Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 8/15 uku. 8
  • Je, Mashaka Juu ya Yesu Yanastahili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Mashaka Juu ya Yesu Yanastahili?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Mashaka Kuhusu Yesu Yalivyoanza
  • Shuhuda Ziondoazo Mashaka
  • Sababu Inayofanya Watu Fulani Washuku Miujiza ya Yesu
  • Je, Mashaka Kuhusu Ufufuo wa Yesu Yastahili?
  • Kwa Nini Hupaswi Kushuku Fungu la Sasa la Yesu?
  • Ile Miujiza—Je! Kweli Ilitukia?
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Miujiza ya Yesu Unaweza Kujifunza Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Ufufuo wa Yesu​—Kwa Nini Ni Muhimu Kwetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Yesu Kristo—Maswali Yetu Yajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 8/15 uku. 8

Je, Mashaka Juu ya Yesu Yanastahili?

JE, KWELI Yesu wa Nazareti alifanya miujiza? Je, alifufuliwa kutoka kwa wafu, kama wanafunzi wake walivyotangaza? Je, aliwahi kuishi? Katika kizazi chetu cha kisasa, wengi ni kama hawawezi kujibu maswali hayo wakiwa na uhakika. Kwa sababu gani? Kwa sababu wanakubali mashaka kuhusu Yesu, na mashaka ni hisia za kukosa uhakika, kutokujua ikiwa jambo ni kweli au si kweli. Lakini hisia za kukosa uhakika kuhusu Yesu zastahili? Acheni tuone.

Jinsi Mashaka Kuhusu Yesu Yalivyoanza

Wanatheolojia Wajerumani fulani wa mwishoni mwa karne ya 19 na mapema karne ya 20 walionyesha Yesu kuwa “mtu wa kuwaziwa wa Kanisa la kale.” Ubishi wao kuhusu ukweli wa historia ya Yesu ulitokeza ubishi miongoni mwa wasomi mwanzoni mwa karne hii uliofikia umma wakati huo na bado una uvutano leo. Kwa kielelezo, uchunguzi wa majuzi katika Ujerumani ulifunua kwamba asilimia 3 ya wale waliohojiwa wanaitikadi kwamba Yesu “hakuwahi kamwe kuishi” na kwamba “mitume walimbuni.” Ndiyo, mbegu za shaka kuhusu Yesu zilizopandwa mapema katika karne hii hata sasa zapata mchanga wenye rutuba mioyoni mwa watu.

Kwa nini mkataa wa kwamba Yesu “alibuniwa” haustahili. Msomi wa Biblia Wolfgang Trilling atoa maelezo haya: “Ubishi wa kama Yesu aliwahi kuishi, kwa maneno mengine kama alikuwa mtu wa kihistoria au ngano, ulisuluhishwa. Swali hilo lilijibiwa kwa njia ya kielimu, hasa kwa njia ambayo watu wenye kufikiri hawaoni tatizo hilo kuwa suala la elimu.” Hata hivyo, wengine bado hushuku kama Yesu aliwahi kuwapo. Kama tokeo, ebu tuchunguze jinsi mtu aweza kuthibitisha uhakika wa kihistoria juu ya Yesu na vilevile kuondoa mashaka mengine kumhusu.

Shuhuda Ziondoazo Mashaka

Uuaji wa Yesu wa aibu kama mhalifu aliyedharauliwa waandaa “sababu yenye kusadikisha zaidi dhidi ya wapingao ukweli wa historia ya Yesu,” asema Trilling. Kwa sababu gani? Kwa sababu mauaji hayo “yalitatiza, hata kuzuia, ule mweneo wa imani mpya miongoni mwa Wayahudi na wasio Wayahudi.” (Linganisha 1 Wakorintho 1:23.) Ikiwa uuaji wa Yesu aliyekuwa Mesiya ulionwa na Wayahudi na vilevile wasio Wayahudi kuwa ufidhuli, kwa hakika haungebuniwa na mitume! Zaidi ya hayo, kifo cha Yesu kimethibitishwa kuwa tukio la kihistoria na zile Gospeli nne na pia mwandikaji Mroma Tacitus na Talmud ya Kiyahudi.a

Matukio mengine wakati wa maisha ya Yesu pia yaonwa kuwa uthibitisho wa kindani wa ukweli wa zile Gospeli, na yale zituelezazo kumhusu. Kwa kielelezo, je, wafuasi wa Yesu wangebuni kutoka kwake Nazareti, mahali paonekanapo kuwa vivi hivi? Au yamkini wangebuni kusalitiwa kwake na Yuda, mwenzi aliyetumainiwa? Je, laonekana kuwa jambo halisi kufikiri kwamba wangebuni hadithi kuhusu kuachwa kwa Yesu na wanafunzi wengineo kwa njia kama hiyo ya woga? Kwa kweli si jambo linalopatana na akili kufikiri kwamba wanafunzi wangebuni mambo hususa yenye kudhuru sana kisha wayatangaze kila mahali! Kwa kuongezea, usanifu wa kufundisha aliotumia Yesu ulikuwa wa muundo wa kipekee. Fasihi ya Kiyahudi ya karne ya kwanza haina chochote cha kulinganishwa na vielezi vyake. Ni mtu gani asiyejulikana angeweza kamwe “kubuni” Mahubiri ya Mlimani yenye ustadi kama yalivyo? Sababu hizi zote zathibitisha utumainifu wa Gospeli kuwa ripoti mbalimbali za maisha ya Yesu.

Pia kuna uthibitisho ulio wazi wa uhakika wa kihistoria juu ya Yesu. Hizo Gospeli nne zinamwonyesha akiishi mahali hususa panaposimuliwa kwa usahihi kihistoria. Mahali mbalimbali, kama vile Bethlehemu na Galilaya; watu mmoja-mmoja na vikundi mashuhuri, kama vile Pontio Pilato na Mafarisayo; na vilevile desturi za Kiyahudi na mambo mengine ya kipekee hayakubuniwa tu. Yalifanyiza sehemu ya muundo wa maisha katika karne ya kwanza, nayo yamethibitishwa na vianzo visivyo vya Kibiblia na magunduzi ya kiakiolojia.

Hivyo basi, kuna uthibitisho wenye kusadikisha, wa ndani na ulio wazi, kwamba Yesu ni mtu aliyekuwapo.

Walakini, watu wengi wana mashaka juu ya miujiza inayomhusu. Kwa kweli, kulingana na uchunguzi ulionukuliwa hapo juu, ni Wajerumani wachache tu kati ya wale ambao huenda kanisani wanaoamini kabisa kwamba miujiza na ufufuo wa Yesu “ulitokea kwa kweli.” Je, mashaka kuhusu miujiza na ufufuo wa Yesu yanastahili?

Sababu Inayofanya Watu Fulani Washuku Miujiza ya Yesu

Mathayo 9:18-36 huripoti kwamba Yesu aliponya wagonjwa, akafufua wafu, na kufukuza roho waovu kimuujiza. Profesa Hugo Staudinger, mwanahistoria, atoa maelezo haya: “Haiwezi kuaminika kamwe, na kwa upande wa historia haiwezekani kabisa, kusema kwamba ripoti hizi za kipekee ni matokeo ya kuwazia tu.” Kwa sababu gani? Kwa sababu inaonekana kwamba Gospeli za mapema zaidi ziliandikwa wakati mashahidi wengi waliojionea miujiza hii walikuwa wangali hai! Uhakika zaidi unapatikana kwa habari ya kwamba, kama Staudinger aendeleavyo kusema, wapinzani Wayahudi “hawakukana kamwe kwamba Yesu alifanya kazi zipitazo nguvu za kibinadamu.” Bila kutafuta ushuhuda mwingine tukitegemea tu uthibitisho huu ulio wazi, twaona kwamba miujiza ya Yesu kwa kweli inastahili itikadi yetu.—2 Timotheo 3:16.

Ingawa “Wajerumani walio wengi wanaamini kwamba Yesu aliponya wagonjwa,” wengi wana mashaka kuhusu nguvu zilizotokeza maponyo hayo. Kwa mfano, Mwanatheolojia Mjerumani aliye mashuhuri alisema waziwazi kwamba maponyo aliyofanya Yesu yalikuwa matokeo ya nguvu za uvutano wa akili zenye kushawishi watu waliokuwa wakipatwa na mkazo mkali wa akili. Je, haya ni maelezo yafaayo?

Ebu fikiria vielelezo hivi. Marko 3:3-5 huripoti kwamba Yesu aliponya mtu mwenye mkono uliopooza. Lakini je, mkono uliopooza ni tokeo la mkazo mkali wa akili? Bila shaka sivyo. Basi, uponyaji huo haungekuwa tokeo la nguvu za uvutano wa akili. Ni nini basi kilimwezesha Yesu kufanya miujiza? Profesa Staudinger akubali hivi: “Ikiwa hakuna kanuni zilizo thabiti kabisa, na ikiwa mtu hamkani Mungu kabisa, basi kwa msingi mtu hawezi kukataa uwezekano wa kwamba Mungu, aliye na uwezo kuliko mwanadamu, anaweza kufanya mambo yasiyo ya kawaida.” Ndiyo, basi kwa msaada wa ‘Nguvu ya Mungu,’ Yesu kihalisi aliponya watu waliokuwa wagonjwa. Hivyo hakuna sababu ya kushuku ukweli wa miujiza yake.—Luka 9:43; Mathayo 12:28.

Kama The American Peoples Encyclopedia isemavyo, ikiwa muujiza mkubwa kuliko yote—ufufuo wa Yesu—ulifanyika, miujiza mingine yote iliyoripotiwa katika Gospeli “yawezekana.” Je, kweli Yesu alifufuliwa kutoka wafu?

Je, Mashaka Kuhusu Ufufuo wa Yesu Yastahili?

Kwanza fikiria uthibitisho wenye nguvu uliotokea unaotegemeza ukweli wa ufufuo wa Yesu—kaburi lake tupu. Uhakika wa kwamba kaburi la Yesu lilipatikana likiwa tupu haukubishaniwa na walioishi wakati wake, hata na wapinzani wake. (Mathayo 28:11-15) Uwongo ungelifunuliwa kwa urahisi! Kitabu cha marejezo kilichotajwa hapo juu kwa kufaa chafikia mkataa huu: “Hakuna maelezo yanayofaa ya kaburi tupu yamewahi kudokezwa ila taarifa hii ya kibiblia, ‘Hayupo hapa; kwani amefufuka’ (Mt. 28:6).”

Wengine hupinga wakisema kwamba ni wanafunzi wa Yesu pekee waliotangaza kila mahali kwamba ndiye aliyekuwa Mesiya aliyefufuliwa. Hiyo ni kweli: Lakini je, ustahilifu wa kuaminika kwa ujumbe wao haukutegemezwa na uhakika wa kihistoria, hasa kifo na ufufuo wa Yesu? Bila shaka. Mtume Paulo alijua upatano wa jambo hilo alipoandika hivi: ‘Tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yetu ni bure. Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo.’—1 Wakorintho 15:14, 15; linganisha Yohana 19:35; 21:24; Waebrania 2:3.

Katika karne ya kwanza, kulikuwa na watu wengi waliojulikana vizuri na ambao wangetoa ushahidi wa kuonekana kwa Yesu baada ya kifo chake. Miongoni mwao mlikuwa wale mitume 12 na Paulo, na vilevile zaidi ya mashahidi wengine 500 waliojionea.b (1 Wakorintho 15:6) Kumbuka pia sababu iliyofanya Mathiya atimize sifa za ustahili ili achukue nafasi ya Yuda mtume aliyekosa kuwa mwaminifu. Matendo 1:21-23 huripoti kwamba Mathiya angetoa ushahidi juu ya ufufuo wa Yesu na juu ya matukio ya mapema yaliyohusu Yesu. Ikiwa maisha na ufufuo wa Yesu ungekuwa jambo la kuwazia tu badala ya kuwa jambo hakika, kuwekwa rasmi kama huko kwa kweli hakungekuwa na maana yoyote.

Kwa sababu mashahidi wengi waliojionea wa karne ya kwanza wangetoa ushahidi juu ya maisha, miujiza, kifo, na ufufuo wa Yesu, Ukristo kwa kadiri fulani ulienea kwa haraka katika Milki yote ya Roma, vijapokuwa vipingamizi vilivyotajwa hapo juu. Wafuasi wake walikuwa tayari kuvumilia magumu, mnyanyaso, na hata kifo ili washuhudie kila mahali ufufuo na kweli ya msingi inayotokana na jambo hilo. Kweli ipi? Kwamba ufufuo wake ulikuwa umewezeshwa tu na uwezo wa Mungu. Na kwa nini Yehova Mungu alikuwa amemfufua Yesu kutoka wafu? Jibu la swali hilo laonyesha ni nani aliye Yesu wa kihistoria.

Siku ya Pentekoste, mtume Petro alitangazia waziwazi Wayahudi waliokuwa wameshangaa katika Yerusalemu hivi: “Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake. Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu [“roho takatifu,” New World Translation], amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia. Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume. Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako. Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha [“mliyemtundika mtini,” NW] kuwa Bwana na Kristo.” (Matendo 2:32-36) Ndiyo, Yehova Mungu alimfanya Yesu wa Nazareti “kuwa Bwana na Kristo.” Je, mashaka kuhusu fungu lake katika upande huu wa kusudi la Mungu yanastahili?

Kwa Nini Hupaswi Kushuku Fungu la Sasa la Yesu?

Mashaka yote kuhusu utambulisho na fungu la Yesu yaweza kuondolewaje? Na uhakika wa kwamba kwa wazi alikuwa nabii wa kweli. Alitabiri juu ya vita, njaa kuu, matetemeko ya dunia, uhalifu, na ukosefu wa upendo tuuonao leo. Kuongezea hilo, alitabiri hivi: “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:3-14) Utimizo wa unabii huu mbalimbali unathibitisha kwamba Yesu ndiye Kristo aliyefufuliwa, anayetawala bila kuonekana ‘kati ya adui zake,’ na hivi karibuni ataleta ulimwengu mpya wa Mungu.—Zaburi 110:1, 2; Danieli 2:44; Ufunuo 21:1-5.

Sasa zaidi ya wakati mwingine wowote, wanadamu wanahitaji sana Mwokozi mwenye hekima ipitayo ile ya kibinadamu. Kwa nini hatupaswi kushuku kwamba Yesu ndiye aliyechaguliwa kwa haki kuokoa wanadamu? Yohana, aliyekuwa shahidi aliyejionea miujiza yenye kuvutia na ufufuo wa Yesu, alitangaza hivi: “Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu.” (1 Yohana 4:14; linganisha Yohana 4:42.) Kama tusivyokuwa na sababu nzuri za kushuku maisha, miujiza, kifo, na ufufuo wa Yesu, ndivyo hatuna sababu nzuri ya kushuku kwamba ametawazwa na Yehova Mungu akiwa Mfalme halali kwenye mkono Wake wa kuume. Bila shaka lolote, Yesu wa Nazareti ni Mfalme wa Ufalme wa Mungu na “Mwokozi wa ulimwengu.”—Mathayo 6:9, 10.

[Maelezo ya chinis]

a Marejezo ya Talmud ya kushambulia Yesu yamekubaliwa kuwa kweli na wasomi fulani pekee. Kwa upande mwingine, marejezo ya Tacitus, Suetonius, Pliny the Younger, na angaa mara moja na Flavius Josephus kuhusu Yesu, kwa ujumla yanakubaliwa kuwa uthibitisho wa ukweli wa historia ya kuwapo kwa Yesu.

b Katika pindi moja, Yesu aliyefufuliwa alikula samaki pamoja na wanafunzi wake, jambo linalohakikisha kwamba kuonekana kwake hakukuwa ono tu, kama wengine wanavyodai leo.—Luka 24:36-43.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki