Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 12/1 kur. 21-23
  • Darasa la 101 la Gileadi Lenye Juhudi Katika Matendo Mema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Darasa la 101 la Gileadi Lenye Juhudi Katika Matendo Mema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Shauri Lenye Kutumika ili Kudumu Wenye Juhudi
  • Mambo Yaliyoonwa Yanayotia Moyo Utendaji Wenye Juhudi
  • Shangilia kwa Tumaini la Ufalme!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Wanafunzi Wenye Kuhitimu wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Ona Mambo Kama Mungu Anavyoyaona
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Mfurahieni Yehova na Kushangilia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 12/1 kur. 21-23

Darasa la 101 la Gileadi Lenye Juhudi Katika Matendo Mema

MUUMBA wetu, Yehova Mungu, ni mwenye juhudi katika matendo mema, ndivyo na Mwana wake, Yesu Kristo. Akiwa kielelezo chetu, Yesu alionyesha juhudi kwa kutimiza mgawo wake wenye kupewa na Mungu, uliotia ndani “[ku]jitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili . . . kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.” (Tito 2:14) Wale washiriki 48 wa darasa la 101 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower kwa hakika wameonyesha juhudi yao katika matendo mema. Programu ya uhitimu kwa ajili ya wamishonari hao ilifanywa Septemba 7, 1996, katika Kitovu cha Kielimu cha Watchtower huko Patterson, New York.

Shauri Lenye Kutumika ili Kudumu Wenye Juhudi

Mwenyekiti wa programu ya uhitimu alikuwa Carey Barber, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, mwenye miaka zaidi ya 70 katika huduma ya wakati wote. Katika maneno yake ya ufunguzi, Ndugu Barber alielekeza uangalifu kwenye utendaji wa kuhubiri na kufundisha wa Yesu, aliyekuwa “nuru ya ulimwengu.” (Yohana 8:12) Alionyesha kwamba Yesu hakujiwekea daraka hilo lenye kuheshimika bali aliwasihi sana wanafunzi wake pia waache nuru yao ing’ae. (Mathayo 5:14-16) Pendeleo hilo la utumishi lafanya maisha ya Mkristo yawe na maana zaidi na lawapa daraka zito wote ‘wanaoenenda kama watoto wa nuru.’—Waefeso 5:8.

Baada ya maneno hayo ya ufunguzi, Don Adams wa Ofisi za Utekelezaji katika makao makuu ya Brooklyn alialikwa jukwaani. Alisema juu ya kichwa “Kusonga Mbele, Si Kurudi Nyuma.” Ndugu Adams alikazia Shule ya Gileadi yenyewe na kusudi layo—kueneza kuhubiriwa kwa habari njema hadi nchi za kigeni. Alisema juu ya maendeleo ya tengenezo la Mungu, ambalo limechapisha fasihi za Biblia kotekote ulimwenguni katika lugha zaidi ya 300. Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kilichochapishwa mwaka wa 1995, kimefanywa kipatikane katika lugha 111 na kimeratibiwa kuchapwa katika lugha nyingine zaidi. Tayari kimetumiwa katika kusaidia wanafunzi wapya wa Yesu kufikia hatua ya wakfu na ubatizo katika muda wa miezi michache tu. Kwa hiyo, hao wamishonari wapya watakuwa na misaada ya karibuni zaidi ya kujifunza Biblia wawezayo kutumia katika kazi yao.

Kisha, Lyman Swingle, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, akasema juu ya kichwa “Endeleeni Kumtolea Yehova Utumishi Wenu Mtakatifu,” chenye msingi wa Ufunuo 7:15. Kwa kuwa Yehova mwenyewe ni Mungu mwenye furaha, kumtumikia kwa kuendelea ndilo jambo linalomfurahisha mtu. (1 Timotheo 1:11) Kwa sababu ya utumishi huu wenye shangwe, umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za dunia wamekuja kumwabudu. Katika miaka ambayo imepita, wale ambao wamezoezwa katika Shule ya Gileadi wamekuwa na sehemu katika kuwasaidia wengi wa watu hao kupata ujuzi sahihi wa kweli. Kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuamini kwamba Yehova ataendelea kubariki wale wanaotumwa sasa ili wapate kukusanya washiriki wengi zaidi wa umati mkubwa unaopanuka.

“Kuonyesha Shangwe ya Yehova” ndicho kichwa kilichokaziwa na Daniel Sydlik, ambaye pia ni mshiriki wa Baraza Linaloongoza. Alionyesha kwamba watumishi wote wa Mungu, kutia na wamishonari wapya, wana pendeleo la kufundisha watu njia ya uhai udumuo milele na njia ya kupata faida zote za maisha sasa. “Kufundisha,” akataarifu Ndugu Sydlik, “ni kazi ya kujithawabisha. Hilo linaonyeshwa kwenye nyuso za watu wanaofundisha na katika nyuso za watu wanaojifunza.” (Zaburi 16:8-11) Alimnukuu mishonari mmoja katika Estonia aliyesema, “Tuna ujumbe wenye umaana zaidi usoni pa dunia, na ni uso wetu uonyeshao hilo.” Sura yetu yaweza kufanya watu watusikilize na kuamsha upendezi. Watu wanataka kujua ni nini kinachowafurahisha watumishi wa Yehova. “Kwa hiyo elekeza fikira kwenye sura yako,” akashauri Ndugu Sydlik. “Watu hufurahia kuona watu wenye furaha.”

Ulysses Glass, ambaye ameshiriki katika kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa Gileadi tangu darasa la 12 katika mwaka 1949, alihutubia wasikilizaji juu ya kichwa “Kwa Subira, Lindeni Nafsi Zenu.” Subira ni nini? Inawasilisha wazo la kungojea jambo fulani kwa utulivu na kudhihirisha ustahimilivu unapochokozwa au ukiwa chini ya mkazo. Mtu mwenye subira hudumu mtulivu; mtu asiye na subira huwa mwepesi wa kutenda na kuudhika. “Wengi hufikiri kwamba subira huonyesha udhaifu au hali ya kusitasita,” akaonelea Ndugu Glass, lakini “kwa Yehova sifa hiyo huonyesha nguvu na kuwa na kusudi.” (Mithali 16:32) Subira ina matokeo gani mema? “Kuwa na subira wakati wa hasira kutakuepusha na siku mia moja za maumivu makali,” yasema mithali moja ya Kichina. “Subira huboresha utu wa mtu,” akaeleza Ndugu Glass. “Kwa kweli, hiyo huzipaka zile sifa nyingine njema mng’ao wa kudumu. Yafanya imani itamanike, amani idumu muda mrefu, na upendo usitikisike.”

“Ni pendeleo kupokea mgawo kutoka kwa Yehova Mungu kupitia tengenezo lake,” akataarifu Mark Noumair, aliyetumikia akiwa mishonari Kenya kwa miaka 11 na sasa ni mfunzi wa Gileadi. Alipoeleza kichwa “Usipokuwa na Imani, Hutavumilia Muda Mrefu,” Ndugu Noumair alielekeza uangalifu kwenye kielelezo cha Mfalme Ahazi wa Yuda. Isaya alimhakikishia huyo mfalme utegemezo wa Yehova katika mgawo wake, lakini bado Ahazi alishindwa kuwa na itibari katika Yeye. (Isaya 7:2-9) Kisha Ndugu Noumair akaonyesha kwamba wamishonari—kwa kweli, sisi sote—wahitaji kuwa na imani katika Yehova ili kuvumilia kwa muda mrefu katika migawo yao ya kitheokrasi. Magumu mahususi ya mgawo wa umishonari yataka imani yenye nguvu. “Kumbukeni sikuzote kwamba hakuna hali kamilifu katika mfumo huu wa mambo,” akataarifu Ndugu Noumair.

Mambo Yaliyoonwa Yanayotia Moyo Utendaji Wenye Juhudi

Wakati wa mazoezi yao ya Gileadi, wanafunzi walitumia kila mwisho-juma katika huduma ya hadharani, itakayokuwa pia shughuli yao kuu katika migawo yao ya umishonari. Wallace Liverance, aliye mshiriki wa kitivo cha Gileadi, aliwahoji wanafunzi 15, waliosimulia mambo waliyoona. Ndipo Leon Weaver wa Halmashauri ya Idara ya Utumishi na Lon Schilling wa Halmashauri ya Utendaji-Kazi za Betheli wakahoji washiriki wa halmashauri za tawi kutoka Afrika na Amerika ya Latini waliosimulia mambo yaliyoonwa kutoka katika shamba la umishonari na hao walikuwa na shauri jema la kuwatolea hao wamishonari waliokuwa wakihitimu. Ilionyeshwa kwamba katika Sierra Leone, karibu asilimia 90 ya wale waliobatizwa katika mwaka wa utumishi wa 1995 walikuwa wamesaidiwa na wamishonari. Hiyo ilikuwa rekodi njema kama nini ya utendaji wenye juhudi!

Mwishowe, Milton Henschel, msimamizi wa Sosaiti, aliwahutubia wale wasikilizaji 2,734 juu ya kichwa “Tengenezo la Yehova Lionekanalo Ni la Kipekee.” Ni nini kinachofanya tengenezo la Mungu lisiwe na kifani? Si ukubwa walo wala nguvu zalo bali ni jambo la hakika la kwamba linaongozwa na amri na maamuzi ya kihukumu yenye uadilifu ya Mungu. Katika nyakati za kale, watu wa Yehova, taifa la Israeli, ndio waliokabidhiwa matamko yake yaliyo matakatifu, yaliyolifanya taifa hilo liwe la kipekee. (Warumi 3:1, 2) Leo, tengenezo la Yehova limeunganika litendapo kazi chini ya mwongozo wa Yesu Kristo. (Mathayo 28:19, 20) Linasitawi na kukua. Je, kuna tengenezo jingine duniani ambalo Baraza lalo Linaloongoza hupata shauri kutoka katika Neno la Mungu, Biblia, kabla ya kufanya maamuzi ya maana? Katika njia hii na nyinginezo, tengenezo lionekanalo la Yehova ni la kipekee kwelikweli.

Programu ya kupendeza sana ilimalizia kwa kutolewa kwa diploma na usomaji wa barua kutoka kwa hilo darasa yenye kuonyesha shukrani kwa hayo mazoezi ya pekee.

[Sanduku katika ukurasa wa 22]

Takwimu za Darasa

Idadi ya nchi zilizowakilishwa: 9

Idadi ya nchi walikogawiwa: 12

Idadi ya wanafunzi: 48

Wastani wa umri: 31.7

Wastani wa miaka katika kweli: 13.8

Wastani wa miaka katika huduma ya wakati wote: 9.8

[Picha katika ukurasa wa 23]

Darasa la 101 Lililohitimu la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower

Katika orodha iliyo chini, safu zimepewa nambari kutoka mbele kuelekea nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto kuelekea kulia katika kila safu.

(1) Swint, H.; Zezenski, A.; Highfield, L.; Mercado, S.; Diehl, A.; Chavez, V.; Smith, J.; Selenius, S. (2) Kurtz, D.; Clark, C.; Leisborn, J.; Mortensen, W.; Bromiley, A.; Toikka, L.; Marten, A.; Smith, D. (3) Zezenski, D.; Bjerregaard, L.; Garafalo, B.; Kaldal, L.; Chavez, E.; Fröding, S.; Khan, R.; Selenius, R. (4) Swint, B.; Bjerregaard, M.; Garafalo, P.; Holmblad, L.; Keyzer, M.; Fröding, T.; Palfreyman, J.; Palfreyman, D. (5) Minguez, L.; Leisborn, M.; Mercado, M.; Kurtz, M.; Diehl, H.; Toikka, J.; Clark, S.; Khan, A. (6) Minguez, F.; Marten, B.; Highfield, L.; Holmblad, B.; Bromiley, K.; Kaldal, H.; Mortensen, P.; Keyzer, R.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki