Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 3/15 kur. 3-4
  • Unaweza Kutajirishaje Sala Zako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kutajirishaje Sala Zako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Boresha Sala Zako Kupitia Funzo la Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 3/15 kur. 3-4

Unaweza Kutajirishaje Sala Zako?

SALA haina kifani kati ya maandalizi ya upendo ya Yehova Mungu. Wapinzani huenda wakunyang’anye Biblia yako au kukuzuia usikutane na waabudu wenzako, lakini hakuna yeyote anayeweza kukunyang’anya sala. Sala ni ya muhimu sana. Basi, ni muhimu kadiri gani kwa kila mmoja wetu kuihazini na kujinufaisha kikamili kwa pendeleo hili. Ni nini kinachoweza kukusaidia utajirishe sala zako?

Biblia si kitabu cha sala. Hata hivyo, kingeweza kufafanuliwa kuwa kitabu cha jamii ya binadamu cha sala kilicho kikubwa kuliko vyote. Maandiko ya Kiebrania peke yake yana zaidi ya sala 150. Baadhi yazo ni fupi; nyingine ni ndefu. Zilisemwa hadharani au faraghani, na wafalme au na watekwaji, katika ushindi au katika dhiki. Kama Daudi alivyoimba katika Zaburi 65:2, ‘watu wote’ mgeukieni Yehova, ‘Msikiaji wa sala.’ Kwa nini Mungu aliwapulizia waandikaji wa Biblia kurekodi namna nyingi hivyo za sala?

Ili kujibu swali hilo, fikiria 2 Timotheo 3:16. Lasema: “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa.” Hivyo, sala za Kibiblia zipo ili kutuongoza, kama ulivyo unabii, kanuni, na historia za Kimaandiko. Sala hizi zaweza kutunufaishaje?

Kwa kuchunguza kwa makini sala za Kimaandiko, twaweza kutambua zile zilizosemwa katika hali zinazofanana na zetu. Twaweza kujifunza jinsi sala zinavyotofautiana katika kusudi na muundo. Zaidi ya hilo, tutagundua semi mpya za kusifu na kutoa shukrani nasi tutapata maneno mapya ya kusihi na kutoa dua zetu. Kwa ufupi, sala za Kibiblia zaweza kutusaidia kutajirisha sala zetu wenyewe.

Mariamu, aliyekuja kuwa mama ya Yesu, ni dhahiri alikuwa mtu aliyenufaika kutokana na semi zilizotumiwa katika sala zilizorekodiwa katika Biblia. Yeye alimtembelea mtu wa ukoo wake Elisabeti baada ya kila mmoja wao kupata mimba ya mtoto wa kiume kwa msaada wa kimungu. Mariamu alitoa sifa na shukrani kwa Mungu, na baadhi ya maneno yake yaonekana yanafanana na yale yaliyomo katika sala kwenye Maandiko ya Kiebrania. Yaonekana kwamba yawezekana Mariamu alifahamu sala iliyosemwa na Hana, mama ya nabii Samweli. Hana alikuwa pia amepata mimba ya mtoto wa kiume kwa msaada wa Mungu, zaidi ya miaka 1,000 mapema. Je, ingewezekana kwamba Mariamu alitafakari juu ya sala hii kwa sababu ilionyesha hisia zake mwenyewe?—1 Samweli 2:1-10; Luka 1:46-55.

Vipi kuhusu wewe? Je, waweza kukumbuka sala ya Kibiblia iliyosemwa chini ya hali zinazofanana na zako mwenyewe? Kutafuta, kusoma, na kutafakari juu ya sala kama hizo kutakusaidia utajirishe kuwasiliana kwako na Mungu. Katika makala ifuatayo, twakukaribisha uchunguze sala tatu kutoka kwa Maandiko Matakatifu. Zilisemwa chini ya hali tofauti, pengine zinazofanana na zako.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki