nini ujuzi sahihi wa Biblia ni muhimu katika nyakati hizi zisizotulia?

Kwa Nini Biblia Iliandikwa?

Kujifunza Neno la Mungu nyakati zote kumekuwa sharti kwa wale watakaopata kibali na upendeleo wa Mungu Aliye Juu Sana, Yehova. Wafalme, makuhani, wazazi, wanaume, wanawake, na watoto—matajiri na maskini vilevile—waliagizwa kutwaa nafasi kutoka kwenye mambo ya kila siku ya maisha na kulitolea Neno la Mungu lililorekodiwa uangalifu mzito wenye sala.—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7; 17:18-20; 31:9-12; Nehemia 8:8; Zaburi 1:1, 2; 119:7-11, 72, 98-100, 104, 142; Mithali 3:13-18.

Kwa mfano, Yoshua aliagizwa: “Hakikisha kuwa kitabu cha Sheria kinasomwa wakati wote katika ibada yenu. Kisome kila mchana na usiku, na hakikisha kutii yote yaliyoandikwa humo. Nawe utasitawi na kufanikiwa.” (Yoshua 1:8, Today’s English Version) Funzo lenye uangalifu la jinsi hiyo na kutenda kulingana na Sheria ya Mungu kungeleta fanaka na furaha. Yehova alikusudia kwamba “watu wote” waelewe Neno lake, Biblia, na pia kuitii, wakiwa na taraja la kupokea zawadi ya uhai.—1 Timotheo 2:3, 4; Yohana 17:3.

Je, Biblia Ni Ngumu Sana Kueleweka?

Kabla ya kupaa mbinguni, Yesu alieleza wazi kuwa alitaka programu kubwa ya elimu ya Biblia iendelee duniani kote. (Matendo 1:8) Alijua kuwa Biblia ilikusudiwa ieleweke. Baada ya kueleza kwamba Yehova amempa mamlaka yote mbinguni na duniani, alitoa amri ya moja kwa moja: “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu [“roho takatifu,” NW], na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi.”—Mathayo 28:19, 20.

Kabla ya ubatizo, ilibidi wanafunzi wapya wafundishwe juu ya Yehova, Mwanaye na utendaji wa roho takatifu. Pia, ilibidi waagizwe katika sheria ya mfumo wa mambo wa Kikristo. (1 Wakorintho 9:21; Wagalatia 6:2) Ili wapate tokeo hili, wenye kustahili walipaswa kwanza kuamini kwamba Biblia ilitoka kwa Yehova na pili ilikusudiwa ieleweke.—Mathayo 10:11-13.

Wewe wapaswa ufanyeje ili uelewe Biblia? Mwana wa Mungu alifanya jitihada ya pekee kueleza Maandiko. Alijua kuwa Maandiko Matakatifu ni ya kweli na kuwa yaeleza mapenzi ya Yehova yaliyotajwa. (Yohana 17:17) Yesu Kristo alisema hivi kuhusu mgawo wake wa kazi: “Mimi nilizaliwa nikaja ndani ya ulimwengu kwa kusudi hili moja, kusema juu ya kweli. Yeyote aliye wa hiyo kweli hunisikiliza.” (Yohana 18:37, TEV; Luka 4:43) Yesu hakuacha kufundisha wenye mioyo na akili sikivu. Kwenye Luka 24:45, twaambiwa: “Ndipo [Kristo Yesu] akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.”

Wakati wa huduma ya Yesu yeye alinukuu katika Neno lililoandikwa kwa uhuru, akieleza na kurejezea maandiko katika “Torati ya Musa, na katika Manabii, na Zaburi.” (Luka 24:27, 44) Wale waliomsikia akieleza Maandiko walisukumwa sana kwa uelewevu wake, pamoja na uwezo wake wa kufundisha. (Mathayo 7:28, 29; Marko 1:22; Luka 4:32; 24:32) Kwa Yesu, Maandiko yalieleweka wazi.

Biblia na Wafuasi wa Yesu

Mtume Paulo, mwigaji wa Yesu Kristo, aliona uhitaji wa kufundisha wengine yaliyomo katika Maandiko. Yeye pia alijua kuwa yalikusudiwa yaeleweke. Ndiyo sababu alifundisha waziwazi na bila shaka kueleza Maandiko katika nyumba za wale waliotaka kuyaelewa. Paulo alijulisha msimamo wake aliposema: “Mwajua ya kuwa sikuwanyima chochote ambacho kingeweza kuwasaidia nilipowahubiri na kufundisha peupe na katika nyumba zenu.” (Matendo 20:20, TEV) Wakati wa mazungumzo yake alitoa sababu kwa kutumia Maandiko, akieleza na kuthibitisha hoja zake kwa marejezo. (Matendo 17:2, 3) Alipendezwa na kusaidia wengine kuelewa maana ya Maandiko.

Je, watamani kuelewa yale Yesu na wanafunzi wake walifundisha? (1 Petro 2:2) Wakaaji wa Beroya ya kale walikuwa na tamaa kama hiyo, na walitamani kuamini yale mtume Paulo alifundisha kuhusu Kristo. Hivyo walitiwa moyo kujifunza Maandiko kila siku na basi kuhakikisha kwamba habari njema walizosikia zilikuwa kwa hakika ile kweli. Kwa kuwa akili zao zilikuwa sikivu, “wengi miongoni mwao wakaamini.”—Matendo 17:11, 12.

Ili kuelewa Biblia, mtu apaswa kuwa na hali njema ya moyo, tamaa ya moyo mweupe ya kutaka kujifunza, na ‘kutambua uhitaji wa kiroho.’ (Mathayo 5:3, NW) Yesu alipoulizwa: “Kwa nini wasema nao kwa mifano?” alijibu: “Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa.” Ilitabiriwa kwamba, ‘nitafumbua kinywa changu kwa mifano, nitayatamka yaliyositirika tangu awali.’ (Mathayo 13:10, 11, 35) Kwa hiyo Yesu alisema kwa njia ya vielezi ili kutenganisha msikilizaji asiyejali na mwenye udadisi kutoka kwa yule mwenye kuuliza maswali kwa moyo mweupe. Wanafunzi wa Yesu walionyesha weupe wa moyo pindi moja walipoenda pamoja naye ndani ya nyumba na kusema: “Tufafanulie mfano wa magugu ya kondeni.”—Mathayo 13:36.

Ni wazi kwamba twahitaji msaada ikiwa tutaelewa Biblia. Kasisi Hal Llewellyn, ambaye ni katibu wa theolojia, imani, na ushirika wa United Church, alisema: “Ni jambo la maana sana kueleza wazi ni nini maana ya Biblia kwetu na jinsi isomwavyo na kufafanuliwa.” Lakini hata kama si wote wang’amuao jambo hilo, uhakika ni kwamba hatuwezi kuelewa Biblia kivyetu. Twahitaji msaada.

Ni Msaada Gani Upatikanao?

Ndani ya Biblia mna semi zenye fumbo, maswali yenye kutatanisha, na misemo yenye kina inayohitaji kufafanuliwa. Zaweza kuwa hazieleweki kimakusudi, zikiweka maana zenye ulinganifu ambazo hazikuhitaji kueleweka wakati wa kuandikwa. Lakini zilihusu makusudi ya Yehova. Kwa mfano, Ufunuo 13:18 husema kwamba “hesabu ya mnyama huyo” ni “mia sita, na sitini na sita.” Ingawa mstari unaposema kwamba “hapa ndipo penye hekima,” hauelezi maana ya nambari hiyo. Hata hivyo, Yehova, kupitia tengenezo lake, ameruhusu watumishi wake waaminifu-washikamanifu kuelewa maana yake leo. (Ona sanduku, “Njia ya Kuelewa Biblia.”) Wewe pia waweza kupata uelewevu huu kwa msaada wa wale wenye ujuzi wa “kutumia kwa halali neno la kweli.”—2 Timotheo 2:2, 15, 23-25; 4:2-5; Mithali 2:1-5.

Nyakati nyingine Yesu alitumia vielezi kuonyesha itikio au ukosefu wa itikio kwa ujumbe wa Ufalme. Alionyesha kwamba wengine wangekosa kufanya maendeleo kwa sababu ya kuvunjwa moyo kupitia upinzani wa marafiki na watu wa ukoo. Wengine wangeruhusu “dhiki au udhia” kuharibu uthamini wao wa ujumbe wa Ufalme. Wengine pia wangeruhusu mambo ya kila siku ya maisha, “na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali,” kufunika upendo wowote wawezao kuwa nao kuelekea habari njema. Kwa upande mwingine, kuna wale waitikiao kwa furaha na wanatamani kusikia neno lenye thamani na kupata ufahamu walo. Wao ‘wanaugua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika’ katika Jumuiya ya Wakristo, wakidhani ni kwa jina la Yesu Kristo. Watu kama hao watamani kuagizwa katika njia ya Yehova na hivyo kuelewa yale wasomayo ndani ya Biblia.—Mathayo 13:3-9, 18-23; Ezekieli 9:4; Isaya 2:2-4.

Kwa watu wanaotaka kuwa na ufahamu wa ndani juu ya makusudi ya Yehova, Yehova aweza kuhakikisha kwamba msaada unaotakiwa umetolewa. Kwa kielezi, Biblia huripoti kuwa roho ya Yehova ilimwongoza mwevanjeli Filipo kusaidia Mwethiopia aliyekuwa akisoma kitabu cha Biblia cha Isaya akisafiri kutoka Yerusalemu. Akilisoma ndani ya kigari chake, alipokuwa akirudi nyumbani. Kwa kutii mwongozo wa roho takatifu ya Yehova, Filipo alikimbia kando ya kigari na kuuliza: ‘Je, yanakuelea haya unayosoma?’ Mtu huyu alikuwa mnyenyekevu na mnyoofu vya kutosha kukubali kwamba alihitaji msaada. Kwa furaha Filipo alimwagiza mtu huyu mwenye njaa ya kiroho na mwenye kufundishika. Maagizo hayo yalimsaidia kuelewa Maandiko. Alijifunza yale aliyopaswa kufanya sasa ili kufurahia msimamo wenye kibali pamoja na Yehova ili kupata uhai wa milele. Akawa mtumishi wa Yehova mwenye furaha aliyebatizwa, aliyefuata mwendo wa maisha uliompendeza Mungu.—Matendo 8:26-39.

Waweza kuwa una Biblia nyumbani, na waweza kuwa umeisoma mara nyingi. Yawezekana sana umeona tatizo kama lile ambalo Mwethiopia mnyenyekevu, mwenye moyo mweupe aliona. Yeye hakuweza kuelewa alichokuwa akisoma. Alihitaji msaada ambao Yehova Mungu alifurahi kumpa, na bila kukawia aliukubali. Kama vile Filipo, Mashahidi wa Yehova wanafurahi kukusaidia uelewe mambo yahusuyo Mungu yaliyoandikwa ndani ya Neno lake, Biblia. Wanajua kuwa Yehova alitoa Biblia naye alitaka kwamba ieleweke.—1 Wakorintho 2:10; Waefeso 3:18; 2 Petro 3:16.

Kwa Nini Biblia Ni Muhimu?

Tunaishi katika wakati wenye uharaka zaidi wa historia ya binadamu. Biblia yaueleza kuwa “mwisho wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3, NW) Mambo mengi yanayotukia kwa kutimiza unabii wa Biblia tangu mwaka wa 1914 yaonyesha kwamba karibuni sana sasa Ufalme wa kimbingu wa Mungu “utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu.”—Danieli 2:44.

Jisomee mwenyewe mambo yanayotabiriwa katika Biblia katika Mathayo sura ya 24, Marko sura ya 13, na Luka sura ya 21. Utaona kwamba matukio yanayoonyeshwa yahusu ulimwengu mzima. Yatia ndani vita vya ulimwengu—vikiwa tofauti na vita vinginevyo. Tangu Vita ya Ulimwengu 1, tumeshuhudia upungufu wa chakula, matetemeko ya nchi, na wakati wa uvunjaji sheria usio wa kawaida uliotabiriwa. Na sasa mataifa yakaribia sana kufanya tangazo litakalotupa ishara ya wazi kwamba uharibifu wa ulimwengu unakaribia sana. Kuhusu hili, mtume Paulo aliandika hivi: “Siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, . . . wala hakika hawataokolewa.” (1 Wathesalonike 5:2, 3) Ni nani ambao hawataponyoka? Paulo aeleza hivi: “Wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu.” (2 Wathesalonike 1:7-9) Sehemu ya ishara yenye kutia mambo mengi itatimizwa na wale watiio amri iliyotolewa kwenye Mathayo 24:14 ya kuhubiri “habari njema ya ufalme . . . katika ulimwengu wote.”

Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova hutii amri hiyo katika nchi na visiwa vya bahari 231. Wao hutembelea nyumba za watu na kuwaalika watu hao binafsi kujifunza juu ya serikali ya Ufalme wa Yehova. Kwa fadhili wao hueleza hatua ambayo kila mmoja lazima achukue ili kuwa mwokokaji wa mfumo huu wa mambo na kuishi katika dunia-paradiso ambayo haitakuwa na maombolezo, kuugua, maumivu, wala kifo.—Ufunuo 21:3, 4.

Wakati waisha haraka wa ulimwengu huu mwovu, na ni lazima kwa wote watakao kuokoka mwisho wa ulimwengu huu wajifunze yale yahusikayo katika ‘kutii habari njema’ na hivyo kuokoka uharibifu. Mashahidi wa Yehova wakija nyumbani kwako wakati ujao, kwa nini usikubali mwaliko wa funzo la Biblia la kila juma? Kwa kufaa zaidi, kwa nini usiwaulize wajifunze Biblia pamoja nawe kwa sababu wataka kuielewa?

[Sanduku katika ukurasa wa 8]

NJIA YA KUELEWA BIBLIA

YESU alituhakikishia kwamba baada ya kifo na ufufuo wake, angetokeza “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ambaye angetumikia akiwa njia ya uwasiliano. (Mathayo 24:45-47, NW) Mtume Paulo alitambulisha njia hii kwa Wakristo Waefeso alipoandika kwamba “kwa njia ya kanisa [“kutaniko,” NW], hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane, . . . kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu.” (Waefeso 3:10, 11) Lilikuwa kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, lililozaliwa katika Pentekoste 33 W.K., ambalo lilikabidhiwa “mambo yaliyofunuliwa.” (Kumbukumbu la Torati 29:29) Wakiwa kikundi, Wakristo watiwa-mafuta hutumikia wakiwa mtumwa mwaminifu na mwenye busara. (Luka 12:42-44) Mgawo waliopewa na Mungu ni kutoa uelewevu wa kiroho wa “mambo yaliyofunuliwa.”

Kama vile unabii wa Biblia ulivyoelekezea Mesiya, unatuelekeza pia kwenye mwili ulioungamana wa Mashahidi Wakristo watiwa-mafuta wanaotumikia sasa wakiwa mtumwa mwaminifu na mwenye busara.a Jamii hiyo hutusaidia kuelewa Neno la Mungu. Wote watakao kuelewa Biblia wapaswa kufahamu kwamba “hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi” yaweza kujulikana kupitia njia ya pekee ya uwasiliano na Yehova, mtumwa mwaminifu na mwenye busara.—Yohana 6:68.

[Maelezo ya Chini]

a Ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1981, kurasa 19-24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki