Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 2/1 uku. 3
  • Je, Wewe Umeokolewa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Umeokolewa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Lazima Tufanye Nini Tuokolewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Jambo Ambalo Ni Lazima Tufanye Ili Tuokolewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Wokovu—Inachomaanisha kwa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Yesu Huokoa—Jinsi Gani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 2/1 uku. 3

Je, Wewe Umeokolewa?

JOHNNY alikuwa mwenye umri wa miaka kumi mtu fulani alipomsimamisha katika maonyesho fulani na kumwuliza hivi: “Kijana, unamkubali Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wako?” Swali hilo lilionekana kumshangaza Johnny, kwa kuwa sikuzote alikuwa amemwamini Yesu. Kwa hiyo akajibu, “Bila shaka ndiyo.” “Bwana asifiwe!” mtu huyo akapaaza sauti ili watu wote wasikie. “Nafsi nyingine imeokolewa kwa ajili ya Kristo!”

Je, wokovu ni rahisi hivyo? Je, Johnny “aliokolewa” aliposema tu maneno hayo, hata kama atafanya nini katika maisha yake yanayobaki? Watu wengi wanyoofu wangejibu ndiyo. Trakti fulani za kidini husema uandike tarehe “uliyookolewa” ili uweze kuikumbuka.

Kasisi mmoja aliandika kwamba katika “pindi tu ya kuonyesha imani ya kijuu-juu tu katika Kristo . . . wakati wako ujao umeamuliwa daima.” Alidai kwamba Biblia yasema wokovu wategemea ‘tendo moja tu la imani, lionyeshwalo mara moja pekee, bali hautegemei kuonyesha imani kwa kuendelea.’ Mwandikaji mwingine wa kidini aliandika hivi: “Hilo ni tendo lililomalizwa. Tayari umepata wokovu . . . ‘Vita yako imekwisha.’ ‘Dhambi yako imeondolewa.’” Lakini hata watu ambao wameamini kabisa kwamba hilo ni kweli waweza kuona kasoro hapa. Ni wazi kwamba watu wengi ambao wameambiwa kwamba “wameokolewa” hawaishi kulingana na vile Biblia husema wapaswa kuishi. Maelezo ambayo hutolewa kwa kawaida ni kwamba wao hawakuwa “wamemkubali” Kristo kabisa.

Basi, “kumkubali” Yesu kwamaanisha nini hasa? Je, ni tendo la imani la wakati mmoja tu, au ni njia ya maisha yenye kuendelea? Je, ni lazima itikadi yetu iwe yenye nguvu sana kuweza kutuchochea tutende? Je, kweli twaweza kukubali manufaa za dhabihu ya Yesu bila daraka la kumfuata?

Watu wengi hutaka baraka lakini si daraka la kumfuata na kumtii Yesu. Hakika, neno “kutii” huwakera. Lakini Yesu alisema: “Njoo unifuate.” (Luka 18:18-23) Na Biblia husema: ‘Wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu wataadhibiwa kwa maangamizi ya milele.’—2 Wathesalonike 1:8, 9; Mathayo 10:38; 16:24.

Biblia husema mambo mengi ambayo huzusha maswali kuhusu yale ambayo yamefundishwa kuhusu wokovu. Kama ungependa kuthibitisha yale ambayo Biblia husema hasa juu ya habari hii, utapata kurasa zinazofuata kuwa zenye kupendeza hasa. Fungua Biblia yako, usome maandiko yaliyotajwa uone yale Yesu na mitume wake walifundisha juu ya suala hili muhimu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki