Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 5/15 kur. 15-20
  • Soma Neno la Mungu na Umtumikie Katika Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Soma Neno la Mungu na Umtumikie Katika Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Manufaa Zenye Kudumu
  • Muhimu kwa Wote
  • Soma Neno la Mungu kwa Sauti Kubwa
  • Kujifunza kwa Kufuata Vichwa
  • Sikuzote Enenda Katika Kweli
  • Kunufaika kwa Usomaji wa Biblia Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Jitoe Mwenyewe kwa Usomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Fuata Kielelezo cha Wafalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kubali Biblia Kama Ilivyo kwa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 5/15 kur. 15-20

Soma Neno la Mungu na Umtumikie Katika Kweli

“Ee BWANA, unifundishe njia yako; nitakwenda katika kweli yako.”—ZABURI 86:11.

1. Toleo la kwanza la gazeti hili lilisema nini hasa kuhusu kweli?

YEHOVA hutoa nuru na kweli. (Zaburi 43:3) Yeye hutupa pia uwezo wa kusoma Neno lake, Biblia, na kujifunza kweli. Toleo la kwanza la jarida hili—Julai 1879—lilisema: “Kweli, kama ua dogo kati ya mimea mingi sana, imezungukwa na hata karibu kusongwa na usitawi mwingi wa magugu ya makosa. Ili uipate ni lazima uwe macho wakati wote. Ili uone umaridadi wayo ni lazima uondoe magugu ya makosa na michongoma ya ushupavu. Ili uipate ni lazima uiname kuichukua. Usiridhike na ua moja la kweli. Kama ua moja la kweli lingalitosha kusingalikuwa na mengine. Endelea kukusanya, tafuta mengine zaidi.” Kusoma na kujifunza Neno la Mungu hutuwezesha kupata ujuzi sahihi na kutembea katika kweli yake.—Zaburi 86:11.

2. Matokeo yalikuwa nini Ezra na wengine waliposoma Sheria ya Mungu mbele ya Wayahudi katika Yerusalemu la kale?

2 Baada ya kuta za Yerusalemu kujengwa upya katika 455 K.W.K., kuhani Ezra na wengine waliwasomea Wayahudi Sheria ya Mungu. Hilo lilifuatwa na Msherehekeo wa Mabanda wenye shangwe, ungamo la dhambi, na kumalizia kwa “agano la hakika.” (Nehemia 8:1–9:38) Twasoma: “Nao wakasoma katika kitabu, katika torati ya Mungu, kwa sauti ya kusikilika; wakaeleza maana yake, hata wakayafahamu yaliyosomwa.” (Nehemia 8:8) Wasomi fulani hudokeza kwamba Wayahudi hawakuelewa Kiebrania vizuri na basi fasiri ilifanywa katika Kiaramu. Lakini hilo andiko halionyeshi kueleweshwa kwa lugha ya Kiebrania. Ezra na wengine walifafanua Sheria ili kwamba watu waweze kushika kanuni zayo na kuzitumia. Vichapo na mikutano ya Kikristo pia ‘hueleza maana’ ya Neno la Mungu. Ndivyo ilivyo na wazee waliowekwa rasmi, ‘wajuao kufundisha.’—1 Timotheo 3:1, 2; 2 Timotheo 2:24.

Manufaa Zenye Kudumu

3. Ni zipi baadhi ya manufaa zipatikanazo kutokana na usomaji wa Biblia?

3 Familia za Kikristo zisomapo Biblia pamoja, yaelekea zitapata manufaa zenye kudumu. Hizo huja kujua sheria za Mungu na kujifunza kweli kuhusu mafundisho, mambo ya kiunabii, na mambo mengineyo. Baada ya sehemu ya Biblia kusomwa, kichwa cha familia aweza kuuliza: Hili lapasa kutuathirije? Ni katika njia gani hili lahusika na mafundisho mengine ya Biblia? Tunaweza kutumiaje mambo hayo katika kuhubiri habari njema? Familia hupata ufahamu wa ndani inaposoma Biblia ikiwa inafanya utafiti kwa kutumia Watch Tower Publications Index au faharisi nyinginezo. Mabuku mawili ya Insight on the Scriptures yaweza kurejezewa kwa manufaa.

4. Yoshua alipaswa kutumiaje agizo lililorekodiwa kwenye Yoshua 1:8?

4 Kanuni zitolewazo katika Maandiko zaweza kutuongoza maishani. Na zaidi, kusoma na kujifunza ‘maandiko matakatifu kwaweza kutuhekimisha hata tupate wokovu.’ (2 Timotheo 3:15) Tukiacha Neno la Mungu lituongoze, tutaendelea kutembea katika kweli yake na tamaa zetu zenye uadilifu zitatimizwa. (Zaburi 26:3; 119:130) Hata hivyo, twahitaji kutafuta uelewevu, kama alivyofanya Yoshua, aliyechukua mahali pa Musa. ‘Kitabu cha torati’ hakikupaswa kuondoka kinywani mwake, naye alipaswa kukisoma mchana na usiku. (Yoshua 1:8) Kutoacha ‘kitabu cha torati’ kiondoke kinywani mwake kulimaanisha kwamba Yoshua hakupaswa kuacha kuwaambia wengine mambo yenye kuelimisha ambayo kilisema. Kusoma Sheria mchana na usiku kulimaanisha kwamba Yoshua alipaswa kuitafakari na kujifunza. Mtume Paulo vilevile alimhimiza Timotheo ‘atafakari’ juu ya mwenendo, huduma, na ufundishaji wake. Akiwa mzee Mkristo, Timotheo alihitaji hasa kuwa mwangalifu kwamba maisha yake yalikuwa yenye kielelezo kizuri na kwamba alifundisha kweli ya Kimaandiko.—1 Timotheo 4:15.

5. Ni nini ambacho kinahitajika ili tupate kweli ya Mungu?

5 Kweli ya Mungu ni hazina yenye thamani kubwa sana. Kuipata kwahitaji kuchimba, kudumu katika kuchunguza Maandiko. Ni kwa kuwa tu kama watoto wenye kujifunza wa Mfunzi Mtukufu ndipo twapata hekima na kuja kuelewa hofu yenye kicho ya Yehova. (Mithali 1:7; Isaya 30:20, 21) Bila shaka, twapaswa kujithibitishia mambo Kimaandiko. (1 Petro 2:1, 2) Wayahudi katika Beroya “walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo [yaliyosemwa na Paulo] ndivyo yalivyo.” Waberoya walipongezwa badala ya kushutumiwa kwa kufanya hivyo.—Matendo 17:10, 11.

6. Kwa nini Yesu alionyesha kwamba hakukuwa na manufaa kwa Wayahudi fulani kuchunguza Maandiko?

6 Yesu aliwaambia Wayahudi fulani: “Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima.” (Yohana 5:39, 40) Wao walichunguza Maandiko wakiwa na lengo zuri—kwamba hayo yaweze kuwaongoza kwenye uhai. Kwa kweli, Maandiko yalikuwa na unabii mbalimbali wa Kimesiya ulioelekeza kwa Yesu kuwa njia ya kupata uhai. Lakini Wayahudi walimkataa. Basi, kuchunguza Maandiko hakukuwaletea manufaa yoyote.

7. Ni nini ambacho kinahitajika kukua katika kuelewa Biblia, na kwa nini?

7 Ili kukua katika kuelewa Biblia, twahitaji mwongozo wa roho ya Mungu, au kani yake ya utendaji. “Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu” ili kudhihirisha maana yayo. (1 Wakorintho 2:10, NW) Wakristo katika Thesalonike walipaswa ‘kujaribu mambo yote’ katika unabii wowote ule waliousikia. (1 Wathesalonike 5:20, 21) Paulo alipowaandikia Wathesalonike (karibu 50 W.K.), sehemu ya pekee ya Maandiko ya Kigiriki iliyokuwa tayari imeandikwa ilikuwa Gospeli ya Mathayo. Hivyo, Wathesalonike na Waberoya waliweza kuhakikisha mambo yote, yaelekea kwa kuchunguza fasiri ya Septuagint ya lugha ya Kigiriki ya Maandiko ya Kiebrania. Wao walihitaji kusoma na kujifunza Maandiko, na ndivyo ilivyo na sisi.

Muhimu kwa Wote

8. Kwa nini wazee waliowekwa rasmi wapaswa kufahamu sana ujuzi wa Biblia?

8 Wazee waliowekwa rasmi wapaswa kufahamu sana ujuzi wa Biblia. Ni lazima ‘wajue kufundisha’ na ‘kulishika lile neno la imani.’ Mwangalizi Timotheo alipaswa ‘kutumia kwa halali neno la kweli.’ (1 Timotheo 3:2; Tito 1:9; 2 Timotheo 2:15) Mama yake, Eunike, na nyanya yake, Loisi, walikuwa wamemfundisha maandiko matakatifu tangu utoto-mchanga, wakimkazia ‘imani isiyo na unafiki,’ ingawa baba yake alikuwa asiyeamini. (2 Timotheo 1:5; 3:15) Baba wenye kuamini wanapaswa kulea watoto wao “katika adabu na maonyo ya Bwana,” na hasa wazee ambao ni akina baba ni lazima wawe na watoto ‘waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.’ (Waefeso 6:4; Tito 1:6) Basi, hata tuwe na hali gani twapaswa kuchukua kwa uzito sana uhitaji wa kusoma, kujifunza, na kutumia Neno la Mungu.

9. Kwa nini tujifunze Biblia pamoja na Wakristo wenzi?

9 Pia twapaswa kujifunza Biblia pamoja na waamini wenzetu. Paulo alitaka Wakristo Wathesalonike wajadiliane juu ya shauri lake. (1 Wathesalonike 4:18) Ili kuboresha uelewevu wetu juu ya kweli, hakuna jambo bora kuliko kujiunga na wanafunzi wengine waliojitoa katika kuchunguza Maandiko. Mithali hii ni ya kweli: “Chuma hunoa chuma; ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.” (Mithali 27:17) Chombo cha chuma huweza kushika kutu kisipotumiwa na kunolewa. Vivyo hivyo, sisi huhitaji kukutana kwa ukawaida na kunoana kwa kushiriki pamoja ujuzi ambao tumepata kutokana na kusoma, kujifunza, na kutafakari Neno la Mungu la kweli. (Waebrania 10:24, 25) Na zaidi, hii ni njia moja ya kuhakikisha kwamba twanufaika na mimweko ya nuru ya kiroho.—Zaburi 97:11; Mithali 4:18.

10. Yamaanisha nini kuenenda katika kweli?

10 Tunapojifunza Maandiko, twaweza kwa kufaa kumwomba Mungu kama alivyofanya mtunga-zaburi: “Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze.” (Zaburi 43:3) Tukitamani kupata kibali cha Mungu, ni lazima tuenende katika kweli yake. (3 Yohana 3, 4) Hili latia ndani kufuata matakwa yake na kumtumikia kwa uaminifu na unyoofu. (Zaburi 25:4, 5; Yohana 4:23, 24) Ni lazima tumtumikie Yehova katika kweli, kama ifunuliwavyo katika Neno lake na kudhihirishwa katika vichapo vya “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” (Mathayo 24:45-47) Jambo hilo lataka ujuzi sahihi wa Maandiko. Basi, tunapaswa kusomaje na kujifunza Neno la Mungu? Je, tunapaswa kuanzia Mwanzo sura ya 1, mstari wa 1, na kupitia vitabu vyote 66? Ndiyo, kila Mkristo aliye na Biblia nzima katika lugha yake apaswa kuisoma toka Mwanzo hadi Ufunuo. Na lengo letu katika kusoma Biblia na vichapo vya Kikristo lapaswa kuwa kuongeza ufahamu wetu juu ya kweli nyingi za Kimaandiko ambazo Mungu ameandaa kupitia “mtumwa mwaminifu.”

Soma Neno la Mungu kwa Sauti Kubwa

11, 12. Kwa nini kunanufaisha kusoma Biblia kwa sauti kubwa kwenye mikutano?

11 Twaweza kusoma kwa ukimya tukiwa peke yetu. Hata hivyo, katika nyakati za kale, usomaji wa faragha ulifanywa kwa sauti kubwa. Yule towashi Mwethiopia alipokuwa amepanda gari lake, mweneza-evanjeli Filipo akamsikia akisoma kutoka unabii wa Isaya. (Matendo 8:27-30) Neno la Kiebrania lililotafsiriwa “soma” hasa humaanisha “kuita.” Hivyo wale ambao mwanzoni hawawezi kusoma kwa ukimya na kupata maana ya yale wasomayo waweza kutamka kila neno kwa sauti kubwa. Jambo kuu ni kujifunza kweli kwa kusoma Neno la Mungu lililoandikwa.

12 Kwanufaisha kusoma Biblia kwa sauti kubwa kwenye mikutano ya Kikristo. Mtume Paulo alimhimiza mfanyakazi mwenzake Timotheo: “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma [“usomaji mbele ya watu wote,” NW] na kuonya na kufundisha.” (1 Timotheo 4:13, italiki ni zetu.) Paulo aliwaambia Wakolosai hivi: “Waraka huu ukiisha kusomwa kwenu fanyeni kwamba usomwe katika kanisa la Walaodikia pia; na ule wa Laodikia usomwe na ninyi.” (Wakolosai 4:16) Na Ufunuo 1:3 husema: “Heri asomaye [“Mwenye furaha ni yeye asomaye kwa sauti kubwa,” NW] na wao wayasikiao maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati u karibu.” Basi, msemaji wa watu wote apaswa kusoma maandiko kutoka Biblia ili kuthibitisha yale anayoliambia kutaniko.

Kujifunza kwa Kufuata Vichwa

13. Ni njia ipi iliyo nzuri zaidi ya kujifunza kweli za Biblia, na ni nini ambacho chaweza kutusaidia kupata maandiko?

13 Kujifunza kwa kufuata vichwa ndiko njia nzuri zaidi ya kujifunza kweli za Kimaandiko. Konkodansi, ambazo zimeorodhesha maneno ya Biblia kialfabeti katika muktadha wao kulingana na kitabu, sura, na mstari, hufanya iwe rahisi kutafuta maandiko yanayohusiana na habari fulani. Na maandiko hayo yaweza kupatanishwa moja na jingine kwa sababu Mtungaji wa Biblia hajipingi. Kwa roho takatifu, yeye aliwapulizia wanaume wapatao 40 kuandika Biblia kwa muda uzidio karne 16, na kujifunza Biblia kwa kufuata vichwa ni njia ya kujifunza kweli ambayo imethibitishwa kwa muda mrefu.

14. Kwa nini usome Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo pamoja?

14 Uthamini wetu kwa kweli ya Biblia wapaswa kutuchochea kusoma na kujifunza Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo pamoja na Maandiko ya Kiebrania. Hilo litaonyesha jinsi Maandiko ya Kigiriki hupatana na kusudi la Mungu nalo litaangaza nuru katika unabii mbalimbali wa Maandiko ya Kiebrania. (Warumi 16:25-27; Waefeso 3:4-6; Wakolosai 1:26) Yenye msaada sana kwa habari hii ni New World Translation of the Holy Scriptures. Ilitayarishwa na watumishi wa Mungu waliojiweka wakfu waliotumia ujuzi uliongezeka upatikanao kuhusu maandiko ya awali ya Biblia pamoja na asili yayo na nahau zayo. Vyenye umuhimu pia ni visaidizi vya kujifunza Biblia ambavyo Yehova ameandaa kupitia “mtumwa mwaminifu mwenye akili.”

15. Unaweza kuthibitishaje kwamba ni sawa kunukuu hapa na pale katika Biblia?

15 Huenda wengine wakasema, ‘Vichapo vyenu hufanya maelfu ya manukuu kutoka Biblia, lakini mbona mwayatoa manukuu hayo hapa na pale?’ Kwa kunukuu hapa na pale katika vitabu 66 vya Biblia, vichapo hivyo hutumia mashahidi kadhaa waliopuliziwa ili kuthibitisha ukweli wa fundisho fulani. Yesu mwenyewe alitumia njia hii ya kufunza. Alipotoa Mahubiri ya Mlimani, alifanya manukuu 21 kutoka Maandiko ya Kiebrania. Hotuba hiyo ina manukuu matatu kutoka Kutoka, mawili kutoka Mambo ya Walawi, moja kutoka Hesabu, sita kutoka Kumbukumbu la Torati, moja kutoka Wafalme wa Pili, manne kutoka Zaburi, matatu kutoka Isaya, na moja kutoka Yeremia. Je, kwa kufanya hivyo Yesu alikuwa ‘akijaribu kuthibitisha jambo lolote tu’? La, kwa sababu ‘alifundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi.’ Ndivyo ilivyokuwa kwa sababu Yesu alitegemeza mafundisho yake kwa amri ya Neno la Mungu lililoandikwa. (Mathayo 7:29) Na ndivyo alivyofanya mtume Paulo.

16. Paulo alifanya manukuu gani ya Kimaandiko kwenye Warumi 15:7-13?

16 Katika fungu la maandiko lipatikanalo kwenye Warumi 15:7-13, Paulo alinukuu kutoka sehemu tatu za Maandiko ya Kiebrania—Sheria, Manabii, na Zaburi. Yeye alionyesha kwamba Wayahudi na Wasio Wayahudi wangemtukuza Mungu, na hivyo Wakristo walipaswa kuwakaribisha watu wa mataifa yote. Paulo alisema: “Mkaribishane ninyi kwa ninyi, kama naye Kristo alivyotukaribisha, ili Mungu atukuzwe. Kwa maana nasema, ya kwamba Kristo amefanyika mhudumu wa agano la kutahiriwa kwa ajili ya kweli ya Mungu, kusudi azithibitishe ahadi walizopewa baba zetu; tena ili Mataifa wamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema zake; kama ilivyoandikwa, [kwenye Zaburi 18:49], Kwa hiyo nitakushukuru kati ya Mataifa, nami nitaliimbia jina lako. Na tena anena [kwenye Kumbukumbu la Torati 32:43], Furahini, Mataifa, pamoja na watu wake. Na tena [kwenye Zaburi 117:1], Enyi Mataifa yote, msifuni Bwana; enyi watu wote, mhimidini. Na tena Isaya [11:1, 10] anena, Litakuwako shina la Yese, naye aondokeaye kuwatawala Mataifa; ndiye Mataifa watakayemtumaini. Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.” Kwa njia hii ya kufuata vichwa, Paulo alionyesha jinsi ya kunukuu maandiko ili kuthibitisha kweli za Biblia.

17. Ni kwa kupatana na kielelezo gani Wakristo hunukuu hapa na pale katika Biblia nzima?

17 Barua ya kwanza iliyopuliziwa ya mtume Petro ina manukuu 34 kutoka vitabu kumi katika Sheria, Manabii, na Zaburi. Katika barua yake ya pili, Petro anukuu mara sita kutoka vitabu vitatu. Gospeli ya Mathayo ina manukuu 122 kutoka Mwanzo hadi Malaki. Katika vitabu 27 vya Maandiko ya Kigiriki, kuna manukuu 320 ya moja kwa moja kutoka Mwanzo hadi Malaki na vilevile mamia ya marejezo mengine yanayorejezea Maandiko ya Kiebrania. Kwa kupatana na kielelezo kilichowekwa na Yesu na kufuatwa na mitume wake, Wakristo wa kisasa wajifunzapo kwa kufuata vichwa mbalimbali vya habari ya Kimaandiko, wao hunukuu hapa na pale katika Biblia nzima. Hilo lafaa hasa katika hizi “siku za mwisho,” ambapo karibu Maandiko yote ya Kiebrania na Kigiriki yanatimizwa. (2 Timotheo 3:1) “Mtumwa mwaminifu” hutumia Biblia hivyo katika vichapo vyake, lakini haongezei wala haondoi jambo kwa Neno la Mungu.—Mithali 30:5, 6; Ufunuo 22:18, 19.

Sikuzote Enenda Katika Kweli

18. Kwa nini ‘tuenende katika kweli’?

18 Tusiondoe kamwe chochote kutoka kwa Biblia, kwa kuwa mafundisho yote ya Kikristo katika Neno la Mungu ni “kweli” au ‘kweli ya [“habari njema,” NW].’ Kushikamana na kweli hii—‘kuenenda’ katika hiyo—ni muhimu ili kupata wokovu. (Wagalatia 2:5; 2 Yohana 4; 1 Timotheo 2:3, 4) Kwa kuwa Ukristo ni “njia ya kweli,” kwa kusaidia wengine katika kuendeleza mapendezi yayo, twawa “watenda kazi pamoja na kweli.”—2 Petro 2:2; 3 Yohana 8.

19. Tunaweza ‘kuenendaje katika kweli’?

19 Ikiwa ‘tutakwenda katika kweli,’ ni lazima tusome Biblia na kuwa tayari kupata msaada wa kiroho ambao Mungu huandaa kupitia “mtumwa mwaminifu.” (3 Yohana 4) Na tufanye hivyo kwa manufaa yetu wenyewe na ili tuweze kufundisha wengine juu ya Yehova Mungu, Yesu Kristo, na kusudi la kimungu. Na tushukuru kwamba roho ya Yehova hutusaidia kuelewa Neno lake na kufanikiwa katika kumtumikia katika kweli.

Majibu Yako Ni Yapi?

◻ Ni zipi baadhi ya manufaa zenye kudumu za usomaji wa Biblia?

◻ Kwa nini tujifunze Biblia pamoja na waamini wenzetu?

◻ Kwa nini ni sawa kunukuu kutoka sehemu mbalimbali katika Biblia nzima?

◻ Yamaanisha nini ‘kuenenda katika kweli,’ nasi twaweza kufanyaje hivyo?

[Picha katika ukurasa wa 17]

Wazazi, wafundisheni watoto wenu Maandiko

[Picha katika ukurasa wa 18]

Katika Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu alinukuu kutoka sehemu mbalimbali za Maandiko ya Kiebrania

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki