Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 11/1 kur. 16-22
  • Mwe Wenye Huruma Nyororo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwe Wenye Huruma Nyororo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kazi ya Huruma Isiyo na Kifani
  • Sehemu ya Utu Mpya
  • Wivu—Kizuizi cha Huruma
  • Vikwazo Vingine kwa Huruma
  • Huruma kwa Ajili ya Wagonjwa
  • Huruma kwa Walio Dhaifu
  • Iweni Wenye “Huruma Nyororo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • “Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”
    Mkaribie Yehova
  • Mwige Yehova Katika Kuonyesha Huruma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Yehova Hutawala kwa Huruma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 11/1 kur. 16-22

Mwe Wenye Huruma Nyororo

“Jivikeni wenyewe shauku nyororo za huruma, fadhili.” —WAKOLOSAI 3:12, NW.

1. Kwa nini kuna uhitaji mkubwa wa huruma leo?

HAKUJAPATA kamwe kuwa na wakati wowote katika historia ambao watu wengi mno wamehitaji msaada wenye huruma kama sasa. Wakikabiliwa na ugonjwa, njaa, ukosefu wa kazi, uhalifu, vita, msukosuko, na misiba ya kiasili, mamilioni wanahitaji msaada. Lakini kuna tatizo zito hata zaidi, nalo ni hali ya kiroho iliyo mbaya sana ya wanadamu. Shetani, anayejua kwamba muda wake ni mfupi, ‘anadanganya ulimwengu wote.’ (Ufunuo 12:9, 12) Kwa hiyo, hasa wale walioko nje ya kutaniko la kweli la Kikristo wamo katika hatari ya kupoteza uhai, na Biblia haiandai tumaini lolote kwa wale wanaofishwa katika siku ya Mungu inayokuja ya hukumu.—Mathayo 25:31-33, 41, 46; 2 Wathesalonike 1:6-9.

2. Kwa nini Yehova amejizuia kuharibu waovu?

2 Na bado kufikia wakati huu wa mwisho, Yehova Mungu aendelea kuonyesha saburi na huruma kwa watu wasio na shukrani na walio waovu. (Mathayo 5:45; Luka 6:35, 36) Amefanya hivyo kwa sababu ileile iliyomfanya akawie kuadhibu taifa lisilo na uaminifu la Israeli. “Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?”—Ezekieli 33:11.

3. Tuna kielelezo gani cha huruma ya Yehova kwa wale wasio watu wake, nasi twajifunza nini kutokana na hilo?

3 Yehova pia aliwaonyesha huruma Waninawi waovu. Yehova alimtuma nabii wake Yona awaonye juu ya uharibifu uliokuwa ukikaribia. Wao waliitikia vizuri kwa mahubiri ya Yona na kutubu. Jambo hilo lilimsukuma Mungu mwenye huruma, Yehova, asiliangamize jiji hilo wakati huo. (Yona 3:10; 4:11) Ikiwa Mungu aliwasikitikia Waninawi, ambao wangekuwa na uwezekano wa kufufuliwa, ni lazima awe anahisi huruma kama nini leo kwa watu wanaokabili uharibifu wa milele!—Luka 11:32.

Kazi ya Huruma Isiyo na Kifani

4. Yehova huonyeshaje huruma kwa watu wake leo?

4 Kwa kupatana na utu wake wenye huruma, Yehova ameagiza Mashahidi wake waendelee kuzuru majirani wao wakiwa na “habari njema ya ufalme.” (Mathayo 24:14) Na watu waitikiapo kwa uthamini kwa kazi hiyo ya kuokoa uhai, Yehova hufungua mioyo yao kuufahamu ujumbe wa Ufalme. (Mathayo 11:25; Matendo 16:14) Kwa kuiga Mungu wao, Wakristo wa kweli huonyesha huruma nyororo kwa kuwarudia watu wanaopendezwa, wakiwasaidia, inapowezekana, kwa njia ya funzo la Biblia. Hivyo, katika 1993, Mashahidi wa Yehova wanaozidi milioni nne na nusu, katika nchi 231, walitumia zaidi ya saa bilioni moja wakihubiri nyumba kwa nyumba na kujifunza Biblia pamoja na majirani wao. Kwa upande wao, watu hao wapya wenye kupendezwa wana fursa ya kuweka maisha yao wakfu kwa Yehova na kujiunga na Mashahidi waliobatizwa. Kwa njia hiyo, wao pia wajiunga na kazi hii isiyo na kifani kwa ajili ya wale wanaotazamiwa kuwa wanafunzi ambao wangali wamenaswa katika ulimwengu huu unaokufa wa Shetani.—Mathayo 28:19, 20; Yohana 14:12.

5. Huruma ya kimungu ifikapo kikomo chayo, nini kitatendeka kwa dini iwakilishayo Mungu vibaya?

5 Karibuni Yehova atatenda akiwa “mtu wa vita.” (Kutoka 15:3) Kwa sababu ya huruma kwa ajili ya jina lake na kwa ajili ya watu wake, ataondosha mbali uovu na kusimamisha ulimwengu mpya wenye uadilifu. (2 Petro 3:13) Ya kwanza kupatwa na siku ya ghadhabu ya Mungu ni makanisa ya Jumuiya ya Wakristo. Kama vile Mungu hakuokoa hekalu lake mwenyewe katika Yerusalemu mkononi mwa mfalme wa Babiloni, ndivyo pia hataokoa matengenezo ya kidini ambayo yamemwakilisha vibaya. Mungu ataweka katika mioyo ya washiriki wa Umoja wa Mataifa kuiangamiza Jumuiya ya Wakristo na aina nyingine yote ya ibada isiyo ya kweli. (Ufunuo 17:16, 17) “Nami,” Yehova atangaza, “jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; lakini nitaleta njia yao juu ya vichwa vyao.”—Ezekieli 9:5, 10.

6. Ni katika njia zipi Mashahidi wa Yehova husukumwa kuonyesha huruma?

6 Maadamu kuna wakati, Mashahidi wa Yehova wanaendelea kuwaonyesha majirani wao huruma kwa kuhubiri kwa bidii ujumbe wa Mungu wa wokovu. Na kwa kawaida, inapowezekana, wao pia husaidia watu wenye uhitaji wa kimwili. Ingawa hivyo, kwa habari hiyo, daraka lao la kwanza ni kutunza mahitaji ya washiriki wa karibu wa familia yao na wale wanaohusiana nao katika imani. (Wagalatia 6:10; 1 Timotheo 5:4, 8) Tume nyingi za misaada zinazofanywa na Mashahidi wa Yehova kwa ajili ya waamini wenzao ambao wamepatwa na mikasa mbalimbali zimekuwa mifano yenye kutokeza ya huruma. Hata hivyo, si kwamba Wakristo wangojee mpaka tatizo litokee ndipo waonyeshe huruma nyororo. Wao huonyesha sifa hii haraka wanaposhughulikia mazuri na magumu ya maisha ya kila siku.

Sehemu ya Utu Mpya

7. (a) Kwenye Wakolosai 3:8-13, huruma yalinganishwaje na utu mpya? (b) Huruma nyororo hufanya iwe rahisi kwa Wakristo kufanya nini?

7 Ni kweli kwamba asili yetu ya dhambi na uvutano mbaya wa ulimwengu wa Shetani ni vizuizi kwa hali yetu ya kuwa wenye huruma nyororo. Hiyo ndiyo sababu Biblia hutuhimiza tuondolee mbali “hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi.” Badala ya hivyo twashauriwa ‘tuvae utu mpya’—utu unaopatana na mfano wa Mungu. Kwanza, twaamriwa tujivike “moyo wa rehema [“shauku nyororo za huruma,” NW], utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu.” Kisha Biblia yatuonyesha njia itumikayo ya kuonyesha sifa hizi. “Mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.” Ni rahisi zaidi kusamehe ikiwa tumesitawisha ‘shauku nyororo ya huruma’ kwa ndugu zetu.—Wakolosai 3:8-13.

8. Kwa nini ni muhimu kuwa na roho ya kusamehe?

8 Kwa upande mwingine, kukosa kuonyesha msamaha wenye huruma huhatarisha uhusiano wetu na Yehova. Yesu alionyesha jambo hilo kwa mkazo sana katika kielezi chake cha mtumwa asiyesamehe, aliyefungwa katika jela na bwana-mkubwa wake “hata atakapoilipa deni ile yote.” Mtumwa huyo alistahili kutendewa hivyo kwa sababu kwa njia ya kushangaza sana alikataa kuonyesha huruma kwa mtumwa mwenzake aliyeomba rehema. Yesu alimalizia kielezi chake kwa kusema: “Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.”—Mathayo 18:34, 35.

9. Huruma nyororo yahusianaje na jambo muhimu zaidi la utu mpya?

9 Kuwa mwenye huruma nyororo ni upande muhimu wa upendo. Na upendo ndio ishara ya kutambulisha Ukristo wa kweli. (Yohana 13:35) Kwa hiyo, ufafanuzi wa Biblia wa utu mpya wamalizia hivi: “Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.”—Wakolosai 3:14.

Wivu—Kizuizi cha Huruma

10. (a) Nini chaweza kusababisha wivu kukuzwa mioyoni mwetu? (b) Ni matokeo gani mabaya yawezayo kutokezwa na wivu?

10 Kwa sababu ya asili yetu ya kibinadamu yenye dhambi, hisia za wivu zaweza kukua kwa urahisi katika mioyo yetu. Ndugu au dada aweza kubarikiwa kuwa na vipawa au mali za kimwili ambazo sisi hatuna. Au labda mtu amepokea baraka za kipekee za kiroho na mapendeleo. Tukiwaonea wivu watu kama hao, je, tutaweza kuwatendea kwa huruma nyororo? Labda sivyo. Badala ya hivyo, hatimaye hisia za wivu zaweza kujionyesha katika maneno yenye kuchambua au matendo yasiyo na fadhili, kwa kuwa Yesu alisema hivi juu ya wanadamu: “Kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.” (Luka 6:45) Huenda wengine wakakubaliana na uchambuzi huo. Kwa njia hiyo, amani ya familia au kutaniko la watu wa Mungu yaweza kuvurugwa.

11. Ndugu kumi wa Yusufu waliondoaje huruma kutoka mioyoni mwao, kukiwa na matokeo gani?

11 Fikiria kile kilichotokea katika familia moja kubwa. Wana kumi wenye umri mkubwa zaidi wa Yakobo walimwonea wivu ndugu yao mdogo Yusufu kwa sababu yeye alipendwa zaidi na baba yao. Matokeo yakawa kwamba “hawakuweza kusema naye kwa amani.” Baadaye Yusufu alibarikiwa kwa kupata ndoto za kimungu, jambo lililothibitisha kwamba alikuwa na upendeleo wa Yehova. Hilo liliwapa ndugu zake sababu za ‘kumchukia zaidi.’ Kwa sababu hawakuondoa wivu kutoka mioyoni mwao, huo haukuachia huruma nafasi, nao ukaleta dhambi nzito.—Mwanzo 37:4, 5, 11.

12, 13. Twapaswa kufanya nini hisia za wivu ziingiapo moyoni mwetu?

12 Kwa ukatili, walimwuza Yusufu utumwani. Katika jitihada ya kufunika kosa lao, walimdanganya baba yao afikirie kwamba Yusufu alikuwa ameuawa na mnyama mwitu. Dhambi yao ikaja kujulikana miaka mingi baadaye walipolazimishwa na ukame kwenda Misri kununua chakula. Msimamizi wa chakula, ambaye hawakumtambua kuwa Yusufu, aliwashtaki kuwa wapelelezi na kuwaambia wasitafute msaada wake tena mpaka wamlete ndugu yao mchanga zaidi, Benjamini. Kufikia wakati huu Benjamini alikuwa amekuwa mpendwa zaidi wa baba yao, nao walijua kwamba Yakobo hangetaka kumwacha aende.

13 Kwa hiyo walipokuwa wamesimama mbele ya Yusufu, dhamiri zao ziliwasukuma kukiri: “Kweli sisi tulimkosa ndugu yetu [Yusufu], kwa kuwa tuliona shida ya roho yake, alipotusihi [“alipotusihi huruma,” NW] wala hatukusikia; kwa hiyo shida hii imetupata.” (Mwanzo 42:21) Kwa shughuli zake zenye huruma lakini zenye uthabiti, Yusufu alisaidia ndugu zake kuthibitisha ukweli wa toba yao. Kisha akajitambulisha kwao na kuwasamehe kwa ukarimu. Muungano wa familia ukarudishwa. (Mwanzo 45:4-8) Tukiwa Wakristo, twapaswa kujifunza somo kutokana na hilo. Kujua matokeo mabaya ya wivu, twapaswa kusali kwa Yehova atupe msaada wa kuwa na ‘hisia nyororo za huruma’ mahali pa hisia zenye wivu.

Vikwazo Vingine kwa Huruma

14. Kwa nini tunapaswa kuepuka kujiachilia kusikofaa kwa jeuri?

14 Kikwazo kingine kwa kuwa kwetu wenye huruma kwaweza kutokana na kujiachilia mno kwa jeuri. Michezo na vitumbuizo vinavyoonyesha jeuri huendeleza tamaa mbaya ya kumwaga damu. Katika nyakati za Biblia, wapagani walitazama kwa ukawaida mashindano ya mapigano makali na aina nyinginezo za kutesa wanadamu katika nyanja za michezo za Milki ya Roma. Vitumbuizo hivyo, kulingana na mwanahistoria mmoja, “viliharibu hisia ya huruma kwa mateseko ambayo hutofautisha wanadamu na wanyama.” Vitumbuizo vingi katika ulimwengu wa kisasa wa leo una athari iyo hiyo. Wakristo wanaojitahidi kuwa wenye huruma nyororo, wahitaji kuwa wenye uteuzi sana katika mambo wachaguayo kusoma, sinema, na programu za televisheni. Kwa hekima wao huzingatia akilini maneno ya Zaburi 11:5, NW: “Mtu yeyote anayependa jeuri hakika [Yehova] humchukia.”

15. (a) Mtu aweza kuonyeshaje ukosefu mkubwa wa huruma? (b) Wakristo wa kweli huitikiaje mahitaji ya waamini wenzao na majirani?

15 Mtu mwenye ubinafsi pia aelekea kukosa huruma. Hilo ni jambo zito, kwa kuwa mtume Yohana aeleza hivi: “Mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?” (1 Yohana 3:17) Ukosefu kama huo wa huruma ulionyeshwa na kuhani aliyejiona kuwa mwadilifu na yule Mlawi katika kielezi cha Yesu cha Msamaria mwenye ujirani. Walipoona hali mbaya ya ndugu yao Myahudi aliyekuwa nusu-mfu, wao walivuka upande mwingine wa barabara na kuendelea na safari yao. (Luka 10:31, 32) Tofauti na hivyo, Wakristo wenye huruma huitikia upesi kwa mahitaji ya kimwili na kiroho ya ndugu zao. Na kama yule Msamaria katika kielezi cha Yesu, wao pia huhangaikia mahitaji ya watu wasiofahamu. Hivyo, kwa furaha wao hutoa wakati wao, nishati zao, na mali zao kuendeleza kazi ya kufanya wanafunzi. Kwa njia hii wao huchangia wokovu wa mamilioni.—1 Timotheo 4:16.

Huruma kwa Ajili ya Wagonjwa

16. Ni mapungufu gani tunayokabili tushughulikiapo hali ya magonjwa?

16 Ugonjwa ni fungu la wanadamu wasiokamilika, wanaokufa. Wakristo vilevile, na wengi wao si wastadi wa kitiba, wala hawawezi kufanya miujiza kama walivyofanya baadhi ya Wakristo wa mapema waliopokea uwezo huo kutoka kwa Kristo na mitume wake. Kwa kufa kwa mitume wa Kristo na washiriki wao wa karibu, uwezo huo wa kimwujiza ulikwisha. Kwa hiyo, uwezo wetu wa kusaidia wale wanaougua magonjwa ya kimwili, kutia na kupungua kwa uwezo wa ubongo na kupotewa akili, umepunguka.—Matendo 8:13, 18; 1 Wakorintho 13:8.

17. Twajifunza somo gani kutokana na jinsi Ayubu aliyekuwa mgonjwa na kufiwa alivyotendewa?

17 Mara nyingi kushuka moyo huandamana na ugonjwa. Kwa kielelezo, Ayubu mwenye kumhofu Mungu alishuka moyo sana kwa sababu ya ugonjwa wake mbaya sana na misiba aliyoletewa na Shetani. (Ayubu 1:18, 19; 2:7; 3:3, 11-13) Alihitaji marafiki ambao wangemtendea kwa huruma nyororo na ‘kusema kwa kufariji.’ (1 Wathesalonike 5:14) Badala ya hivyo, wale walioitwa eti wafariji watatu walimtembelea na kurukia uamuzi mbaya. Wao walizidisha kushuka moyo kwa Ayubu kwa kudokeza kwamba misiba yake ilitokana na kosa fulani lake. Wakiwa wenye huruma nyororo, Wakristo wataepuka kuingia katika mtego kama huo wakati waamini wenzao ni wagonjwa au kama wameshuka moyo. Nyakati nyingine, jambo kubwa wanalohitaji ni ziara kadhaa zenye fadhili kutoka kwa wazee au Wakristo wengine waliokomaa ambao watasikiliza kwa huruma, wakionyesha kuelewa mambo, na kuandaa shauri la upendo la Kimaandiko.—Warumi 12:15; Yakobo 1:19.

Huruma kwa Walio Dhaifu

18, 19. (a) Wazee wapaswa kushughulikaje na walio dhaifu na watendao makosa? (b) Hata kama ni lazima kuunda halmashauri ya hukumu, kwa nini ni muhimu kwa wazee kutendea wenye makosa kwa huruma nyororo?

18 Wazee hasa ni lazima wawe wenye huruma nyororo. (Matendo 20:29, 35) “Imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu,” Biblia yaamuru. (Warumi 15:1) Kwa kuwa hatujakamilika, sisi sote hufanya makosa. (Yakobo 3:2) Wororo wahitajika katika kushughulika na mtu ‘aliyeghafilika katika kosa lo lote.’ (Wagalatia 6:1) Wazee hawapaswi kamwe kuwa kama Mafarisayo wajionao kuwa waadilifu ambao hawakuwa na kiasi katika njia waliyotumia Sheria ya Mungu.

19 Kwa kutofautisha, wazee hufuata vielelezo vya huruma nyororo vya Yehova Mungu na Yesu Kristo. Kazi yao kubwa ni kulisha, kutia moyo, na kufariji kondoo za Mungu. (Isaya 32:1, 2) Badala ya kujaribu kuongoza mambo kwa sheria nyingi mno, wao hurejezea kanuni nzuri zilizo katika Neno la Mungu. Kwa hiyo, kazi ya wazee yapasa iwe kujenga, kuleta shangwe na uthamini kwa ajili ya wema wa Yehova katika mioyo ya ndugu zao. Mwamini mwenzi afanyapo kosa dogo, kwa kawaida mzee ataepuka kumsahihisha wengine wasikiapo. Kama ni lazima aseme, hisia za huruma nyororo zitamsukuma mzee huyo kumchukua mtu huyo kando na kuzungumza naye tatizo hilo kama wengine hawasikii. (Linganisha Mathayo 18:15.) Hata mtu awe mgumu namna gani kushughulika naye, mfikio wa mzee wapaswa kuwa wenye saburi na wenye msaada. Hapaswi kamwe kutafuta visababu vya kumwondosha huyo kutanikoni. Hata inapokuwa lazima kuunda halmashauri ya hukumu, wazee wataonyesha huruma nyororo wanaposhughulika na mtu aliyejiingiza katika kosa zito. Uungwana wao waweza kumsaidia mtu huyo atubu.—2 Timotheo 2:24-26.

20. Ni nyakati zipi wonyesho wa kihisia-moyo wa huruma haufai, na kwa nini?

20 Hata hivyo, kuna pindi nyinginezo ambapo mtumishi wa Yehova hawezi kuonyesha huruma. (Linganisha Kumbukumbu la Torati 13:6-9.) Kwa Mkristo, ‘kutochangamana’ na rafiki wa karibu au mtu wa ukoo ambaye ametengwa na ushirika kwaweza kuwa mtihani mgumu sana. Katika hali hiyo, ni muhimu kwa mtu asishindwe na hisia za sikitiko. (1 Wakorintho 5:11-13) Uthabiti kama huo waweza hata kumsaidia yule mkosaji atubu. Zaidi, katika shughuli na mtu wa jinsia tofauti, ni lazima Wakristo waepuke maonyesho yasiyofaa ya huruma yawezayo kutokeza ukosefu wa adili kingono.

21. Ni katika maeneo gani mengine twahitaji kuonyesha huruma nyororo, na kuna manufaa zipi?

21 Nafasi haituruhusu kuzungumzia maeneo yote mengi ambayo huruma nyororo yahitajika—katika kushughulika na walio wazee-wazee, waliofiwa, wale wanaonyanyaswa na wenzi wasioamini. Wazee wafanyao kazi kwa bidii vilevile ni lazima watendewe kwa huruma nyororo. (1 Timotheo 5:17) Uwastahi na kuwategemeza. (Waebrania 13:7, 17) ‘Nyinyi nyote mwe wenye huruma nyororo,’ akaandika mtume Petro. (1 Petro 3:8) Tukitenda kwa njia hiyo katika hali zote zinazohitajika, twaendeleza muungano na furaha katika kutaniko na kuvutia watu wa nje kwenye kweli. Zaidi ya yote, kwa kufanya hivyo twamstahi Baba yetu mwenye huruma nyororo, Yehova.

Maswali ya Kupitia

◻ Yehova huonyeshaje huruma kwa wanadamu wenye dhambi?

◻ Kwa nini ni muhimu kuwa mwenye huruma nyororo?

◻ Ni vipi baadhi ya vikwazo vya kuwa kwetu wenye huruma nyororo?

◻ Twapaswa kutendeaje wagonjwa na walioshuka moyo?

◻ Ni nani hasa anayepaswa kuwa mwenye huruma nyororo, na kwa nini?

[Sanduku katika ukurasa wa 19]

MAFARISAYO WASIO NA HURUMA

SIKU ya Sabato ya pumziko ilikusudiwa kuwa baraka ya kiroho na ya kimwili kwa watu wa Mungu. Hata hivyo, viongozi wa kidini wa Kiyahudi walifanyiza sheria nyingi ambazo hazikustahi sheria ya Mungu ya Sabato na kuifanya kuwa mzigo kwa watu. Kwa kielelezo, ikiwa mtu yeyote alipata aksidenti au akaugua ugonjwa, hangeweza kusaidiwa katika siku ya Sabato ijapokuwa tu kama uhai wake ulihatarishwa.

Kikundi kimoja cha Mafarisayo kilishikilia sana jinsi kilivyofasiri sheria ya Sabato hivi kwamba kilisema: “Mtu hafariji waombolezi, wala mtu hatembelei wagonjwa katika siku ya Sabato.” Viongozi wengine wa kidini waliruhusu ziara hizo katika siku ya Sabato lakini waliamuru: “Machozi hayaruhusiwi.”

Kwa hiyo, kwa kufaa Yesu alishutumu viongozi wa kidini wa Kiyahudi kwa kupuuza matakwa ya maana zaidi ya Sheria, kama vile haki, upendo, na rehema. Si ajabu kwamba aliwaambia Mafarisayo: ‘Mnalitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu’!—Marko 7:8, 13; Mathayo 23:23; Luka 11:42.

[Picha katika ukurasa wa 17]

Katika nchi 231 Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi isiyo na kifani ya huruma katika nyumba za watu, barabarani, hata katika magereza

[Picha katika ukurasa wa 18]

Kujiachilia kwa jeuri, kama ile ionyeshwayo katika televisheni, hudhoofisha huruma nyororo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki