Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 3/1 uku. 7
  • Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • “Njia ya Mungu ya Maisha” Mkusanyiko wa Wilaya na wa Kimataifa wa 1998
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Mikusanyiko ya Wilaya ya 1999 ya “Neno la Mungu la Kiunabii”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 3/1 uku. 7

Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?

KILA mwaka maelfu ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote hukusanyika kwenye mikusanyiko. Huko wao huonea shangwe ushirika na kusikiliza programu bora kabisa ya mafundisho ya Biblia. Baadhi yao hujitahidi sana kuhudhuria mikusanyiko hiyo. Kwa kielelezo, mwaka uliopita katika Malawi wenzi wa ndoa walio katika miaka yao ya 60, pamoja na mwana wao na mke wake na mtoto mchanga, walisafiri kilometa 80 kwa baiskeli ili kuhudhuria mkusanyiko. Waliondoka kijijini mwao saa 12 asubuhi na kufika kwenye uwanja wa mkusanyiko muda wa saa 15 baadaye.

Katika Msumbiji, kikundi fulani kilisafiri siku tatu kwa baiskeli ili kufika kwenye mkusanyiko. Usiku mmoja, walipopiga kambi nje, walisikia simba wakinguruma karibu. Ingawa walitupa kuni upande waliokuwa wanyama hao, hao simba walikaa karibu-karibu hadi mapambazuko. Shahidi mwingine aliyekuwa akisafiri kuelekea kusanyiko hilohilo alikutana uso kwa uso na simba barabarani. Alisimama kimya bila kujongea hadi huyo simba alipoenda zake. Kwenye huo mkusanyiko Mashahidi hao walisimulia kwa uchangamfu jinsi walivyokuwa “[wame]kombolewa kutoka katika kinywa cha simba.”—2 Timotheo 4:17.

Mashahidi wa Yehova walio wengi hujitahidi sana kuhudhuria mikusanyiko au hata mikutano ya kutaniko ya kila juma kwa ajili ya ibada. Kwa nini? Makala zinazofuata zitakusaidia uelewe kwa nini kukusanyika pamoja ni kwa maana sana.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki