Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 10/1 kur. 26-30
  • Je, Unamsaidia Mtoto Wako Kumchagua Yehova?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unamsaidia Mtoto Wako Kumchagua Yehova?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu Inayofanya Vijana Fulani Wamwache Yehova
  • Anza Mapema
  • Wape Watoto Wako Wakati Wako
  • Ushirika Mzuri na Kielelezo Kizuri
  • Furaha Katika Kuona Watoto Wakimchagua Yehova
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Kujenga Familia Yenye Nguvu Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kuwalea Watoto Wako Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kulea Watoto Wenye Furaha Katika Ulimwengu Wenye Mchafuko Mwingi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 10/1 kur. 26-30

Je, Unamsaidia Mtoto Wako Kumchagua Yehova?

“NILIHISI kuwa kujifunza Biblia kulikuwa hakupendezi na kwenye kuchosha sana. Kwa siri, niliamua moyoni mwangu kuwa nitakapokuwa mtu mzima sitakuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova,” kijana mmoja alisema hivyo. Ingawa yatumainiwa kwamba wengi wa watoto katika nyumba za Kikristo watachagua kusimama upande wa Yehova mwishowe, wachanga kama yeye waweza kupitia wakati mgumu kuchagua Yehova kuwa Mungu wao.

Nyakati nyingine wazazi huhisi kutoelewa jinsi ya kuongoza watoto wao kwa kufaa. Wao hupitia uchunguzi-nafsi mwingi, kama baba mwenye masumbufu aliyesema: “Kusema kweli, kuna nyakati nilitazama kwenye nyuso zilizokuwa na usingizi za watoto wangu, machozi ya kuvunjwa moyo yakiwa yangali mashavuni mwao, na kushangaa kama nisingelipaswa kuwa mwenye huruma zaidi.” Wanawe wawili walikua na kuchagua kutumikia Yehova.

Bado kuna vijana wanaomwacha Yehova na kuacha kifungo cha Ukristo na kwenda kwa ulimwengu wa Shetani. Hivyo wazazi wanafanikiwaje katika kusaidia watoto wao kumchagua Yehova? Kujibu swali hilo, acha kwanza tuchunguze ni kwa nini vijana fulani humwacha Yehova wakati wazazi wao wataka sana wakae naye.

Sababu Inayofanya Vijana Fulani Wamwache Yehova

Moja ya mambo ya kawaida ni kuwa vijana fulani hawapati kamwe kabisa kumjua Yehova au njia zake. Ingawa wanahudhuria mikutano ya Kikristo kutoka utotoni, wao huenda tu bila kufikiri, nao hawamtafuti Yehova kikweli. (Isaya 55:6; Matendo 17:27) Kijana aliyetajwa mwanzoni alikuwa amechoshwa na mikutano ya Kikristo kwa sababu hakufahamu kilichokuwa kikisemwa na wasemaji jukwaani.

Mbegu za kweli hupandwa katika watoto fulani, lakini wao huruhusu mioyo yao kuvutwa na ule uonekanao kuwa mtindo-maisha wa Shetani wa kutojali na utafutaji mali wa ulimwengu wa Shetani. Wengine hawawezi kukabiliana na tamaa yenye nguvu sana ya kushirikiana au kuwa kama marika wao.—1 Mambo ya Nyakati 28:9; Luka 8:12-14; 1 Wakorintho 15:33.

Hata hivyo, ulimwenguni pote, watoto wengi katika nyumba za Kikristo wamechagua kusimama upande wa Yehova. Je, kuna jambo tunaloweza kujifunza kutoka kwa hatua zifaazo ambazo wazazi wao walichukua?

Anza Mapema

Ufunguo muhimu katika kusaidia watoto wako kumchagua Yehova ni kuanza mapema. Katika hali nyingi, mawazo yapokewayo na masomo yasomwayo wakati moyo ni mwororo na msikivu yatadumu muda wote wa maisha. (Mithali 22:6) Hivyo anza mapema kuambia watoto wako kuhusu wema wa Yehova, upendo na kicho chake, ukijitahidi kujenga ndani ya mioyo yao upendo na uthamini kwa yale Yehova amewafanyia. Kutimiza hili, wazazi wengi wametumia kwa mafanikio nakala nyingi kuhusu uumbaji wa Yehova zipatikanazo katika vichapo vya Watchtower Society.

Utii na staha kwa Yehova na ibada yake ni kati ya sifa nyinginezo zinazopaswa kukaziwa mapema maishani. Ni jambo la kuchangamsha moyo kuona watoto wasiofika umri wa kwenda shule wakijitahidi kuandika mambo rahisi kwenye mikutano ya Kikristo na kufungua maandiko katika Biblia zao wenyewe au kwenda na wazazi wao kwa bafu kuosha nyuso zao kwa maji baridi wanaposikia usingizi. Haya ni mambo rahisi, lakini ni ya muhimu jinsi gani kukaziwa katika akili changa kwamba staha na utii zapasa kuonyeshwa Yehova!

Mafunzo mazito ya kibinafsi ya Biblia pia yapasa kuanzishwa mapema. Wakati wavulana wao walipokuwa na umri wa miaka miwili, wenzi fulani wa ndoa walianza kusoma nao kitabu Kumsikiliza Mwalimu Mkuu.a Baadaye, wakati wavulana walipoanza shule, wangeamka mapema kila asubuhi na kujifunza pamoja na mama yao vitabu Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.* Hili lingefuatwa na mazungumzo ya andiko la siku yakiongozwa na baba kabla ya kiamsha kinywa. Bidii ya wazazi ilithawabishwa sana wakati wavulana wao walichagua kutumikia Yehova hivi karibuni, wakionyesha wakfu wao kwa kubatizwa majini wakiwa na umri wa miaka 10 na 11.

Kijana mmoja mzuri anayetumika katika ofisi ya tawi ya Watch Tower Society katika Japani akumbuka alipokuwa mchanga sana, mama yake alimsaidia kukuza uhusiano pamoja na Yehova kwa kuketi kando yake usiku, akimsaidia kusali. Hakusahau somo alilofunzwa—popote alipokwenda au chochote alichofanya, sikuzote Yehova alikuwa karibu na tayari kusaidia.

Wazazi wanaofanikiwa hujifunza kutambua maelekeo mabaya yaletwayo na kutokamilika kulikorithiwa kwa watoto wao, nao huanza mapema kusaidia watoto wao kuyarekebisha. (Mithali 22:15) Mwelekeo wa ubinafsi, ushupavu, kiburi, kuwa wenye kuchambua wengine kupita kiasi, lazima yashughulikiwe mapema. Kama sivyo, mbegu kama hizo baadaye zitaota ziwe uasi dhidi ya Mungu na njia zake. Kwa mfano, wazazi walio na nia njema lakini waendekezaji kupita kiasi mara nyingi huacha watoto wao wakuze mitazamo ya ubinafsi. Watoto hawa huona ugumu wa kutii ama wazazi wao ama Yehova, wakiwa kama ‘wasio na shukrani’ wanaotajwa katika Biblia. (Mithali 29:21, NW) Kwa upande mwingine, watoto wanaopewa kazi za nyumbani na kufundishwa kuona mahitaji ya wengine huelekea kuwa wenye shukrani zaidi kwa wazazi wao na kwa Yehova pia.

Jambo jingine muhimu ni kuanza mapema kuweka miradi ya kitheokrasi ambayo mtoto aweza kufikia. Ikiwa hili halitafanywa mapema na kwa uthabiti, wengine waweza kujaza akili na moyo wake kwa miradi tofauti. Kusoma Biblia yote, kujifunza kibinafsi kimoja cha vichapo vya Watchtower Society, kujiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, kuwa mhubiri wa habari njema, na kubatizwa yapasa kutiwa ndani kati ya miradi hii.

Takafumi akumbuka kuwa mama yake alimwingiza katika zoea la kusoma magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa kutayarisha maswali rahisi na kuyaacha juu ya meza jikoni ili ayapate arudipo nyumbani kutoka shuleni. Yuri hukumbuka kwamba kukaa siku chache na mapainiab wakitumika katika maeneo yenye uhitaji mkubwa wa wahudumu Wakristo, kwenda pamoja nao kwenye huduma, kuwaona wakipika chakula kitamu, na kuona furaha na bidii yao ilichochea sana tamaa yake ya kutumikia Yehova kwa njia ileile. Vijana wengi hukumbuka kuwa wazazi wao waliwapeleka kwa kawaida kutembelea makao ya Betheli, kama makao makuu na matawi ya Watch Tower Society yaitwavyo, ambapo wangeona vijana wa kiume na kike wakitumikia Yehova kwa furaha. Wengi wa wale waliotembelea wakiwa watoto sasa hutumika katika Betheli za ulimwenguni pote.

Wape Watoto Wako Wakati Wako

Kadiri na ubora wa wakati unaotumia pamoja na watoto wako huenda utakuwa na uvutano wa moja kwa moja ikiwa watachagua kumtumikia Yehova au la. Wanatambua kwa haraka kadiri ya wakati unaotumia kutayarisha funzo lao la Biblia. Ikiwa huwezi kukumbuka mahali mliachia katika funzo lililopita au kuahirisha kwa sababu hafifu, unapitisha ujumbe kwamba funzo si muhimu sana. Hata hivyo, wanapoona wazazi wakijidhabihu kwa ajili ya funzo, wakijitayarisha vizuri na kuliongoza kwa kawaida hata iweje, ujumbe tofauti kabisa hupitishwa. Ingawa si jambo la lazima, mama fulani huvalia vizuri kwa ajili ya funzo la watoto wao, sawa na jinsi wanapokwenda mikutanoni au wanapoongoza funzo la Biblia na jirani. Wazo wanalopewa ni kwamba ibada ya Yehova ni muhimu.

Wakati mwingi na jitihada nyingi zitahitajiwa kufanya elimu ya Biblia ya watoto wako iwe yenye kufurahisha, ya kufikia moyo wao. Watoto wadogo hasa huvutiwa wanapoona mambo wayasomayo yakifanywa kwa matendo mbele yao. Kwa mfano, baba mmoja alisaidia watoto wake kuwazia ufufuo kwa kuigiza maelezo ya Biblia ya ufufuo wa Lazaro. Aliingia ndani ya kijumba halafu akajitokeza kama Lazaro aliyefufuliwa.—Yohana 11:17-44.

Watoto wanapokaribia kuwa watu wazima, huchukua hata wakati na ufundi mwingi zaidi kushughulika na furiko la hisiamoyo, mashaka, na masumbufu wanayokabili. Wakati unaowekwa kando na wazazi wenye upendo na utambuzi katika kipindi hiki ni muhimu kabisa ikiwa watoto watasitawisha tumaini katika Yehova. Baba mmoja mwenye mafanikio aliye na watoto wanne alisimulia kwamba wakati watoto wake walikabili matatizo mbalimbali, angechunguza habari zihusianazo katika vichapo vya Watchtower na kuzizungumzia kila siku hadi tatizo liishe kabisa.

Mama mmoja mwenye shughuli nyingi akiwa painia na ambaye ana watoto wawili alitambua kuwa binti yake alikuwa anakuwa mnyamavu na kukosa furaha katika utendaji wa kitheokrasi. Kwa hiyo, mama huyo akaazimia kuwa nyumbani wakati mtoto arudipo kutoka shuleni kila alasiri, akimwingiza binti huyo katika mazungumzo wanywapo kikombe cha chai. Kupitia mazungumzo ya kindani ya mama na binti, msichana huyo akapokea msaada aliohitaji. Sasa, alipohitimu kutoka shule ya upili, amejiunga na mamake katika utumishi wa painia.—Mithali 20:5.[9?]

Ushirika Mzuri na Kielelezo Kizuri

Pamoja na kuwapa wakati wao, wazazi lazima wawape watoto wao ushirika ufaao. Mithali 13:20 husema: “Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; bali rafiki wa wapumbavu ataumia.”

Wazazi wengi waliofanikiwa hutambua ukweli wa mithali hiyo. Baba ya watoto wanne asema: “Nitazamapo nyuma, nafikiri ni marafiki wengi wa watoto wetu walio katika kweli waliosaidia kuwasukuma kumtumikia Yehova. Niliwatia moyo kufanya marafiki katika makutaniko mengine vilevile na letu na kutunza urafiki huo.” Mzee Mkristo aliyetumika Betheli kwa miaka mingi hukumbuka: “Nilipokuwa mchanga, tuliishi katika nyumba ndogo, lakini wakati wote ilitolewa kama mahali pa kulala kwa mwangalizi wa mzunguko. Zaidi ya hayo, mapainia wa pekee katika kutaniko letu kwa kawaida walikula chakula cha jioni pamoja nasi. Walioga kwetu na kushiriki pamoja nasi. Kusikiliza maono yao na kuona furaha yao kulinisaidia kukuza uthamini kwa utumishi wa wakati wote.”

Ushirika mzuri husaidia wale wapatao magumu. Mama mmoja ambaye mwanaye alikuwa akipitia wakati wenye masumbufu mengi alizungumzia tatizo hilo pamoja na mwangalizi mmoja wa mzunguko wa Mashahidi wa Yehova. Alipendekeza mama huyo aende pamoja na mvulana huyo katika utumishi wa shambani. “Ukifanya hivyo, hali yake ya kiroho na mambo mengine yote yataboreka,” mwangalizi huyo akasema. Mama huyo aripoti: “Katika kutaniko letu kulikuwa na mpango wa mahubiri ya jioni, na watoto wengi wenye umri wa kwenda shule, mapainia wa kawaida wenye umri mkubwa kidogo, na angalau mzee mmoja alishiriki. Mwanzoni ilikuwa shida kumfanya mwanangu kwenda kwa kawaida, lakini hilo halikuendelea kwa muda mrefu kwa kuwa alikuwa akirudi nyumbani akiwa mchangamfu zaidi na aliyetiwa moyo na ushirika ufaao. Akiwa mwanafunzi katika shule ya upili, alibatizwa naye akawa anatumikia akiwa painia msaidizi kila mwezi, na alipohitimu akawa painia wa kawaida.” Ushirika ufaao kutia ndani na kufanya mapenzi ya Yehova kulileta matokeo mazuri.

Huenda mahali penu pasiwe na walio wachanga wawezao kuwa wenye uvutano ufaao kwa mtoto wako, lakini uchunguzi uliofanywa kwa kurudiarudia kwa vijana wengi wachaguao kumtumikia Yehova hutegemea kielelezo cha wazazi wao. Vijana wengi walipendezwa na wazazi wao na walitaka kuwaiga. Yuri hukumbuka ukaribishaji wa mamaye na jinsi alivyojali wengine, akiwapigia simu na kuwatengenezea wagonjwa chakula. Tatsuo, anayetoka katika familia ya wavulana wanne, wote sasa wamekuwa watu wazima na wamtumikia Yehova, alisema: “Mama hangeweza kusoma nasi kwa kawaida kwa sababu baba alikuwa asiyeamini na alipata upinzani mwingi kutoka kwa watu wa ukoo. Lakini kuchunguza msimamo wake katika kweli na shangwe yake katika kumtumikia Yehova ilivutia sana. Alikuwa tayari pia kukesha hadi usiku wa manane kutusaidia na matatizo yetu.” Maneno ya hekima ya wazazi yana nguvu yanapotegemezwa na kazi ya uaminifu. Yoichiro alisema kuhusu wazazi wake: “Siwezi kukumbuka kamwe wakisema mambo yasiyofaa kuhusu wengine katika kutaniko; wala hawakuturuhusu sisi watoto kusema juu ya makosa ya wengine.”—Luka 6:40-42.

Furaha Katika Kuona Watoto Wakimchagua Yehova

Hakuna njia itegemekayo kabisa katika kusaidia watoto wako kumchagua Yehova. Kutakuwa na nyakati za masumbufu. Lakini baba aliyesumbuka aliyetajwa mapema alisema: “Tukiwa wazazi tulijaribu sikuzote kwa uaminifu kufuata madokezo ya tengenezo lionekanalo la Yehova. Huu ulikuwa msaada mkubwa katika kushinda matatizo.” Jitihada zao zilifanikiwa.

Ndiyo, kwa kufanya uwezalo kufuata mwongozo wa Biblia, ukiwapa watoto wako sababu nzuri za kumpenda Yehova, zikitegemezwa na kielelezo chako cha uaminifu na jitihada nyoofu za kusaidia, wewe pia mwishowe waweza kuona jitihada zako zikifanikiwa. Je, wakumbuka mvulana aliyetajwa hapo awali, aliyekuwa ameazimia wakati mmoja kutokuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova? Baada ya mamake kumsaidia kwa mafanikio kupita miaka ya magumu, alisema: “Nafurahi mama hakuchoka kamwe na kuacha!” Waweza kupata matokeo kama hayo kwa watoto wako.—Wagalatia 6:9.

[Maelezo ya Chini]

a Vilivyotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

b Wahudumu wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova huitwa mapainia. Painia msaidizi hutumia muda wa saa zisizopungua 60 katika huduma kila mwezi, painia wa kawaida saa 90, na painia wa pekee saa 140.

[Picha katika ukurasa wa 30]

Waweza kutazama nyuma ukionea shangwe kumbukumbu la kuwalea watoto?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki