Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 4/15 uku. 27
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Akila na Prisila—Wenzi Walio Kielelezo Chema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Hubiri Ili Kufanya Wanafunzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Akila
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 4/15 uku. 27

Je, Wakumbuka?

Je, umefikiria kwa uangalifu matoleo ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa umefanya hivyo, utaliona kuwa jambo lenye upendezi kukumbuka yafuatayo:

◻ Wenzi wengi wa ndoa leo wamefuataje kielelezo bora kabisa kilichoachwa na Akila na Prisila?

Akila na Prisila walitumikia katika makutaniko kadhaa tofauti-tofauti. Kama wao, Wakristo wengi wa siku ya kisasa wamekuwa tayari kuhamia mahali penye uhitaji mkubwa zaidi. Wao wanakuwa pia na furaha na uradhi utokanao na kuona masilahi ya Ufalme yakikua na utokanao na kuweza kukuza urafiki mbalimbali wa Kikristo wenye thamani.—12/15, ukurasa 24.

◻ Maoni ya Biblia ni nini juu ya vinywaji vyenye alkoholi?

Maoni ya Biblia juu ya vinywaji vyenye alkoholi ni yenye usawaziko. Kwa upande mmoja, Biblia husema kwamba divai ni zawadi kutoka kwa Mungu. (Zaburi 104:1, 15) Kwa upande ule mwingine, hiyo yalaumu kujitia kupita kiasi. (Luka 21:34; 1 Timotheo 3:8; Tito 2:3; 1 Petro 4:3)—12/15, ukurasa 27.

◻ Jambo kuu la kitabu cha Biblia cha Hagai ni nini?

Ingawa kitabu cha Hagai kina mistari 38 tu, jina la Mungu latumiwa mara 35. Unabii huo waonekana kuwa baridi jina la cheo “Bwana” litumiwapo badala ya lile jina Yehova.—1/1, ukurasa 6.

◻ Ni somo gani liwezalo kupatikana kutokana na dhambi za Daudi na Manase?

Ingawa Yehova aliwasamehe Daudi na Manase, wanaume hao—na Israeli pamoja nao—walilazimika kustahimili matokeo ya matendo yao yenye dhambi. (2 Samweli 12:11, 12; Yeremia 15:3-5) Kwa njia hiyohiyo, ingawa leo Yehova husamehe watenda-dhambi wenye kutubu, huenda kukawa na matokeo ya vitendo vyao ambayo hayawezi kuepukwa.—1/1, ukurasa 27.

◻ Ni kwa njia gani ‘miguu ya wale watangazao habari njema’ ya Ufalme wa Mungu ni “mizuri”? (Isaya 52:7)

Kwa kawaida miguu ndiyo humpeleka mtu huku na huku aendapo kuwahubiri wengine. Kwa kweli miguu hiyo inamwakilisha mtu huyo. Kwa hiyo kwa wengi wanaosikia na kuitikia vizuri habari njema ya Ufalme, miguu ya wajumbe hao kwa kweli ni mwono wenye kupendeza.—1/15, ukurasa 13.

◻ Ni kazi gani yenye sehemu mbili inayohusishwa katika ‘kutangaza habari njema’? (1 Wakorintho 9:16)

Kwanza, ni lazima tupige mbiu ya habari njema ya Ufalme. Sehemu ya pili ya kazi hiyo yahusisha kufundisha wale wanaoitikia vizuri kupigwa mbiu kwa Ufalme.—1/15, ukurasa 23.

◻ Ni manufaa gani za kibinafsi zinazotokana na kuimba nyimbo za Ufalme kwenye mikutano ya kutaniko?

Kuimba kunatupa sisi fursa ya kuonyesha hisia zetu kwa Muumba wetu. (Zaburi 149:1, 3) Kuimba kwa moyo wetu wote kutanikoni, kwaweza kutuweka katika hali ifaayo ya akilini na moyoni kwa ajili ya programu inayofuata. Kwaweza kutuchochea kwenye ushiriki mkubwa zaidi katika ibada ya Yehova.—2/1, ukurasa 28.

◻ Yaweza kusemwaje kwamba siku ya kifo ni bora kuliko siku ya kuzaliwa? (Mhubiri 7:1)

Siku ya kifo yaweza kuwa bora kuliko siku ya kuzaliwa kwa mtu ikiwa kufikia wakati huo mtu amesitawisha jina jema pamoja na Yehova, awezaye kuwafufua waaminifu wanaokufa. (Yohana 11:25)—2/15, ukurasa 12.

◻ Kwa nini kitabu cha Mhubiri chapaswa kutusaidia sisi binafsi?

Chaweza kusaidia kila mmoja wetu turekebishe mtazamo wetu juu ya uhai na yale mambo tunayokazia uangalifu. (Mhubiri 7:2; 2 Timotheo 3:16, 17)—2/15, ukurasa 16.

◻ Je, Mashahidi wa Yehova ni washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi za kidini?

La. Ingawa wana masadikisho thabiti ya kidini, wao si washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi za kidini katika maana ambayo usemi huo umekuja kutumiwa. Wao hawafanyi maandamano na vitendo vya jeuri dhidi ya wale ambao hawakubaliani nao. Wanamwiga Kiongozi wao, Yesu Kristo.—3/1, ukurasa 6.

◻ Kutojua wakati barabara wa kuja kwa Yesu kutekeleza kisasi cha Mungu kuna tokeo jipi juu ya Wakristo?

Huko huelekea kudumisha Wakristo wakiwa macho na huwapa fursa ya kila siku ya kuthibitisha kwamba wamtumikia Yehova kwa sababu zisizo zenye ubinafsi.—3/1, ukurasa 13.

◻ Twapaswa kufikiria nini kabla ya kuchukua hatua ya kisheria dhidi ya ndugu ambaye huenda akawa ametupunja?

Twapaswa kufikiria matokeo yawezayo kutupata sisi, kuwapata wengine wahusikao, kulipata kutaniko, na kuwapata walio nje ya kutaniko. (1 Wakorintho 6:7)—3/15, ukurasa 22.

◻ Furaha ya kweli yaweza kupatikanaje?

Furaha ya kweli ni hali ya moyoni, inayotegemea imani ya kweli na uhusiano mzuri pamoja na Yehova. (Mathayo 5:3)—3/15, ukurasa 23.

◻ Mkristo apaswa kufanya nini aitwapo kwa ajili ya kazi ya baraza la mahakama?

Kila Mkristo akabiliwaye na kazi ya baraza la mahakama lazima aazimie ni mwendo gani wa kufuata, kwa kutegemea uelewevu wake wa Biblia na dhamiri yake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)—4/1, ukurasa 29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki