Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 1/1 kur. 3-4
  • Shika Uaminifu wa Maadili Ukaishi!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shika Uaminifu wa Maadili Ukaishi!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Utimilifu Wako!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Ukamilifu wa Ayubu—Ni Nani Anayeweza Kuuiga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Tutatembea Katika Utimilifu Wetu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Ayubu Alilitukuza Jina la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 1/1 kur. 3-4

Shika Uaminifu wa Maadili Ukaishi!

“UMKUFURU Mungu, ukafe.” Jalada la gazeti letu laonyesha mke wa Ayubu, aliyemshambulia kwa maneno hayo. Shambulio hilo lilitokea kama miaka 3,600 iliyopita. Hata hivyo mashambulizi hayo ya maneno juu ya mtumishi mwaminifu wa Mungu yakazia suala fulani linalokabili wanadamu hadi siku ya leo. Ayubu mwaminifu alikuwa amepoteza vitu vingi—mifugo yake, nyumba yake, watoto wake kumi. Na sasa mwili wake ulikuwa ukiteswa kwa ugonjwa wa kudumu, ukimjaribu kufikia kikomo. Sababu ilikuwa nini? Adui mkuu wa Mungu na wa mwanadamu, Shetani Ibilisi, alikuwa akibisha kwamba mtu hawezi kudumisha uaminifu wa maadili kwa Mungu chini ya jaribu kali.—Ayubu 1:11, 12; 2:4, 5, 9, 10.

Leo, kama vile katika siku za Ayubu, ‘dunia yote hukaa katika yule mwovu,’ Shetani Ibilisi. (1 Yohana 5:19) Kwa kweli, hilo ni kweli hata zaidi leo, maana sasa “yule . . . aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote,” amekwisha kutupwa kutoka mbinguni hadi hapa duniani. (Ufunuo 12:9) Tukio hilo latokeza ole mwingi unaohuzunisha wanadamu katika wakati wetu. Kulipuka kwa ile vita ya ulimwengu ya kwanza, katika 1914, kulitia alama “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu” yanayoendelea hata sasa katika karne hii ya 20.—Mathayo 24:7, 8, New World Translation.

Katika ulimwengu huu mkatili, uliopotoka, je, wewe huhisi kwamba umefika kikomo cha uvumilivu wa kibinadamu? Je, hupati kujiuliza, ‘Kuna kusudi lolote katika kuishi?’ Huenda Ayubu alihisi hivyo, lakini hakupoteza kamwe imani katika Mungu, ingawa alifanya makosa. Alieleza azimio lake kwa maneno haya: “Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu [“uaminifu wa maadili,” NW] wangu.” Alikuwa na uhakika kwamba Mungu ‘angepata kujua uaminifu wa maadili wake.’—Ayubu 27:5; 31:6.

Yesu Kristo, Mwana wa Mungu mwenyewe, pia alilazimika kuvumilia majaribu alipokuwa hapa duniani. Shetani alimshambulia Yesu kwa njia mbalimbali. Alitumia mahitaji ya Yesu ya kimwili na kujaribu utegemeo Wake kwa Neno la Mungu, kama vile kwenye mlima wa majaribu. (Mathayo 4:1-11) Alimtaabisha Yesu kwa kutumia waandishi na Mafarisayo waasi imani na wafuasi wao kumtesa, kumshitaki kwamba amekufuru, na kufanya njama ya kumuua. (Luka 5:21; Yohana 5:16-18; 10:36-39; 11:57) Walimfanyia Yesu mambo mabaya hata zaidi kuliko yale Ayubu alifanyiwa na wale wafariji wa uongo watatu.—Ayubu 16:2; 19:1, 2.

Katika bustani la Gethsemane, Yesu alipokaribia upeo wa jaribio hili, aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa.” Halafu, “akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.” Mwishowe, akiwa juu ya mti wa mateso, kwa utimizo wa maneno ya unabii ya Zaburi 22:1, Yesu akalia kwa sauti kuu: “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” Lakini hatimaye Mungu hakumwacha Yesu kwa sababu Yesu alidumisha uaminifu wa maadili ulio mkamilifu Kwake, akitolea Wakristo wote wa kweli kielelezo bora cha kufuata. Yehova alithawabisha ushikaji wa uaminifu wa maadili wa Yesu kwa kumfufua na kumkweza juu ya mbingu zote. (Mathayo 26:38, 39; 27:46; Matendo 2:32-36; 5:30; 1 Petro 2:21) Mungu atawathawabisha vilevile wengine wote wanaoshika uaminifu wa maadili kwake.

Uaminifu wa maadili wa Yesu haukumpa Shetani jibu kamili tu kwa mwito aliotoa bali dhabihu ya uhai wake mkamilifu iliandaa fidia, kwa msingi ambao wanadamu washika uaminifu wa maadili waweza kupata uhai wa milele. (Mathayo 20:28) Kwanza, Yesu akusanya “kundi dogo” la watiwa-mafuta wanaokuwa watawala wenzi pamoja naye katika Ufalme wa kimbingu. (Luka 12:32) Baada ya hao, “umati mkubwa” wanakusanywa ili waokoke “ile dhiki kubwa,” wakitoka ndani yayo ili warithi uhai wa milele kwenye milki ya Ufalme wa Mungu duniani.—Ufunuo 7:9, 14-17, linganisha Habari Njema kwa Watu Wote.

Ayubu mshika uaminifu wa maadili atakuwa miongoni mwa mabilioni waliokufa ambao watafufuliwa wakati huo ili wawe sehemu ya jamii yenye amani ya “dunia mpya.” (2 Petro 3:13; Yohana 5:28, 29) Kama ionyeshwavyo katika jalada la nyuma la gazeti letu, uaminifu wa maadili ulithawabishwa katika siku ya Ayubu wakati Yehova ‘aliubariki huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake.’ Alikuwa amepata nguvu za kiroho kama mmoja ambaye “hakufanya dhambi kwa midomo yake.” Mungu alirefusha maisha yake kwa miaka 140 zaidi. Alimpa Ayubu maradufu ya vitu vya kimwili alivyokuwa navyo mbeleni, Ayubu ‘akawa na wana waume saba, na binti watatu,’ binti hao wakionwa kuwa warembo zaidi katika nchi hiyo yote. (Ayubu 2:10; 42:12-17) Lakini ufanisi huo wote ulikuwa mwonjo tu wa baraka ambazo washika uaminifu wa maadili watafurahia katika Paradiso ya “dunia mpya.” Wewe pia waweza kushiriki katika furaha hiyo, kama kurasa zifuatazo zitakavyoeleza!

[Picha katika ukurasa wa 4]

Yesu aliweka kielelezo kikamilifu akiwa mshika uaminifu wa maadili

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki