Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 5/15 kur. 3-4
  • Chifu Afikiria Wakati Wake Ujao

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chifu Afikiria Wakati Wake Ujao
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Wazazi Wetu wa Kale Wako Wapi?
    Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
  • Je, Wafu Wanaweza Kutuona?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Ni Nani Wanaoishi Katika Makao ya Roho?
    Amkeni!—1996
  • Je! Ibada ya Mababu Waliokufa Yawapasa Wakristo?
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 5/15 kur. 3-4

Chifu Afikiria Wakati Wake Ujao

CHIFU huyo wa Afrika Magharibi alikuwa kiongozi aliyependwa na kustahiwa sana katika jumuiya yake. Katika sherehe ya siku ya kuzaliwa ya mwaka wake wa 78, marafiki wake, familia yake, na wengine wenye kumtakia mema walikusanyika ili kumpongeza. Katika hotuba, chifu huyo alichagua kuzungumzia habari isiyo ya kawaida kwa pindi kama hiyo. Alisema juu ya mawazo yake kuhusu maisha baada ya kifo.

Alisema kwamba baada ya kifo “kuna ulimwengu mpya usio na hila, wivu na pupa.” Aliufafanua kuwa ulimwengu “uliojaa fumbo,” unaokaliwa tu na waadilifu pekee, ambao wangeshirikiana na Mungu.

Itikadi kama hizo ni za kawaida miongoni mwa watu kotekote Afrika. Kulingana na dini ya kimapokeo ya Kiafrika, kifo si mwisho wa uhai bali ni mpito tu, kupita kuingia katika maisha ya makao ya roho. Wakati wa kifo mtu husemwa kuwa amevuka kutoka ulimwengu unaoonekana hadi usioonekana. Kisha mtu huyo, akiwa roho, huingia katika makao yakaliwayo na wazazi wake wa kale waliokufa.

Wengi wa Waafrika wa Magharibi huamini kwamba wazazi wa kale waliokufa, au roho za wazazi waliokufa, huhakikisha kwamba familia zao duniani zina hali-njema. Kitabu West African Traditional Religion chasema hivi: “Hakuna tofauti kamili ya uvutano kati ya washiriki wa jumuiya ambao wangali duniani, na wale walio katika ulimwengu huo mwingine. Walipokuwa duniani, [wazazi wa kale] walikuwa wazee wa familia zao. Sasa kwa kuwa wamesitiriwa kutoka kwetu, wangali wazee katika ulimwengu wa roho. Wao hawakomi kupendezwa na hali-njema ya ujumla ya familia zao.”

Basi, yule chifu mzee-mzee aliyetajwa mwanzoni alitazamia kujiunga na wazazi wa kale waliokufa na kufanya kazi pamoja nao katika makao ya roho. Yeye alisema hivi: “Nimesadiki kabisa maisha baada ya kifo na uwezekano wangu wa kuendelea kutumika—hata baada ya kifo.”

Hata hivyo, kwa sababu ya lile ambalo chifu huyo alifuatia kusema, gazeti la habari Sunday Times lilidokeza kwamba “hakuonekana kuwa na uhakika kabisa” kuhusu maisha baada ya kifo. Alieleza umati uliokuwa umekusanyika kwamba alikuwa amesikia juu ya kitabu fulani kilichozungumza juu ya maisha baada ya kifo. Chifu huyo amekuwa akikitafuta kwa miaka mitano. Alitamani sana kukisoma hivi kwamba alitoa pesa zinazotoshana na karibu dola 1,500 (za Marekani) kwa mtu yeyote ambaye angemletea nakala moja.

Chifu huyo hangesumbuka kama angekiendea kitabu kisicho kigumu kupata. Ni kitabu kinachopatikana kwa urahisi ambacho hakikutokezwa na mwanadamu bali na Muumba wa wanadamu wote. (1 Wathesalonike 2:13) Kitabu hicho ni Biblia. Kinasema nini juu ya maisha baada ya kifo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki